Ijue KADCO, kampuni hewa iliyokuwa ikiendesha uwanja wa ndege wa Kilimanjaro International Airport

Man, let's face it. Hakuna Mystery hapo.

Serikali inayo majibu yote. Ni vile hakuna anayeweza kuilazimisha serikali itoe majibu yanayoeleweka. Hakuna wa kuiwajibisha.

Nchi yetu ina aina ya watu wa kugawana vipande.Mimi nile huku, nyie kuleni huko. Tusifuatiliane! Muda ukifika mambo yakabuma, kila mtu hajui kitu.

What a Sad Country?

Imagine, mkataba upo na umesainiwa lakini maelezo mengine hakuna! Hakuna taarifa za aliyesainisha mkataba ni nani? Aliyeandaa huo mkataba na kuupitisha ni nani? Kwanini mapato yalikua hayaendi serikalini? Au kama mapato yalikua yanatumwa lakini hayafiki, aliyekua anayachukua kihuni ni nani?

Ni kwanini sintofahamu itokee after f*cking two decades and a half? Hiyo miaka mingine watendaji walikua wamelala ndio wameamka this November au?

Hakuna mystery hapo. Airport inatafutiwa Angle nyingine ya kupigwa for next decades.

Mjiandae pia na mystery ya Bandari 25 yrs later
 
๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…Hatari sana
 
Wanaitafutia mwekezaji Mwarabu
Kwanza tuliambiwa dipiworld wamechukua.
Mbarawa ametuona wajinga amaโ€ฆ
Serikali iwawajibishe wahusika sio story tu kila siku
KIA apewe wenye KLM na SWISS Air tutakuwa tume overtake jirani zetu
 
Hapo hujanisaidia kuijua hiyo Kampuni maana Lugha ni kikwazo
 
Yaani shetani yuleyule wa miaka yote anaendelea kuwakamata viongozi wetu na kuwatumia kuharibu na kuumiza wananchi na nchi...

Angalieni, huyu mama (Rais Samia Suluhu Hassan) naye keshamvaa shetani huyo huyo na keshaingizwa mkenge na yeye mwenyewe kwa mkono wake kusaini mkataba hatari na angamizi na kampuni ya waarabu iitwayo DP World...

USHAURI:

Wandugu, haya mambo hayako kama tunavyoyaona Kwa macho ya damu na mwili huu tulionao. It's beyond that..

Hii kitu haiwezi kukoma unless nguvu kuu inayozidi ile iliyowashika viongozi na watawala wetu itachukua nafasi yake..

Ni Rahisi tu. Zingatieni haya๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

1. Kila mwana wa nchi hii mwenye mapenzi na nchi yake, na anayeamini kuwa yupo Mungu aliye hai aliyetupa nchi hii kuwa urithi wetu na vizazi vyetu, basi aombe kwa lugha yake ili kuruhusu mkono wa Mungu wetu aliye hai uwe juu ya nguvu hii ya uharibifu inayowatawala na kuwaongoza viongozi wetu kufanya maamuzi hatari na angamizi kwa nchi yetu..

2. Kila mwana wa nchi hii anayeamini katika nguvu na mamlaka iliyo kuu zaidi (yaani Mungu - Yehova katika Yesu Kristo) akiombee KITI CHA U - RAIS wa nchi yetu. Katika kiti cha u - Rais wa nchi yetu ndipo ambapo chanzo (source) ya maamuzi yote ya nchi na taifa hili la Tanzania yawe mabaya au mazuri yanapotoka...

Na kwa jinsi ilivyo sasa, ni wazi kuwa nguvu ya MKUU WA MAPEPO na WACHAWI ndiye inayekimiliki na kukitawala kiti hicho. Yeyote anayekikalia hata awe msafi namna gani, hata awe na makusudi na malengo mazuri kiasi gani juu ya nchi yetu wakati anaingia, lakini mara akikaliapo kiti hicho kama nguvu hana iliyo kuu kuliko inayokitawala kiti hicho, Rais huyo lazima ata - compromise na matakwa na miongozo ya ubaya ya yule mwenye nguvu mchawi mkuu - shetani anayekimiliki kiti hicho...

Wakati mwingine nguvu hii ya kishetani na kichawi, huchagua yenyewe mtu wa kuja kukikalia kiti hicho kuanzia ktk hatua za michakato ya uchaguzi...

