IGP Sirro, huyo ni mtoto wa nani?

IGP Sirro, huyo ni mtoto wa nani?

Huyo ni Mtoto wa Sirro anasumbua watu sana mtaani kwa ubabe wake na anavuta bangi hadharani. Muda Mwingi anashinda Chanika kwenye Bar ya Baba yake.
Huyo kijana nilikutana naye kwenye bar ya Siro huko Makongo - DTV. Ni takataka zaidi ya takataka.
 
Naona anazidi kupalilia chuki na visasi zaidi kwa Ndugu zake na Jamaa wa Hamza! Ipo siku watamjibu kwa vitendo kwa hii kauli yake
 
that makes sense....siyo bar
Screenshot_2021-08-30-10-54-53-1.png

Ni muwekezaji mkubwa tu aisee na mimi namkubali sana huyu jamaa amewekeza pesa bongo na kaajiri nduguzetu sio kama wengine wanaowekeza ulaya

Ila kwenye kauli ya kulaumu wazazi ndo nahisi amepotoka

Kuna msemo ule kwamba Ukiwa na hasira sana au furaha sana usiongee sana/usitoe ahadi. Kwak maneno yako yatakua clouded na hisia

Nahisi alikua na hasira sana vijana wake kuuwawa
 
Unashangaa nini? Huyu kila mkoa anajengewa nyumba na ma rpc na rto
Glenn umenikumbusha kitu. Kuna IGP mmoja alimuambia RPC mmoja huko mikoani amtafutie mbao za kujengea gesti zake. Kweli RPC alikusanya mbao za kujaza Lori Zima. Mbao zilipotimia RPC akamrukia IGP hewani na kumtaarifu kwamba mbao ziko tayari hivyo IGP atume hela ya kununulia mbao na pesa ya usafiri.
IGP baada ya kuona kamanda ana akili ya ndezi alichofanya ni kumrudisha huyo ndezi makao makuu na kupeleka kijana mwenye nidhamu ya uoga kule.
Ndezi hakukua kwamba IGP akikuomba kitu inabidi utumie uwezo wako kuchangishana na majambazi ili hela ipatikane mzigo ufike.
 
Sio hajaja mjini akiwa mlinzi kulinda bank n wakubwa zake,lenana imejengwa miaka ya tisini...siro akiwa hana cheo
Vitu huwa vinauzwa mkuu.je unajua nyumba ya lenana ya bwiru aliiuza kipindi anataka kujenga ilo gholofa la kwanza?.lakin watu bado nyumba yake wanaoaita kwa lenana.nenda mj jiran na ms ameipangisha kwa miaka 20 ila watu wanajua niya mzee ulasa ndio anaiendesha.hata lenana inaweza kuwa imeuzwa maana kunakipindi aliyumba sana wakati wa magu.hvyo hatuwezi jua
 
IGP Sirro jana umetoa kauli nzito na ngumu mno kutolewa na kiongozi wa aina yako na mtu mwenye umri mkubwa kama wewe na mtu anayeheshimika kwa cheo chake kama wewe.

Angalia sana ulimi wako jinsi unenavyo, muombe sana Mungu akupe hekima ili kabla ya kutamka neno lolote hekima ikutangulie.

Jana ulitamka maneno haya nami nakunukuu.

"Watanzania kuweni makini msije mkazaa mtoto wa hovyo hovyo kama Hamza aliyetuletea majanga Watanzania, wazazi wa Hamza mnajisikiaje kuzaa mtoto kama huyo? Na nyie ndugu zake mnajisikiaje kuwa na ndugu kama Hamza?". Mwisho wa kunukuu.

IGP Sirro, hakuna mzazi anayepanga azae mtoto wa aina gani, Binadamu tunazaa mwili hatuzai Roho.

Kuna kijana anasumbua sana mitaani, anajitapa kwamba hakuna wa kumfanya lolote kwa sababu Baba yake ana cheo kikubwa mno serikarini, kijana huyo huvuta unga na kwenda hadi kwenye Hotel ya Baba yake iliyoko Chanika ambako hufanya vituko vya ajabu, ukiwemo kupiga watu.

Je, unajua huyo mtoto ni wa nani? Tafadhali sana, wazazi wa Hamza hawakujua kama wanazaa mtoto wa aina gani, hata wazazi wako wewe Sirro hawakujua kama ipo siku utakuja kuwa IGP.

JITOKEZE UIOMBE MSAMAHA FAMILIA YA HAMZA ILI ULINDE HESHIMA YAKO.
Ni aibu tupu na dharau kubwa mno kwa familia na Wazazi wote wenye watoto Tanzania. Hamza kazaliwa na Baba na Mama yake, kama yeye alivyozaliwa na Baba na Mama yake?

