Hotuba ya Rais Samia naifananisha na ile ya Mzee Kikwete alivyoingia madarakani

Hotuba ya Rais Samia naifananisha na ile ya Mzee Kikwete alivyoingia madarakani

Wilderness Voice

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2016
Posts
921
Reaction score
1,649
Wakati Mhe. Rais kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alitoa hotuba safi sana, ambayo kweli tulikuwa na matumaini ya kuwa na Tanzania mpya, na yenye maendeleo ya kasi. Aliongelea mambo mengi ikiwepo uwekezaji, na kujali wawekezaji, kweli milango ilifunguliwa tulipata wawekezaji wa kila namna hata kule kariakoo walijaa wakiuza karanga na ufuta. Wawekezaji walipata sauti na kuwa wasemaji wa mwisho kwani hatukutaka kuwaudhi bali kuwabembeleza na kujikomba kwao.

Vibali vya kazi vilitolewa kama njugu, ili kuwafanya wawekezaji kuwa na wafanyakazi wenye vigezo wanayotaka wao. Tuliona makampuni ya uwekezaji yakiwa na maafisa wote wa juu kutoka nje ya nchi, huku watanzania wakiishia kuwa vibarua na kufukuzwa kazi muda wowote. Huku wakilipwa mishahara ya chini kabisa.

Leo rais wetu kasisitiza kuwa vibali vya kazi vitolewe haraka, bila usumbufu, na pia milango ifunguliwe kwa wewekezaji. Najiuliza tu, hivi nchi kama China, India, Singapore, na hapa africa kuna Ethiopia uchumi wake unakuwa kwa kasi zinategemea wawekezaji kutoka nje pekee? Kama ingekuwa hivyo kwa Kikwete tulijaza wawekezaji, ni nini Taifa lilipata au kufaidika?

Kwanini tusiimarishe uwekezaji wa ndani, ambao serikali iwawezeshe wazawa kuwekeza na si kudhani tutaendelea kwa huu uwekezaji kutoka nje pekee. Sipingi wawekezaji wa nje lakini nawasiwasi kulingana na historia hapo nyuma. Wawepo ila serikali isiwekwe mfukoni, na si vizuri kutoa vibali vya kazi kama njugu.

Mhe. Rais kaongelea Kuboresha ufugaji kwa kuwa na ufugaji wa kisasa, na kupunguza mifugo. Sawa na Rais kikwete wakati huo alitamba na hii hoja na kudai mifugo inakoda na mchungaji anakonda. Akadai kuondoa tatizo katika serikali yake. Sikuwahi kuona jitihada zozote zilizofanyika, mpaka anaondoka madarakani.

Hii leo rais wetu nae anakuja na mapambio yale yale ufugaji wa kisasa, kupunguza mifugo. Hapa katika kupunguza mifungo sioni kama ni hoja. Mungu katupatia mifugo, ni nchi ya pili kwa mifugo Afrika baada ya Ethiopia. Mbona Ethiopia hawana hoja ya kupunguza mifugo, ila wao wanaviwanda vikubwa na vidogo vya ngozi, wanatengeneza viatu, mabegi, mikanda nk. wanasoko la ndani na nje ya nchi tena kubwa sana.

Sisi tunafikiria kupunguza mifugo. Badala ya kuboresha mifugo. Tunataka ng`ombe wa kisasa! Ethiopia ng´ombe wengi ni wakienyeji.

Rais anasema atakusanya kodi kwa kubembeleza, kuchekeana, anasahau enzi za Kikwete kulileta dharau kwa serikali, watu walikwepa kodi hakuna alie fatilia.

Uzuri rais kakiri mwenyewe kuwa serikali ilikuwa katika maongezi na baadhi ya wawekezaji sasa wameanza kugoma. Mie niseme ngoja wagome tu maake mama yeye ndo amedai tuwabembeleze. Namshangaa analalamika. Anadai yeye na Magufuli ni wamoja, sidhani! Yeye amejitangaza kubembeleza kukusanya kodi, aendelee kubembeleza. Tutalipa tu.

Mwisho Rais naona anarudisha wazo la kujenga bandari ya Bagamoyo tena kasema tutake tusitake. Sisi tunataka lakini mkataba upelekwe bungeni ili ujadiliwe na kupitiwa na watanzania tujue.

Nashukuru Rais hajafuata mienendo ya Magufuli bali kachagua mienendo ya Kikwete. Upole kubembeleza, kusamehe, na kuiweka nchi kwa wawekezaji. Safi sana! Wakati wa Kikwete watu tulisema tunataka kiongozi mkali, asie ogopa, na mwenye uthubutu.

