Huu mjadala wa kususia bidhaa na huduma ni hatari kwa uchumi wa nchi

Ulisikiliza space jana?
 
Ukiingia twitter eneo lililotawaliwa na kigogo & the co utahisi Tanzania pana upinzani mkali mno ila njoo mitaani hakuna response yoyote.

Hao hao chadema walishawishi watu wavunje laini zao za voda ila kiko wapi na kilifikia wapi
 
Subiri uone mamilioni ya raia wakubali kujinyima kununua huduma na vitu fulanifulani ili kuinyima serikali kodi, hapo ndo utajua mbinu ya economic boycott inafanya kazi au la!

Kwa hiyo mbinu ya kuua uchumi utaitumia mwenyewe? Utawaambia nini wananchi kuhusu uharibifu huo wa uchumi? Wananchi watalipokeeje?
Au hayo ni ya kwenye ulimwengu wa Twitter pekee?
 
Wananchi wenyewe ndo watashiriki kwa hiyari yao, wasiotaka basi wanaendelea na maisha yao kiroho safi
Ila kwa wale watakaojitolea kushiriki hiyo boycott lazima joto lifike magogoni huko, maana serikali hata ikiporeza bilion 10 tu kwa mwezi hiyo ni pesa nyingi sana!
 

Mtawashirikishaje wananchi? Kumbuka Twitter hamzidi hata 500k.
 
Huko ndiko kuishiwa mbinu!

Mwenzako anacheza DEMOGHASIA na si DEMOKRASIA wewe unataraji fair play?

Bado unatumia mbinu zilezile za wazi ambazo unajua piga uwa anazimudu?

Kama hujaishiwa mbinu ni nini hiki?
Waendelee kutumia non violence it pay off in the future, tofauti na hapo unawaambia watumie violence
 
Eh! Wewe una akili nyingi sana, na kwa kitendo hicho ulichomfanyia jamaa yako Nafikiri kila mmoja ana kuona shujaa! Utalinganishwa na watu kama Gandhi, Mandela, Martin Luther, Lumumba na Che kwa kitendo hicho ulichomfanyia jamaa yako! Una matendo mema sana!
 
Hao wapumbavu wa twitter nani ana habari nao? Tukisusia watatuletea maendeleo?
Mkuu lakususia linawezekana kabisa tena linafanya kazi vizuri.

Hukumbuki Wakenya walivyosusia bidhaa zitokanazo na wanasiasa wa upande wa Jubilee ulivyoteteresha uchumi hadi kufikia kukaa meza moja na wapinzani?

Mfano mimi ndo baba wa familia mbona hilo lakususia linawezekana vizuri kabisa na wala sipigwi mabomu.
 
Ulisoma chuo gani mkuu?
 
Hao wapumbavu wa twitter nani ana habari nao? Tukisusia watatuletea maendeleo?
Msipuuze kila kitu vingine vitakuja kutokea kwa surprise.

Mfano tu suala la miamala ya simu kushuka kwa zaidi ya 75% huoni Serikali inavyohaha kulishughulikia?
 
Kwasabu chadema wapo wachache hawatofanikiwa ,labda wananchi kwa ujumla bila kujali vyama ndio hiyo kitu itawezekana kumbuka walisusia voda mpaka sasa inadunda
Voda iliyumba pakubwa sana hadi wanahisa wakubwa kama kina Rostam kufikia kuuza hisa zao zote unadhani ni mchezo?

Na hapo waliosusia walikuwa wachache sana maana hapakuwa na hamasa kubwa.
 
Mkuu are you serious kususia bidhaa hakuwezi kuleta athari za kiuchumi?
 
Mtaani watu wanapambana na mambo yao, hawana habari na mambo ya kususia.
Hivi huko mtaani mnakokuzungumziaga ni wapi? Maana sisi tuliopo humu ndo hao hao tunaoishi mtaani.
 
Waweza kususia huduma zingine za voda ukabaki na M-PESA tu kwa malengo fulani.
 
Na wewe unaamini wametengeneza hasara?

Na hata kama wametengeneza hasara ni kwa ajili ya uzembe wao.

Mfano mimi mwaka jana sikuweka salio kabisa sababu ya ughali wa vifurishi vyao.
Kwanini halotel, airtel na tigo wao wapate faida wakati ughali wa vifurushi ulikuwa kwenye makampuni yote?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…