Huku Mtwara msimamo wa watu maarufu uko tofauti kidogo namba 1. Misso Misondo, 2. Harmonize, 3. Chibu, 4. Alikiba

MSAGA SUMU

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2015
Posts
6,661
Reaction score
21,656
Aisee hii Tanzania ni kubwa sana, niko Mtwara linapokuja suala la burudani kwa mikoa ya Lindi na Mtwara hamna mtu aneyemfikia Dj Missondo kwa kusepa na kijiji.

Huyu jamaa akiwa sehemu anafanya yake hamna msanii yoyote atayethubutu kufanya show, maana itakuwa hasara.

Kwa huku Mtwara, msimamo wa vijana maarufu wenye ushawishi huko tofauti kidogo na Tanzania sehemu nyingine.

Kwa utafiti mdogo niliofanya top 5 yao iko hivi.
1.Dj Miso Misondo
2.Harmonize
3. Diamond
4. Ali Kiba
5. Marioo.
Unawaambia nini wana Mtwara?
 
Hii ni kama Shinyanga vijijini. Kuna mtu anaitwa Nyanda madeleka , Kuna Nyanda madirisha!.

Hao watu hata aje Chris brown hawez kusikilizwa mbele yao
 
Huyu misso, apewe maua yake, nimeona dogo ana trend mwaka jana, nakumbuka ruangwa pale aliwashaga moto, nilikua kwenye pikipiki. Anatuma watu wavue nguo na wakavua😂😂😂👏🏼Nimeona ana trend nimefurahi sana.
 
Mimi Niko Mtwara na huyo misondo hata simjui...
Ukija kwenye suala la burudani Harmonize ni baba lao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…