Uchaguzi 2020 Hotuba ya Tundu Lissu kutangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Juni 08, 2020

Barrick nimeitolea kama mfano tu,lakini hapa Tanzania kuna kampuni nyingi tu za nje ambazo zimewekeza na kusema FDR imeshuka sio kweli.
Kama haki za binadamu zinakiukwa sidhani kama Usaid wangekuwa wanatoa misaada. Tukio la Lissu kushambuliwa isiwe sababu ya kusema haki za binadamu zinavunjwa.
Tungekuwa tunaona watu wanapigwa risasi kama mbwa mabarabarani na polisi hapo tungesema kuna tatizo. Ndio maana watu hawamchagui mtu kwa kumhurumia bali kwa uchapa kazi wake na uzalendo.
 
-hauna taarifa za kutosha FDI imeshuka kwenye nchi yetu
-haki ya kuishi imeelezwa kwenye katiba na sio lazima wauawe wengi kiasi gani,
- kingine yule ni mbunge na alikuwa ametoka bungeni hivyo kunaleta wasiwasi was kwa nini mbunge apigwe risasi kwenye eneo lenye CCTV na ulinzi juu hivyo hilo peke yake linaleta mashaka makubwa
-kingine kwa nini CCTV camera zilitolewa lile eneo? Kwa nn watoe? Nalo hilo linaleta shaka zaidi juu ya shambulizi la lissu kwa nn watoe CCTV
-kutokufanyika uchunguzi hadi Leo au kama kuna uchunguzi wowote leteni ripoti tuisome tujuwe
- kwa nini mbunge anapigwa risasi hakufanyiki uchunguzi? Sasa kama ni mbunge anapigwa risasi na hakuna uchunguzi unaofanyika vipi kuhusu RAIA wa kawaida?
- kura za huruma zinaweza zikapigwa tu kutokana na 'matashi ya MTU'
-kuhusu uzalendo tundu lissu ni mzalendo mzuri tu
 
Rudi home bro Mungu ana jambo na ww...kupona kwenye risasi zaidi ya 30 kuna maana iliyojificha
 
Nafikiri usibadili mada iliyopo mezani. Kuwa JPM amefnya maajabu wiki mbili bado mwaka wa fedha kuisha lakini anato pesa za kujenga hospital.Kitu ambacho ni nadra kwa nchi za Africa,hata hapa Tanzania tulikuwa hatujazoea kuona hii kitu.
Suala la Tundu Lissu waachie vyombo vya dola. Kama kungekuwa na uminywaji wa haki ya kuishi kwa watanzania ungesikia UN human rights council imetuma wachunguzi. Acha kukaririshwa.
Hoja hapa ni mwendo mdundo kwa maendeleo ya Tanzania. Hata kama bajeti inasomwa pesa zinatolewa kuleta maendeleo.
 
-hatuwezi kuachia vyombo vya usalama kwa sababu jambo hilo linagusa maisha ya watu/mtu hivyo sisi wananchi tunapaswa kujuwa
-kafanya hayo unayoyaita maajabu lakini huku mtaani maisha ni magumu,hakuna ajira,watumishi waa umma wamekaa miaka mitano bila ya nyongeza ya mshahara,Uhuru wa kujieleza na vyombo vya habari umeshuka sana,ukuaji wa uchumi unasuasua,kuzorota kwa Uhuru wa mahakama,haki za binadamu
-kuna uminywaji wa haki ya kuishi ndiyo maana US wamempiga marufuku RC WA DAR asiingie marekani kutokana na hizo tuhuma
-utekelezaji wa bajeti uko chini sana fuatilia hansad za bunge utaona jinsi utekelezaji wa bajeti ulivyokuwa chini
 
Kama huwezi kuachia vyombo vya usalama, sasa mbona hujachukua hatua yoyote?
Bajeti inatekelezwa 93% unasema ipo chini. Au wewe upo Usa?
Kwani Rc wa Dar akizuiwa kwenda Us ndio Tanzania kuna uminywaji wa haki za raia? Huko Usa mbona kila siku watu wanauliwa na polisi?
Wanajeshi wa Usa wanafanya mauaji Afhghanistan mbona hulalamiki?
Kama Tanzania kuna ukandamizaji wa haki za raia. Ungesikia UN wanalalamika tumia akili.
 
Nani mwenye uwezo wa kurekebisha hayo iwapo wewe na mimi kutwa tunalaumu na kulalamika wakati hatutimizi wajibu wetu na hatuheshimu mipaka ya uhuru wetu?

