Ijue Historia ya Firauni na uongo aliozushiwa

Ijue Historia ya Firauni na uongo aliozushiwa

Wewe huyo Pharaoh ushawahi kumuona hadi useme babu yako?!
Evidence za mummies za mafarao ndo zinathibitisha hilo mzee, Kuna mummies kibao pale Giza tembea uone, we unaweza kunionyesha mummies ya hao unaowataja, ili twende tukapate proof maabara?
 
Tuna kazi ya kuamsha ndugu zetu hawa wamelala fofofo bila shaka!
Na bila ya ukombozi wa kiutamaduni na kujitambua, maendeleo ya kiuchumi na kijamii Africa tusahau kabisa. Lazima tujikomboe, mapigano ya kifikra lazima yaimarishwe. Mi sijui hata hawa wa utamaduni wana majukumu yapi, eti utalii.

Chinese, Indians wote wamejitambua ndo kisa cha kusonga kwao. Utumwa wa ubongoni ni mbaya zaidi kuliko mwingine wote. Wazungu wanautumia kututawala kiuchumi, kiteknolojia,kisiasa na kijamii.

Sukuma legal system ni bora sana kwa Afrika na inakisi sana uafrika wetu kuliko common law legal system, hata sijui tunashindwaje. Afrika tunauushi utumwa saana.
 
Mnaemuita firauni ni babu yenu, wa asili! alikuwa ni Mweusi tii!! jina lake aliitwa Mkuu Ramesses wa II!

Nimekuwa nikiona habari kutoka kwa watu, kuwa mwili wa Ramesses ll huwa ukizikwa, unarudi juu kesho yake!!![emoji4][emoji5][emoji5]

Hivi hili linawezekanaje!! tena watu wenye akili timamu kabisa wanaamini hili! wenye Degree na PHD!! Kwa kweli ni maajabu makubwa mno haya! hapa utaamini kuwa Binadamu ni dhaifu sana kwenye imani!, na ni rahisi sana kumteka mtu yoyote akili kwa kutumia kivuli cha Dini/Imani..

Leo hii kitabu chochote kitakatifu kingesema Kuiba si dhambi na mtu ili ufike mbinguni ni lazima uwe mwizi, basi tungeshuhudia watu wengi wasomi na wasio wasomi wakiwa ni wevi!! Yote ni kwa sababu binadamu wengi zaidi ni weak mno kwenye Imani!

Turudi kwenye maada.

Great ramesses ll alizikwaje?

Mwanzo alizikwa kwenye kaburi KV7 katika Bonde la Wafalme, lakini kwa sababu ya uporaji wa vitu vya thamani alivyokuwa amevishwa, makuhani walihamisha mwili kutoka eneo hilo na kuupeleka ndani ya kaburi la malkia Inhapy.

Miaka mingi baadae waliuhamishia tena mwili kwenye kaburi la kuhani mkuu Pinudjem II. Yote hii ni sababu ya kumbukumbu katika hieroglyphics.
Kutokana na matetemeko yaliyoikumba Giza miaka kati ya miaka 1000 AD hadi 1500 AD vitu vingi vilipotea huku baadhi ya masanamu mengi yakiharibiwa vibaya na matetemeko hayo, na baadhi ya makaburi, majumba, na makumbusho mengine kupotea kabisa!
Huku mwili Wa Great Ramesses ll Nao ukipotea katika matetemeko hayo.

Mwanzoni mwa miaka ya 1800, mwili huu ulipatikana tena pembezoni kidogo mwa Red sea.

Ramesses ll, hakufa kwenye Gharika la Mussa kama watu wanavyodai, mwili wake hadi sasa unathibitisha kuwa alikufa akiwa mzee, zaidi ya miaka 80 kwa maradhi ya kawaida.

Pia si mwili wa ramesses ll tu uliopo kwenye makumbusho ya misri, ni miili mingi ya Mapharao tofauti na baadhi ya watu walioishi kwenye Egypt ya kale.

View attachment 463571
MWILI WA PHARAO RAMESSES ll / Firauni Uliopo kwenye maonyesho ya Ancient Egypt.
View attachment 463572
SANAMU YA GREAT RAMESSES II ILIYOPO GIZA EGYPT

Nawasilisha
Secret Star
Kaka nimesoma andiko lako vizuri mno.Na nimeona mapungufu yafuatayo.

