Huu Mkutano wa SADC Samia alitoa maoni gani tufahamishwe watanzania

Kasema history itamhukumu kwa ubaya
 
Nawaasa M23 wale kwa urefu wa kamba yao... Nawe kagame waambie wanajeshi wako wasikanyage watoto
 
Nenda YouTube yapo tu
 
Mkuu mbona kama unataka kutuchpnganisha na serikali😅😅
 
Hiyo siyo kitchen party, mkuu!
 
Hakuna kitu cha maana amesema.....warudi wakalitizame jinsi kupata suluhu....sasa angewatumia whatsapp tu??PK amekasirikaa ....kupotezewa muda
 
Dar es Salaam, Tanzania

Azimio lafikiwa Mazungumzo ya Luanda na Nairobi kuhusu Amani Congo yaunganishwa kuwa kitu kimoja
Saa 6 zilizopita - Viongozi waliofanya mkutano wa pamoja katika jiji la bandari la Dar es Salaam nchini Tanzania walikubaliana kuunganisha mchakato wa Luanda unaosimamiwa na rais wa Angola mheshimiwa João Lourenço pia na Nairobi chini ya rais Uhuru Kenyatta ili kuharakisha...



Toka maktaba :

Mazungumzo ya Nairobi I na Nairobi II kuhusu Congo chini ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta akihojiwa (lugha kiswahili) kuhusu utatuzi wa mzozo wa Congo


View: https://m.youtube.com/watch?v=BI5HRv7WVrA
Uhuru Kenyatta, rais wa zamani wa Kenya, aliyeteuliwa kuwa mwezeshaji wa mchakato wa Nairobi na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), anatathmini safari yake ya saa 48 mjini Kinshasa tangu Jumapili, Novemba 13, 2022. Pia inashughulikia suala la usalama mashariki mwa DRC.

Mstaafu Uhuru Kenyatta alikutana na mheshimiwa Rais Felix Tshisekedi wa DR Congo na kiongozi mkuu wa MONUSCO (SRSG-Head of MONUSCO), Bi. Bintou Keita .... kuhusu vita inayoendelea na kuona kwa njia gani wanaweza kusaidiana na wananchi wa kabila mbalimbali na jamii mbalimbali mbalimbali

Mwezeshaji wa mchakato wa Nairobi rais mstaafu Uhuru Kenyatta anasema wakutoka nje wenye maslahi binafsi wanawagawa siyo kwa mapendo bali wanaangalia madini kwa manufaa yao na kuwa bunduki na risasi haziwezi kuleta amani juu ya mzozo wa Mashariki ya Congo

Nimepewa jukumu hili na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki EAC kuwa bunduki na risasi haziwezi kuleta ushindi wowote, mimi nimetoka Ethiopia kule wamakubali Tigray na Amhara kuwa bunduki na risasi hazileti amani na ujumbe wangu kwa Congo ni huo huo asisitiza rais mstaafu Uhuru Kenyatta

Jukumu letu kama viongozi ahadi kubwa unayoweza kutoa kwa raia ni usalama wao kwa kuhakikisha hakuna umwagaji wa damu ili watu waendelee na maisha yao ya kujiletea maendeleo

Shida zilizopo zitatuliwe kisiasa na tusiwe na fikra kuwa jamii moja inaweza kushinda pekee bali wakongomani wa aina zote wakae pamoja kwa mazungumzo

Mazungumzo ya mèzani ni muhimu iwe M23 au serikali wote kwa kuweka bunduki chini, njia ya nguvu haitafauli na wala haitaleta ushindi ...
 
Afafanua waziri wa Rwanda kuhusu kilichojiri katika mkutano wa faragha wa viongozi wa nchi za SADC / EAC kuhusu amanì Congo

Habari kutoka kwa Waziri Nduhungirehe kuhusu Mkutano wa pamoja wa wakuu wa nchi wanachama wa EAC na SADC unaofanyika jijini Dar es Salaam


View: https://m.youtube.com/watch?v=9JDBZOqCKYoWaziri Olivier Jean Patrick Nduhungirehe wa Rwanda akitoa maelezo ya ndani kuhusu mkutano wa Dar es Salaam kuhusu jitihada na mikakati ya kuufanikisha amani Congo...

Kuunganisha mchakato wa Luanda unaosimamiwa na rais wa Angola mheshimiwa João Lourenço pia na mchakato wa Nairobi chini ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta ili kuharakisha...

Michakato ya amani ya Luanda na Nairobi, ni miongoni mwa maazimio muhimu ya mkutano wa pamoja wa viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika uliofanyika Dar es Salaam, Tanzania, Jumamosi, Februari 8.

Msisitizo tena wa wito wa mkutano huo kwa Tshisekedi 'kuzungumza moja kwa moja' na waasi wa M23 Jambo lingine muhimu ni wito wa viongozi wa kutekelezwa kwa mpango ulioidhinishwa wa awali wa upatanishi .....

Jopo la wakuu wa nchi 3 kuundwa kufuatilia maazimia ya mkutano wa Dar es Salaam ili maazimio hayo ya usitishwaji yatakayo simamiwa na Wanadhimu wakuu wa Majeshi (Joint Chief of Staffs) wa majeshi ya nchi za SADC kusimamia usitishwaji wa mapigano Mashariki ya Congo ..

Sekretariati kuundwa kufuatilia kwa ukaribu uimarishwaji amani kila siku na kutoa ripoti ya hali halisi ya siku kwa siku inavyoendelea ...

Makubaliano ya mwezi Machi tarehe 23 mwaka 2009 ambayo yanavunjwa na serikali ya Kinshasa kila siku, lazima yaheshimiwe ili kundi la M23 liweze kuiamini serikali ya Congo

Sisi kama nchi jirani na Congo pamoja na za ukanda wa SADC pia EAC zipo tayari kuisaidia serikali ya Kinshasa ipate amani kupitia mchakata wa Luanda / Nairobi ambayo sasa imeunganishwa ili kuharakisha amani ipatikane Congo
 
Je Angekuwepo Jiwe unahisi angetoa Kauli gani?
Ila hili angekuwepo Nyerere lazima kikao kingekuwa na habari ya kusikilizwa dunia nzima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…