Hotuba ya Rais Samia naifananisha na ile ya Mzee Kikwete alivyoingia madarakani

Hotuba ya Rais Samia naifananisha na ile ya Mzee Kikwete alivyoingia madarakani

Wakati Mhe. Rais kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alitoa hotuba safi sana, ambayo kweli tulikuwa na matumaini ya kuwa na Tanzania mpya, na yenye maendeleo ya kasi...
Nchi zilizofanikiwa zilibeba wawekezaji wa ndani, hawq wa nje wengi ni wa kuja kuchota rasilimali.

Amezungumzia uchumi wa bahari na kusema serikali itanunua meli nane ambazo nne zitatumika bara na nne visiwani. Tanzania bara ina eneo kubwa la bahari kuanzia bagamoyo, Dar es salaam, Tanga, Lindi na Mtwara kwanini agawe nusu bara na nusu visiwani, asitumie pesa za watanyika kuendeleza Zanzibar kama angetaka kuwapendelea angewapa meli mbili
 
Nakupinga namba 1 na mbili. Vibali vya kazi yupo sahihi. Ni upuuzi uliotukuka nakuja kuwekeza kwa kurisk mtaji wangu alafu unanipangia huyu nimuajiri na huyu nisimuajiri. Kama hujui haya ni mambo yaliyosabisha maelfu ya wawekezaji kuondoka Tanzania maana unamlazimisha kumuajiri mtanzania katika sehemu ambayo akikaa anafanya Wizi na mwekezaji anapata hasara.

Kuhusu ATCL amesema sawa. Solution ni kuipunguzia mzigo wa madeni na kuifanya iwe na management Bora inayotengeneza faida. Tatizo liko wapi??
Hicho kitu kipo kila nchi, hivi unajua hasara ya kukaa bila wananchi wako kuwa na ajila . Unazalisha vibaka, majambazi, mateja, malaya na shuguri nyingine zisizo halali.
 
Wakati Mhe. Rais kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alitoa hotuba safi sana, ambayo kweli tulikuwa na matumaini ya kuwa na Tanzania mpya, na yenye maendeleo ya kasi. Aliongelea mambo mengi ikiwepo uwekezaji, na kujali wawekezaji, kweli milango ilifunguliwa tulipata wawekezaji wa kila namna hata kule kariakoo walijaa wakiuza karanga na ufuta. Wawekezaji walipata sauti na kuwa wasemaji wa mwisho kwani hatukutaka kuwaudhi bali kuwabembeleza na kujikomba kwao.

Vibali vya kazi vilitolewa kama njugu, ili kuwafanya wawekezaji kuwa na wafanyakazi wenye vigezo wanayotaka wao. Tuliona makampuni ya uwekezaji yakiwa na maafisa wote wa juu kutoka nje ya nchi, huku watanzania wakiishia kuwa vibarua na kufukuzwa kazi muda wowote. Huku wakilipwa mishahara ya chini kabisa.

Leo rais wetu kasisitiza kuwa vibali vya kazi vitolewe haraka, bila usumbufu, na pia milango ifunguliwe kwa wewekezaji. Najiuliza tu, hivi nchi kama China, India, Singapore, na hapa africa kuna Ethiopia uchumi wake unakuwa kwa kasi zinategemea wawekezaji kutoka nje pekee? Kama ingekuwa hivyo kwa Kikwete tulijaza wawekezaji, ni nini Taifa lilipata au kufaidika?

Kwanini tusiimarishe uwekezaji wa ndani, ambao serikali iwawezeshe wazawa kuwekeza na si kudhani tutaendelea kwa huu uwekezaji kutoka nje pekee. Sipingi wawekezaji wa nje lakini nawasiwasi kulingana na historia hapo nyuma. Wawepo ila serikali isiwekwe mfukoni, na si vizuri kutoa vibali vya kazi kama njugu.

Mhe. Rais kaongelea Kuboresha ufugaji kwa kuwa na ufugaji wa kisasa, na kupunguza mifugo. Sawa na Rais kikwete wakati huo alitamba na hii hoja na kudai mifugo inakoda na mchungaji anakonda. Akadai kuondoa tatizo katika serikali yake. Sikuwahi kuona jitihada zozote zilizofanyika, mpaka anaondoka madarakani.

Hii leo rais wetu nae anakuja na mapambio yale yale ufugaji wa kisasa, kupunguza mifugo. Hapa katika kupunguza mifungo sioni kama ni hoja. Mungu katupatia mifugo, ni nchi ya pili kwa mifugo Afrika baada ya Ethiopia. Mbona Ethiopia hawana hoja ya kupunguza mifugo, ila wao wanaviwanda vikubwa na vidogo vya ngozi, wanatengeneza viatu, mabegi, mikanda nk. wanasoko la ndani na nje ya nchi tena kubwa sana.

Sisi tunafikiria kupunguza mifugo. Badala ya kuboresha mifugo. Tunataka ng`ombe wa kisasa! Ethiopia ng´ombe wengi ni wakienyeji.

Rais anasema atakusanya kodi kwa kubembeleza, kuchekeana, anasahau enzi za Kikwete kulileta dharau kwa serikali, watu walikwepa kodi hakuna alie fatilia.

