Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Hata hizi serikali tatu tunajisumbua tu. wangekuja na maoni pia ya ambao hawautaki kabisa huu muungano.
 
"Kama kuna jambo moja ambalo wazanzibari wa makundi yote wanakubaliana, ni Zanzibar kuwa nchi" kasema Warioba.

Ni hatari aisee, DVD ya nondo hizi hata kama itauzwa elf50 nitanunua. Nondo za kufa mtu, ni hatari tena kwa ueledi na utaalam wa hali ya juu. Kazi kwanu wanaCCM wa huku bara, wenzenu inapokuja issue ya Uzanzibar tofauti zote huzitupa na kuunga mkono Uzanzibar kwanza. Nyie sinzia tu wenzenu Zanzibar!
 
Mkuu umechanganywa wapi?
Au nawe ni miongoni mwa wale wasiopenda kuambiwa ukweli?
Dah mkuu, kiukweli nimecheka sana jinsi nilivyoandika hapo juu. Warioba amenichanganya anavyotetea utengano ndani ya Muungano. Sipendi serikali mbili na nachikia huu muundo wa serikali tatu. Mie ni muumini wa serikali moja
 
Kama CCM hawajamwelewa Warioba then itakuwa ni ukweli zaidi kwamba wanafikiria kwa kutumia matumbo (Komba, Kificho, Leonidas Gama) na/au makalio
Mzee msomi ameeleza kila kitu wazi, vizuri, taratibu na kwa mtiririko wenye mantiki, very nice
CC
Chabruma
 
Last edited by a moderator:
JI jambo jema kupima maoni kwa idadi ya waliochangia kitu husika.Kwani aliyechangia kitu kingine ktk jambo asilochangia hana tofauti na asiyechangia kabisa.Hili jambo nadhai sasa ni clear sana kwa maCCM. Sasa TV zetu zitakuwa na uchambuzi mzuri kidogo ,sasa porojo na kuweka hisia...
 
Najiuliza hivi yale wasaa mawili ambayo mzee SIX alitaka kumpa Warioba alitumia vigezo gani? Kama sikosei kashatumia masaa 3:30 still more to count!
 
Kasema muungano wa serikali mbili waliotuachia waasisi sio huu wa sasa. waasisi walituachia nchi moja yenye serikali mbili, siyo nchi mbili zenye serikali mbili. Babu anaua kinoma.
 
Jamani mbona mawaziri na wabunge wa CCM wanaonekana kukata tamaa kabisa!
 
Back
Top Bottom