Ikulu mnaalika watu wenye heshima kijanja kisha mnawazodoa

Ikulu mnaalika watu wenye heshima kijanja kisha mnawazodoa

Fr. Kitima nae aachage kupenda mialiko ya Ikulu.
Haipendezi kuibuka leo wakati walishaenda na wakashiriki!
Kama aligundua utofauti wa kadi na MUKTADHA alioukuta alipaswa kuondoka!
Kwenye hili siwezi kuilaumu serikali na genge lake!
Unaondoka tu kama unaondoka Grocery?
 
Kuna Watu Wanakera sana. Hivi Huyu Kitimuuu anajitetea kwa Muda Mrefu kama vile Mwana Mama anayetetea ndoa yake. Au Kule Chadema kuna mtandao wa Tigo manatoaga huko. Kuna Vitu vinakera Mpaka siyo poa.
Nilichokigundua kumbe siyo changamoto za Mkataba bali ni Udini na Ukabila ndivyo vinavyowasumbua akina Nongwa.
Rais anashauriwa siyo Kukoromewa kama nyie mnavyotaka. Rais akishauriwa anaupokea ushauri na kuufanyia kazi na ndivyo alivyofanya lakini huo udini na Ukabila hautotufikisha popote Keng nyie
Huna UWEZO wa kutoa USHAURI.
Kwasababu, unaonekana una msongo wa mawazo na unahitaji COUNSELING.
( Sasa ni nani anapenda kushauriwa na mtu mtukanaji?, Hata mtoto atakwepa).
 
Kwani, mapambo ni CONTENT?
Umeelewa? Au unabwabwaja?

Excuse aliyotoa Fr Kitima, naiona haitoshi unapoalikwa na kufika eneo la tukio na kuona hukubaliani na kinachoendelea kuna sababu ipi ya kukufanya kukaa pale, unless atuambie Kama alilazimishwa kuhudhuria!
 
Kanisa ni moja, takatifu katoliki na la mitume. Sasa ni kwa nini Fr. asingemtuma hata katekista au mseminarist akamuwakilishe?
 
Mpoto ametumia Kipaji chake kuonyesha unafiki wa watu fulani

Wakiwa wanaomba kuchangiwa wanakuaga wapole sana😂 ( Mapilau)
 
Umeelewa? Au unabwabwaja?

Excuse aliyotoa Fr Kitima, naiona haitoshi unapoalikwa na kufika eneo la tukio na kuona hukubaliani na kinachoendelea kuna sababu ipi ya kukufanya kukaa pale, unless atuambie Kama alilazimishwa kuhudhuria!
Kubwabwaja kuko wapi? Hujawahi kuona mabango ya COCA-COLA lakini kinachojadiliwa ni upandaji miti?Inaonekana ULINZI unaokuwepo eneo alipo RAIS na PROTOKALI yake huijui.
Ukishaingia kutoka kwa mtu mkubwa kama KITIMA siyo RAHISI namna hiyo( bear in mind ni targeted group).
 
Kuna sehemu tatu za hili jambo

Kwanza, kitendo cha kumtangaza DAB kwa nafasi ya uenezi siku ile ile ya mkutano kinaashiria nia ovu iliyokuwepo kupoteza mjadala. Kama kuna jambo jema kwanini zitumike mbinu za kijima kama hizo?
I'd like to differ, it was just a coincidence, hakuna nia ovu yoyote!.
Pili, kukaribisha watu kwa kadi zisizoeleza tukio kulikuwa na nia ovu, kama nia ilikuwa njema kwanini hawakuandika?
I'd like to differ, it was for discreet reasons na hakuna nia ovu yoyote!. Enzi za Blaza, mialiko ilikuwa inatoka Ikulu, media tunatakiwa tuwepo bandarini saa 2 asubuhi, bila kuambiwa ni nini, halafu saa 4:00 Mwamba anaibuka bandarini katika ziara ya kushtukiza!.

Au shughuli fulani mgeni rasmi ni Rais, hadi backdrops banners zimeandaliwa, unaambiwa ujio wa rais ni siri for security reasons. Hivyo Ikulu wako right kutoa mwaliko bila kusema ni mwaliko wa nini!.
Tatu, waalikwa kwenye shughuli isiyofahamika ni tatizo. Unakwendaje kwenye tukio usilojua?
Kitendo cha kuitwa na the highest authority hata bila kuambiwa unaitiwa nini, justifies wewe kuitika mwito huo!.
Akili ni uwezo wa kutambua au kuyaona mambo kwa haraka. Busara ni uwezo wa kuchanganua habari kwa uyakinifu

Waliokwenda hawakutumia busara

JokaKuu Pascal Mayalla
I'd like to differ, ukiitwa na a trusted source, the highest authority, huhitaji kutumia busara yoyote kujiuliza uende au usiede!, ni unakwenda fasta!.
P
 
Walimuita kijanja ili wamtumie yule zumbukuku kumzodoa yeye na wapingaji wengine wa vipengele vya mkataba
 
Kila mara nimekuwa nikisema humu, nchi hii ina watu wajinga na pengine ni namba moja Duniani huwa naona sieleweki.