Uzuri rais kakiri mwenyewe kuwa serikali ilikuwa katika maongezi na baadhi ya wawekezaji sasa wameanza kugoma. Mie niseme ngoja wagome tu maake mama yeye ndo amedai tuwabembeleze. Namshangaa analalamika. Anadai yeye na Magufuli ni wamoja, sidhani! Yeye amejitangaza kubembeleza kukusanya kodi, aendelee kubembeleza. Tutalipa tu.

Mwisho Rais naona anarudisha wazo la kujenga bandari ya Bagamoyo tena kasema tutake tusitake. Sisi tunataka lakini mkataba upelekwe bungeni ili ujadiliwe na kupitiwa na watanzania tujue.

Nashukuru Rais hajafuata mienendo ya Magufuli bali kachagua mienendo ya Kikwete. Upole kubembeleza, kusamehe, na kuiweka nchi kwa wawekezaji. Safi sana! Wakati wa Kikwete watu tulisema tunataka kiongozi mkali, asie ogopa, na mwenye uthubutu.

Mungu akasikia maombi yetu akatupatia Magufuli. Tukalalamika kwa Mungu Magufuli mkali, haya Mungu katusikia katupatia tena mama wa kubembeleza, pacha kama Kikwete tusije lalamika tena.

Nampenda mama, kama Rais kipenzi ila naona kivuli cha Kikwete ndani. Mama ningetamani ungekuwa na style ya uongozi wako kivyako vyako. Najua Kikwete ni mshauri wako kama ulivyokiri weye mwenyewe. Ungekuja kivyako vyako. Ila ili swala la machimbo kwenye mbuga zetu tafadhali mama lifikirie mara mbili.

Kuwekeza shirika la ndege, ATCL ilishawahi kuwekezwa hata shirika la reli matokeo kila kitu kilikufa, kuwa makini ktk hili. Ethiopia waliambiwa wawekeze shirika lao, waligoma hadi leo linajiendesha vizuri tu.

Hivi hatuna kabisa watanzania ambao ni wataalamu maswala ya anga na usafiri wa ndege wenye kuweza kuboresha shirika letu. Tuwaazime basi waethiopia walau waje kutuelekeza na kutupatia ujuzi. Shirika la ndege la Ethiopia wana miliki chuo cha marubani, chuo cha wahudumu katika ndege, wanachuo cha uongozi na usimamizi wa ndege, wanachuo cha ufundi wa ndege, pia Shirika la ndege linamiliki hotel kubwa ya nyota tano. Mambo yote wanafanya wenyewe. Kwanini sisi watanzania tushindwe, na kuamini wengine wanaweza sisi hatuwezi? Kwanini narudia kwanini?

Kero za watanzania toka nazaliwa hadi leo ni zile zile, wawe wabunge, wanalalamikia mambo yale yale, hivi serikali imeshindwa maliza kero za wananchi. Migogoro ya ardhi , hivi kweli migogoro ya ardhi haiwezi malizwa? Viongozi tumewachoka, hakuna maono, nini kifanyike! tunahitaji sasa viongozi wenye maono mapya, na kutekeleza maono hayo bila kuogopa. Wanao sababisha migogoro ya ardhi ni serikali za mitaa, tunashindwa kweli kuwabana maafisa ardhi? Tunashindwa kupima ardhi yetu?

Tunasikia madawa hakuna, hivi serikali ili linashindikana? Kweli madawa ati yanakosekana? Ati maji hatuna wakati nchi imebarikiwa kwa maziwa, mito na bahari! Dubai ni kukame, lakini wameondoa shida ya maji! sisi tunaviongozi wapo tu! Kuna muda nawaza kuwa hatuhitaji mawaziri? Yaani sioni wafanyacho zaidi kujipendekeza kwa Rais.
Yote uliyoandika ni mawazo ya Kimasikini, yaani wewe hutaki Maendeleo

Hutaki kuona Bandari ya Bagamoyo ikijengwa na Tanzania kuchukua nafasi yake kama lango kuu la Africa Mashariki na Kati, huku mamia kwa mamia ya Watanzania wakipata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja. Mji ukikua na uchumi kupanda.

Wewe hutaki vibali vya kazi vitolewe ili tupate wataalamu wakati na sisi tunajitahidi kutengeneza skills za maana badala ya degree za ukarani tunazotoa. Mfano mtu anaanzisha kiwanda cha kurefine mafuta hapa analeta Bleacher hakuna mtu wa kuiendesha Tanzania kwanini anyimwe kule Muhindi hata kama hajasoma?
 
"Safi sana! Wakati wa Kikwete watu tulisema tunataka kiongozi mkali, asie ogopa, na mwenye uthubutu.
Mungu akasikia maombi yetu akatupatia Magufuli. Tukalalamika kwa Mungu Magufuli mkali, haya Mungu katusikia katupatia tena mama wa kubembeleza, pacha kama Kikwete tusije lalamika tena"

HIVI MUNGU YEYE HAJUI TANZANIA TUNAHIATAJI RAIS WA AINA GANI??
HAFAHAMU NI RAIS YUPI MZURI ATAKEYETUFAA??
AU NI UJINGA WENU WA KUTAKA KUAMNINISHA WATU MUNGU ANAWASIKILIZA SANA RAIA WA TANZANIA??


