Ifikie hatua tuachiane nafasi

Ifikie hatua tuachiane nafasi

Sio mara ya kwanza nasikua hii kauli, Hivi mnaposemaga mnapenda mwanaume mwenye soko huwa mnamaanisha anae-chepuka au anatafutwa na wanawake wengine ila asichepuke kabisa ?

Mwanaume wa kuombaomba misamaha hatumtakii…. Kila kitu ninekosea wapi nisamehe tunaonaga ni kelele….kuna vikosa vidogovidogo hupaswi kutamka nisamehe na hata ukiomb usiwe unaulizauliza umenisamehee mwanaume una kazaaa[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Lejend, haya ni maneno tu ya karatasi. Mapenzi bila mawasiliano ya kila siku ni uongo, huyu huyu akiachwa siku nzima bila kutafutwa ataanza lawama.
..kuna wakati tunataka space ili tufanye uhuni tu sio kingine. Na uzee wangu bado napenda visms vya mahaba[emoji1787]

Tunapenda ila sasa sio kila dakika 15 ni sms halafu hakuna cha maana… mapenzi ya kumisiana ndio matamu

Ukipiga simu asubuhi… mchana tukichart na jioni usiku kuaganaaa kulala
 
Tunapenda ila sasa sio kila dakika 15 ni sms halafu hakuna cha maana… mapenzi ya kumisiana ndio matamu

Ukipiga simu asubuhi… mchana tukichart na jioni usiku kuaganaaa kulala
Unakutana na mwanaume anakutafuta mara moja kwa wiki, si hutaki kero mkuu!! Ukiona kutafutwa ni kero, ujue kuna namna hujapenda tu.
 
Mwanaume wa kuombaomba misamaha hatumtakii…. Kila kitu ninekosea wapi nisamehe tunaonaga ni kelele….kuna vikosa vidogovidogo hupaswi kutamka nisamehe na hata ukiomb usiwe unaulizauliza umenisamehee mwanaume una kazaaa[emoji23][emoji23][emoji23]
🤣
 
Kwa uzoefu wangu wa mahusiano nikijumlisha na ninayoona kwa mashostisto zangu na wafanyakazi wenzangu wa kiume ni kwambaaaa….
Mtu ukimchoka au ukiwa haumpendi simu zake huwa ni kero sanaa. Na kila saa lazima uwe busy kwake hata kama unachat na watu wengine ikiingia ya kwake unaipotezea. Hata kama upo online whatsapp unaview status za watu (maana yake haupo busy) text yake ikiingia ni kero tu hata kujibu.

Ila kwa mtu ambaye unampenda kweli na penzi ni la motoo hamna ubusy utakaofanya ushindwe kuwasiliana naye. Na hata ukiwa busy ule muda mdogo ukipata ukishika simu tu lazima uangalie kwanza kama alikutafuta. Ukikuta kakutafuta unafuraaaahi mwenyewe unamjibu ukikuta holaaa unanyong’onyea unamtafuta wewe.

Watu wapo sehemu mtandao unasumbua ila wanapanda hadi juu ya miti wa wasiliane na wapenzi wao. Ni suala la kumpenda mtu tu hakunaga ubusy tofauti na hapo ni UMALAYA unaona simu za kila saa zitakuharibia.
Kila mtu ana masaaa 24 ila mtu unayempenda hupewa priority kubwa hata akusumbue vipi haboi na wala hapoi .....kama akiwa busy atajua tu kulingana na schedule yenu
 
HuuKweli kabisa,,,yaani eti niwe na mpenzi hujui kaamkia wapi? anaendeleaje,ana ratiba gani, jamani hiyo sio maana ya mapenzi.....Mimi sikasiriki hata mara Moja nikipata simu ya nimpendae hata kidogo! kwanza napata zile feeling za Upendo.... anyway tumetofautiana
Hamna mtu ambaye hapendi kufanya hivyo ila je unayemfanyia hivyo amekushiba kiasi gani. Mtu kama hajakupenda vizuri lazma aone kero. Hata wewe kama mtu humfeel simu yake ni kero tu. Ila unayempenda asipokutafta lazma ujiskie vibaya ila akikucheki burudani ya nafsi 😀
 
Siyo unambanaaa, mpaka anakosa hamu ya mahusiano kabisa. Sawa upo nae lakini kuna muda anapaswa apate wakati wa kuwa peke yake. Kuna muda mtu anakuwa na mambo yake binafsi, mawazo yake binafsi na huwezi kutaka kilakitu chake ukijue. Kila mtu ana private yake (mtakataa ila ndiyo ukweli).

Sasa ndugu, dk 2 nyingi mara video call, simu muda wote, mara hujibu sms Kwa wakati😳 nyiee, tena bora kidogo mwanamke akichungwa kidogo (nimesema kidogo kwa sababu tuna majukumu pia hivyo isiwe too much) lakini si mwanaume. Waweza dhani ndo waimarisha penzi kumbe ndiyo wamkimbiza.

Haya sasa msije sema sijawaambia.
Hii ni shida ya kuolewa kabla hujawa tayari.

Umeolewa lakini bado unataka uishi kama bachelor? Ndoa ni kifungo.
 
Back
Top Bottom