Nguvu hii ndiyo inayodhibiti mifumo ya kisiasa na kiutawala ya nchi yetu ili ibaki kama ilivyo na ubovu wake pasipo kuruhusu mwanya wa mtu anayemjua Mungu na anayejua siri ya utendaji kazi wa nguvu za kipepo na kichawi zinavyofanya kazi ktk tawala za nchi kuchukua uongozi wa nchi..

Mashetani, wachawi na MAPEPO yanajua mtu wa namna hii akichukua nafasi ya kukikalia kiti cha maamuzi katika nchi a.k.a Kiti Cha U - Rais, basi ndo itakuwa mwisho wa nguvu na utawala wao na ndiyo itakuwa ndo mwisho wa mifumo yao ya uovu kuendelea kutawala nchi...

KWA HIYO;

โœ๏ธTatizo siyo watu. Tatizo sio Mkapa wala Kikwete wala Magufuli na wala tatizo sio Rais Samia Suluhu Hassan kwa sasa. Tatizo ni nguvu iliyo nyuma yao kusukuma maamuzi yao ambayo huleta athari hasi katika nchi..

โœ๏ธKwa kuwa akili na ufahamu wao halisi unakuwa umedhibitiwa na nguvu za kipepo na kichawi, obvious wao huwa hawaoni ubaya wa maamuzi yao. Wao huona wamefanya kwa wanachokiita "uzalendo wa nchi yao", lakini ukweli ukiwa kinyume chake. Huja kugundua kuwa wamefanya maamuzi ya hovyo baadaye wakiwa hawapo kwenye position zao..

โœ๏ธKwa hiyo, tukitaka kumshinda adui huyu asiyeonekana kwa macho ya mwili na tukitaka kuikoa nchi yetu, basi hatupaswi kufanya vita kwa jinsi mwili na damu. Badala yake vita viwe vya kiroho kama ilivyoandikwa;


2 Kor 10:3โ€ญ-โ€ฌ6 SUV

"......Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome๐Ÿ˜‰ tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia..."

โœ๏ธPia silaha zetu za kutumia katika vita hii si hizi tunazohimizwa na kina Mwabukusi na kina Dr Wilbroad Slaa (physical congratulation) kama vile kuandamana, migomo nk . Bali silaha zetu za kumwangamiza kabisa na kumtiisha adui huyu zimeanishwa very clearly na Mungu mwenyewe katika Neno lake..

Wefeso 6:11โ€ญ-โ€ฌ14โ€ญ, โ€ฌ16โ€ญ-โ€ฌ18 SUV
".......Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu; kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;...."


Walio upande wangu na kuijua elimu hii wamenielewa vizuri sana..

Namtakia kila mtu kila la kheri ktk kuchukua hatua..
 
Huyo shetani kwa wazungu hayupo? Mijitu myeusi ni hasara tupu. Po pote pale duniani mambo ni yale yale tu - ubinafsi, uvivu, ufisadi wa kinyama, ushirikina...and the list goes on and on. Halafu badala ya kutafuta suluhisho mtambuka unakuja na ngonjera za mapepo na shetani.

Huko nchi za Scandinavia hakuna mapepo? Walioendelea na kujenga transparent societies wakaushinda ufisadi huko shetani hayupo na mapepo hayafiki? Kwamba hawa wanaochota haya matrilioni siyo wao bali ni shetani na mapepo? Jizazi ๐Ÿ˜ณ๐Ÿ˜ณ๐Ÿ˜ณ

Kama ni hivi basi hakuna matumaini kwa mtu mweusi aisee - iwe ni Afrika, visiwa vya Caribbean, Australia, Haiti na kwingineko!

Tupambaneni na shetani na mapepo ili kutokomeza ufisadi !!!
 
Hiyo ndio ccm sasa
 
Pa kuanzia ni kuzima mwenge. Huu mwenge ndio unapumbaza watanzania. Fikiria baada ya maendeleo makubwa ya teknolojia bado vijana wetu wanakimbia na mwenge wakivuta moshi mweusi ambao ni hatari kwa afya. Kumbuka issue hapo kwenye mwenge sio mwanga kwa sababu clean energies zinazoweza kuzalisha mwanga zipo.
 
Hahaha mkubwa hii rangi inaonekana huikubali sana. Kiukweli kabisa kuna upumbavu mkubwa mno tunaofanyiana.

Huwa napenda sana kumsikiliza Prof Lumumba ananipa taswira ya mambo mengi sana.
Imagine leo hii kuna shule vyoo ni vya makuti lakini serikali inafanya sherehe kusheherekea kununua ndege ya bilioni 200.
Eti korona ndio ilikuja na neema baahi ya shule zikapata vyoo vya kisasa na madarasa ya kisasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