Mods pls TUNZENI HII KOMENTI, SAWA!??? (Hata kama mtahitaji malipo kidogo tutawapeni 🙂 )
 
Nchi zilizofanikiwa zilibeba wawekezaji wa ndani, hawq wa nje wengi ni wa kuja kuchota rasilimali.
Amezungumzia uchumi wa bahari na kusema serikali itanunua meli nane ambazo nne zitatumika bara na nne visiwani. Tanzania bara ina eneo kubwa la bahari kuanzia bagamoyo, Dar es salaam, Tanga, Lindi na Mtwara kwanini agawe nusu bara na nusu visiwani, asitumie pesa za watanyika kuendeleza Zanzibar kama angetaka kuwapendelea angewapa meli mbili


Au kwa vile Zenj imezungukwa na bahari!??? (May be!???)
 
Wakati Mhe. Rais kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alitoa hotuba safi sana, ambayo kweli tulikuwa na matumaini ya kuwa na Tanzania mpya, na yenye maendeleo ya kasi. Aliongelea mambo mengi ikiwepo uwekezaji, na kujali wawekezaji, kweli milango ilifunguliwa tulipata wawekezaji wa kila namna hata kule kariakoo walijaa wakiuza karanga na ufuta. Wawekezaji walipata sauti na kuwa wasemaji wa mwisho kwani hatukutaka kuwaudhi bali kuwabembeleza na kujikomba kwao.

Vibali vya kazi vilitolewa kama njugu, ili kuwafanya wawekezaji kuwa na wafanyakazi wenye vigezo wanayotaka wao. Tuliona makampuni ya uwekezaji yakiwa na maafisa wote wa juu kutoka nje ya nchi, huku watanzania wakiishia kuwa vibarua na kufukuzwa kazi muda wowote. Huku wakilipwa mishahara ya chini kabisa.

Leo rais wetu kasisitiza kuwa vibali vya kazi vitolewe haraka, bila usumbufu, na pia milango ifunguliwe kwa wewekezaji. Najiuliza tu, hivi nchi kama China, India, Singapore, na hapa africa kuna Ethiopia uchumi wake unakuwa kwa kasi zinategemea wawekezaji kutoka nje pekee? Kama ingekuwa hivyo kwa Kikwete tulijaza wawekezaji, ni nini Taifa lilipata au kufaidika?

Kwanini tusiimarishe uwekezaji wa ndani, ambao serikali iwawezeshe wazawa kuwekeza na si kudhani tutaendelea kwa huu uwekezaji kutoka nje pekee. Sipingi wawekezaji wa nje lakini nawasiwasi kulingana na historia hapo nyuma. Wawepo ila serikali isiwekwe mfukoni, na si vizuri kutoa vibali vya kazi kama njugu.

Mhe. Rais kaongelea Kuboresha ufugaji kwa kuwa na ufugaji wa kisasa, na kupunguza mifugo. Sawa na Rais kikwete wakati huo alitamba na hii hoja na kudai mifugo inakoda na mchungaji anakonda. Akadai kuondoa tatizo katika serikali yake. Sikuwahi kuona jitihada zozote zilizofanyika, mpaka anaondoka madarakani.

Hii leo rais wetu nae anakuja na mapambio yale yale ufugaji wa kisasa, kupunguza mifugo. Hapa katika kupunguza mifungo sioni kama ni hoja. Mungu katupatia mifugo, ni nchi ya pili kwa mifugo Afrika baada ya Ethiopia. Mbona Ethiopia hawana hoja ya kupunguza mifugo, ila wao wanaviwanda vikubwa na vidogo vya ngozi, wanatengeneza viatu, mabegi, mikanda nk. wanasoko la ndani na nje ya nchi tena kubwa sana.

Sisi tunafikiria kupunguza mifugo. Badala ya kuboresha mifugo. Tunataka ng`ombe wa kisasa! Ethiopia ng´ombe wengi ni wakienyeji.

Rais anasema atakusanya kodi kwa kubembeleza, kuchekeana, anasahau enzi za Kikwete kulileta dharau kwa serikali, watu walikwepa kodi hakuna alie fatilia.

Uzuri rais kakiri mwenyewe kuwa serikali ilikuwa katika maongezi na baadhi ya wawekezaji sasa wameanza kugoma. Mie niseme ngoja wagome tu maake mama yeye ndo amedai tuwabembeleze. Namshangaa analalamika. Anadai yeye na Magufuli ni wamoja, sidhani! Yeye amejitangaza kubembeleza kukusanya kodi, aendelee kubembeleza. Tutalipa tu.

Mwisho Rais naona anarudisha wazo la kujenga bandari ya Bagamoyo tena kasema tutake tusitake. Sisi tunataka lakini mkataba upelekwe bungeni ili ujadiliwe na kupitiwa na watanzania tujue.

Nashukuru Rais hajafuata mienendo ya Magufuli bali kachagua mienendo ya Kikwete. Upole kubembeleza, kusamehe, na kuiweka nchi kwa wawekezaji. Safi sana! Wakati wa Kikwete watu tulisema tunataka kiongozi mkali, asie ogopa, na mwenye uthubutu.

