Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Leo Rais samia Amekata kiu ya watanzania na kulituliza Taifa ambapo muda mwingi walikuwa wanataka kusikia kauli yake juu ya changamoto ya kukatika kwa umeme. Kwa utulivu ,upole,uthabiti na uimara wa hali ya juu sana amelieleza Taifa sababu ya chagamoto hiyo na mikakati ya serikali yake kuimaliza. Ameliambia Taifa kuwa hali hiyo imetokana na serikali kufanya ukarabati na matengenezo ya mitambo ambayo ilikuwa haijafanyiwa matengenezo kwa muda mrefu. Hivyo serikali inalazimika kuzima mingine na kuwasha mingine ambayo inakuwa haitoshelezi umeme unaohitajika.
Lakini pia Amelieleza Taifa kuwa mabadiliko ya hali ya hewa yameathiri uzalishaji wa umeme kutokana na nchi kukumbwa na ukame kwa baadhi ya maeneo na hivyo maji yanayohitajika katika mabwawa yetu kuwa pungufu.Hata hivyo ameelezea jitihada za serikali yake kumaliza changamoto hiyo ambayo itabakia historia katika Taifa letu baada ya miezi sita tu. Ambapo kwa sasa serikali inajitahidi kuongeza na kutumia vyanzo vingine vya umeme kama vile umeme wa gas na jua.
Naamini watanzania wenzangu sote ni mashahidi wa namna jua linavyowaka kwa kipindi hiki na namna maeneo mengi yanavyoendelea kuwa kame na kukauka maji .sote tunakubaliana na ukweli kuwa hata shughuli za uchumi zinazotegemea umeme zimeongezeka kwa kiasi kikubwa sana kutokana na kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi wetu, unaotokana mazingira mazuri na sera nzuri za serikali yetu katika kuchochea ukuaji wa uchumi na Biashara.
Tuendelee kuwa wavumilivu katika miezi hiyo sita ambayo mh Rais na serikali yake wanaendelea kupambana kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme nchini ,lakini pia Tuendelee kumuomba Mungu atuletee mapema mvua zenye baraka zisizo na madhara zitakazo jaza mabwawa yetu.lakini pia tukumbuke pia mwakani bwawa la mwalimu Nyerere litaanza nalo uzalishaji wa umeme na hivyo kufanya Taifa kuwa na umeme wa kutosha na mwingine kuuza nje ya nchi kama vile kenya na nchi nyingine zenye uhitaji wa umeme.
Rais samia ni kiongozi mkweli sana ,Ni kiongozi ambaye anaendana na Baba wa Taifa Hayati mwalimu Nyerere ambaye alikuwa haoni haya kuusema ukweli kutwambia watanzania,kama ambavyo amewahi kutuambia kuwa Tufunge Mikanda. Huo ndio uongozi na huo ndio uungwana .Rais samia Hataki kuendesha serikali kwa udanganyifu na ulaghai wakati anajuwa mwisho wa siku ukweli hujitenga na uongo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Leo Rais samia Amekata kiu ya watanzania na kulituliza Taifa ambapo muda mwingi walikuwa wanataka kusikia kauli yake juu ya changamoto ya kukatika kwa umeme. Kwa utulivu ,upole,uthabiti na uimara wa hali ya juu sana amelieleza Taifa sababu ya chagamoto hiyo na mikakati ya serikali yake kuimaliza. Ameliambia Taifa kuwa hali hiyo imetokana na serikali kufanya ukarabati na matengenezo ya mitambo ambayo ilikuwa haijafanyiwa matengenezo kwa muda mrefu. Hivyo serikali inalazimika kuzima mingine na kuwasha mingine ambayo inakuwa haitoshelezi umeme unaohitajika.
Lakini pia Amelieleza Taifa kuwa mabadiliko ya hali ya hewa yameathiri uzalishaji wa umeme kutokana na nchi kukumbwa na ukame kwa baadhi ya maeneo na hivyo maji yanayohitajika katika mabwawa yetu kuwa pungufu.Hata hivyo ameelezea jitihada za serikali yake kumaliza changamoto hiyo ambayo itabakia historia katika Taifa letu baada ya miezi sita tu. Ambapo kwa sasa serikali inajitahidi kuongeza na kutumia vyanzo vingine vya umeme kama vile umeme wa gas na jua.
Naamini watanzania wenzangu sote ni mashahidi wa namna jua linavyowaka kwa kipindi hiki na namna maeneo mengi yanavyoendelea kuwa kame na kukauka maji .sote tunakubaliana na ukweli kuwa hata shughuli za uchumi zinazotegemea umeme zimeongezeka kwa kiasi kikubwa sana kutokana na kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi wetu, unaotokana mazingira mazuri na sera nzuri za serikali yetu katika kuchochea ukuaji wa uchumi na Biashara.
Tuendelee kuwa wavumilivu katika miezi hiyo sita ambayo mh Rais na serikali yake wanaendelea kupambana kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme nchini ,lakini pia Tuendelee kumuomba Mungu atuletee mapema mvua zenye baraka zisizo na madhara zitakazo jaza mabwawa yetu.lakini pia tukumbuke pia mwakani bwawa la mwalimu Nyerere litaanza nalo uzalishaji wa umeme na hivyo kufanya Taifa kuwa na umeme wa kutosha na mwingine kuuza nje ya nchi kama vile kenya na nchi nyingine zenye uhitaji wa umeme.
Rais samia ni kiongozi mkweli sana ,Ni kiongozi ambaye anaendana na Baba wa Taifa Hayati mwalimu Nyerere ambaye alikuwa haoni haya kuusema ukweli kutwambia watanzania,kama ambavyo amewahi kutuambia kuwa Tufunge Mikanda. Huo ndio uongozi na huo ndio uungwana .Rais samia Hataki kuendesha serikali kwa udanganyifu na ulaghai wakati anajuwa mwisho wa siku ukweli hujitenga na uongo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.