IKULU: Rais Magufuli amteua Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

IKULU: Rais Magufuli amteua Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

Yule Bashiru niliyezoea kumuona wakati wa mijadala ya kwenye TV kwenye vipindi vya mzee Makwahia wa Kuhenga jina la kipindi "Je tutafika?"misimamo yake na huyu wa sasa ni watu wawili tofauti!!!
kweli hujafa hujaumbika
 
Mkuu hivi vitu vina traditions. Na ndio maana hata Marekani na uliberali wao wote, kuna baadhi ya mambo walikuwa wanamshangaa Trump kufanya.

Shida ya urais karibu dunia nzima, inategemea sana busara na kujiheshimu, mambo mengi ni unwritten.

Bashiru ataweza kufanya kazi, kama ameweza CCM hatashindwa, lakini inawaambia nini Civil Servants? Kwamba hakuna hata mmoja wao aliyeonekana anafaa? Huyu jamaa juzi tu katoka kusema "CCM inatumia dola kubaki madarakani". Leo anaenda kupewa madaraka makubwa ambayo yanasimamia pia vyombo vya dola, loyalty yake iko wapi Chama au Serikali?

Katika miaka ya hivi karibuni, this will be the most political CS ever
Bashiru alivyoteuliwa kuwa KM wa CCM kutoka kwenye Civil Servant mbona hukulalamika? Sasa ameeudishwa alikotoka nayo iwe nongwa?
 
Yale yale ya kulalamikia kila kitu!

Yeyote yule ambaye angeteuliwa na Magufuli mngemtafutia kasoro tu!

Angemteua Freeman Mbowe kuwa ndo katibu mkuu kiongozi, mngesema Mbowe kanunuliwa.

Sioni tatizo la Bashiru kuwa katibu mkuu kiongozi.

Kateuliwa kihalali na Rais aliyepo madarakani. Hata kwenye nchi zenye demokrasia zilizopevuka, viongozi wake huteua watu wa mirengo na itikadi zinazofanana na za kwao kwenye nafasi mbalimbali, zikiwemo mahakama, vyombo vya usalama, nk.

Apewe nafasi ya kufanya kazi tuone utendaji wake ukoje kabla hatujaanza kumtafutia kasoro.
Trump fan bana
 
Katibu Mkuu Kiongozi ni zaidi ya White House Chief of Staff.Huyo ni Head of Civil Service ukiondoa politicians.

Basically mawaziri, manaibu waziri na rais ni politicians, sio pure civil servants.

Civil service wizarani inaongozwa na katibu mkuu wa wizara.

Na huyu "Katibu Mkuu Kiongozi" ndiye kinara wao.

Kuna miongozo very specific inayokataza watu wa civil service kujiingiza katika siasa.

Sasa mtu party stalwart kama Bashiru, katoka kuwa Katibu Mkuu wa CCM, unaenda kumpa kazi ya kuongoza civil service, eti atenganishe civil service na siasa!

Kituko.
Katibu Mkuu kiongozi ndio Serikali yenyewe,yani kumteua bashiru hapa kuna kitu Magu anataka kutuchezea keusi kekundu sio bure.
 
Bashiru alivyoteuliwa kuwa KM wa CCM kutoka kwenye Civil Servant mbona hukulalamika? Sasa ameeudishwa alikotoka nayo iwe nongwa?
Pitia historia ya wote waliowahi kushika hiyo nafasi hivi karibuni. Hakuna hata mmoja amewahi kuwa mwanasiasa, tena wote wameondoka kwenye utumishi hawajaingia kwenye siasa.

Hivi kweli unaweza fananisha utumishi wa umma wa Kijazi na Bashiru?

Ngoja tuone
 
Jf ya siku hizi ina vilaza sana. Balozi Kijazi alipokuwa KM alikuwa balozi wa nchi gani? Balozi Sefue alipokuwa KM alikuwa balozi wa nchi gani? Vipi kuhusu Balozi Mahiga alipokuwa waziri alikuwa balozi wa nchi gani pia?
Bosi, hao wote uliowataja hapo juu walishawahi kuwa mabalozi wetu nchi za nje. Ndo maana wakabaki na tittle hizo!
 
Hongera sana Classmate wangu PS 2000

He was very intelligent

Alituongoza kuanzia mwaka wa kwanza hadi watatu

Alikuwa na uwezo mkubwa wa kujenga hoja kwa kuandika na kuzungumza
Hakuwa na muda wa mambo ya kipuuzi na kiujumla mwenendo wake ulikuwa mzuri sana

Ni mswalihina sana

Katibu Mkuu Utumishi Dkt Ndumbaro ni Mwalimu wake pale Mlimani

Anafaa sana kushika wadhifa huo
 
Katibu Mkuu Kiongozi ni zaidi ya White House Chief of Staff.Huyo ni Head of Civil Service ukiondoa politicians.

