Ijumaa ya leo ikukumbushe tu Sabato ni Jumamosi

Ijumaa ya leo ikukumbushe tu Sabato ni Jumamosi

Siku ukila Kitimoto iliyo kaangwa na kukaushwa vizuri + ndizi, utaiheshimu tu Jumapili.
Daaa.
Wanaokula nyama ya nguruwe wrote wataangamizwa.

Ushahidi.
Isaiah 66:17
[17]They that sanctify themselves, and purify themselves in the gardens behind one tree in the midst, eating swine's flesh, and the abomination, and the mouse, shall be consumed together, saith the LORD.
Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma yake aliye katikati; wakila nyama ya nguruwe, na machukizo, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA.


Suala la mtu aleje, anaelekeza Mungu aliyeumba sio Mate na uroho wa mlaji.
 
Daaa.
Wanaokula nyama ya nguruwe wrote wataangamizwa.

Ushahidi.
Isaiah 66:17
[17]They that sanctify themselves, and purify themselves in the gardens behind one tree in the midst, eating swine's flesh, and the abomination, and the mouse, shall be consumed together, saith the LORD.
Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma yake aliye katikati; wakila nyama ya nguruwe, na machukizo, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA.


Suala la mtu aleje, anaelekeza Mungu aliyeumba sio Mate na uroho wa mlaji.
Wasabato na Waislam mnakosa mambo mazuri sana kwa kutokumla huyu mdudu 🐖
 
Mungu muweza wa yote anashindwaje kufafanua kuwa siku ya 7 ni lini,hadi anawaachia nyie binadamu ndio muhangaike kuifahamu.
 
The days were named after the planets of Hellenistic astrology, in the order: Sun, Moon, Mars (Ares), Mercury (Hermes), Jupiter (Zeus), Venus (Aphrodite) and Saturn (Cronos). The seven-day week spread throughout the Roman Empire in Late Antiquity.

Walio zipa siku majina,naona hawakufafanua zaidi,waliweka just assumptions.
 
Yesu alifufuka Siku ya kwanza ya Juma.
Leo Ijumaa ndicho kile kinachoitwa Siku Maandalio ya Juma au Siku ya sita.

Jumapili ni Siku ya kwanza ya Juma. Na Sabato kesho ni Jumamosi.

Mambo ya kutafakari.

1: Ni dharau na ukosefu wa adabu kwa Mungu mfalme kuiita Jumapili au ijumaa Sabato. Ni kuhariri sentensi za Mungu.

2: Inatukumbusha Dunia iliumbwa Siku sita za wiki. Hii ya Saba ya Sabato ilikuwa in ofa kwa mwanadamu. Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu. Isingekuwa Sabato wiki ingebaki na Siku sita tu.

3: SABATO imetajwa Mara ya kwanza katika maandiko kabla ya dhambi. Hivyo wazo LA Sabato Galina uhusiano na vivuli vya maagizo ya jangwani.

4: Yesu sio Sabato, wala Sabato sio Yesu. Yesu ni mmiliki au Bwana wa hiyo Sabato. Sabato sio Siku ya wayahudi ni ya Yesu na wanaomfuata.

5: Kukusanyika kwa ibada baada ya Siku sita za kazi kwa Siku isiyo Sabato ya Jumamosi ni kumkosoa na kumdharau Mungu na maagizo yake.

6: Sabato sio kwa ajili ya wakristo. Ni mwanadamu wote. Kama ni mwanadamu na ulikuwa hujui hujachelewa. Nakukumbusha. Ikumbuke Siku ya Sabato.

7: Mungu hakuumba weekend. Alitutengenezea Siku sita za kazi na ya saba ya sabato sio Siku mbili zinazoitwa weekend. Hii taarifa ni muhimu kwako.


Niwatakie ijumaa njema.

Maelekezo ya Mungu hayataki mjadala mrefu yanataka utekelezaji. Huwezi kuhoji kauli za mfalme asiyekosea.
Nimekupenda buree, ufafanuzi murua mtumishi wa mungu, nimependa Sana ulivofafanua ' yesu hakuumba weekend'
 
Mtumishi kuna madhehebu zaidi ya 600 ambayo hayamtambui nabii E.G White lakini wanaikumbuka Sabato nje ya Judaism na SDA.