Ni rahisi kunyoosha kidole kimoja wakati vilivyobaki vinakusuta. Kwa mfano, hakuna chama chochote cha upinzani kimeonesha rekodi nzuri na mfano wa kuigwa kiungonzi na maendeleo. Kila kukicha tunasikia na kushuhudia migogoro. Chama Kikuu cha Upinzani, kiongozi wake mkuu anatuhumiwa matumizi mabaya ya chama, uongozi dhaifu, udharilishaji wa jinsi ya kike nk. Lakini ni hao hao viongozi ambao wako msitari wa mbele kuilaumu Setikali, jana kwamba wenyewe ni bora!
 
Wamekaririshwa hao. Jahazi lao linazama bado wanajitutumua huku viongozi wao wakitapatapa kama wafa maji.

Badala ya kuwauliza viongozi wao Sera za maendeleo wamebaki kushangilia agenda za viongozi wao zisizo na maslahi mapana ya kimaendeleo.
 
-serikali ina nafasi kubwa kwa sababu yenyewe ndiyo inapeleka bajeti bungeni,yenyewe ndiyo inapeleka sheria mbalimbali bungeni,yenyewe ndiyo yenye vyombo vya dola
-wapinzani wameonyesha dira nzuri tu kwa kuishauri serikali vizuri bungeni mfano kwenye sakata la korosha (sheria ya cashew nut industry) kuhusu export levy,wapinzani wameishauri serikali kuhusu hali ya uchumi kwenye kipindi cha korona na hadi kushauri kuletwa bajeti/mpango wa serikali kwenye korona kiuchumi,no
-sio kweli kama chadema na hizo ni tuhuma zinazoundwa kumchafua mbowe kwa sababu mmemtafuta sana mfano mmebomoa bilicanas,mmemuharibia shamba lake Kule hai lakini bado yuko imara, kingine ripoti ya CAG imetoa hati safi kwa chadema maana yake ni kwamba mbowe anazingatia sheria na katiba za chama kwenye matumizi ya fedha
-sio kweli kwamba Mbowe ni dhaifu ni imara kwa sababu ameweza kukifanya chama kuwa chama kikuu cha upinzani yaani ameongeza Wabunge,madiwani,halmashauri
-Hao waliodhalilishwa ni waongo wanataka kumchafua mbowe baada ya mbinu zote za kumchafua kushindikana na kama walidhalilishwa walipaswa wao kuthibitisha sio mbowe hivyo waende takukuru wakashitaki rushwa ya ngono.
 
-hatua ambazo sisi wananchi tunapaswa kuchukua ni kuhoji na wala sio kufanya fujo tunahoji ili tupewe taarifa
-Bajeti haitekelezwi kwa 93% taja ni mwaka gani/miaka gani ndani ya awamu hii bajeti ilitekelezwa kwa 93% kama sio uongo, wizara ngapi?
-RC kuzuiwa kuingia USA, nenda kasome vizuri ile taarifa ya US walitoa sababu zinazohusu kukikukwa kwa haki ya kuishi hivyo ni kwamba kuna ukikukwaji wa haki za binadamu
-kuhusu USA kufanya mauaji jibu ni kwamba huwezi kusema wewe ni msafi kwa kuwa na mwenzako anafanya mambo yanayofanana na yako Yale mabaya, hata ukiona USA watu wanauawa unaona watu wanaruhusiwa kujieleza kabisa, wanaandamana kupinga uonevu je Tanzania watu wanahiyi haki? Ikiwa mikutano ya vyama vya siasa hamuitaki maandamano mtaruhusu?
- sio lazima UN waseme Luna taasisi kibao ikiwamo human rights watch,EU,US hao nao wanayasemea yanayohusu haki za binadamu
 
Kamanda uliyekariri.
 

Wimbo wewe na wenye mawazo kama yako hayo, ni ule ule mmekaririshwa, kwamba:

√ Serikali inakusanya kodi - kwani kuna Serikali duniani isiyo kusanya kodi? Fedha iliyojenga na kuboresha miundo mbinu na huduma za jamii kama siyo matumizi mazuri ya hiyo kodi ni nini? Mwrnye macho haambiwi tazama;

√ Dira nzuri inaoneshwa na upinzani. Kuna jipya kutoka upinzani zaidi ya kupinga kila kitu kwa lugha ya mitaani. Korosho, korosho, korosho umekuwa wimbo wa viongozi wa upinzani wakati kuna ushahidi wakulima kwa kipato walichopata mwaka uliopita wa mavuno baadhi yao walimwagilia bia miti yao ya korosho!