Mungu akasikia maombi yetu akatupatia Magufuli. Tukalalamika kwa Mungu Magufuli mkali, haya Mungu katusikia katupatia tena mama wa kubembeleza, pacha kama Kikwete tusije lalamika tena.

Nampenda mama, kama Rais kipenzi ila naona kivuli cha Kikwete ndani. Mama ningetamani ungekuwa na style ya uongozi wako kivyako vyako. Najua Kikwete ni mshauri wako kama ulivyokiri weye mwenyewe. Ungekuja kivyako vyako. Ila ili swala la machimbo kwenye mbuga zetu tafadhali mama lifikirie mara mbili.

Kuwekeza shirika la ndege, ATCL ilishawahi kuwekezwa hata shirika la reli matokeo kila kitu kilikufa, kuwa makini ktk hili. Ethiopia waliambiwa wawekeze shirika lao, waligoma hadi leo linajiendesha vizuri tu.

Hivi hatuna kabisa watanzania ambao ni wataalamu maswala ya anga na usafiri wa ndege wenye kuweza kuboresha shirika letu. Tuwaazime basi waethiopia walau waje kutuelekeza na kutupatia ujuzi. Shirika la ndege la Ethiopia wana miliki chuo cha marubani, chuo cha wahudumu katika ndege, wanachuo cha uongozi na usimamizi wa ndege, wanachuo cha ufundi wa ndege, pia Shirika la ndege linamiliki hotel kubwa ya nyota tano. Mambo yote wanafanya wenyewe. Kwanini sisi watanzania tushindwe, na kuamini wengine wanaweza sisi hatuwezi? Kwanini narudia kwanini?

Kero za watanzania toka nazaliwa hadi leo ni zile zile, wawe wabunge, wanalalamikia mambo yale yale, hivi serikali imeshindwa maliza kero za wananchi. Migogoro ya ardhi , hivi kweli migogoro ya ardhi haiwezi malizwa? Viongozi tumewachoka, hakuna maono, nini kifanyike! tunahitaji sasa viongozi wenye maono mapya, na kutekeleza maono hayo bila kuogopa. Wanao sababisha migogoro ya ardhi ni serikali za mitaa, tunashindwa kweli kuwabana maafisa ardhi? Tunashindwa kupima ardhi yetu?

Tunasikia madawa hakuna, hivi serikali ili linashindikana? Kweli madawa ati yanakosekana? Ati maji hatuna wakati nchi imebarikiwa kwa maziwa, mito na bahari! Dubai ni kukame, lakini wameondoa shida ya maji! sisi tunaviongozi wapo tu! Kuna muda nawaza kuwa hatuhitaji mawaziri? Yaani sioni wafanyacho zaidi kujipendekeza kwa Rais.
 
Mama anaingizwa mkenge baadhi ya mambo

1. Vibali vya kazi, kuna hatari ya kurudi kule kule, wageni hadi wafagiaji

2. ATCL solution ni kulifanya liwe la umma Kwa kuuza hisa Kwa wananchi na bodi mpya itaajiri
Watu wapya. Wazalendo na hisa kidogo Kwa wageni kama ilivyo Bank ya NMB.

3. Migogoro ya ardhi ..maafisa ardhi hawafukuzwi wakiboronga hili ndo tatizo
Mtu anatoa hati mbili kiwanja kimoja na hafukuzwi..

4. Bandari ya Bagamoyo ijengwe ndio lakini mkataba uwe wazi ujadiliwe ..tukatae mkopo ..

5U kwepaji Kodi bado tatizo sugu
Uwazi uongezwe...

6.Utalii ndo hakusema cha maana
Akiendeleza ya Magufuli tutazidi poteza watalii... asilimia 80 ya watalii hawarudi
 
8 Reasons Why Rome Fell
  • Invasions by Barbarian tribes. ...
  • Economic troubles and overreliance on slave labor. ...
  • The rise of the Eastern Empire. ...
  • Overexpansion and military overspending. ...
  • Government corruption and political instability. ...
  • The arrival of the Huns and the migration of the Barbarian tribes. ...
  • Christianity and the loss of traditional values.
  • 8. Weakening of the Roman legions​

 
Mama anaingizwa mkenge baadhi ya mambo

1.Vibali vya kazi ...kuna hatari ya kurudi kule kule ..wageni hadi wafagiaji...
Expert atalipwa 20m, mbongo kwa kazi Hiyo hiyo atalipwa 2m halafu mtu na akili yake nzuri tu anategemea tija ya huyu akiye lipwa 2m iwe sawa na anaye lipwa 20 M.

