Mimi ni whistleblower tu, ninalifanyia upelelezi maana wamekomba bosi mmoja milioni mia mbili. Wameanza kumpanga kuanzia mwaka 2021. Ila kumpigia rasmi wameanza 2023.Yaani viongozi wa jeshi waku pm?
Subiria huyo General tapeli aku pm mkamalizane huko
Sasa fikiria unadanganywa na mtu anayeamua kujiita waziri mkuu,na waziri mkuu unamjua,mkuu wa kulaumiwa sio wewe kweli???Huyo anajiita Generali Yani cheo baada ya Luteni Generali. Maana anadai mwaka Jana alikuwa Luteni Generali ila akapandishwa cheo kuwa Generali.
Ndugu sio kwamba sichukuliwi hatua hapana,shida watanikamataje???Habari, naomba nitoe taarifa kwa JWTZ ya kwamba Kuna mtu anajiita Generali Charles Mwamwega na kudanganya watu yeye ni makubwa jeshini na anafanya kazi kwenye ofisi ya Rais wa Zanzibar Ikulu. Ukienda pale ikulu Zanzibar hayupo mtu Kama huyo na ukienda kwenye data base ya JWTZ Hilo jina halipo kabisa, ukiachana na cheo Cha uongo Cha Generali ambacho ni kimoja tu kwa CDF.
Mpaka Sasa ameshatapeli watu wengi lakini hachukuliwi hatua yeyote. Maana Mimi najua Generali wa JWTZ ni mmoja inakuaje wawepo majenerali wawili?. Pia huyu Generali anatumia jina la Waziri Mkuu kuibia watu Magari pale bandarini. JWTZ ingilieni kati raia wanalizwa, wasaidieni.
Shida anayetapeliwa hataki kukubali kwamba anatapeliwa. Yeye anaamini kwamba huyo Generali Mwamwega yupo. Na Cha kushangaza hawajahi kuonana na huyo Generali Mwamwega. Wanaongea kwenye simu tu.Poleni. Sema hawa matapeli huwa wanaangalia IQ za watu wanaowaibia, kwa akili ya kawaida tu Generali anafanya nini bandarini mpaka kufikia hatua ya kutapeli magari?!!!
Mkuu niliwahi kuleta ushahidi hapa wote Hadi namba na majina halisi ya wahusika JF wkauotoa Uzi, Sasa Mimi nifanyeje?Jf ni jukwaa wazi, haikuwa na haja ya kuanzisha uzi bila kutoa ka ushahidi kadogo.
Humu tumefichua mengi na yametatuliwa.
Pm hata wewe unaweza kumwendea kwa id yoyote na ukajifanya kiongozi
Mkuu sio Mimi niliyetapeliwa , Mimi ni whistleblower. Kuna mtu Katapeliwa milioni mia mbili , na hao jamaa kwa kushirikiana na polisi waongo, wakamdanganya huyo bosi kuwa ana kesi ya utakatishaji fedha. Sasa jamaa anahangaika mpaka Leo anawalipa fedha ili wasimkamate. Kwa kifupi Tanzania Ina matapeli waliokubuhu. Wanaweza kukutengenezea scenario mpaka ikakubali. Ni stori ndefu siku Jamii forum wakikubali nitaiweka hapa.Ukipenda kitonga mjini lazima utapeliwe kilaini pia.
Matapeli ngome yao kuu ni njia za mkato na zisizofata sheria za nchi.
Hapa naona tu umemkosea heshima PM kwa swala dogo sana.
Sasa ikiwa mtu aliagiza kwa bf ameibiwaje? Je huyo jeneral ana kampuni ya clearing?Huyo bosi aliagiza gari kupitia befoward Toyota Hilux silver. Sasa huyo Generali Mwamwega akamuungiza kingi. Niliwahi kuleta ushahidi wote JF wakautoa.
Mkuu, Mimi ni whistleblower najaribu kumsaidia huyo bosi kiongozi. Niliwahi kuleta ushahidi hapa JF wakauondoa Uzi haraka.Mkuu, kama umeamua kufichua hili jambo basi nivyema ukaweka kilakitu wazi hapa pamoja na ushahidi ulionao.
Angalizo: Usipende sana mambo ya PM hasa unapo fichua mambo mazito kwa maslahi ya uma.
Punguza dharau Mimi na jeshi wapi na wapi. Mimi ni whistleblower najaribu kupaza sauti kuhusu huyu jamaa anayeharibu maisha ya watu. Kafilisi watu Kwa kesi za kuchonga na kuhack account zao ili kuwazulia kesi za utakatishaji fedha. I hope JWTZ wataingia kazini.Ukute uyo general mwenyewe kaomba laki 2 akuingize jeshini..sasa General aombe laki kwel
Mkuu niliwahi kuleta ushahidi hapa JF wakauzuia Uzi wangu. Sasa Mimi nifanye Nini. Najaribu kuokoa Jamii na Hawa matapeli wasiokuwa na huruma.Huyo Tapeli atakufuata PM na atakuumiza vibaya. Wewe wka kila kitu hapa ili wahusika wa-deal nae.
Mkuu Mimi sijatapeliwa Bali ni bosi kwenye moja ya taasisi kubwa. Kapigwa milioni mia mbili na kutengenezewa kesi ya utakatishaji fedha. Shida Sasa huyo bosi hakubali Kama anatapeliwa ndio shida.Pole mtoa mada, huo ndio ukubwa.
Kila wakati jeshi linatoa taarifa ya kuepukana na matapeli.
Mkuu Kuna watu hawaelewi Hilo. Wakishadanganywa tu wanakubali. Kuna watu hawajui hata mfumo wa jeshi upoje.Majenerali wako wengi sio mmoja,wanapishana tu ngazi.
Lakini hakuna utaratibu huo jeshini wa kushikwa mkono na jenerali kutoka ofisi ya rais.
Mkuu kwa unyama alioufanya kwa bosi nimeamini ni kwanini Kuna watu wanapotezwa bila kuonekana. Aisee Kuna watu hawana huruma wanahakikisha wanakukomba kila kitu bila wewe kushtuka na vitisho juu.Mkimkamata huyo mutu pigeni na kumtia dole gumba kwenye tigo yake.
Anapenda vya bure mwambieni aolewe mapema kabla sisi hatujamshika.
Inaonekana huyo Generali Mwamwega alitumia jina la Waziri Mkuu kumtapeli huyo bosi. Shida ya huyo bosi naye kichwani hazitoshi. Kila analoambiwa Wala hashtuki. Mtu anapigiwa simu anaambiwa una kesi ya utakatishaji naye anajaa na kuanza kulipa faini bila hata kuhoji. Huyo Generali Mwamwega kamshika kweli huyo bosi kamfanya mradi wake. Siku JF wakinikubalia nitatoa stori nzima hapa.Sasa fikiria unadanganywa na mtu anayeamua kujiita waziri mkuu,na waziri mkuu unamjua,mkuu wa kulaumiwa sio wewe kweli???