Huyu ndiyo Rais Kagame nimpendae kutokana na IQ yake Kubwa

Huyu ndiyo Rais Kagame nimpendae kutokana na IQ yake Kubwa

Rwanda ina wananchi milion 12

Zanzibar ina wananchi milion 1


Vipi Zanzibar inalisha raia wake ?

Kubali hamna Akili.

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
Asante kwa kulikazia hilo Mkuu na hawana Akili kweli wasibishe. Na wasichokijua ni kwamba Chuki zao za kila Siku kwa Rais Kagame ndiyo Mwenyezi Mungu anazigeuza Baraka Kwake na mpaka anapata Akili za Kuiendeleza zaidi Rwanda huku Wao ( Fools ) wakiwa Wanashagilia tu Sinema ya Mmarekani na Dada ( Binti ) zao Kufuzu Kombe la Dunia la Wanawake kwa mara ya Kwanza.
 
Umemla mnyarwanda nn? sas Kama kagame Ana akili ajaribu kupigana na Congo Dr
 
Mwanasiasa wa Afrika akizungumza jambo fulani usishangilie,shangilia pale atakapolitimiza.Mifano hai tunayomingi tu kutoka kwa hawa wazee wa upembuzi yakinifu umeishafanyika,mzabuni keshapatikana,tarehe fulani itakuwa tayari.kila siku kutupanga tu.
 
Mr Slim namkubali sana
Nikiangalia miaka 25 iliyopita yale mauwaji na leo alivyoibadilisha na kuwa nchi ya 9 duniani kwa amani na usalama
Sina usemi kwa kweli

Jamaa kaitoa mbali nchi yao hata kama katumia njia za kibabe ila kuna heshima na utulivu kwao

Mleta mada hata kama ni Mtusi ila anaipenda asili yake Big up
Nategemea mwaka huu niongeze list yangu ya nchi nitakazotembelea iwe ya 33
Unaambiwa hata ukiwa unatembea manane ya usiku ukakutana na police wanaweza kukusindikiza mpaka hotel uliyofikia FACT
Ila kuna nchi zingine jirani ikifika usiku bora ukutane na jambazi

Hebu jisomee kidogo uone hata kwa gender equality upande wa serikali wamempita [emoji631]
IMG_6890.jpg




Na kwa usalama fact hizo hapo
IMG_6891.jpg

Hapa lazima nikakae kijiweni pia
IMG_6888.jpg
 
Leo tumewaza sawa mkuu. Niimeshangaa. Nikiwa barabarani nikawaza Kagame alivyo na akili kubwa. Kiukweli kama ulivyosema namchukia,lakini napenda anavyoikimbiza Rwanda. Napenda sana alivyo advanced kuhusu usalama wa Taifa. Rwanda (FBI) ya ndani ya nchi na (CIA) ya nje. Yaani ipo inayohusika na maswala ya usalama ya upelelezi wa ndani tu na ipo inayohusika nje ya mipaka ya Rwanda. Kama ilivyo mfumo wa Marekani na Israel. Na wanafanyakazi vizuri sana. Hapo Kagame saluti kwake. Namchukia tu kwa anachowafanyia wapinzani kama kuwapoteza na mengine.

Rwanda nchi ndogo,isiyo na chochote,ukilinganisha na Tanzania,lakini iko mbali kiuchumi,kiusalama pia kijeshi. Kagame akili kubwa. Kwa ujumla ni kama anai-control Afrika mashariki na kati bila wao kujua.

Kagame ameifanya Rwanda iwe tajiri kwa rasilimali za nchi zingine.

Kwa andishi la hivi karibuni la The bold ni kwamba Jamhuri ya Africa ya kati inalindwa na wanajeshi wa Rwanda na Polisi wa Rwanda huku hao wanajeshi zaidi ya 3000 wakichukua mishahara mizuri toka vyanzo vingine visivyo vya Rwanda. Wapo pia Mozambique kupambana na waasi. Kwa hiyo Kagema anaajiri vijana wengi jeshini na polisi kwa mikataba na nchi zingine.

