Hukumu zenye utata kama hii ya Askari Morogoro huwa zinasababishwa na nini?

Zibadilishwe zisilinde ujuha. Itofautishe professional liability na ujinga binafsi
Wanadai kuwa yeye huwa anatafsiri kilicholetwa mahakamani na kuhukumu endapo upande wa pili utashindwa kujibu hoja
 
Tatizo ni ujinga kuamini kila mtu anajua kiswahili! Mi sikijui kiswahili bro!
Usifikili wote tulisoma kiswahili! Wahindi kibao kariakoo wanafanya biashara kwa kiswahili hikohiko kibovu!
Unataka watu wote tuwe kama wafanyakazi wa BAKITA
'Usifikili.' hakuna mtu ata kuchulia serious. Tuliza munkari, anza kujipa mazoezi ya ra re ri ro ruuu, rudia tena, kwa wiki mbili, tatizo linaisha. Ni aibu.
 
'Usifikili.' hakuna mtu ata kuchulia serious. Tuliza munkari, anza kujipa mazoezi ya ra re ri ro ruuu, rudia tena, kwa wiki mbili, tatizo linaisha. Ni aibu.
Asante kwa ushauri! Walimu wa viswahili ndivyo mlivyo! Mna gubu kama lote! Ndiyo maana hamuendelei!
Wengi mnamalapa mabovu, maisha mabovu, ujuaji mwingi mfukoni hamna kitu,
Haiwezekani watu wote tukaijua lugha kama walimu!
Wazungu kibao hawajui lugha, wachina kibao hawajui lugha, wahindi n. Na wanamarndeleo makubwa!

Wewe na lugha yako inakusaidia nini! Hujawahi hata kuandika hoja humu kazi kukosoa!
 
Sasa wewe kiswahili hujui, kingereza chali. Shida unazo wewe.
 
Mahakama za mwanzo ni za hovyo saana mkuu...ni rahisi kuhonga sana hapo...nikiwa na kesi sitarajii kupata haki mahakama za mwanzo...nadhani pia mahakimu wake huwa sio wabobevu sana kwenye sheria za aina mbali mbali. Inawezekanaje watu waliokaa darasani kwa muda unaofanana wakasoma kitu kile kile na wakafanyia mazoezi halafu waje wahukumu tofauti kiasi hicho? Hapo Kuna mlungula boss.
Haki ipo rufaa mkuu huko hawakuachi pasi na shaka labda kama Kuna siasa ndani yake.
 
Ukubali hapo ni rushwa na uchawi tu.

Usijipige kifua kuhalalisha ubakaji wa watoto. Siku wambake mtoto wako uone how it reacts.

Mpaka kufikia kifungo cha maisha ushahidi ulikuwepo wa kutosha.

Au tuseme walifikia makubaliano na wazazi alipe tu .
 
Kazi kwelikweli
 
Nafikiri hukumu kama hizo zinatakiwa abebe hakimu wa mwanzo. Apewe hiyo miaka kwa ujinga alioufanya mwanzo. Sheria zinafilishwe
Hivi mtaalam wa kazi yake pale anapo jikosesha kazi yake kwa kutofuata sheria kwa makusudi,alafu upande wa pili unakata rufaa kwa kutumia hayo mapungufu kwa makusudi kabisa ya kunyanganya haki za watu, mi huwa naona huo unakua ni mpango.wa watu wabaya!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…