Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tafadhali sana acha kumhusisha Mungu kwenye upuuzi. Kwahiyo kama Mungu amaketaza kuhukumu utaacha jambazi akupore tu? Wewe dada umekuja kuwaje aisee?Lakini Mungu ametukataza kuhukumu pia, hivyo tumuache na mambo yake anayoyafanya.
Noo. Kwa hiyo wewe unasapoti Mange anachofanya? Au wewe ni Mange?Mkuu, calm down.
Mange muache na maisha yake aliyoyachagua.
Ndo jibu lenyewe hilo, siku moja utaniambia.Kwamba nini Mkuu? Naomba isiwe hivi nilivyoelewa please!
Humpunguzii chochote[emoji23]Mwanaume anayevaa chochote iwe bangili, pete tofauti na ya ndoa, cheni, hereni yani vyote hivyo kwangu anavuliwa vyeo vyote.
🤣🤣🤣🤣🙌KhaaaaKudate na mmama nyie mnaita mushangaz kuna mda ni kipengele sana🤔🤔labda uwe huna hela, wanakera sana....ukute mnene afu anazuga kudeka
Mungu ana siri kubwa, njia zake Mungu hazichunguziki kamwe, kuhusu mustakabali wa binadamu humpa amtakaye humnyima yeyote. Wangapi wametulia hawana ndoa, wangapi wahuni wana ndoa?!!Maisha ya ndoa ni ibada huna Mungu ndani yako sahau kuhusu ndoa
Leo wadau mnatema madini mazito mazito 🙌🏾🙌🏾Mungu ana siri kubwa, njia zake Mungu hazichunguziki kamwe, kuhusu mustakabali wa binadamu, humpa amtakaye humnyima yeyote, wangapi wametulia hawana ndoa, wangapi wahuni wana ndoa?!!
Ndoa ni mapenzi ya Mungu akikupangia hata binti awe anajiuza barabarani ataolewa tu hata akiwa hoyahoya atampata wa kumstiri,hata wanaume sisi tuwe walevi kupindukia au hauna maisha utampata wa kukufaa.
Mungu hajali nini wala nini, akitaka kukupa mchongo anakupa tu,hana baya.
Wolper angetulia tu asije akavuka mkojo akaenda kwenye majanga zaidi bora ajikite kwenye kazi sasa hvi ni mamaView attachment 2831270Ndoa ndoano! Mambo sio mambo!
Muigizaji aliyegeukia biashara, mwanadada Jackline Wolper Massawe ‘Wolper’ inaripotiwa kupata bwana mpya baada ya ndoa yake kukumbwa na sintofahamu nyingi.
Ikumbukwe Wolper alifunga ndoa takatifu na aliyekuwa baba wa mtoto wake Richard ‘Rich Mitindo’ 19/11/2022.
Wawili hao walioonekana kuwa na huba la moto, shatashata lililokolea nazi enzi za uchumba wao uliopelekea Wolper kufikia uamuzi wa kumzalia kabisa mtoto Rich hata kabla ya kufunga ndoa.
Mara nyingi walionekana wenye furaha na mapenzi tele, wakipop champagne kila uchwao na kushona sare!
Wambea na wenye husda walinyanyasika vya kutosha!
Jinamizi liliyasogelea mapenzi yao baada ya kufunga pingu za maisha, na Wolper kubarikiwa mtoto wa pili.
Ilianza kuripotiwa ndoa kuingia mdudu baada ya mumewe kuonekana akila maraha China, mbaya zaidi kwa kipindi kirefu aliendelea kubaki huko bila kurejea nchini ilipo familia yake kitendo kilichozua minong’ono!
Wolper alishindwa kujizuia, akaanza kuongea mengi ya uchungu hata alipopata nafasi ya kuhojiwa na waandishi aliongea ambayo wengi waliyatafsiri kama alama nyekundu ktk ndoa yao.
Baada ya kipindi kirefu cha mumewe kuwa nje ya nchi, ni wazi Wolper uvumilivu umemshinda nae kaamua kujipa ‘raha’ kwa kutoka kimapenzi na mwanaume anayefahamika kama Vincent Azrone almaarufu G Nex.
Mwanaume huyo imebainika kuwa ni meneja katika ukumbi maarufu wa starehe, Havoc Night Spot uliopo Masaki jijini Dar Es Salaam.
Wapenzi hao wameonekana mara nyingi pamoja, hadi katika sherehe ya kuzaliwa kwa mwaume huyo, wawili hao walikaa pamoja bila kificho!
Taarifa za uhakika ni kwamba G Nex yeye bado hajaoa, na kiumri anaonekana mdogo kuliko Wolper.
Mara nyingi ameonekana akiwa anaendesha gari yake Toyota Crown nyeusi.
My take; Wolper, najua ilivyo vigumu kuishi ktk stress za mapenzi na ndoa kwa mwanaume asiyeeleweka.
Sitaki kukuhukumu kwamba ulikosea kuolewa na kijana mdogo kwako kiumri ambaye damu bado ya moto anahitaji kufanya mengi kama ambavyo wewe ulifanya kwa wakati wako…
Nakuombea kheri, haya yawe ni mapito mpate kuyaweka sawa na mumeo, ndoa na iheshimiwe na watu wote!
Pichani ni mpenzi mpya mjini wa Jack Wolper, Vincent Azrone ‘G Nex’
Wenu katika ubuyu,
Nifah.
Naongea haya Kwa uzoefu, afu huwa haina kuachana ni kimya kimya mnapotezeana ni mwendo wa vijembe, mkikutana baada ya kupeana space mnaendelea mlipoishia🤣🤣🤣🤣🙌Khaaaa
It’s either your business or non of your business.Noo. Kwa hiyo wewe unasapoti Mange anachofanya? Au wewe ni Mange?
Andiko la dhati namna hii lazima ka[emoji485] kahusike pia, otherwise umeandika in a very real and touching!Baada ya kipindi kirefu, nimeweka thread hii ya ubuyu katika jukwaa hili kama sehemu ya kumuenzi rafiki & binamu yangu warumi
Endelea kupumzika kwa amani binamu, niko hapa kuendeleza kile ulichokuwa unakipenda zaidi hapa JF.
Hadi tutakapoonana tena, RIP!