Hotuba za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Hotuba za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

nitakutumia namba ya simu ya jamaa hapa moshi anaziuza kama njugu,amepiga hema lake posta kuu kila siku anaonyesha watu lakini katika pitapita yangu hapa moshi sijawahi kuona watu au mtu ananunua zaidi ya kusikiliza na kuangua vicheko kwa jinsi mwal. anavyotoa hotuba zake na kuchekesha kama mtoto mdogo,kesho jumanne utapata simu ya huyo jamaa au baadaye kidogo jioni,yote aliyokuwa anayasema hayatekelezwi nashangaa gazeti la uhuru leo wanatoa tahariri wanasema tumuenzi mwal. kwa kutoruhusu watu wasivuruge muungano.

mbona uhuru hawasemi tumuenzi mwal. kwa kuwasaka wezi na mafisadi wa mali za umma ambao wameua viwanda alivyoviacha mwal.?
 
CAMINITO nduguyangu mbona umemtafsiri kiugovi huyo mama? hukumchokoza yeye ila umegusa hisia za waumini wa dini ya uislam kwamaana huyo mama hakutoa aya wala hadithi yakuthibitisha alicho kisema amezungumzia mawazo yake tu. ambayo hakuya weka kwenye imani ya dini sasa hiyo harufu ya udini nani kaiweka kama sio wewe? yaan wewe ndio unatufanya tuzungu mzie udini badala ya kumshauri au kumjibu muhusika wa swali MTAZAMO WANGU USIRUMBANE NAMIMI UTAKUA HUJA UTENDEA HAKI UHAI ALIO KUPA MUNGU
 
jamaa kaomba tu aelekezwe wapi kupata hizo hotuba,afu watu wanajibu utumbo
 
Mleta mada anaomba audio, video za Nyerere sasa black widow mbona amekuja kubadilisha topic ya watu mpaka mleta uzi hasaidiwi tena??
Black widow atakuwa akili yake haiko vizuri, something wrong ktk brain yake.
 
Nimejaribu kujikumbusha lakini nimepata harufu ya chuki binafsi au zenye mzukumo wa kiimani

Maelezo ya wapambe wote uliowanukuu wanatofauti gani na wewe?



Uzuri ni kwamba mtaandika weeeeeeeeee lakini ukweli unabaki palepale hata 1000 ijayo kuwa J.K.Nyerere aliku Rais wa Kwanza wa Tanganyika na mzalendo kuliko yeyote yule!
Hivi inaingia akilini unaleta stori za Mhaini na kuita hoja za kujadiliwa?

Pokea likes zangu milioni
 
Onyesha cha maana kimoja cha Nyerere tukijadili halafu tuone kweli kina maana? angekuwa na maana angeiacha hii nchi baada ya miaka 24 ya kutawala kidikteta, kuwa maskini duniani?
Na miaka ishirini baada ya yeye kuondoka madarakani, tumekuwa matajiri duniani?
 
Nimewahi kuwasikia TV sibuka wakitangaza kuwa wanauza hotuba za Nyerere. Office zao zipo maeneo ya Bamaga.
 
Mkuu kuna bwana mmoja yuko Moshi anauza videos za hotuba za Mwalimu Nyerere. Nikipata contact zake nitakufahamisha.

Anapatikana nje ya posta kuu ya mjini Moshi, anatumia gari lenye kila aina ya video na vitabu vya hotuba zake.
 
Haya wewe ambae "hujalogwa" tuoneshe kimoja cha maana ulichokisikia kwenye hizo hotuba.

FaizaFoxy una maoni gani kuhusu Rais Mh. J.K. kuwashauri wananchi kuskiliza hotuba za nyerere?

Alisema haya jana huko Iringa wakati wa maadhimisho ya kumbu kumbu ya kifo cha Mwl. Nyerere.
 
Anapatikana nje ya posta kuu ya mjini Moshi, anatumia gari lenye kila aina ya video na vitabu vya hotuba zake.

Mkuu uko sawa. Nikipita hapo leo kama atakwepo nitachukua contact zake.
 
FaizaFoxy una maoni gani kuhusu Rais Mh. J.K. kuwashauri wananchi kuskiliza hotuba za nyerere?

Alisema haya jana huko Iringa wakati wa maadhimisho ya kumbu kumbu ya kifo cha Mwl. Nyerere.

Sijamsikia.

Hata mimi ukinisoma huko juu nawaambieni mzisikilize ziwajaze ujinga halafu mrudi mnambie kimoja cha maana mlichokisikia humo.

Zaidi ya hapo nimeshawahi kusema humu, Nyerere posses a gift of barney. Kama hujui ni nini hicho, unaweza Google "barney". Utanielewa tu.
 
FaizaFoxy ni STAGNANT kifikra na nahisi anaropoka tuu kwa kua yawezekana haijui vizuri historia ya nchi hii. Hajui mwaka 1947 nchi hii ilikuaje ukilinganisha na 1999. Hajui ROLE OF NYERERE IN BUILDING NATIONAL INTEGRITY AND AWARENESS. Hajui mchango wa wazee wa nchi hii katika kuifanya Tanzania ya leo ilivyo. Navyoona ni kuwa Kwao hakuna wakubwa wa mfano ndo maana hana pa kuiga kama point of reference.
 
Hapa watajitokeza wa kusema Mwalimu alikuwa mdini!! Hawatajali kusoma neno kwa neno kubaini dhamira ya huyu kiongozi kwa tanzania na watu wake wote.R.I.P Mwalimu
 
Good speech..! Ni kiongozi aliyebeba dhamira ya wananchi wake,alijinyenyekeza kwao,kujishusha ili kutafuta mstakabali wa watu wote bila uonevu.Yeye mwenyewe alikiri ubinadamu wake,kwamba kuna mahali alikosea lakini pamoja na makosa yake aliungwa mkono kwa dhati na wananchi..Ni wakati muafaka wa kusahau yaliyopita na kuanza kuganga yajayo na kutengeneza dira nzuri kwa manufaa yetu sote.
 
Back
Top Bottom