Hebu fikiria, mtu anasema Mtumishi wa kanisa anayetunzwa na kanisa, Dkt na mwalimu wa chuo kikuu ana uroho wa ubwabwa.

Unaweza kukuta ni mtu mzima kabisa huyo na anategemewa na familia yake, halafu anauona ubwabwa kama kitu kikuubwa sana. Hajafikiria kitu kingine, ila ubwabwa. Ubwabwa kwake ndio kitu cha maana sana.
Uko sahihi, mkuu.
 
'Hafla Maalum', wangeandika utiaji sahini asingeenda
kwa hili waliteleza, huwezi kumualika mtu kwa kumficha dhima ya huo mwaliko wenyewe, hakuna mwaliko wa namna hiyo. unajua mialiko ya namna hii unaweza kuingizwa kwenye inshu ngumu bila kujua Wala kukusudia kufanya hivyo.
 
Hata haya so called Maridhiano na Vyama vya Siasa yanendeshwa hivi hivi Kisela sela na Mrisho Mpoto anapewa "Vikaratasi" kutoka Juu ili maudhui ya Nyimbo zake yafurahishe masikio ya Wakubwa wa Chama na Serikali.
 
Kama kitima
Kama kitima ndo kaamua kuusambaza huu mwaliko basi naiomba mamlaka imkamate mana anajiona kwamba serikali Iko answerable kwake na ameiweka mfukoni
Umeonyesha hadharani udhaifu wa akili yako ilivyo. Kwani mwaliko ulikuwa wa siri? Kwani document hiyo ya mwaliko ilikuwa ya siri?
Kama Kitima ndio kaisambaza amefanya jambo la kishujaa maana tumeona uhuni wa Ikulu kuita watu kwa hadaa kisha kuwatuma chawa kuwadhihaki watu wenye heshima zao.
 
Nae uroho wa ubwabwa wa ikulu umemponza, mtu umetoka kumzodoa juzi tu leo anakualika halafu bila kujiuliza we huyo kufuata ubwabwa.
Ni ajabu sana miaka 60 ya uhuru bado watu wenye fikra kama zako bado wanaishi. Hivi Fr Kitima anaweza kufuata ubwabwa ikulu? We ni mwehu hustahili kuheshima kabisa, hata ubwabwa huo ungekuwa ulaya bado hakimbilii
 
Hata haya so called Maridhiano na Vyama vya Siasa yanendeshwa hivi hivi Kisela sela na Mrisho Mpoto anapewa "Vikaratasi" kutoka Juu ili maudhui ya Nyimbo zake yafurahishe masikio ya Wakubwa wa Chama na Serikali.
Ndio tunapopata tafsiri kuwa hao wakubwa wa Chama na Serikali wanastahili kupimwa uwezo wao wa akili maana mambo ya wazi kama haya hawawezi kuelewa?
Wanatofauti gani na yule mfalme Juha aliyedanganywa kaveshwa joho na kutembezwa mtaani huku akisifiwa kupendeza (na wapambe/chawa wake) hadi mtoto mdogo asiyejua kitu alipopiga kelele "mfalme yuko uchi!"
 
It doesn't matter alikuwepo na alikula as long as alisema ukweli wake na mwalikaji anajua aliyemwalika ali simamia katika lipi basi wanajua hawapo njia moja, mwalikaji alifanya janja janja haitaufanya mkataba kuwa sawa ikiwa tu una mapungufu.

Ukweli haujawahi kushindwa wala kufichwa milele, wala kutafutiwa kivuli cha kujifichia, haijalishi ukweli utachelewa kiasi gani lakini utafichuka tu ni swala la muda.

Nb: Wapo waliopiga push-up jukwaani kuonyesha uimara wao kiafya kutuaminisha kwamba wako fit 100%, kumbe walikuwa spana mkononi afya zao behind the scenes, lilikuwa swala la muda tu, leo hii hatunao tena[emoji24]

Muda ni mwalimu mzuri.
 
Padre ubwabwa umemponza,
kaalikwa kwenye hafla ila hajui hiyo hafla inahusu nini alichozingatia tu kuwa ubwabwa upo basi ye kaenda.
 
Yesu: Ukialikwa harusini kaa siti za nyuma Ili akija Bwana harusi akuulize unakaaje Siti za nyuma Njoo Siti za mbele ufurahie kalamu

Kwa Kawaida ukiwahi Siti za mbele ndio akina Mrisho Mpoto watakuona na kukuletea dhihaka
Daaah wewe jamaa huwa na comedy sana [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom