Uchaguzi 2020 IGP Simon Sirro akutana na Wadau wa Uchaguzi 2020, aitaja JamiiForums na Mitandao mingine kama changamoto ya Uhalifu wa Kimtandao sababu ya Teknolojia

Uchaguzi 2020 IGP Simon Sirro akutana na Wadau wa Uchaguzi 2020, aitaja JamiiForums na Mitandao mingine kama changamoto ya Uhalifu wa Kimtandao sababu ya Teknolojia

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869


Ikiwa imebaki miezi michache kufikia mwezi Oktoba, mwezi ambao uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 utafanyika nchini, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, Inspekta Jenerali, Simon Sirro, leo Agosti 19, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa vyama vya siasa, pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

-----
INSPEKTA JENERALI WA POLISI AWASILISHA MADA KATIKA MKUTANO WA TUME YA UCHAGUZI, VYAMA VYA SIASA NA WADAU WA UCHAGUZI NCHINI.

Inspekta Jenerali wa Polisi Simon Nyakoro Sirro ametoa mada leo tarehe 19.08.2020 kuhusu ulinzi na usalama katika mkutano uliofanyika ukumbi wa Julius Nyerere Convention Centre (JNICC) jijini Dar es Salaam ikiwa ni mikakati ya kuhakikisha amani na usalama vinatawala wakati wote wa kuchukua fomu kwa Wagombea, urejeshaji wa fomu, kampeni, upigaji kura, kuhesabu kura, kutangaza matokeo na kusherehekea ushindi.

Pia alizungumzia kuhusu hali ya uhalifu nchini, amesema hali ya uhalifu nchini imepungua kwa kiasi kikubwa sana na askari wamejiandaa vizuri sana kusimamia uchaguzi uliopo mbele yetu kwa kubaini makosa hata kabla hayajatokea na kumchukua hatua ikiwa pamoja na kuandaa mashtaka na kuwapeleka watuhumiwa mahakamani kwa mujibu wa sheria.

Makosa hayo ambayo yamekuwa yanajitokeza ni makosa ya mitandao ya kijamii kama Jamii Forum, Facebook, Instagram, twitter, Blogs na Whatsapp.

Aidha Katika mada hiyo Inspekta Jenerali wa Polisi alihitimisha kwa kusema amani ni muhimu kwa mustakabali wa nchi yetu hivyo viongozi wa vyama vya siasa kufuata sheria za uchaguzi na tume ya uchaguzi kuweka taratibu zote za uchaguzi mapema ili kuondoa mapungufu yanayoweza kuleta taharuki.

Alisema viongozi wa siasa watapita lakini nchi itabaki kama nchi, pia Hasira huondoa busara na ukitaka kufa tafuta njia nyingine ya kufa na si kutumia siasa.

Mwisho tumejipanga vizuri kutoa ulinzi kwa wahombea na wagombea wenza kwa wagombea wote watakaopitishwa na Tume ya Uchaguzi.
 
..huyu Afande kuna HILA anazifanya dhidi ya CDM.

..matamshi yake yanaonyesha ana CHUKI / KISASI dhidi ya CDM.

..CDM wanapaswa kuwa makini sana na michezo michafu inayopangwa dhidi yao.

NB:

..IGP siyo mtoto wa sekondari asiyejua nini cha kipi kinafaa, na kipi hakifai, kuwa ktk presentation sensitive kama ile.
 
Huyo Sirro anajulikana wazi matamko yake mengi anayoyatoa huwa yanalenga kumfurahisha bosi wake, hapo hata sioni kipi cha maana atachoongea.

Wale wanaochoma moto ofisi za Chadema kila siku hata hatumsikii akikemea vile vitendo, yupo tu.
 
Siro anaharibiwa na viongozi wa ccm.Kule tunduma polis wanatengeza mazingira ya kuwakasirisha wananchi.Chadema wamwambie siro awaagize polis kufuata sheria, siasa awaachie wanasiasa.
 
Igp kakosea kutoa documentary moja, alipaswa kuleta documentary za vyama mbalimba ikiwemo ile ya ccm ya yule kiongozi was iringa aliyesema viongozi wa upinzani wauawe.Polis mnapaswa kuwa impartial kwa vyama vyote.
 
Hapa angegusia kwamba mamlaka ya Rais kuzuia mikutano ya hadhara ya kisasa ambayo katiba na sheria za nchi inaruhusu kwa miaka mitano - Je hayo mamlaka kayapata kutoka wapi?
 
..huyu Afande kuna HILA anazifanya dhidi ya CDM.

..matamshi yake yanaonyesha ana CHUKI / KISASI dhidi ya CDM.

..CDM wanapaswa kuwa makini sana na michezo michafu inayopangwa dhidi yao.

NB:

..IGP siyo mtoto wa sekondari asiyejua nini cha kipi kinafaa, na kipi hakifai, kuwa ktk presentation sensitive kama ile.

Ndiyo maana tunamleta hapa mahakama ya wananchi wajadili muenendo wake.

Nimeona hata Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi akamuhoji IGP ana maana gani na aina yake ya uwasilishaji hoja.

IGP ikabidi ajiumeume na kuomba radhi kama ameeleweka 'vibaya' na kukwaza hadhira iliyopo ukumbini.

Sasa tumemleta katika hadhira kubwa zaidi huku kwa wananchi nao watoe maoni yao.
 
Huyo IGP ni mchekeshaji wa mfalme. Kila anachoongea ni kile alichoagizwa na jiwe, na yeye anakitapika hivyo hivyo.
 
Back
Top Bottom