Mungu akasikia maombi yetu akatupatia Magufuli. Tukalalamika kwa Mungu Magufuli mkali, haya Mungu katusikia katupatia tena mama wa kubembeleza, pacha kama Kikwete tusije lalamika tena.

Nampenda mama, kama Rais kipenzi ila naona kivuli cha Kikwete ndani. Mama ningetamani ungekuwa na style ya uongozi wako kivyako vyako. Najua Kikwete ni mshauri wako kama ulivyokiri weye mwenyewe. Ungekuja kivyako vyako. Ila ili swala la machimbo kwenye mbuga zetu tafadhali mama lifikirie mara mbili.

Kuwekeza shirika la ndege, ATCL ilishawahi kuwekezwa hata shirika la reli matokeo kila kitu kilikufa, kuwa makini ktk hili. Ethiopia waliambiwa wawekeze shirika lao, waligoma hadi leo linajiendesha vizuri tu.

Hivi hatuna kabisa watanzania ambao ni wataalamu maswala ya anga na usafiri wa ndege wenye kuweza kuboresha shirika letu. Tuwaazime basi waethiopia walau waje kutuelekeza na kutupatia ujuzi. Shirika la ndege la Ethiopia wana miliki chuo cha marubani, chuo cha wahudumu katika ndege, wanachuo cha uongozi na usimamizi wa ndege, wanachuo cha ufundi wa ndege, pia Shirika la ndege linamiliki hotel kubwa ya nyota tano. Mambo yote wanafanya wenyewe. Kwanini sisi watanzania tushindwe, na kuamini wengine wanaweza sisi hatuwezi? Kwanini narudia kwanini?

Kero za watanzania toka nazaliwa hadi leo ni zile zile, wawe wabunge, wanalalamikia mambo yale yale, hivi serikali imeshindwa maliza kero za wananchi. Migogoro ya ardhi , hivi kweli migogoro ya ardhi haiwezi malizwa? Viongozi tumewachoka, hakuna maono, nini kifanyike! tunahitaji sasa viongozi wenye maono mapya, na kutekeleza maono hayo bila kuogopa. Wanao sababisha migogoro ya ardhi ni serikali za mitaa, tunashindwa kweli kuwabana maafisa ardhi? Tunashindwa kupima ardhi yetu?

Tunasikia madawa hakuna, hivi serikali ili linashindikana? Kweli madawa ati yanakosekana? Ati maji hatuna wakati nchi imebarikiwa kwa maziwa, mito na bahari! Dubai ni kukame, lakini wameondoa shida ya maji! sisi tunaviongozi wapo tu! Kuna muda nawaza kuwa hatuhitaji mawaziri? Yaani sioni wafanyacho zaidi kujipendekeza kwa Rais.
Kikwete alitoa hotuba nzuri kwa sababu alikuwa anamaanisha kufanya kile alichokuwa anaongea toka ndani ya roho yake. Hata hivyo, alivyoanza kazi akaja akagundua kuwa anapokuwa anatuambia twende kulia ili tuweze kufanya kile alichotka tukifanye, sisi tunakwenda kushoto, na aanaposema twende kushoto sisi tunageuka tena tunakwenda kulia.

Mama naye pia ameongea akiwa anamaanisha kile alichoongea, toka ndani ya roho yake. Kisipotokea kama alivyoongea, ujue kuwa tatizo lililotokea wakati wa Kikwete limejirudia
 
Hicho kitu kipo kila nchi, hivi unajua hasara ya kukaa bila wananchi wako kuwa na ajila . Unazalisha vibaka, majambazi, mateja, malaya na shuguri nyingine zisizo halali.
Wapi ukiajiri mtu wanakwambia huyo vigezo vyake havifai?
 
Kikwete alitoa hotuba nzuri kwa sababu alikuwa anamaanisha kufanya kile alichokuwa anaongea toka ndani ya roho yake. Hata hivyo, alivyoanza kazi akaja akagundua kuwa anapokuwa anatuambia twende kulia ili tuweze kufanya kile alichotka tukifanye, sisi tunakwenda kushoto, na aanaposema twende kushoto sisi tunageuka tena tunakwenda kulia.

Mama naye pia ameongea akiwa anamaanisha kile alichoongea, toka ndani ya roho yake. Kisipotokea kama alivyoongea, ujue kuwa tatizo lililotokea wakati wa Kikwete limejirudia
Kwa hiyo unamaanisha utawala wa Kikwete wananchi ndo tulikuwa na matatizo? Wananchi ndo walikula rushwa. Wananchi ndo walishindwa kupanga bajeti imara? Wananchi ndo walisababisha huduma mbovu ktk sekta mbalimbali na ofisi za umma? Je wananchi ndo walifanya ufisadi wa EPA na Richmond?
Najiuliza tu unavyosema wananchi tulishindwa kufanya alichotaka tufanye.
 