Au kumtuhumu kwamba mbongo mwizi, wakati mazingira yana msababisha awe mbunifu.
 
Ziko saba
Ya nane iko wapi??
Ina relate vipi na Tanzania?
Relevance inaweza kuwa kwenye political instability , corruption n.k
Pia economic problems na kutolipwa kwa kodi

2. Economic troubles and overreliance on slave labor​

Even as Rome was under attack from outside forces, it was also crumbling from within thanks to a severe financial crisis. Constant wars and overspending had significantly lightened imperial coffers, and oppressive taxation and inflation had widened the gap between rich and poor. In the hope of avoiding the taxman, many members of the wealthy classes had even fled to the countryside and set up independent fiefdoms. At the same time, the empire was rocked by a labor deficit.

Rome’s economy depended on slaves to till its fields and work as craftsmen, and its military might had traditionally provided a fresh influx of conquered peoples to put to work. But when expansion ground to a halt in the second century, Rome’s supply of slaves and other war treasures began to dry up. A further blow came in the fifth century, when the Vandals claimed North Africa and began disrupting the empire’s trade by prowling the Mediterranean as pirates. With its economy faltering and its commercial and agricultural production in decline, the Empire began to lose its grip on Europe.

3. The rise of the Eastern Empire​

The fate of Western Rome was partially sealed in the late third century, when the Emperor Diocletian divided the Empire into two halves—the Western Empire seated in the city of Milan, and the Eastern Empire in Byzantium, later known as Constantinople. The division made the empire more easily governable in the short term, but over time the two halves drifted apart. East and West failed to adequately work together to combat outside threats, and the two often squabbled over resources and military aid.

As the gulf widened, the largely Greek-speaking Eastern Empire grew in wealth while the Latin-speaking West descended into economic crisis. Most importantly, the strength of the Eastern Empire served to divert Barbarian invasions to the West. Emperors like Constantine ensured that the city of Constantinople was fortified and well guarded, but Italy and the city of Rome—which only had symbolic value for many in the East—were left vulnerable. The Western political structure would finally disintegrate in the fifth century, but the Eastern Empire endured in some form for another thousand years before being overwhelmed by the Ottoman Empire in the 1400s.

4. Overexpansion and military overspending​

At its height, the Roman Empire stretched from the Atlantic Ocean all the way to the Euphrates River in the Middle East, but its grandeur may have also been its downfall. With such a vast territory to govern, the empire faced an administrative and logistical nightmare. Even with their excellent road systems, the Romans were unable to communicate quickly or effectively enough to manage their holdings.

Rome struggled to marshal enough troops and resources to defend its frontiers from local rebellions and outside attacks, and by the second century the Emperor Hadrian was forced to build his famous wall in Britain just to keep the enemy at bay. As more and more funds were funneled into the military upkeep of the empire, technological advancement slowed and Rome’s civil infrastructure fell into disrepair.

5. Government corruption and political instability​

If Rome’s sheer size made it difficult to govern, ineffective and inconsistent leadership only served to magnify the problem. Being the Roman emperor had always been a particularly dangerous job, but during the tumultuous second and third centuries it nearly became a death sentence.

Civil war thrust the empire into chaos, and more than 20 men took the throne in the span of only 75 years, usually after the murder of their predecessor. The Praetorian Guard—the emperor’s personal bodyguards—assassinated and installed new sovereigns at will, and once even auctioned the spot off to the highest bidder. The political rot also extended to the Roman Senate, which failed to temper the excesses of the emperors due to its own widespread corruption and incompetence. As the situation worsened, civic pride waned and many Roman citizens lost trust in their leadership.

6. The arrival of the Huns and the migration of the Barbarian tribes​

The Barbarian attacks on Rome partially stemmed from a mass migration caused by the Huns’ invasion of Europe in the late fourth century. When these Eurasian warriors rampaged through northern Europe, they drove many Germanic tribes to the borders of the Roman Empire. The Romans grudgingly allowed members of the Visigoth tribe to cross south of the Danube and into the safety of Roman territory, but they treated them with extreme cruelty.

According to the historian Ammianus Marcellinus, Roman officials even forced the starving Goths to trade their children into slavery in exchange for dog meat. In brutalizing the Goths, the Romans created a dangerous enemy within their own borders. When the oppression became too much to bear, the Goths rose up in revolt and eventually routed a Roman army and killed the Eastern Emperor Valens during the Battle of Adrianople in A.D. 378.