1.Hujaonyesha ushahidi wa kutosha ya kuwa ni kweli firauni hakufa katika gharika lililotokea wakati wa Musa alayhi salaam.Kwa kuwasingizia wale wenye kuamini hivyo ya kuwa wanadai tu na si wa kweli au hawana uhakika juu ya hilo.Kanuni za ujibuji wa hoja ni kuwa wewe mwenye kukanusha jambo hutangulizwa sababu unaonekana una elimu ya ziada juu ya jambo husika.Cha kusikitisha umeshindwa kulithibitisha hilo.

2. Jambo la pili ni kuhusu umri.Imekuja katika historia ya kuwa watu wa kale walikuwa wanaishi mpaka zaidi ya miaka 900,huo nimetoa mfano wa kukuzindua juu ya uhakiki wa habari za kihistoria. Kila zama zilikuwa na tabia kadiri ambavyo Mola aliye juu amepanga.Kwanza huwezi kunithibitishia ya kuwa Firauni alikufa akiwa na miaka 80.
Je unaweza kunithibitishia ya kuwa kwa umri umati za zamani mtu mwenye miaka 80 ni mzee ?

3.Unaonekana ya kuwa,kutokana na uelewa wenye imanai za dini huwa wanafata vitu kibubuswa yaani kichwa mchunga,kama una amini hivyo unakosea sana.Mathalani uma huu sisi huwa tunauita umma wa Muhammad,ni kuwa wastani wa kuishi ni miaka 70.Jua ya kuwa na umati zilizopita zilikuwa zina makadirio yao ya kuishi.Hapa nimekupa faida tu.

4.Pia kuwa na shahada,shahada ya uzamili au shahada ya uzamivu,si kipimo cha mtu kuwa na upeo wa juu kabisa wa kuhoji mambo au kung'amua mambo.Mawazo haya si sahihi.Mola wetu muadilifu sana,wapo watu hata hawajaenda huko kwenye usekula lakini wanang'amua mambo kwa upeo wa juu zaidi.
 
Mimi niliyeukubali Uafrika wangu na nyie ambao mara mjinasibishe na Wayahudi mara mjinasibishe na akina Farao; ni kati yetu anayestahili kuitwa nyani?! Ni nani kati yetu anayejidharau?! Unaona ulivyo na akili za kitumwa?! Kumbe kutokuwa tayari kujinasibisha na akina Farao ni sawa na kuwa takataka! Na ili usiwe takataka ndio maana hamuishi kujinasibisha na akina Farao na Wayahudi?! Halafu ona unavyotoa mifano irrelevant! Sasa hao Wachina wamejinasibisha na Mafarao?!

Mtu kama mimi ninayekubali Uafrika wangu bila kujinasibisha na yeyote siwezi kujisikia takataka lakini wewe unaeamini eti Farao huenda alikuwa babu yako ndie unayejiona takataka cuz' you can't stand on your own!

Badala ya kunyesha mapovu; jibu hoja!
Hapana, ninyi nyote mko na msimamo mmoja ila njia tu nitofauti. Hajasema sisi ni akina Farao, bali Farao alikuwa mweusi na alifanya yaliyo makuu. Hapa anawaamsha weusi wajionao hawawezi kwakuwa tu ni weusi.
 
Inawezekana alikuwa mtu mwema ila hizi dini zinatudanganya! asili haibadiliki Waisrael hadi leo tabia zao ni mbovu mbovu! lazima hata mababu zao nao walikuwa hivihivi!
Kwanini huwa hamsemi vitu mkiwa na uhakika navyo.Huku mkatanguliza "mimi nadhani.." mara "Inawezekana..." mara "Nafikiri...".Matamko haya huonyesha dalili ya kukata tamaa katika kuutafuta ukweli wa jambo fulani hasa jambo hili la kielimu.Kama kitu hukijui bora kunyamaza kuliko kudhani dhani....
 
Kaka nimesoma andiko lako vizuri mno.Na nimeona mapungufu yafuatayo.

1.Hujaonyesha ushahidi wa kutosha ya kuwa ni kweli firauni hakufa katika gharika lililotokea wakati wa Musa alayhi salaam.Kwa kuwasingizia wale wenye kuamini hivyo ya kuwa wanadai tu na si wa kweli au hawana uhakika juu ya hilo.Kanuni za ujibuji wa hoja ni kuwa wewe mwenye kukanusha jambo hutangulizwa sababu unaonekana una elimu ya ziada juu ya jambo husika.Cha kusikitisha umeshindwa kulithibitisha hilo.