Yote uliyoandika ni mawazo ya Kimasikini, yaani wewe hutaki Maendeleo

Hutaki kuona Bandari ya Bagamoyo ikijengwa na Tanzania kuchukua nafasi yake kama lango kuu la Africa Mashariki na Kati, huku mamia kwa mamia ya Watanzania wakipata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja. Mji ukikua na uchumi kupanda.

Wewe hutaki vibali vya kazi vitolewe ili tupate wataalamu wakati na sisi tunajitahidi kutengeneza skills za maana badala ya degree za ukarani tunazotoa. Mfano mtu anaanzisha kiwanda cha kurefine mafuta hapa analeta Bleacher hakuna mtu wa kuiendesha Tanzania kwanini anyimwe kule Muhindi hata kama hajasoma?
Nadhani umekurupuka. Wapi nimesema sitaki bandari ya Bagamoyo ijengwe. Tulia soma uelewe. Nimesema hakuna anae kataa Bandari kujengwa. Kikubwa mkataba wa ujenzi uwekwe wazi hata upelekwe bungeni.
Wewe ndo unamawazo ya kimasikini na haujui dunia inaendaje. Kokote kule ulimwenguni nchi ujali wataalamu wake kwanza. Unawekeza kwa wazawa. Tanzania inawataalamu kila aina.Hata hayo mafuta unayosema kurefine wataalam tunao. Ukikoswa ndo unatafuta wataalamu nje. Hapo nimeongelea vibali kutotolewa ovyo.
Uwe unasoma mada unaelewa usikurupuke kujibu tu bila kuwa na tafakuri ya kina.
 
Wakati Mhe. Rais kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alitoa hotuba safi sana, ambayo kweli tulikuwa na matumaini ya kuwa na Tanzania mpya, na yenye maendeleo ya kasi. Aliongelea mambo mengi ikiwepo uwekezaji, na kujali wawekezaji, kweli milango ilifunguliwa tulipata wawekezaji wa kila namna hata kule kariakoo walijaa wakiuza karanga na ufuta. Wawekezaji walipata sauti na kuwa wasemaji wa mwisho kwani hatukutaka kuwaudhi bali kuwabembeleza na kujikomba kwao.

Vibali vya kazi vilitolewa kama njugu, ili kuwafanya wawekezaji kuwa na wafanyakazi wenye vigezo wanayotaka wao. Tuliona makampuni ya uwekezaji yakiwa na maafisa wote wa juu kutoka nje ya nchi, huku watanzania wakiishia kuwa vibarua na kufukuzwa kazi muda wowote. Huku wakilipwa mishahara ya chini kabisa.

Leo rais wetu kasisitiza kuwa vibali vya kazi vitolewe haraka, bila usumbufu, na pia milango ifunguliwe kwa wewekezaji. Najiuliza tu, hivi nchi kama China, India, Singapore, na hapa africa kuna Ethiopia uchumi wake unakuwa kwa kasi zinategemea wawekezaji kutoka nje pekee? Kama ingekuwa hivyo kwa Kikwete tulijaza wawekezaji, ni nini Taifa lilipata au kufaidika?

Kwanini tusiimarishe uwekezaji wa ndani, ambao serikali iwawezeshe wazawa kuwekeza na si kudhani tutaendelea kwa huu uwekezaji kutoka nje pekee. Sipingi wawekezaji wa nje lakini nawasiwasi kulingana na historia hapo nyuma. Wawepo ila serikali isiwekwe mfukoni, na si vizuri kutoa vibali vya kazi kama njugu.

Mhe. Rais kaongelea Kuboresha ufugaji kwa kuwa na ufugaji wa kisasa, na kupunguza mifugo. Sawa na Rais kikwete wakati huo alitamba na hii hoja na kudai mifugo inakoda na mchungaji anakonda. Akadai kuondoa tatizo katika serikali yake. Sikuwahi kuona jitihada zozote zilizofanyika, mpaka anaondoka madarakani.

Hii leo rais wetu nae anakuja na mapambio yale yale ufugaji wa kisasa, kupunguza mifugo. Hapa katika kupunguza mifungo sioni kama ni hoja. Mungu katupatia mifugo, ni nchi ya pili kwa mifugo Afrika baada ya Ethiopia. Mbona Ethiopia hawana hoja ya kupunguza mifugo, ila wao wanaviwanda vikubwa na vidogo vya ngozi, wanatengeneza viatu, mabegi, mikanda nk. wanasoko la ndani na nje ya nchi tena kubwa sana.

Sisi tunafikiria kupunguza mifugo. Badala ya kuboresha mifugo. Tunataka ng`ombe wa kisasa! Ethiopia ng´ombe wengi ni wakienyeji.

Rais anasema atakusanya kodi kwa kubembeleza, kuchekeana, anasahau enzi za Kikwete kulileta dharau kwa serikali, watu walikwepa kodi hakuna alie fatilia.

Uzuri rais kakiri mwenyewe kuwa serikali ilikuwa katika maongezi na baadhi ya wawekezaji sasa wameanza kugoma. Mie niseme ngoja wagome tu maake mama yeye ndo amedai tuwabembeleze. Namshangaa analalamika. Anadai yeye na Magufuli ni wamoja, sidhani! Yeye amejitangaza kubembeleza kukusanya kodi, aendelee kubembeleza. Tutalipa tu.