The shocked Romans negotiated a flimsy peace with the barbarians, but the truce unraveled in 410, when the Goth King Alaric moved west and sacked Rome. With the Western Empire weakened, Germanic tribes like the Vandals and the Saxons were able to surge across its borders and occupy Britain, Spain and North Africa.

7. Christianity and the loss of traditional values​

The decline of Rome dovetailed with the spread of Christianity, and some have argued that the rise of a new faith helped contribute to the empire’s fall. The Edict of Milan legalized Christianity in 313, and it later became the state religion in 380. These decrees ended centuries of persecution, but they may have also eroded the traditional Roman values system.

Christianity displaced the polytheistic Roman religion, which viewed the emperor as having a divine status, and also shifted focus away from the glory of the state and onto a sole deity. Meanwhile, popes and other church leaders took an increased role in political affairs, further complicating governance. The 18th-century historian Edward Gibbon was the most famous proponent of this theory, but his take has since been widely criticized. While the spread of Christianity may have played a small role in curbing Roman civic virtue, most scholars now argue that its influence paled in comparison to military, economic and administrative factors.

8. Weakening of the Roman legions​

For most of its history, Rome’s military was the envy of the ancient world. But during the decline, the makeup of the once mighty legions began to change. Unable to recruit enough soldiers from the Roman citizenry, emperors like Diocletian and Constantine began hiring foreign mercenaries to prop up their armies. The ranks of the legions eventually swelled with Germanic Goths and other barbarians, so much so that Romans began using the Latin word “barbarus” in place of “soldier.”

While these Germanic soldiers of fortune proved to be fierce warriors, they also had little or no loyalty to the empire, and their power-hungry officers often turned against their Roman employers. In fact, many of the barbarians who sacked the city of Rome and brought down the Western Empire had earned their military stripes while serving in the Roman legions.

leadership.
 
Mama anaingizwa mkenge baadhi ya mambo

1.Vibali vya kazi ...kuna hatari ya kurudi kule kule ..wageni hadi wafagiaji...
5.Ukwepaji kodi bado tatizo sugu. (Nakubaliana nawe).

Kwa maoni yako unadhani ni nini chanzo au sababu ya ukwepaji kodi hadi kufanya uwe sugu?

Nini kifanyike ili watu walipe kodi kwa hiari au wajisikie au waelewe kulipa kodi ni wajibu wa kila mwananchi?
 
Tzn hapa hakuna ma CEO wa kuendesha kampuni binafsi za kiuwekezaji zifaulu ndio maana hilo la vibali linasisitizwa.

Imagine elimu ya bongo na nature ya wabongo hatuna gati za biashara binafsi nani atakubali kuajiriwa mtu asiye na skills.

Serikalini huko ni mamiradi mengi wanaanzisha na hasara tupu,kwa nini watu wasilete experts wao?

Ni wajibu wa watoa vibali kuhakikisha vibali vinatolewa kama walivyoomba na ufuatiliaji uwepo

Mama ameamua kutatua tatizo la ajira kwa broader look na limbukeni yeye amewahi fanya Kazi huko

Bora maisha ya kipindi cha JK kuliko Sana za Magufuli,nani anapenda kuwa maskini kama Limagu lilivyokuwa kinataka tuwe
 
Mama anaingizwa mkenge baadhi ya mambo

1.Vibali vya kazi ...kuna hatari ya kurudi kule kule ..wageni hadi wafagiaji...
Mkenge gani, kipindi cha Magu watu wamefaidikaje zaidi ya wizi kushamili?

Serikali yenyewe ilitegemea mikopo na wahisani kwenye miradi huku ikilisha watu propaganda
 
Wakati Mhe. Rais kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alitoa hotuba safi sana, ambayo kweli tulikuwa na matumaini ya kuwa na Tanzania mpya, na yenye maendeleo ya kasi...
Kati ya yote uliyoongea labda cha maana ni Kuhusu shirika la ndege

Hayo mengine ni mashaka yako tuu,mathalani kipindi cha Kikwete biashara ilishamiri na watu tulijiajiri,kipindi cha Magu biashara zilikolapse na kila mtu akawa anawaza kuajiriwa na Serikali

Sasa wewe awamu ipi unataka,ya kuogopana huku Nchi inakopa kujiendesha au ya leize afair ambapo watu wataishi maisha mazuri na Serikali inapunguza mzigo wa kutegemewa Ili iweze kufanya mambo ya msingi ya watu wake
 
"Safi sana! Wakati wa Kikwete watu tulisema tunataka kiongozi mkali, asie ogopa, na mwenye uthubutu. Mungu akasikia maombi yetu akatupatia Magufuli. Tukalalamika kwa Mungu Magufuli mkali, haya Mungu katusikia katupatia tena mama wa kubembeleza, pacha kama Kikwete tusije lalamika tena".

