Inaoenaka CCM tukiwa peke yetu na tukiwa sehemu siri tunataka serekali 3 tukiwa mbele ya vyombo vya habari na watu tunataka srekali 2.
hapa ni wazi ndani ya CCM kuna tatizo.
KWANINI NIMESEMA HIVI
Kama tulivyomsikia Jaji warioba. Sehemu muhimu ndani ya serekali wamependekeza serekali 3.
Kwa mfano afisi ya waziri mkuu, afisi ya makamo wa rais. hizi kama sitakosea zimependekeza muundo wa serekali 3. Hizi ni Ofisi nyeti ambazo kazi yake ni kutatua kero za Muungano.kama zimependekeza muundo wa serekali 3 ni wazi kwamba kuna tatizo.
Hapa CCM tumeshika hatamu. Hapa kuna makatibu wakuu licha ya kutokwa watendaji wa Chama lkn wengi wao ni wakereketwa wa Chama. wakurugenzi na hata mawaziri wote hawa ni Chama chetu.
Kama haya ndio mapendekezo ya ofisi hizi mbele ya jaji Warioba ni wazi CCM pia inataka serekali 3 nyuma ya pazia lkn mbele ya vyombo vya habari inataka serekali 2.
Ofisi ya Bunge na ofisi ya baraza la wawakilishi. Hili kwa kiasi kiikubwa ndio wawakilishi wa wananchi. Kwa mujibu wa warioba hawa pia wamepndekeza serekali 3. hapa CCM imejaa.hapa ndipo alipo spika wa CCM , hapa ndipo penye wenyeviti wa CCM wa kamati za Bunge.Mapendekekezo haya yanaushawishi mkubwa kutoka ccm.
HII NI SEHEMEU YA MAPENEDEKEZO YA TAASISI ZA SEREKALI
103 .Baadhi ya taasisi za kiserikali, ama moja kwa moja au kwa tafsiri ya
mapendekezo yao, pia zilipendekeza au kukubali muundo wa Serikali Tatu. Kwa
mfano, Baraza la Wawakilishi Zanzibar lilipendekeza kuwepo kwa mamlaka huru ya
Zanzibar, mamlaka huru ya Tanganyika na mamlaka ya Muungano na iwekwe wazi maeneo, uwezo, nguvu, utendaji na mipaka ya kila mamlaka. Baraza la Ofisi ya Makamu wa Rais lilipendekeza, kuhusu Muundo wa Serikali kwamba, nanukuu
"kuwe na Rais mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wakuu wa Serikali za Washirika wa Muungano wapewe vyeo vingine 32 vinavyoendana na hadhi na mamlaka zao. Pia katika kutaja hizo serikali tatu inabidi zitenganishwe ili Serikali ya Muungano ionekane ndio ya juu"
104. Baraza la Ofisi ya Waziri Mkuu lilipendekeza, kuhusu uongozi wa taifa kwamba kuwe, na "Rais wa Jamhuri ya Muungano, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, Waziri Mkuu wa Serikali ya Tanganyika na Waziri Mkuu wa Serikali ya Zanzibar. Mapendekezo hayo ni kwa sababu hakuna umuhimu wa kuwa na marais watatu (3) katika nchi moja na wala neno Rais halimuongezei hadhi kiongozi yeyote. Pia kutoa nafasi kwa Mawaziri Wakuu kuwa watendaji zaidi na hivyo kusimamia Serikali za Washirika." Aidha, Bunge la Jamhuri ya Muungano katika maoni yake
lilipendekeza kuwepo kwa Tume ya Utumishi wa Bunge ambayo o inajumuisha, katika Wajumbe, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano (Mwenyekiti), Spika wa
Bunge la Tanzania Bara na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.