Mwisho Rais naona anarudisha wazo la kujenga bandari ya Bagamoyo tena kasema tutake tusitake. Sisi tunataka lakini mkataba upelekwe bungeni ili ujadiliwe na kupitiwa na watanzania tujue.

Nashukuru Rais hajafuata mienendo ya Magufuli bali kachagua mienendo ya Kikwete. Upole kubembeleza, kusamehe, na kuiweka nchi kwa wawekezaji. Safi sana! Wakati wa Kikwete watu tulisema tunataka kiongozi mkali, asie ogopa, na mwenye uthubutu.

Mungu akasikia maombi yetu akatupatia Magufuli. Tukalalamika kwa Mungu Magufuli mkali, haya Mungu katusikia katupatia tena mama wa kubembeleza, pacha kama Kikwete tusije lalamika tena.

Nampenda mama, kama Rais kipenzi ila naona kivuli cha Kikwete ndani. Mama ningetamani ungekuwa na style ya uongozi wako kivyako vyako. Najua Kikwete ni mshauri wako kama ulivyokiri weye mwenyewe. Ungekuja kivyako vyako. Ila ili swala la machimbo kwenye mbuga zetu tafadhali mama lifikirie mara mbili.

Kuwekeza shirika la ndege, ATCL ilishawahi kuwekezwa hata shirika la reli matokeo kila kitu kilikufa, kuwa makini ktk hili. Ethiopia waliambiwa wawekeze shirika lao, waligoma hadi leo linajiendesha vizuri tu.

Hivi hatuna kabisa watanzania ambao ni wataalamu maswala ya anga na usafiri wa ndege wenye kuweza kuboresha shirika letu. Tuwaazime basi waethiopia walau waje kutuelekeza na kutupatia ujuzi. Shirika la ndege la Ethiopia wana miliki chuo cha marubani, chuo cha wahudumu katika ndege, wanachuo cha uongozi na usimamizi wa ndege, wanachuo cha ufundi wa ndege, pia Shirika la ndege linamiliki hotel kubwa ya nyota tano. Mambo yote wanafanya wenyewe. Kwanini sisi watanzania tushindwe, na kuamini wengine wanaweza sisi hatuwezi? Kwanini narudia kwanini?

Kero za watanzania toka nazaliwa hadi leo ni zile zile, wawe wabunge, wanalalamikia mambo yale yale, hivi serikali imeshindwa maliza kero za wananchi. Migogoro ya ardhi , hivi kweli migogoro ya ardhi haiwezi malizwa? Viongozi tumewachoka, hakuna maono, nini kifanyike! tunahitaji sasa viongozi wenye maono mapya, na kutekeleza maono hayo bila kuogopa. Wanao sababisha migogoro ya ardhi ni serikali za mitaa, tunashindwa kweli kuwabana maafisa ardhi? Tunashindwa kupima ardhi yetu?

Tunasikia madawa hakuna, hivi serikali ili linashindikana? Kweli madawa ati yanakosekana? Ati maji hatuna wakati nchi imebarikiwa kwa maziwa, mito na bahari! Dubai ni kukame, lakini wameondoa shida ya maji! sisi tunaviongozi wapo tu! Kuna muda nawaza kuwa hatuhitaji mawaziri? Yaani sioni wafanyacho zaidi kujipendekeza kwa Rais.
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maono na maarifa!
Uko na familia unalialia kila kukicha kwa jilani akufanyie mambo yako kwa kujiona huwezi huu nao ni ujuha! Ndio maana nitaendelea kumpenda na kumkumbuka Magufuli wetu! Tz na watz kwanza, wengine baadaye! Nchi inajengwa na wenyewe wenye moyo wa kujitoa hata uhai wao!
Hii 'dependency syndrome' haipo sawa kabisa! Kutegemea mjomba eeh🙊!
Uwekezaji wowote Yz lazima uwe na tija, utoe ajira 'decent' zenye staha siyo za kikoloni za kufagia tuuúuuuuu😡! Unakuwa na kampuni la nje ambalo halina mtz hata mmoja ktk safu ya uongozi na utoaji maamuzi, mwishowe mnaishia kudanganywa tu kwa kinachoendelea 😭! Kodi inabembelezwa🤣😂🤣😂🤣!
 
Yote uliyoandika ni mawazo ya Kimasikini, yaani wewe hutaki Maendeleo

Hutaki kuona Bandari ya Bagamoyo ikijengwa na Tanzania kuchukua nafasi yake kama lango kuu la Africa Mashariki na Kati, huku mamia kwa mamia ya Watanzania wakipata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja. Mji ukikua na uchumi kupanda.

Wewe hutaki vibali vya kazi vitolewe ili tupate wataalamu wakati na sisi tunajitahidi kutengeneza skills za maana badala ya degree za ukarani tunazotoa. Mfano mtu anaanzisha kiwanda cha kurefine mafuta hapa analeta Bleacher hakuna mtu wa kuiendesha Tanzania kwanini anyimwe kule Muhindi hata kama hajasoma?
Sijui ni utapiamlo wa akili au nini 🤔 kinachokutatiza I see!
Hebu msome vizuri mleta uzi kwanza kabla ya kujibu kwa kukurupuka i see!
 
