Uchaguzi 2020 Huyu siyo Abood ninayemjua. Huwezi kuwa mwema utotoni ukawa shetani uzeeni

Uchaguzi 2020 Huyu siyo Abood ninayemjua. Huwezi kuwa mwema utotoni ukawa shetani uzeeni

Sio kweli. Kwenye ukweli pasemwa, jamaa hakuna anaeweza kusimama nae na akashinda hapo morogoro. wananchi wanamkubali sana. Huwa anashinda kihalali kabisa bila zengwe.
Mimi Morogoro napajua. Huyu mzee hana lolote lile
 
Abood pesa zake za kupigia kampeni kahonga polisi na tume ili apite bila kupingwa sababu anajua hawezi shinda Morogoro
 
Tume na polisi washalamba Chao hawawezi kitema wakitolee wapi Ni lazima kuhakikisha mgombea apite bila kupingwa ili wasirudishe pesa
 
Huu uhuni wa Hawa wakurugenzi unabarikiwa na watz sababu hawajaamua kuwafundisha Hawa wahuni jinsi ya kusimamia vyema uchaguzi ili kuepusha uvunjifu.

Kuwanyima wananchi haki ya kuchagua wawakilishi wao huu ni uhuni.
 
Sasa kipi bora? Kuwagawia watu hizo riziki au kula peke yake? Alichifanya kawagia wenzie riziki ni uungwana pia.
 
Anakusaidieni kuzika
Huyu mzee hajawahi kuingia kwa sanduku la kura. Yeye ni mapingamizi, kuhonga na kununua. Hiyo ndiyo jadi yake, amezoea vya kunyonga sasa safari hii amekutana na kisiki.
 
Watz Kama tutawaacha Hawa wakurugenzi wahuni ndio watakaovuruga amani yetu ni vyema kuwadhibiti mapema kwa kuwalazimisha kutenda haki
 
Kumshinda Abood Morogoro mjini inahitajika ufanye zaidi ya kampeni zinazoonekana. Hata angeenda Lisu akagombee hawezi fika hata robo ya kura za huyu jamaa, ni nabii anayekubalika kwao anasaidia sana sana wanamorogoro. Kama anahonga tume mwambieni anaharibu tu pesa zake hakuna wa kumshinda labda CCM waje wafanye ujinga wa kumuengua. Huyu jamaa haongei sana bungeni ila jimboni kwake matendo yake yanaongeleka sana. Mimi sio mwanamorogoro ika nimekaa sana huko
 
CCM lao ni moja hata mgombea mkuu alijishindanisha mwenyewe akapitishwa kwa kura rundo..
 
Ukiruhusu kuwa na upinzani kwenye jimbo lako

1) Hata ukiwashinda, upinzani utaanza kupata nguvu pole pole. Awamu mbili za uchaguzi wawezajikuta huna chako. Hata kwenye uraisi. Kwa hiyo mtu hataki upinzani uzoeleke.

2) Kuna watu wanaweza kujieleza majukwaani na ushawishi kwenye kujieleza wakawafungua wananchi akili. Wanananchi wakajua wanastahili zaidi ya wanachokipata. Kwahiyo hataki wananchi wamsikie MTU mwingine.

3) Mtu anaweza akawa ana kashfa ambazo zinajulikana na wachache,mpinzani wako humchagulii cha kusema jukwaani. Kashfa zinawezaelezwa kwa mifano iliyoshiba mpaka ikaaminika.

Kuepuka yote hayo MTU anaona bora awe peke yake
 
Chama cha Mapinduzi kitapeleka wengi sana jehanamu kwenye moto wa milele.
Imeandikwa, ashirikianaye na mwovu au kuunyamazia uovu machoni pake hata kimbia hasira za Mungu.
Mkuu, acheni kulinganisha vitu vya kipumbavu na Mandiko matakatifu,

Ni lini Umeona vyama vinaleta wokovu?

Kwenye Chadema Wala Rushwa hawako? Majizi na majambazi yenye Nia mbaya na nchi Hayako huko?

Mfuate Kristo Yesu uwe na huo wokovu,
 
Ni bahati mbaya sana amejiunga kwenye genge la wachawi (CCM) hivyo hana budi bali kua mmoja wao. Hakuna mtu ataweza kujiunga na hilo genge la wachawi na washirikina la CCM linaloongozwa na misingi ya roho mbaya na ulafi halafu akabaki salama!
 
Back
Top Bottom