2. Jambo la pili ni kuhusu umri.Imekuja katika historia ya kuwa watu wa kale walikuwa wanaishi mpaka zaidi ya miaka 900,huo nimetoa mfano wa kukuzindua juu ya uhakiki wa habari za kihistoria. Kila zama zilikuwa na tabia kadiri ambavyo Mola aliye juu amepanga.Kwanza huwezi kunithibitishia ya kuwa Firauni alikufa akiwa na miaka 80.
Je unaweza kunithibitishia ya kuwa kwa umri umati za zamani mtu mwenye miaka 80 ni mzee ?

3.Unaonekana ya kuwa,kutokana na uelewa wenye imanai za dini huwa wanafata vitu kibubuswa yaani kichwa mchunga,kama una amini hivyo unakosea sana.Mathalani uma huu sisi huwa tunauita umma wa Muhammad,ni kuwa wastani wa kuishi ni miaka 70.Jua ya kuwa na umati zilizopita zilikuwa zina makadirio yao ya kuishi.Hapa nimekupa faida tu.

4.Pia kuwa na shahada,shahada ya uzamili au shahada ya uzamivu,si kipimo cha mtu kuwa na upeo wa juu kabisa wa kuhoji mambo au kung'amua mambo.Mawazo haya si sahihi.Mola wetu muadilifu sana,wapo watu hata hawajaenda huko kwenye usekula lakini wanang'amua mambo kwa upeo wa juu zaidi.
Mi nimsaidie kujibu hoja moja tu juu ya umri, kwanza mafarao si watu wakale wa kuishi miaka hiyo 900, kiimani Musa aliishi miaka kama 3500 tu iliyopita. Mke wa Ibrahimu, miaka mingi kabla ya akina Musa, alipata ujauzito wa Isiaka uzeeni, ni miaka yake ya 80s. Sijui nimelijibu.
 
Nimesikia hadithi nyingi kutoka kwa wazee mbalimbali, lakini sijapata kuisikia inayozungumzia maisha ya Misri ya kale. Natambua kuwa Waafrika hatuna fasihi andishi bali fasihi simulizi tunayo. Kukosa masimulizi ya Maisha ya Misri japo inayofanana kuna maanisha historia hiyo siyo ya kwetu, imebuniwa tu.
 
Na bila ya ukombozi wa kiutamaduni na kujitambua, maendeleo ya kiuchumi na kijamii Africa tusahau kabisa. Lazima tujikomboe, mapigano ya kifikra lazima yaimarishwe. Mi sijui hata hawa wa utamaduni wana majukumu yapi, eti utalii.

Chinese, Indians wote wamejitambua ndo kisa cha kusonga kwao. Utumwa wa ubongoni ni mbaya zaidi kuliko mwingine wote. Wazungu wanautumia kututawala kiuchumi, kiteknolojia,kisiasa na kijamii.

Sukuma legal system ni bora sana kwa Afrika na inakisi sana uafrika wetu kuliko common law legal system, hata sijui tunashindwaje. Afrika tunauushi utumwa saana.
Aisee umeongea jambo kuu mno.
 
Watu weusi tuna taabu!! Tusipojiegesha kwa Wayahudi utasikia Misri ya Kale tulikuwa sisi!!

Tulivyo maboya, upande mwingine tunaamini sisi ni watoto wa Ibrahim! Na kuhitimisha uboya kama sio ukila.za wetu hapo hapo tunakubali, Ishmael ni mtoto wa Ibrahim na huyu Ishmael mama ake alitokea Misri! Na kutokana na unduze huo huo tulionao tunakubali Ishmael ndie chimbuko la Waarabu-- kwamba mtoto wa mama Mmisri ndie chimbuko la Waarabu na hivyo kuwa na uwezekano mkubwa kwamba mama ake Ishmael nae alikuwa Mwarabu wa Misri!

Sasa hao Waarabu walienda wapi hadi Misri ikageuka kuwa ya Wamatumbi akina Firauni?! Mbona hawa Wamatumbi hatusikii kwamba ndio wanadamu wa kale nchi jirani na Misri?!

Miafrika bhana... kusikia Wayahudi eti ma-genius na yenyewe inataka kujinasibisha na Wayahudi! Kusikia Mzungu na jeuri yake yote hadi leo hafahamu mapiramidi yalijengwaje... Wamatumbi hao; kama mkojo wa asubuhi kwamba eti mapiramidi yalijengwa na mababu zao!!

