KERO Huu mfumo wa Employee Self Service wa Utumishi haufanyi kazi

KERO Huu mfumo wa Employee Self Service wa Utumishi haufanyi kazi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Huu mfumo hauna msaada kwa mtumishi kwenye mambo nyeti mengi.

Umejaa ukiritimba uleule wa awali. Nasikia ukitaka uhamisho lazima uwasiliane na mkuu wako wa idara pamoja na viongozi wengine wa mkoa kama katibu tawala ili waweze ku-approve maombi yako ndo taarifa ziende TAMISEMI kwa ajili ya uidhinishaji wa mwisho wa maombi.

Mfumo umeongeza usumbufu uleule tuliokuwa tunaulalamikia. Ila ninasikia kwenye suala la mikopo ya benki kwa watumishi kupitia e-loan wako faster ukitumia mfumo kuliko kujaza form.

Kwenye mambo ya kumkandamiza mtumishi wako fasta ila kwenye masuala ya kumsaidia mtumishi mfumo unamkandamiza zaidi inasikitisha sana
 
Shida ni kila Wilaya ina HR wake na IT Wake **** maswala ambayo kila wilaya inayo ni tofauti na wilaya zingine..

Kwa mfano ni Vigumu kwa Afisa Utumishi wa Tamisemi ni Vigumu kumjua Jackson Abdalla alieajiriwa Tunduma na Jackson abdallah alieajriwa Lushoto..

Ndo maana Kila mtumishi Customer care yake ataipata katika halmashauri yake kuepuka mkanganyiko...

Yes ni kweli kabisa wapo waliosaidiwa na Watu wa TEHAMA na Ma HRs na wapo ambao wanaona kuwa watu hao wako humble na wapo wanaoona hawafanyi kazi..

Ubovu na ubora unategemea na halmashauri
.
Mkuu samahani, unamaanisha nini unaposema wilaya zinatofautiana? Kuna halmashauri ina idara au muundo tofauti na halmashauri nyengine?

Kila mtumishi ana namba zake tofauti na mtumishi mwengine zinazomtambulisha, ndio maana ya kuwa NIDA na check number.

Hayo ya kumjua mtu personally hayahusiani na uhamisho, ndio mianya ya rushwa na upendeleo.
 
Sioni sababu na nashangaa kwanini UTUMISHI wamekimbilia kutumia ESS na huku ukweli haufanyi kazi, unaingia Online wanakwambia wanashidnwa ku-retrieve taarifa zako, unaomba uhamisho, unajaza kila taarifa then unakuta hakuna kiytu chochote na hakuna mtu wa kukusadiai.

Naupenda sana Mfumo wa NEST (National E-procurement System) wana kitengo cha msaada na mnafanya wote online na mnapata suluhu mara moja, yaani UTUMISHI wanashindwa hata na Customer care wa TANESCO? Mfumo gani ambao hauna msaada? huu ni mwanya wa kukaribisha rushwa na mambo mengine. Mjipange au mtoke humo ofisini. na mnavyojiona Miungu watu sasa.
Jambo gani utumishi waliwahi kufanikiwa zaidi ya kuinua inua mabega na kuweka tai zao sawa
 
mimi hapa niliwahi kusaidiwa na IT

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app

Wanasaidia ikiwa unawapita kiwango cha mshahara, au unao ushawishi wa kubadilisha mapato yao, au kuna personal relationship, au yeye ana shida flani kwako, au kwa kuwapa hela ya soda, or something of that kind.
 
Mkuu samahani, unamaanisha nini unaposema wilaya zinatofautiana? Kuna halmashauri ina idara au muundo tofauti na halmashauri nyengine?

Kila mtumishi ana namba zake tofauti na mtumishi mwengine zinazomtambulisha, ndio maana ya kuwa NIDA na check number.

Hayo ya kumjua mtu personally hayahusiani na uhamisho, ndio mianya ya rushwa na upendeleo.
Umeweka vizuri sana
 
Mkuu samahani, unamaanisha nini unaposema wilaya zinatofautiana? Kuna halmashauri ina idara au muundo tofauti na halmashauri nyengine?

Kila mtumishi ana namba zake tofauti na mtumishi mwengine zinazomtambulisha, ndio maana ya kuwa NIDA na check number.

Hayo ya kumjua mtu personally hayahusiani na uhamisho, ndio mianya ya rushwa na upendeleo.
Mkuu Mahotera habari,
Naba nikukumbushe kuwa katika Sheria kuna Sheria kuu na pia kuna By laws..

Sheria kuu Hutumika Nchi nzima ila By laws hutumika Katika eneo fulani na Kila halmashauri ina By laws Zake ambazo hutungwa na Baraza la Madiwani..

Kwahyo kulingana na Sheria Halmashauri hazilingani kwa Sheria na Taratibu mchi nzima..japo zimaweza kuwa.na mfanano wa kimadaraka..

Kuhusu Mtumishi na Taarifa zake kama nilivyosema sema awali..

Uhamisho una Vigezo vyake na masharti yake..
Anayejua umetimiza vigezo vyote ni HR wako na Mwajiri wako huko Halmashauri..

Kwa mfano anayejua Uko shule kwa sasa ni Mwajiri wako (Na ndo unayesaini naye mkataba wa kutokuhama huwapo shuleni)..