Basically mawaziri, manaibu waziri na rais ni politicians, sio pure civil servants.

Civil service wizarani inaongozwa na katibu mkuu wa wizara.

Na huyu "Katibu Mkuu Kiongozi" ndiye kinara wao.

Kuna miongozo very specific inayokataza watu wa civil service kujiingiza katika siasa.

Sasa mtu party stalwart kama Bashiru, katoka kuwa Katibu Mkuu wa CCM, unaenda kumpa kazi ya kuongoza civil service, eti atenganishe civil service na siasa!

Kituko.

Kwenye mazingira kama haya, it’s natural to be unease, lakini naamini Bashiru ni mtu anayeelewa vizuri sana scope ya kazi anazopewa. Kama KM wa CCM amefanya precisely what katibu mkuu wa chama anapaswa na kutarajiwa kufanya!

Hakuna record inayoonesha kwamba Bashiru alikuwa anapigania CCM hata kabla hajawa KM wa CCM. Kwa hiyo, hakuna sababu ya kuamini kwamba atapigania CCM hata asipokuwa na nafasi ya uongozi ndani ya chama.

Kwa ujumla, hakuna mtu ambaye ideologically haegemei chama fulani, hata kama sio mwanachama rasmi. Katika civil service wapo hata watumishi ambao ideologically wanaegemea vyama vingine mbali na CCM. Ndiyo maana wakati mwingine baadhi ya siri za Serikali zinakuwa leaked to the Opposition!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kazi kubwa ya katibu mkuu( General Secretary) wa CCM, ni kuwa msimamizi mkuu wa ilani ya uchaguzi ya CCM kwa kupitia nafasi yake kama mwenyekiti wa sekretarieti ya CCM

Kwa sasa chama cha mapinduzi ( CCM) ndio kinaongoza serikali, baada ya kupata ushindi kwenye uchaguzi mkuu uliopita

Baada ya watanzania wengi kuridhishwa na ilani ya uchaguzi ya CCM( 2020- 2025), watanzania waliamua kuipa kura CCM

Sasa baada ya uchaguzi, ilani ya CCM( chama kilichoshinda uchaguzi) ya miaka 5, upelekwa bungeni na kuwa mpango wa maendeleo wa taifa kwa miaka 5( mpango wa taifa wa maendeleo utengenezwa kutokana na ilani ya chama kilichoshinda uchaguzi mkuu)

Sasa katibu mkuu kiongozi( Chief Secretary) kwa nafasi yake kama mkuu wa utumishi wa umma kwa niabaya Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, yeye ndie msimamizi mkuu wa watumishi wote wa umma, ambao utekekeza majukumu yao kulingana na mpango wa maendeleo wa taifa unavyoelekeza

Sasa kwa mheshimiwa Rais kumteua katibu mkuu wa chama tawala, ambaye ndie alikuwa msimamizi mkuu wa ilani ya chama tawala, ambayo kimsingi ndio mpango wa maendeleo wa taifa wa miaka 5( 2020-2025), kwenda kuwa katibu mkuu kiongozi ( Chief Secretary) na kuwa mkuu wa watumishi wote wa umma, ambao watakuwa wanatekeleza mpango wa maendeleo wa taifa,

B³inafsi naona ni jambo sahihi kabisa kwa sababu Dr Bashiru Ally atakuwa anaujua upasavyo mpango wa taifa wa maendeleo wa miaka 5, ambao umetokana na ilani ya uchaguzi ya CCM ambapo yeye ndio alikuwa msimamizi mkuu wa ilani hiyo
Hakuna uhusiano wo wote baina ya utumishi serikalini na ilani ya chama cha siasa. Mtumishi wa serikali anafanya kazi kwa kuzingatia kanuni za utumishi wa umma na anaweza kufanya kazi katika mazingira yo yote ya kisiasa bila kujali itikadi ya chama kilichopo madarakani.

Hivyo katibu mkuu kiongozi hapaswi kuwa mwanasiasa!
 
Bashiru alivyoteuliwa kuwa KM wa CCM kutoka kwenye Civil Servant mbona hukulalamika? Sasa ameeudishwa alikotoka nayo iwe nongwa?
Bashiru hajawahi kuwa civil servant bali public servant, muda wote alikuwa mwanaharakati akifundisha chuo kikuu. Labda kama huelewi, waalimu siyo civil servants bali ni watoa taaluma ambao wanaweza kuwa serikalini au kwenye siasa.
 
..kwa baadhi it is a big.

..na wengine wanaona it is not a big deal.

NB:

..hata Gavana wa BOT aliyeteuliwa na Jpm ni mwanasheria, wakati sheria inaelekeza Gavana wa BOT anapaswa kuwa mtaalamu wa uchumi ama fedha.

Jiwe hana hulka ya kuheshimu sheria ingawa yeye anasisitiza kuwa watu wafuate sheria!! He is an anarchist by nature!
 
Back
Top Bottom