Ajabu ni kwamba, hawafananii na chochote na hao kimaarifa! Japo miaka elfu kadhaa ishapita, ndo kwanza wengine tunajiita Tanzania ya Viwanda lakini viwanda vyenyewe ni vile ambavyo Ulaya vilikuwepo miaka 500 iliyopita!
Wewe utakuwa mwarabu koko.
 
Kwanini huwa hamsemi vitu mkiwa na uhakika navyo.Huku mkatanguliza "mimi nadhani.." mara "Inawezekana..." mara "Nafikiri...".Matamko haya huonyesha dalili ya kukata tamaa katika kuutafuta ukweli wa jambo fulani hasa jambo hili la kielimu.Kama kitu hukijui bora kunyamaza kuliko kudhani dhani....
Kitabu cha dini unayoiamini kilitokea wapi? na kama hukuona kilikotokea, ni una uhakika ama unadhani? Nini maana ya Mungu kukupa Macho?
 
Nimesikia hadithi nyingi kutoka kwa wazee mbalimbali, lakini sijapata kuisikia inayozungumzia maisha ya Misri ya kale. Natambua kuwa Waafrika hatuna fasihi andishi bali fasihi simulizi tunayo. Kukosa masimulizi ya Maisha ya Misri japo inayofanana kuna maanisha historia hiyo siyo ya kwetu, imebuniwa tu.
Historia ya Misri ni fasihi andishi, imeandikwa Kwenye mapyramid na matempo kule Giza, Mabavu hao wa kale waliangalia mbali sana na ndiyo maana waliandika, na kuchora michoro ili wenye vichwa vigumu waone picha, hivyo picha na maandishi mengi, vimetawala kwenye pyramid na temple vya misri. Ile si fasihi simulizi!
 
Watu weusi tuna taabu!! Tusipojiegesha kwa Wayahudi utasikia Misri ya Kale tulikuwa sisi!!

Tulivyo maboya, upande mwingine tunaamini sisi ni watoto wa Ibrahim! Na kuhitimisha uboya kama sio ukila.za wetu hapo hapo tunakubali, Ishmael ni mtoto wa Ibrahim na huyu Ishmael mama ake alitokea Misri! Na kutokana na unduze huo huo tulionao tunakubali Ishmael ndie chimbuko la Waarabu-- kwamba mtoto wa mama Mmisri ndie chimbuko la Waarabu na hivyo kuwa na uwezekano mkubwa kwamba mama ake Ishmael nae alikuwa Mwarabu wa Misri!

Sasa hao Waarabu walienda wapi hadi Misri ikageuka kuwa ya Wamatumbi akina Firauni?! Mbona hawa Wamatumbi hatusikii kwamba ndio wanadamu wa kale nchi jirani na Misri?!

Miafrika bhana... kusikia Wayahudi eti ma-genius na yenyewe inataka kujinasibisha na Wayahudi! Kusikia Mzungu na jeuri yake yote hadi leo hafahamu mapiramidi yalijengwaje... Wamatumbi hao; kama mkojo wa asubuhi kwamba eti mapiramidi yalijengwa na mababu zao!!

Ajabu ni kwamba, hawafananii na chochote na hao kimaarifa! Japo miaka elfu kadhaa ishapita, ndo kwanza wengine tunajiita Tanzania ya Viwanda lakini viwanda vyenyewe ni vile ambavyo Ulaya vilikuwepo miaka 500 iliyopita!
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji115] mbavu zangu zafwaaaa
 
Mimi niliyeukubali Uafrika wangu na nyie ambao mara mjinasibishe na Wayahudi mara mjinasibishe na akina Farao; ni kati yetu anayestahili kuitwa nyani?! Ni nani kati yetu anayejidharau?! Unaona ulivyo na akili za kitumwa?! Kumbe kutokuwa tayari kujinasibisha na akina Farao ni sawa na kuwa takataka! Na ili usiwe takataka ndio maana hamuishi kujinasibisha na akina Farao na Wayahudi?! Halafu ona unavyotoa mifano irrelevant! Sasa hao Wachina wamejinasibisha na Mafarao?!

Mtu kama mimi ninayekubali Uafrika wangu bila kujinasibisha na yeyote siwezi kujisikia takataka lakini wewe unaeamini eti Farao huenda alikuwa babu yako ndie unayejiona takataka cuz' you can't stand on your own!

Badala ya kunyesha mapovu; jibu hoja!
Naam umenena mkuu
 
Back
Top Bottom