Anayejua kuwa Unashida ya kinidhamu na upo kwenyr Probation ya Kinidhamu ni wilaya yako na Si tamisemi hivyo ni vyema Kutoku-centralise hii huduma ili wale wanaostahili waipate na wale wasio stahili wasiipate..

mbona tunajifanya kama hatujui Lazma supervisors wako wakujue na hata mwajiri wako ajue information zako ajiridhishe kweli una vigezo...

Nafikiri nimekujibu kama una swali la nyongeza karibu
 
Mkuu Mahotera habari,
Naba nikukumbushe kuwa katika Sheria kuna Sheria kuu na pia kuna By laws..

Sheria kuu Hutumika Nchi nzima ila By laws hutumika Katika eneo fulani na Kila halmashauri ina By laws Zake ambazo hutungwa na Baraza la Madiwani..

Kwahyo kulingana na Sheria Halmashauri hazilingani kwa Sheria na Taratibu mchi nzima..japo zimaweza kuwa.na mfanano wa kimadaraka..

Kuhusu Mtumishi na Taarifa zake kama nilivyosema sema awali..

Uhamisho una Vigezo vyake na masharti yake..
Anayejua umetimiza vigezo vyote ni HR wako na Mwajiri wako huko Halmashauri..

Kwa mfano anayejua Uko shule kwa sasa ni Mwajiri wako (Na ndo unayesaini naye mkataba wa kutokuhama huwapo shuleni)..

Anayejua kuwa Unashida ya kinidhamu na upo kwenyr Probation ya Kinidhamu ni wilaya yako na Si tamisemi hivyo ni vyema Kutoku-centralise hii huduma ili wale wanaostahili waipate na wale wasio stahili wasiipate..

mbona tunajifanya kama hatujui Lazma supervisors wako wakujue na hata mwajiri wako ajue information zako ajiridhishe kweli una vigezo...

Nafikiri nimekujibu kama una swali la nyongeza karibu
Asante kwa majibu, sasa kama mambo yako hivi, huu mfumo una maana gani? Waache tu mambo yafanyike locally, wamewaongezea matatizo wafanyakazi wenye matatizo badala ya kuwasaidia, maana sasa uende kwenye mfumo halafu ufanye yote yale ya awali.

Wakati huo huo mfumo haukusaidii kukuenesha wapi kuna fursa ya kuhamia kwa kada yako, hauna sehemu watumishi wanaweza kuwasiliana, haumuwezeshi mtumishi hata kuweka namba za mawasiliano yake...

Kuhusu taarifa za mtumishi ambazo HR anazijua kama suspension, probation, au kuwepo shuleni, kwanini mfumo usimuwezeshe HR ku-update status hizo za mtumishi, nini maana ya mfumo unaoshidwa kuweka taarifa muhimu kama hizi kwenye uhamisho?
 
Asante kwa majibu, sasa kama mambo yako hivi, huu mfumo una maana gani? Waache tu mambo yafanyike locally, wamewaongezea matatizo wafanyakazi wenye matatizo badala ya kuwasaidia, maana sasa uende kwenye mfumo halafu ufanye yote yale ya awali.

Wakati huo huo mfumo haukusaidii kukuenesha wapi kuna fursa ya kuhamia kwa kada yako, hauna sehemu watumishi wanaweza kuwasiliana, haumuwezeshi mtumishi hata kuweka namba za mawasiliano yake...

Kuhusu taarifa za mtumishi ambazo HR anazijua kama suspension, probation, au kuwepo shuleni, kwanini mfumo usimuwezeshe HR ku-update status hizo za mtumishi, nini maana ya mfumo unaoshidwa kuweka taarifa muhimu kama hizi kwenye uhamisho?
Umewahi kusikia Kitu kinaitwa Local Public?
Au Public but Locally?
Ndo mfumo huu unavyofanya kazi..

VItu vyote vimewekwa Public but kwa manufaa yanayofanyika local na hata maelezo yake yako clear kabisa.. Nitayaweka..baadae..

Kuhusu Sehemu ya kuweka Namba sio kweli (Nahisi mfumo huujui)..Kuhusu wanaobadilishana kubadilishana namba kwenhe mfumo ipo kuna namba yako na hata namba ya mwingine kuna sehemu ya Transfer incoming na outgoing utaona wanaotaka kuja Sehemu ulipo na namba zao ukiridhishwa unaweza kuwacontact na mkapanga kubadilishana..
Upitie mfumo ndugu utauelewa..
Na hii ndo process nzma ya uhamisho..Mkuu
Screenshot_20240126_111320_Chrome.jpg


Kuna kosa lolote hapo niulize nitakujibu
 
Tangu mfumo uanze kuna mtumishi yeyote aliyefanikiwa kupata uhamisho wa let's say kutoka mkoa A kwenda mkoa B baada ya kuomba uhamisho huo kupitia mfumo?
Mfumo umewekwa ili kuzuia watu wasiwe wanahama. Au kama ikitokea wanahama isiwe simple, matokeo yake wakate tamaa waendelee kutumika na halmashauri zao.
 
Kuweni waangalifu sana ni hiyo mifumo ya IT.
Unaweza shituka unaletewa barua ya Kuachishwa kazi bila kujua.
Unabonyeza bonyeza bila tahadhari utajikuta umeomba kuacha kazi masaa 24.
Kuna watu bila kubonyeza bonyeza kwenye mifumo ya Serikali hawaridhiki kabisa.
Nimecheka Sana Sana, ukute jamaa labda ndio lengo lao, ukosee ujikute mfumo unakuletea Meseji " Ombi lako la kuacha KAZI ndani ya saa 24 limefanikiwa"
 
Back
Top Bottom