5.Ukwepaji kodi bado tatizo sugu. (Nakubaliana nawe).

Kwa maoni yako unadhani ni nini chanzo au sababu ya ukwepaji kodi hadi kufanya uwe sugu?

Nini kifanyike ili watu walipe kodi kwa hiari au wajisikie au waelewe kulipa kodi ni wajibu wa kila mwananchi?
Hakuna nchi duniani watu wanalipa kodi kwa hiari. Bali nchi zilizoendelea kuna mifumo ya malipo (electronic) inalolazimisha mtu kulipa kodi bila kugombana naye. Wewe unajua ni kwa nini mpaka leo miamala mingi zaidi hufanyika kwa cash? Siku serikali ikiacha uvivu na akili ndogo tutapata suluhu ya kodi. Ila kutaka kuwabembeleza ni kichekesho. Tutaanza kucheka muda si mrefu.
 
Kwenye suala la Kazi mkuu Hongera kama wewe ni mchapa Kazi, ila UKWELI ni kwamba asilimia kubwa ya Watanzania ni wavivu kupindukia kuanzia wa chini mpaka mabosi wao, unaenda ofisini kwa mtu anakukalisha masaa manne Kazi ambayo angeifanya dakika 15,mimi ni HR, katika kampuni ambazo nimewahi kuajiri wageni hakuna hata mgeni mmoja aliwahi kuharibu Kazi, nilijaribu kuwatafutia makosa wale walikuwa wananyanyasa wabongo, walifukuzwa tuu kwa sababu mimi nlikuwa naaminika lakini hawakuwa wameshindwa Kazi. Wabongo seriousness ni zero alaf tunapoteza muda kwenye mambo ya kijinga hospitali manesi wa zamu usiku wanakesha wanachati,tusipobadilika wageni watakuja kuwa hata waosha vyoo sisi tukiwa tunalalamika.
 
Kwa hiyo unamaanisha utawala wa Kikwete wananchi ndo tulikuwa na matatizo? Wananchi ndo walikula rushwa. Wananchi ndo walishindwa kupanga bajeti imara? Wananchi ndo walisababisha huduma mbovu ktk sekta mbalimbali na ofisi za umma? Je wananchi ndo walifanya ufisadi wa EPA na Richmond?
Najiuliza tu unavyosema wananchi tulishindwa kufanya alichotaka tufanye.
Mzee wa msoga na masalia yake akili ndogo sana kuongoza nchi. Mpaka leo sijui ni kwa nini Bro Magu alipeleka majina mawili kamati kuu 2015. Angepeleka la Mwinyi peke yake huenda leo hii nchi isingeshikwa tena na haya majangili.

Kwa kifupi mleta mada alizisikia vema hotuba za JK 2005. Hotuba ya huyu bi mkubwa ilipofika nusu saa tu kuna mtu nilimwambia kuwa ile hotuba iliandaliwa na watu wale wale walioandaa ya bosi wake 2005.

Sijajadili content kwa kuwa mleta mada ni kama kaudukua ubongo wangu. Bandiko lake litasimama kwa miaka yote ya utawala huu akili ndogo.
 
Kwenye suala la Kazi mkuu Hongera kama wewe ni mchapa Kazi, ila UKWELI ni kwamba asilimia kubwa ya Watanzania ni wavivu kupindukia kuanzia wa chini mpaka mabosi wao, unaenda ofisini kwa mtu anakukalisha masaa manne Kazi ambayo angeifanya dakika 15,mimi ni HR, katika kampuni ambazo nimewahi kuajiri wageni hakuna hata mgeni mmoja aliwahi kuharibu Kazi, nilijaribu kuwatafutia makosa wale walikuwa wananyanyasa wabongo, walifukuzwa tuu kwa sababu mimi nlikuwa naaminika lakini hawakuwa wameshindwa Kazi. Wabongo seriousness ni zero alaf tunapoteza muda kwenye mambo ya kijinga hospitali manesi wa zamu usiku wanakesha wanachati,tusipobadilika wageni watakuja kuwa hata waosha vyoo sisi tukiwa tunalalamika.
Sasa hapo ukiwa mzalendo suluhu siyo tu kuendelea kuajiri hao wageni. Bali suluhu ni kuleta hiyo nidhamu kazini. Ndiyo sababu Magufuli alikazania hicho kitu.

Baba mwenye akili hawezi tu kulemaa eti "shambani kwangu siwapeleki wanangu kulima, wavivu sana wale; nawatumia wa jirani yangu ndiyo wachapakazi!".

Lazima serikali itatue matatizo yetu ya msingi ili tuajirike badala ya kuwatukuza hao wageni. Rais wenu alidai kuwa kwenye miradi wataalam wa kibongo hawawezi kukuelezea kitu kikaeleweka. Binafsi najua hilo hajalitoa field bali ni mtazamo wake tu wa kitumwa.

Wataalam tunao. Tuwekeze kwa Watanzania. Tuwajengee uwezo zaidi. Tujenge pia mifumo imara ya kuwa-check. Tulikwisha anza vema ila sasa tunarudi nyuma.
 