√ Mbowe anatafutwa. Atafutwe na nani wakati kauli na matendo yake ndiyo yamemfikisha kutuhumiwa, kufunguliwa mashtaka na hatimaye kutiwa hatiani. Iwapo mashtaka yalikuwa ya uonezmvu au wivu tu, kama amekata rufaa tusubiri matokeo. Lakini jiulize mbona mwenyewe hajatoka hadharani kukanusha tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za chama, unyanyasaji na ulevi wa kupindukia hadi kuteguka kisigino? Kwa nini wewe unamtetea bila ushahidi ila ushabiki tu? Mbowe ni mtu mzima HOVYO;

√ Ni kweli Mbowe siyo dhaifu ndani ya CHAMA CHAKE kwa sababu yeye ndiye mwamuzi wa mwisho wa kila jambo. Hilo la kuamuru wabunge wajifungie majumbani mwao ati kuepuka kuambukizwa korona na baadaye kurejea tena kuungana na wagonjwa walewale, limethibitisha busara na maamuzi ya KIJINGA;

√ TAKURURU imeanza uchunguzi wa tuhuma dhidi yake Mbowe, hivyo tusubiri matokeo.
 
-korosho mmeliharibu zao like mmechukua export levy,ambayo ilikuwa inatumika kuboresga zao la korosho
- - siyo miundombinu yote imejengwa na kodi zetu,nyingine imejengwa kwa mikopo
-zao la korosho mmeliharibu kwa kuchukua export levy ambayo ilikuwa inatumika kuboresha zao
- mnawabambikizia kesi halafu mnawatia hatiani refer the case of akwilina yule aliyempiga risasi ametolewa kwa mole prosequi halafu eti kina mbowe ambao hawajapiga risasi wametiwa hatiani inaingia akilini?
-juhusu matumizi mabaya ya fedha ripoti ya CAG ya 2018/19 imetoa hati safi tafsiri yake ni kwamba mahesabu yako clear hakuna ufisadi
-hakuna aliyenyanyaswa kingono hao ni waongo na ni tuhuma za kupika waende takukuru basi halafu watoe maelezo kwamba walinyanyaswa vipi kingono? Ilikuwaje ?
-Mbowe hakuwa amelewa huo ni uongo kuthibitisha hilo mbona hawataki kuzungumzia footage za CCTV camera? Kwa nini wameruka ushahidi wa kielektroniki ambao unakubalika mahakamani kwa mujibu wa sheria ya ushahidi, kwa nini wategemee ushahidi wa kuambiwa (hear say) wakati footage zipo? Kwa nn wasingechukua ushahidi wa footage halafu waCorroborate na ushahidi wa kuambiwa kuona kama vinamatch?
-mbowe siyo mwamuzi wa mwisho chama kinaendeshwa kwa vikao na maamuzi yanaendeshwa na vikao ndiyo maana unaona kikao cha kamati kuu kinakutana halafu baadae unasikia 'Resolution' za kamati kuu maana yake hayo ni maamuzi ya kamati kuu siyo ya mtu mmoja, pia kuna baraza kuu, kuhusu korona lazima ujue kila mtu analinda usalama wake kujitenga ilikuwa sawa kwa sababu kwa hali ilivyokuwa ilikuwa ni sawa kujitenga ili kujilinda kwa sababu ukiupata mateso utayapata wewe binafsi hautapata mateso hayo na ndugu zako nk
-kuhusu takukuru kinachofanyika ni kutumia muda vibaya tu kwa sababu ripoti ya CAG iko wazi kuhusu usafi wa chama kifedha, katiba iko wazi kuhusu makato hayo ya wanachama
-
-
 

Fahamu wazi kuwa tuhuma juu ya Viongozi wa CHADEMA, hasa Mbowe, zitatumika kwenye kampeni kukibomoa chama. Wananchi sasa wanataka viongozi wasio na makandokando. Kama mnavyofanya humu JF, wagombea watatumia muda wao mwingi wa kampeni kujibu tuhuma.

Nitakuona mtu makini kama utatumia muda, na wenzako, humu JF na mitandao ya kijamii, kujadili Sera mbadala za maendeleo ili kuondokana na hayo mapungufu ya Serikali yanayo orodhesha badala ya kung'ng'ania kutetea viongozi wenu pasipo ushahidi.
 
-Kama ni kukibomoa chama mmeshashindwa
-wewe unayetuhumu una ushahidi?
 
-Kama ni kukibomoa chama mmeshashindwa
-wewe unayetuhumu una ushahidi?
Kulalamika kwako hakukisaidii chama zaidi ya kuonesha kiwango chako cha kutambua, kupima na kuchambua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…