Najiuliza Tanzania tumekosea wapi? Nchi kubwa yenye kila rasilimali za kutuendeleza zaidi hata ya Israel. Tanzania nchi yenye kila aina ya madini yapatikanayo duniani. Tanzania ina madini yasiyopatikana kokote isipokuwa Tanzania. Tanzania yenye mbuga zote kubwa duniani. Tanzania yenye gesi,mafuta. Tanzania yenye bandari kubwa ya kuhudumia nchi zaidi ya 5 mpaka 6,7 kufuatana tu kujipanga kwetu. Nchi yenye watu wengi lakini imekosa maarifa kabisa. Wapo wansojiita wasomi akina miguru na makatani wanawaongezea tu tozo kila kona za kuwakamua watu ambao hawajawatengeneza. Tuna watu wanajiita maprofeser humu nchini lakini hakuna hata mmoja na uprofeser wao mwenye plan moja yenye nguvu ya kutuvusha kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine,kiuchumi. Tanzania nchi inayojisogeza tu bila dira,wala mwelekeo ,tunaishi leo tu. Wengi viongozi wanaangalia matumbo yao tu. Kweli Kagame ni bonge la kichwa
 
Ila bana kama hujawahi kufika rwanda unaweza sema yaani ni bonge la nchi kumbe utopolo tu kigali inazidiwa na mwanza mbali
Mwanza inaweza kudhamini timu ys ligi kuu Uingereza kama Arsenal?.
 
Ila bana kama hujawahi kufika rwanda unaweza sema yaani ni bonge la nchi kumbe utopolo tu kigali inazidiwa na mwanza mbali
Mwongo mkubwa we. Rwanda Kigali kuna miji imepangika utasema ni jobeg .
Labda tuanzie hapo sehemu gani ulifikia? Tembelea sehemu kama nyabisindu, kabagabaga au hata pale kiyovu uone mitaa ilivyonyooka. Kazi kubwa ya mipango miji ilivyofanyika.
Kumbuka hii nchi ilikua kwenye vita nzito miaka ya 90s hapa.
Hayya njoo tz vita iliyopiganwa miaka ya 70s lakini mpaka leo bado athari zake kiuchumi haziko covered.
 
Ila bana kama hujawahi kufika rwanda unaweza sema yaani ni bonge la nchi kumbe utopolo tu kigali inazidiwa na mwanza mbali
Sure.... Nimeishi na ninapaelewa, kuanzia 07/05/2015 mpaka 25/06/2020.... Wabongo tunadanganyana sana🤣🤣🤣🤣
 
Paul Kagame.. Kiongozi mahiri ambaye huwa nampenda sana kwa maana ni "Visionary ' Bill Clinton alipata kuhojiwa kuhusu Africa. Alisema Kagame kiongozi wa kupigiwa mfano... Niliomba siku moja na huwa naandika kwa page yake, Naitaji siku moja niende Rwanda na ikiwezekana niongee mawili matatu...

Kagame Simba anayeongoza kondoo Africa
 
Ananufaika sana na vita kwa jirani yetu wa kati pale, ni mjanja sana, ana akili sana, kawekeza vizuri kwenye ujasusi, watu wake wapo kila mahali barani hata nje pia.
 
"It is unacceptable that Ukraine a Country of 44 Milion people will feed Africa a Continent of 1.4 billion people. I promise all Rwandans that Rwanda will attain Food self sufficiency before 2025. I have authorized 1 billion dollars worth of Farming Materials, and all Logistics involved in boosting up our Farming industry" President Kagame.

Ukiona tu GENTAMYCINE nampenda (namkubali) sana Mtu jua nimeshampima na Kujiridhisha pasi na Shaka kuwa ni Mwerevu (Genius) na Visionary kuliko Watu wengine.