HIVI MUNGU YEYE HAJUI TANZANIA TUNAHIATAJI RAIS WA AINA GANI?

HAFAHAMU NI RAIS YUPI MZURI ATAKEYETUFAA?

AU NI UJINGA WENU WA KUTAKA KUAMNINISHA WATU MUNGU ANAWASIKILIZA SANA RAIA WA TANZANIA?
Wakati Mhe. Rais kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alitoa hotuba safi sana, ambayo kweli tulikuwa na matumaini ya kuwa na Tanzania mpya, na yenye maendeleo ya kasi....
 
Mama anaingizwa mkenge baadhi ya mambo

1.Vibali vya kazi ...kuna hatari ya kurudi kule kule ..wageni hadi wafagiaji...
Nakupinga namba 1 na mbili. Vibali vya kazi yupo sahihi. Ni upuuzi uliotukuka nakuja kuwekeza kwa kurisk mtaji wangu alafu unanipangia huyu nimuajiri na huyu nisimuajiri. Kama hujui haya ni mambo yaliyosabisha maelfu ya wawekezaji kuondoka Tanzania maana unamlazimisha kumuajiri mtanzania katika sehemu ambayo akikaa anafanya Wizi na mwekezaji anapata hasara.

Kuhusu ATCL amesema sawa. Solution ni kuipunguzia mzigo wa madeni na kuifanya iwe na management Bora inayotengeneza faida. Tatizo liko wapi?
 
Safi sana kwa kumpa za uso. Hakuna Rais aliyeweka mazingira Safi ya uwekezaji na kusababisha watu wengi kuajiriwa na kujiajiri Kama Kikwete. Sasa huyu mpuuzi anataka kutuletea akili za Magufuli zilizokuwa zinatupeleka Venezuela na Cuba. Hana akili huyu
Kati ya yote uliyoongea labda cha maana ni Kuhusu shirika la ndege...
 
Kwanini tusiimarishe uwekezaji wa ndani, ambao serikali iwawezeshe wazawa kuwekeza na si kudhani tutaendelea kwa huu uwekezaji kutoka nje pekee
Watanzania msikosoe kila kitu bwana.

Mama SASHA anakazia volipengele ambavyo vilikuwa vimedorora na katika vipengele hivyo ni uwekezaji wa nje.

Hivyo inamlazimu kuondoa changamaoto na kupigia debe uwekezaji wa nje kwanza kwa sababu hapo changamoto ipo kubwa.

Na wala mama hakusema kuwa hatojali uwekezaji wa ndani.mbaya zaidi wa tz ukisisitiza jambo moja wanadhani jingine unapuuza,na wewe ndio mtz mwenye mawazo hayo.

Mama akisema atadumisha uwekezaji wa nje hana maana huu wa ndani ataupuuza,huko pia atafika lakini anaondoa changamoto hii ya wawekezaji wa nje ambao ilikuwa na shida kubwa.
 
Wakati Mhe. Rais kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alitoa hotuba safi sana, ambayo kweli tulikuwa na matumaini ya kuwa na Tanzania mpya, na yenye maendeleo ya kasi...
Muache huyu mama Samia Suluhu Hassan. Kama huwezani kama kasi hama nchi.

As a nation we need new hope, hata Kama hatotekeleza but at least kaleta tumaini jipya after 6 years of ❤️ broke.
 
Kati ya yote uliyoongea labda cha maana ni Kuhusu shirika la ndege

Hayo mengine ni mashaka yako tuu,mathalani kipindi cha Kikwete biashara ilishamiri na watu tulijiajiri,kipindi cha Magu biashara zilikolapse na kila mtu akawa anawaza kuajiriwa na Serikali

Sasa wewe awamu ipi unataka,ya kuogopana huku Nchi inakopa kujiendesha au ya leize afair ambapo watu wataishi maisha mazuri na Serikali inapunguza mzigo wa kutegemewa Ili iweze kufanya mambo ya msingi ya watu wake
Duuuh
 
Back
Top Bottom