Ifike hatua, wanawake muwe na huruma dhidi yetu wanaume

Ifike hatua, wanawake muwe na huruma dhidi yetu wanaume

Ndiomana wengine unakuta yupo kama taahira kumbe keshalipuliwa huko!
Sometime akili sio zetu. Watu kibao wanaomba hadi misamaha kwa makosa yasiyo yao. Wengine wanasomesha kabisa ๐Ÿ˜…
 
Waganga wanawatapeli sana wanawake. Mlipulipu ni mti wenye asili ya kutambaa kama tu mpensheni. Ukikaushwa kisha kusangwa na kuwa unga unakuwa tayari kwa matumizi.
Unga wa mlipulipu ukiuchoma kwenye makaa ya moto au kwa kibiriti unalipuka kama baruti na inaaminika ukifanya manuizi kisha ukachoma mlipulipu jambo au adhima yako itatimia.
Hutumiwa sana kwenye katika kukinga mashamba, mji/nyumba kuhusu mapenzi sijawahi kusikia.
Sasa wanawake badala wautumie kulinda nyumba zao, wanatulipua sisi
 
unaacha kuogopa magonjwa ka hao mabinti watatu unaogopa kurogeka hii ni nchi yangu kwakweli
Magonjwa niyaogope vipi mkuu? Nilidhani yafaa kujikinga dhidi ya magonjwa, na sio kuyaogopa.
 
hayo umeyaskia machache huku uswahili utawao ea huruma me wanavyoinamishwa nimwendo wa shuntama tu[emoji28][emoji28]
 
Inabidi tu muanze kumtafuta Mungu aisee. Ukute na mama yako mzazi alishatangulia mbele za haki na hauna wa kukuombea! Hatari fire!
Hapa kwa mama kukuombea naunga mkono my mom mtu wa maombi na mara zote hua ananiombea. Kuna mambo hua nakutana nayo afu nachomoka hadi hua najiuliza imewezakanaje? Nabaki kumshukuru Mungu kwa kudra zake! Nani kama mama??
 
Muda mchache uliopita nimesikia mambo ambayo yamenistaajabisha sana. Nilienda salun kwa ajili ya kunyoa, kwavile palikuwa na foleni, nikawa nimekaa kwenye benchi nje, nachezea simu huku nasubiria zamu yangu ifike. Pale pembeni palikuwa na salun ya kike, yaliyokuwa yanazungumzwa humo ndio yaliniacha mdomo wazi.

Walikuwa wanapiga story za waganga na kuelekezana dawa.

Maongezi yao sasa "Shoga wala sio ngumu, ww unajifukiza dawa huku unanuiza tu, tena hakikisha unapata mlipu, huo mlipu ndio kiboko, unamlipua mlengwa wako popote alipo,chochote utakachoomba, lazima akutimizie"

Walitaja na dawa zingine kama 3 au 4 hivi, ambazo sikuzisikia vizuri.

Kiuhalisia, wanaume wengi hatuna Kinga yoyote, kwa Mungu hatupo, kwa waganga hatupo, hizi dawa kama zinafanyakazi kweli siwatatupa ukichaa? Imagine mabinti watatu kila mmoja aamue kukulipua??

Dah, kumbe ndio wamedhamiria kiasi hiki??
Wewe huna tofauti na hao wanawake,,
 
Ndio muache kuranda randa mtylue na wake zenu au mwenzi mmoja


Imagine una wanawake 5 wote wakulipue si utapata kichaa????
 
Back
Top Bottom