Nina uhakika 99% ya Watu (Watanzania) wanaomchukia Rais wa Rwanda Paul Kagame Mioyoni mwao Wanampenda, Wanamkubali na wanatamani hata Siku moja tu aje Kuiongoza Tanzania ili iwe Tajiri haraka ( kuliko ilivyo sasa ) kwa kutumia vyema Rasilimali zake.

Hivi kwa Madini kama haya ya Rais Kagame ukiwa kweli una Akili utaachaje Kumpenda na Kuwakumbatia tu akna Van Dame wa Zanzibar?
Achana na huyo, tuangalie kilimo chetu tunakiboresha vipi, chakula sio ngano tu, Tz mahindi na mchele vinakosa soko, halafu mnasema Ukraine anatulisha sisi? Kama si utaahira huo ni nini?
 
Yani me nashindwa kuelewa kabisa,mfano sisi tanzania tunashindwa nini??tatizo no viongozi tu.

Kagame yuko bright sana.

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
Acha kupagawa na propaganda za hawa vilaza. Ukiona unakula halafu unakwenda chooni unajisaidia mpaka unamaliza, tena kwaamani jua kunawatu hawalali usiku na mchana ili tuu nchi hii iwe kama ilivyo, hicho kinnchi wanacho kisifia sifia kila uchao, kuna vikundi vya waasi wanao kilimbilia Kongo na wakimbizi wanao kimbilia kwetu Ili kuokoa roho zao...Acha kuchanganyikiwa na hizi soga.
 
Kajamaa kajiizi hako na miwani lake kama fidodido,..na Felix kashamshitukia huko tabia yake ya kukwapua midini ya DRC
 
Ananufaika sana na vita kwa jirani yetu wa kati pale, ni mjanja sana, ana akili sana, kawekeza vizuri kwenye ujasusi, watu wake wapo kila mahali barani hata nje pia.
Safi sana Mkuu umemaliza kila Kitu hapa.
 
"It is unacceptable that Ukraine a Country of 44 Milion people will feed Africa a Continent of 1.4 billion people. I promise all Rwandans that Rwanda will attain Food self sufficiency before 2025. I have authorized 1 billion dollars worth of Farming Materials, and all Logistics involved in boosting up our Farming industry" President Kagame.

Ukiona tu GENTAMYCINE nampenda (namkubali) sana Mtu jua nimeshampima na Kujiridhisha pasi na Shaka kuwa ni Mwerevu (Genius) na Visionary kuliko Watu wengine.

Nina uhakika 99% ya Watu (Watanzania) wanaomchukia Rais wa Rwanda Paul Kagame Mioyoni mwao Wanampenda, Wanamkubali na wanatamani hata Siku moja tu aje Kuiongoza Tanzania ili iwe Tajiri haraka ( kuliko ilivyo sasa ) kwa kutumia vyema Rasilimali zake.

Hivi kwa Madini kama haya ya Rais Kagame ukiwa kweli una Akili utaachaje Kumpenda na Kuwakumbatia tu akna Van Dame wa Zanzibar?
Sifahamu kipimo gani hutumika kupima hiyo IQ ila binafsi ninapenda watu wenye uthubutu kama huyo bwana, na wengine wachache waliowahi kuongoza baadhi ya nchi za Afrika.
 
Amahkuru?

Nikirudi safari hii nitaomba nipige picha nae hata ile ya cut out box, Ili mradi tu.


Hilo jambo analolisema, ni muhimu. Haiwezekani tukawa tunaagiza sukari, samaki, sia ajabu mpaka simenti? wakati tukiwa na Na mashamba yanaozalisha chakula ambacho kinaishia katika meza za matajiri duniani huku sisi tunalishwa samaki wa kopo kutoka nje! katika nchi kama Tanzania. Tujitathmini.

Ni jambo jema sana. Lazima uamshe bongo na hilo.
 
Back
Top Bottom