Yaani leo, unatoa kauli ya kuhoji uumbaji wa MUNGU? Sawa, amekula, ameshiba na sasa anasaza....subiri wamuone Mungu ni nani....Nenda Misri kawaulize MUNGU ni nani watakwambia.
 
Kamanda Sirro huyu huyu aliyesoma Tosamaganga. Sina hakika sana kama lenana ni ya kwake ila mzee kajitahidi kuwekeza sana katika lodges na bar na aliona mbali kufungua kiwanda cha kuzalisha unga kinachoitwa musoma food ambacho kipo shinyanga.

ila kwa watoto tu, mzee kazaa watoto wake ni watukutu walevi na wanapenda sifa mno kwa cheo cha baba yao.
Nani kakudanganya kiwanda cha musoma food nicha siro.hcho kiwanda nicha musoma food mwenyewe alikuwa na kaka yake alipofaliki ndio akakiendeleza mpaka kufikia hapo.acheni uongo.mwenyenacho anaitwa said.
 
Glenn umenikumbusha kitu. Kuna IGP mmoja alimuambia RPC mmoja huko mikoani amtafutie mbao za kujengea gesti zake. Kweli RPC alikusanya mbao za kujaza Lori Zima. Mbao zilipotimia RPC akamrukia IGP hewani na kumtaarifu kwamba mbao ziko tayari hivyo IGP atume hela ya kununulia mbao na pesa ya usafiri.
IGP baada ya kuona kamanda ana akili ya ndezi alichofanya ni kumrudisha huyo ndezi makao makuu na kupeleka kijana mwenye nidhamu ya uoga kule.
Ndezi hakukua kwamba IGP akikuomba kitu inabidi utumie uwezo wako kuchangishana na majambazi ili hela ipatikane mzigo ufike.
Mkuu acha tu kwa taarifa yako panga pangua huwa ni kuweka watu wenye mkono mrefu.
Mambosasa aliondoka kwa machozi Dar, siku anaaga alikuwa dhaifu sana. Alikuwa ni mkono wa mzee kwa hapa dar ndio maana kulikuwa ma uhalifu mwingi lkn mzee alikuwa haoni sababu kumwondoa hadi rais alipoingilia kati..
Kwa uthibitisho sasa amerudishwa dar kwa mgongo wa kuwa mkuu wa chuo.
Unajua kilichomkuta Mamboleo Dodoma?
Alipopelekwa alijikuta anakuwa chini ya mtu aliyemwondoa Dar kwa hila na aibu ili yeye ale matunda ya mama Dar.
Akamlilia mzee kuwa kumbuka siku za dar nilivyokutii niondoe hapa baba[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nani kakudanganya kiwanda cha musoma food nicha siro.hcho kiwanda nicha musoma food mwenyewe alikuwa na kaka yake alipofaliki ndio akakiendeleza mpaka kufikia hapo.acheni uongo.mwenyenacho anaitwa said.
Unaweza niambia ni nani yuko nyuma ya umliki wa GSM?
 
Nani kakudanganya kiwanda cha musoma food nicha siro.hcho kiwanda nicha musoma food mwenyewe alikuwa na kaka yake alipofaliki ndio akakiendeleza mpaka kufikia hapo.acheni uongo.mwenyenacho anaitwa said.
Musoma food Ni ya kitambo tangu jamaa ana ofisi inaitwa musoma battery.,Sirro Hana hata 0% ya shares pale.
 
Mkuu acha tu kwa taarifa yako panga pangua huwa ni kuweka watu wenye mkono mrefu.
Mambosasa aliondoka kwa machozi Dar, siku anaaga alikuwa dhaifu sana. Alikuwa ni mkono wa mzee kwa hapa dar ndio maana kulikuwa ma uhalifu mwingi lkn mzee alikuwa haoni sababu kumwondoa hadi rais alipoingilia kati..
Kwa uthibitisho sasa amerudishwa dar kwa mgongo wa kuwa mkuu wa chuo.
Unajua kilichomkuta Mamboleo Dodoma?
Alipopelekwa alijikuta anakuwa chini ya mtu aliyemwondoa Dar kwa hila na aibu ili yeye ale matunda ya mama Dar.
Akamlilia mzee kuwa kumbuka siku za dar nilivyokutii niondoe hapa baba[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Duh. Kumbe mamboleo Yuko mjini?
Nadhani atastaafu kabla ya umri.
Sijui anamuangaliaje mhindi aliyemvisha Dera.
I always say
Karma is real
 
Nilichojifunza ukiwa kiongozi mkubwa inabidi kuchagua maneno ya kuongea public. Ukicheki kwa jicho la 3[emoji102] igp Sirro , kimwili yupo na mama lakini kiroho hayupo naye
 
Back
Top Bottom