Hivyo tujitahidi kujenga hoja kwa mtazamo wa dunia nzima sio kitanzania au kiyahudi maana sabato ni hoja ya mwanadamu na sio nchi au kikundi cha imani.

Ni kweli Mimi ni Muadventista msabato na mission kuu ni kuwaandaa watu waende mbinguni Yesu anapokuja.


Ndio maana tunawakumbusha na sabato kwa sababu mbinguni hatutaingia na MAPOKEO. Na mbingu sio kwa watu korofi wasiotaka kutii maelekezo ya Mfalme. Hii ni roho au pepo la kiburi. Wasiofahamu wanarehema ila ukipuuza haya baada ya elimu Mungu hatafurahishwa na wewe.

Tuko pamoja mtumishi.
Mtumishi ngoja nikuulize swali. Unaamini kwamba mtu asiyeshika sabato ya jumamosi hataenda na Yesu ikiwa unyakuo ukitokea sasa hivi? Au hataenda mbinguni na kurithi nchi mpya?
 
Jumapili ni Siku ya kwanza ya Juma. Na Sabato kesho ni Jumamosi.
1 Wakati ule Yesu alipita katika mashamba siku ya sabato; wanafunzi wake wakaona njaa, wakaanza kuvunja masuke, wakala.
2 Na Mafarisayo walipoona, walimwambia, Tazama! Wanafunzi wako wanafanya neno ambalo si halali kulifanya siku ya sabato.
3 Akawaambia, Hamkusoma alivyotenda Daudi, alipokuwa na njaa, yeye na wenziwe?
6 Lakini nawaambieni, kwamba hapa yupo aliye mkuu kuliko hekalu.
8 Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.
 
Siku ya leo wakristu walikuwa wamefunga, waislam , wamefunga ila hawa jamaa wa 7 na wafuasi wa zumaridi ndio walionekana mitaani wakitafuna nyama na sijui nyama za wapi maana mabucha yote Tanzania leo hayakuchinja
 
Mimi Ni Anglican,Ila nakubaliana na wewe Sabato Ni jumamosi,,sijui hata kwa Nini naendelea kuivunja hii amri......Nje ya mada lakini,niliwahi sikia msemo "there's no Christmas without snow"Hivi ule mti tunaopamba Christmas Ni wanini jamani??maana naona barafu zimeanguka je wakati Messiah anazaliwa Bethlehem barafu zilikuwa zinaanguka hapo mjini?
 
SASA WEWE NA WANAFUNZI WA YESU MWENYE AKILI NANI? WAO JUMAMOSI WANALIKUWA WANAPUMZIKA.

JUMAPILI SHAMBANI KUPIGA JEMBE,TENA SIKU YA UFUFUO KABISAA.
ENDELEENI KUINGIZANA CHAKA.

MARKO 16 :12

9Yesu alipofufuka mapema Jumapili, alijionesha kwanza kwa Maria Magdalene, ambaye Yesu alikuwa amemtoa pepo wabaya saba.

10Maria Magdalene akaenda, akawajulisha wale waliokuwa pamoja na Yesu, na wakati huo walikuwa wanaomboleza na kulia.

11Lakini waliposikia ya kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria Magdalene amemwona, hawakuamini.

Yesu anawatokea wanafunzi wawili

(Luka 24:13-35)

12Baadaye Yesu aliwatokea wanafunzi wawili akiwa na sura nyingine. Wanafunzi hao walikuwa wanakwenda shambani.
Mkuu,Yesu alifufuka Siku ya kwanza ya juma,na si Sabato ndio maana hao wanafunzi walikuwa wanakwenda shambani.
 
Shida iko wapi..au kusema ukweli wa maandiko ndio shida?kama vile umeamua kuwa na denial mode..mana ukweli unajua ila huwezi kuufuata hivyo unaamua kuukana makusudi.

#MaendeleoHayanaChama
Ni kweli makanisa yote tunayosali jumapili sio kwamba hatujui sabato Ni jumamosi tumeamua tu kwa makusudi kabisa kuvunja tu hiyo amri Kama tunavyovunja nyingine.
 
