Ila haya maisha wakati mwingine yanaweza kukufanya utamani kujiua

Ila haya maisha wakati mwingine yanaweza kukufanya utamani kujiua

Huyo dogo alikuwa chief accountant DHL Tanzania kabla hajaenda vodacom.

Kwa kozi za udbs. Ukibahatika kuingia Big 4 auditing firms na kukaa miaka kazaa tu. Kupata nafasi kubwa kwenye corporates ni rahisi sana.

Unajua CEO wa NMB amemaliza b com yake pale udsm miaka ya 2000s tu na hana mzunguko mrefu wa kufikia U CEO huku hapo hapo NMB kawakuta watu wana miaka kibao kazini. Ila kawaruka yeye kaingia kama CFO baada ya mwaka akapewa U CEO

Wengi waliosoma nae wapo halmashauri wanasema maneno kama yako
Dah,maisha haya bana.anyway ila ili tuendelee kuheshimiana lazima haya magap yawepo ingawa kibinadamu inaumiza unapoona mtu mliyekua nae level moja kakupiga gap kubwa la maisha.lazima mtu ujitafakari umekosea wapi.
 
Usikate tamaa.Mimi nimemaliza B.comm 2003 mbona silalamiki?Pambana kuna siku unaweza kuwa Rais wa nchi ukampiga Robin gap! BTW nilisoma na Jamaa anaitwa Max Kimambo way back in 1995.Nadhani atakuwa kaka yake na huyu.Mama yao ni Mrusi.Bila shaka Max na Robin watakuwa ndugu.
Yeah,huyu jamaa mama yake ni mrusi na baba yake mchaga wa marangu huko kama sikosei ingawa nadhani mzee wake anaishi iringa ambako ndiko amewekeza miradi yake ikiwemo moja ya shule maarufu huko iringa.
 
Hiyo ni kawaida mbona?
Mwenyewe ninae room mate wangu pale mabibo hostel kala shavu akati me bado navua samaki huku kilombero.binafsi naamini kila mtu ana bahati yake katika maisha
 

Attachments

  • Screenshot_20220719-045158_Opera Mini.jpg
    Screenshot_20220719-045158_Opera Mini.jpg
    38.3 KB · Views: 33
Bora hata wewe unamshahara wengine tumejiajiri kwa mtaji mdogo, ya mwisho wa mwezi hatuyajui kama kuna chochote kitapatikana.

Kutofautiana kwa vipato katika maisha ndio huleta maana na umuhimu wa kupambana ili kufikia malengo yako. Kifupi kama una afya na nguvu mshukuru Muumba wako na pambana huku ukiamini utafika unapotaka. Get rich or die trying !
 
Kikubwa nilichoona jamaa huna shukrani na ni mtu mwenye roho ya husda yaani unaumia mtu akipata...
Kiufupi humu wengi tunatamani tupate hata hiyo laki mbili kwa mwezi lkn hatupati kabisa .. sasa wewe unaipata hiyo fursa unamkufuru mungu kweli??
 
Mshukuru Mungu Kwa Kila jambo,inaumiza sana ila hatuna budi kushukuru Kwa Kila jambo
 
Pole mkuu Ila ni kawaida saana, mimi kuna watu wengi saana nilisoma nao, na wengi tu wamenipiga gap Ila nashukuru mungu kwa kipato kidogo nilichojaaliwa na Hao watu sijawachukia Ila nimewaweka kama back up na connection, mfano nimesoma na Humprey Polepole na Nusrat Hanje ambae sasa ni mbungee wa Tanzania pia mdogo wangu tumbo moja sasa anapokea mshahara Mara tatu ya ninaopokea mimi wakati nimempita umri zaidi ya miaka 4. Kwa Hiyo ni kumshukuru mungu kisha kuendelea kupa mbona na kutokata Tamaa na kuwa tumia Hao watu kama daraja au connection na loop ya kutokea unapokwama mahali
 
Kwenye maisha kwa sasa tunapambana na vingi sana. Kwanza hali zetu wenyewe, pili ni afya ya akili juu ya vitu kama kuchanganywa na mafanikio ya wengine(hili lipo kabisa). Lakini mi naamini kama mtu ukiweza kuiweka akili yako sawa ikawa haitingishwi na mafanikio ya wengine, utaishi vizuri sana mana hali zetu pekeake sio kitu kigumu sana
 
Huyo jamaa hapo chini anaitwa Robin Ernest kimambo.ni class mate wangu pale udbs miaka kadhaa iliyopita.

Leo wakati mimi bado nawaza ni lini utumishi watatoa majina ya written interview nikagombanie salary ya TGS D ambayo ni sawa na shillings 710,000/=, huyu class mate wangu kateuliwa na vodacom Tanzania kuwa acting CFO na naamini soon anakua promoted kuwa CFO kamili.kwa haraka haraka mshahara wa CFO wa vodacom ni around 25M.

Yani hapa niko natafakari haya maisha naona kama sisi wengine hayatutendei haki pamoja na kwamba tunapambana sana tu pasipo kuchoka.

Ukiwa na moyo mdogo unaweza kujikuta unajinyonga kwa msongo wa mawazo.

Sio kwa haya magape aisee

View attachment 2295845
Usiache kupambana lakini ...money won't follow you ukiwa kwa grave
 
Back
Top Bottom