Iko hatari ya bandari kubaki bandari bila mizigo

Iko hatari ya bandari kubaki bandari bila mizigo

..kuna dalili kwamba kila upande unalipa watu kutetea hoja na misimamo yake.

..pia kila upande unatumia uelewa mdogo wa wananchi kupenyeza mawazo na propaganda.

..Samia amekuwa akitumia JINSIA yake kutafuta kuungwa mkono.

..Ni kiongozi anayetaka kuchukuliwa, kuheshimiwa, kuvumiliwa, na kunyenyekewa, kama " MAMA MZAZI " badala ya Rais kiongozi mwanasiasa.
Ni rais wetu wa kwanza wa jinsia ya kike. Na pengine Mungu alipanga iwe hivi kwamba 2021 March Tanzania ianze kuongozwa na mwanamke baada ya kuwa na marais watano wa kiume watangulizi.
 
Ni rais wetu wa kwanza wa jinsia ya kike. Na pengine Mungu alipanga iwe hivi kwamba 2021 March Tanzania ianze kuongozwa na mwanamke baada ya kuwa na marais watano wa kiume watangulizi.

..Ni kweli.

..Samia ni RAISI wetu.

..sio mama mzazi wa Watanzania.

..She needs to focus on being our PRESIDENT, na tunamheshimu.

..Hatuhitaji nyonyo.🤣
 
..Ni kweli.

..Samia ni RAISI wetu.

..sio mama mzazi wa Watanzania.

..She needs to focus on being our PRESIDENT, na tunamheshimu.

..Hatuhitaji nyonyo.🤣
Ni rais mstaarabu mwenye kuzingatia utu na haki za anaowaongoza. Tuwe na staha akiwa anatimiza ahadi za ilani ya CCM moja baada ya nyingine.
 
Nimetoa mfano mdogo tu, pili Zambi, Burundi na Congo ni wateja wa kudumu.

Tunataka tuingie ubia na hao DP wenu na sio kuwauzia...msitudanganye muuze bandari
Ndiyo hao wazambia,Congo muwakamate wapeni huduma bora
Syo kila mara mnawaibia tu mizigo yao,mnawacheleqeshea kuwatolea mizigo yao
Bandari mnayo mnambwelambwela tu....

Ova
 
..Ni kweli bandari yetu ina matatizo sugu.

..Je, DP ndio kampuni pekee yenye uwezo wa kutatua matatizo ya bandari ya Dsm?

..Dp ndio kampuni bora duniani au kuna nyingine?

..Kwanini tusitangaze ZABUNI YA KIMATAIFA ili makampuni mbalimbali yaombe kazi na Tanzania ichague kampuni tunayoitaka?

..Halafu hakuna haja ya BUNGE letu kubadili sheria za nchi ili kuleta kampuni ya kurekebisha bandari yetu.
Wafanyakazi hapo wezi ,wavivu
Wanafanya kazi kwa mazoea

Ova
 
DPW ndiye mwenye mzigo wote uliopo DRC na Rwanda. Na ndiye mwenye kuutoa huko akauleta bandarini na kuupeleka sokoni.

Logistic supply chain yote ameikamata huyu mwarabu. Rais Tshisekedi alikuja nchini na siku hiyo hiyo akaenda kuikagua bandari.

JPM ziara yake ya kwanza kabisa alikwenda Rwanda akaonana na Kagame akapewa ngombe kadhaa walionona, wajuaji tukasema madikteta wawili wanatafutana kisiasa kumbe ni kuweka sawa suala zima la kuuleta hiyo mzigo kutoka Rwanda.

Baada ya ziara ile ikajengwa reli ya SGR na JPM akapinga kuiona ikienda DRC akapambana mpaka imekwenda Kigali, ili kuuchukua mzigo na kuiwahi hii tenda ya DPW.

Haya yote yanafanyika kimkakati tangu 2015, hivyo Samia anaendeleza kile ambacho JPM iwapo angekuwa hai leo hii angekuwa anakifanya.

Na tumeamua tu kuwa wabaguzi. JPM angekuwa amepewa siku za kuishi mpaka muda huu angeshamaliza hii shughuli na hakuna yoyote ambaye angehoji wala kuleta fyokofyoko.

Tumemuona mwanamama wa kizanzibari tena mpenda demokrasia ndio kila mtu sasa hivi anafungua mdomo wake eti kupinga uwekezaji.
Na watu hawajui tu,rais wa kongo
Alipokea lawama nyingi kutoka kwa wafanya biashara,wanaopitisha mizigo ya wakongo hapo jinsi wanavyofanyiwa hapo bandarini
Uwizi,dhulma nk

Ova
 
Na watu hawajui tu,rais wa kongo
Alipokea lawama nyingi kutoka kwa wafanya biashara,wanaopitisha mizigo ya wakongo hapo jinsi wanavyofanyiwa hapo bandarini
Uwizi,dhulma nk

Ova
Wengi wanaopinga huu uwekezaji wamepewa pesa na matajiri wanaofaidika na hiyo bandari kuendeshwa kizamani.

Pesa imetembea sana usione watu wanajitoa akili humu JF ukadhani ni uzalendo.
 
Balozi wa kongo tz haipiti siku 3 anaenda hapo bandarini kupeleka malalamiko ya wafanyabiashara wa wakongo wanavyofanyiwa hapo
Mijitu hapo bandari wavivu,wezi tu

Ova
Ndiyo hao wanaopinga DP World wasije, wanafahamu DP World hawana longo longo kwenye biashara.
 
Seems like mwamakula was all happy with everything before DP world
 
Hivi nchi bila bandari, kwa mfano Botswana , Zambia, Luxembourg, Switzerland n.k si bado ni nchi tu?
Ukikosa bandari ndio uchumi unakuwa kuishney?
Na je Bandari bila DP world haiwezi endeshwa?
Na vipengele vyenye mapungufu kwenye hayo makubaliano, si vikarekebishwe?
Mimi nasema Tanzania kwanza.
Naunga mkono uwekezaji wowote wenye manufaa kwa Taifa.
 
"4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?"
 
"4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?"
Niko Japan hapa kuna bandari nyingi zote ziko chini ya serekali, madalali msiwasikilize sio watu wazuri wao wanataka chajuu Kisha mtajijua wenyewe. Ogapa sana hawa watu leo mkataba ukivunjwa wapongeza na maandamano juu.
 
Niko Japan hapa kuna bandari nyingi zote ziko chini ya serekali, madala msiwasikilize sio wstu wazuri wao wanataka chajuu Kisha mtajijua wenyewe. Ogapa sana hawa watu leo mkataba ukivunjwa wapongeza na maandamano juu.
Wakuu wa Nchi wapate hii.
 
Back
Top Bottom