Hakuna nchi duniani watu wanalipa kodi kwa hiari. Bali nchi zilizoendelea kuna mifumo ya malipo (electronic) inalolazimisha mtu kulipa kodi bila kugombana naye. Wewe unajua ni kwa nini mpaka leo miamala mingi zaidi hufanyika kwa cash? Siku serikali ikiacha uvivu na akili ndogo tutapata suluhu ya kodi. Ila kutaka kuwabembeleza ni kichekesho. Tutaanza kucheka muda si mrefu.
Naheshimu maoni yako.
Kwa bahati nzuri,sikufahamu na hunifahamu pia.Unapoongelea nchi zilizoendelea inakuwa kama wajisemea kwamba wewe pekee ndiye wazifahamu nchi zilizoendelea? Ungenifahamu,hii isingekuwa hoja,ungejikita kwenye hoja tu.Itoshe kusema kwamba ninapoongelea hiari katika kulipa kodi ninamaanisha kujua umuhimu wa kulipa kodi kwa ajili ya kuchochea maendeleo kuanzia mtu binafsi hadi taifa kwa ujumla wake.
 
Mimi ni mmoja wa watu waliomuunga mkono JPM kwa mambo mengi tu aliyokuwa akiyafanya kwa mustakabali wa Taifa hili.

Lakini hili suala la kuwanyanyasa wafanyabiashara kama sio raia wenye haki na nchi hii ni kosa kubwa sana lililoutia doa muda wote aliokuwa rais wetu.

Kuna unyama mkubwa wamefanyiwa wafanyabiashara. Rais Samia anayo haki kubadilisha mentality ya ukusanyaji wa kodi. Ukimtesa mtu anayo haki ya kukimbia na kwenda kwingine ambapo biashara yake inaheshimiwa.

Kunyanyasa wafanyabiashara kunaenda sambamba na kutovithamini vipaji vya kitanzania. Mohamed Dewji alitekwa na watu ambao mpaka leo hawajulikani lakini Rais wa Afrika ya Kusini amemteua kama mmoja wa washauri wake wa masuala ya uwekezaji.

Na tunao wengi tu wa aina ya Mo Dewji, wazalendo wenye vipaji vya kila aina lakini mwisho wa siku wananyanyaswa na kunyanyapaliwa mpaka wanakatishwa tamaa ya kuutumia uwezo wao kwa faida ya jamii nzima.

Mojawapo ya kanuni za TANU inasema nitautumia uwezo wangu kwa faida ya wote, ukikutana na kukatishwa tamaa au kunyanyaswa huwezi kuutumia uwezo huo kwa faida ya mtu yoyote yule.

Mama Samia anayo haki ya kuja na mtazamo wa kiungwana kwa wafanyabiashara, Huwezi kumtesa Bakhresa ukafikiri unamkomoa, utaishia kuwaumiza wafanyakazi wake maelfu na familia zao.
 
Naheshimu maoni yako.
Kwa bahati nzuri,sikufahamu na hunifahamu pia.Unapoongelea nchi zilizoendelea inakuwa kama wajisemea kwamba wewe pekee ndiye wazifahamu nchi zilizoendelea? Ungenifahamu,hii isingekuwa hoja,ungejikita kwenye hoja tu.Itoshe kusema kwamba ninapoongelea hiari katika kulipa kodi ninamaanisha kujua umuhimu wa kulipa kodi kwa ajili ya kuchochea maendeleo kuanzia mtu binafsi hadi taifa kwa ujumla wake.
Kama unafanya utafiti lazima ufanye mapitio ya machapisho. Naongelea kitu nacho kifahamu. Na hakuna sehemu nimesema ni mimi tu nae jua hzo nchi. Sijaandika kushindana na mtu.
Kikubwa nimetoa mifano ninayo ifahamu. Hata hivyo nimeizunguka dunia hivyo niliyojifunza na share na yeyote. Kila mtu ana haki kuongea au kutoa uzoefu alonao. Mlinganisho na nchi nyingine ni jambo la kawaida. Ndo maana usafiri wa BRT nchi kadhaa zilikuja kujifunza Tanzania uendeshaji wake. Na vivyo hivyo Watanzania tutajifunza kutoka nchi zingine.
 
Kama unafanya utafiti lazima ufanye mapitio ya machapisho. Naongelea kitu nacho kifahamu. Na hakuna sehemu nimesema ni mimi tu nae jua hzo nchi. Sijaandika kushindana na mtu.
Kikubwa nimetoa mifano ninayo ifahamu. Hata hivyo nimeizunguka dunia hivyo niliyojifunza na share na yeyote. Kila mtu ana haki kuongea au kutoa uzoefu alonao. Mlinganisho na nchi nyingine ni jambo la kawaida. Ndo maana usafiri wa BRT nchi kadhaa zilikuja kujifunza Tanzania uendeshaji wake. Na vivyo hivyo Watanzania tutajifunza kutoka nchi zingine.
Naheshimu mawazo yako.

Wakati huo huo: Mimi pia mbali na kuizunguka dunia,nimeishi muda mrefu "kwa mabepari" tena katika nchi tofauti.Ni mtafiti pia kwa "nature" ya kazi yangu...
 
Back
Top Bottom