Utii ni muhimu sana katika kupokea neema ya Mungu. Adam, Hawa, Kaini, Lameki... walishindwa kutii maagizo ya Mungu. Na matokeo yake unayajua. Hauwezi kuwa rebellious halafu ukategemea somehow kuingia mbinguni.
Jumamosi ndio itakupeleka mbinguni?
 
Wewe Hujui tu, Hapo walikuwa hawajui km atafufuka.Hata hivyo kwenda shambani sio hoja kwasababu Biblia haijasema km walikuwa wanaenda shambani kufanya nini? km walikwenda kutembea tu je??.
Yaani mtu akatembee shambani kweli? seriously?
 
Ni kweli makanisa yote tunayosali jumapili sio kwamba hatujui sabato Ni jumamosi tumeamua tu kwa makusudi kabisa kuvunja tu hiyo amri Kama tunavyovunja nyingine.
Sio kweli.

Mimi ninasali jumapili na ndio siku sahihi kwa wakristo sababu ni siku ya UFUFUKO WA YESU MWENYEWE, ni siku ya USHINDI, NI SIKU KUKOMBOLEWA TOKA UTUMWA DHAMBI NA MAUTI, hiyo ndio sabato ya agano jipya, sio KIVULI TENA CHA SABATO YA KWANZA JUMAMOSI, sabato ya agano la kale.

Ni kweli sabato ni jumamosi kama siku ya saba ya juma. Lakini kwa sasa tangu ufufuko wa Yesu ni kivuli cha mambo ya kale agano la kale. Kwa lugha ingine ni Unasali jumapili kama kumbukunbu ya kukombolewa toka katika utumwa wa dhambi kwa tendo la ufufuko wa Yesu siku ya kwanza ya juma jumapili, sabato ya jumamosi kama siku ya saba ya juma ilikuwa ni siku ya kumbukumbuu ya wana wa israeli kukombolewa toka utumwani misri, sasa wewe Joann na wakristo wengine wote ni lini ulikombolewa toka utumwani misri ?, kilichofanyika ni wewe na wakristo wengine wote mlikombolewa toka katika UTUMWA WA DHAMBI NA KRISTO MWENYEWE SIKU YA KWANZA YA JUMA JUMAPILI, na hiyo ndio siku ya wewe kufanya kumbukumbu na sio jumamosi sabato ya kiyahudi kumbukumbu ya kukombolewa toka utumwani MISRI.

Ndio maana hata wayahudi haters wa yesu walipomletea habari za sabato yao aliwaambia "MIMI NDIYE HUYO BWANA WA SABATO", na mbele huko aliwaambia wanafunzi wake nisikilizeni MIMI (refer tukio la kutokewa na mabii wa kale musa na eliya kule mlimani). Na baadae baada ya yesu kupaa mbinguni wanafunzi wake walifafanua zaidi juu ya hilo na kuwaambia wayahudi na wengine waliokywa wakingangania sabato ya kale kuwa HIYO ILIKUWA NI KIVULI CHA MAMBO YAJAYO YAANI KRISTO MWENYEWE ALIYE KUFA NA KUFUFUKA KAMA ALAMA YA UKOMBOZI NA KUISHINDA MAUTI.
 
Unachanganya

Sabato
Bwana wa Sabato
Pumziko la Sabato ypa siku ya Saba lililotamkwa kabla ya dhambi.

Pumziko la kuwa na Yesu Moyoni.

Watu wa imani zako huwa wanabidii katika Mungu ila sio katika maarifa.

Hatari ni kuangamizwa kwa ukosefu wa maarifa..

Mungu akupe wepesi wa kupokea maarifa haaya.

Ukitaka kumpotosha MTU MPR taarifa nyingi zinazojichanganya. Hii ndicho nakiona kwako. Yesu humjui ikiwa Bado unachanganya Sabato na Kuwa na Yesu.

Haya ni mapokeo yaliyoingia katika ukristo wpua New Age Movements. Post reformation charisma tic movements.

Hizi kauli hazikuwahi kusikika vinywani mwa wakristo kabla ya machafuko ya kiimani na kiroho katne kadhaa baada ya Mitume kulala usingizi wa mauti.
Unachanganya mambo.
Amri ya kupumzika siku ya Saba haikuanzia Edeni.
 
Back
Top Bottom