Ikiwa wewe ndiye Masikini zaidi kati ya ndugu zako, epuka mikusanyiko ya Kifamilia

Anhaa Nyafwili hatujaonana bwana toka mwaka uanze kheri ya mwaka mpya ndugu yangu .

Umesema ukweli kabisa , mimi na ndugu zangu nawakwepa kama ukoma japo wanahisi nina hela ila sipendi kuwahudumia.

Nimeamua kuwa na namba special ninayoweka status daily za vitu vya gharama picha kali nikila bata na hizo namba nimewapa mpaka ndugu wa kitongoji kwahivyo huko nyumbani mitaa ya uswahilini Dasalama wanatangaziana yule mwamba ana hela chafu sana .

Mara wengine wanasema nimezizalisha vizuri hela za urithi yaani ni purukushani ila simu zao napokea kwa mood tu .

Nimewaigizia vya kutosha mpaka nawaonea huruma kwa jinsi wanavyohisi mimi ndiye tajiri wa ukoo kumbe niko Mbeya nakunywa spirit bar ili nikawahudumie wajawazito .[emoji3][emoji3]



Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
UmenigusaπŸ˜€
 
Kwenye msiba wa bibi 2013s ndo nlikuwa naagizwa kununua vinywaji moto ,nahesabiwa hela naandikiw kwenye karatasi[emoji23][emoji23].Chenji ikibak kidogo nanunua viroba vya malawi vya mia mia rider ,muamafumu zile whiskey,bia wanapiga wanaukoo (wajomba) wenye pesa.Nanunua mkanda wa buku 2000 kisha najitenga naanza kujimiminia aloooo umaskini mbaya.Leo nipo kwangu nakumbuka mengi sana
 
Duh umasikini ni wakupambana nao.
 
Anhaa @Nyafwili hatujaonana bwana toka mwaka uanze kheri ya mwaka mpya ndugu yangu
Salama Kabisa ndugu MENEMENE TEKERI NA PERESI , Mwaka mpya umefika Salama tunaendelea na mapambano 🀝, Habari ya mbeya??


Nimeamua kuwa na namba special ninayoweka status daily za vitu vya gharama picha kali nikila bata na hizo namba nimewapa mpaka ndugu wa kitongoji kwahivyo huko nyumbani mitaa ya uswahilini Dasalama wanatangaziana yule mwamba ana hela chafu sana .
😬😬, Mkuu sasa hii mbinu huoni kama ina expire date yake, Maana hapo ndugu wakikuomba hela, lazima danadana ziaze mara moja.
 
😟😟, Haya ndo maisha hali tunayo pitia, ukiwa maskini kwenye ukoo, yani huonekani kama mtu wa maana, zaidi zaidi ni kupelekwa pelekwa tu kama punda.
 
Mbeya kuzuri sana .
Njia haina expire date kwenye maisha yangu kwasababu hata uwezo wa kuwasaidia ninao ila siwezi kuwasaidia Nyafwili

Nimeumizwa na mengi na ndugu bad enough kwa baba na mama kwasasa nimebaki mimi tu hivyo hawa ndugu wa pembeni hawawezi kunipa stress zozote sababu siwazingatii maana washaniumiza sana na hilo wanalijua so wataongea sana ila hakuna mwenye access ya kuniingia kwa undani.

Ndugu ni wazuri lakini ndugu ni wabaya pia tuishi humo blood.

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 


Nimeumizwa na mengi na ndugu bad enough kwa baba na mama kwasasa nimebaki mimi tu
Pole sana mkuu, Dunia ndo ilivyo na tupo tunapita tu, endelea kula maisha MENEMENE TEKERI NA PERESI ,

Hao wengine ni kama extra tu, katika maisha maana hawawezi kukupa support ya kimaendeleo kama wazazi wanvyotoa support kwa mtoo/Watoto wao.
 
Ala



Ukisogea kidogo usikie stori zao ,utasikia mjomba inabidi ujenge uoe saizi utafikiri mtaji wanakupa .Wakati ndo kwanza unazulula kuwatajilisha kwenye miradi Iringa,njombe umo unapigwa na bariiidi mpaka sio poa yao alooo i
😬😬, Hapo wanakuwa wanakutega tu akili, waone unasemaje,, Maana ukiwa na vitita hawawezi kukupa ushauri wa namna hiyo.
 
Maeneo flani kule kwetu pwani kama huna pesa kazi yako kubwa kwenye shuhuli ni kuweka moto kwenye chetezo na kunawisha wageni maji kabla hawajapata chakula.

Ikitokea mtu kajamba kwa haraka unaangaliwa wewe.
Maskini mjambaji kajamba (kimoyomoyo) dah!!!
Aisee umaskini ni laana.
 


kama huna pesa kazi yako kubwa kwenye shuhuli ni kuweka moto kwenye chetezo na kunawisha wageni maji kabla hawajapata chakula.
β€’ Na kama hushtuki, utawanawisha sana wanajamii 😁😁,

β€’ Unaweza dhani wanakupendelea hiyo kazi, kumbe wamekudhalau
 
😟😟, Haya ndo maisha hali tunayo pitia, ukiwa maskini kwenye ukoo, yani huonekani kama mtu wa maana, zaidi zaidi ni kupelekwa pelekwa tu kama punda.

😟😟, Haya ndo maisha hali tunayo pitia, ukiwa maskini kwenye ukoo, yani huonekani kama mtu wa maana, zaidi zaidi ni kupelekwa pelekwa tu kama πŸ˜‚πŸ˜‚
Watakufariji kwa maneno mazuri ila hulambi ata mia,njombe-makete πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…