Ila kutapeliwa kunauma wakuu

Ila kutapeliwa kunauma wakuu

Huu mwaka umekua wa hovyo mapema mnoo aisee,

Habari zenu kwanza wakuu

Mwenzenu jana nimetapeliwa, na nikiri tu kuwaambia uchawi upo wakuu, Ilikua jana kuna hela nilipatiwa nikamlipie dogo Ada, Nimeenda bank( NMB)nimelipa, ile wakati natoka nikawa naelekea ile njia ya sokoni ili nikapite vile NBC then Mtaa wa zanzibar nichukue baadhi ya vitu halafu nirudi Nyumbani.. Asa wakati natembea mbele yangu kulikua na Gari Hillux ( sijui ndio hilohilo jina, ila ni haya wanatembeleaga sana wakandarasi sikufanikiwa kukariri plate number zake) Limeandikwa St. Joseph ila sikuweza kumalizia ni St Joseph nini maana kuna mtu alikua ameegemea pale kwenye Maandishi..

Napita akaniita kwa majina yangu matatu kabisa, Dada Lee habari?,, nikaitikia salama za kwako?, akanijibu tu safi za masiku nikamwambia salama nikawa nataka kuendelea kuondoka sikuwaza kwasabu nilijua huenda mteja niliwahi kumuhudumia kunijua majina yangu sio kesi,. Kabla sijafika mbali akaniita tena Akaniambia nashida mara moja naomba nisaidie nikamuuliza shida gani?,. Akasema yuko na sister mle ndani na kweli alishusha kioo ni mama mmoja hivi kavaa mavazi yale ya masista,.
Akaniambia mwanangu nina shida naomba nisaidie,. Nilikua natoa hela pale Atm bahati mbaya nimekosea pin mara3, Kadi Yangu imemezwa nasiwezi kwenda ndani kutoa sina kitambulisho,, sasa nataka uende kuna mtu nimeongea nae akahamishie hela kwenye account yako halafu utoe unipatie,,. ( Kwanza kwa maelezo kama hayo wakuu mtu mwenye akili timamu anaona kabisa hayana mashiko, kwanza kutoa hela kwenye Account yako na kitambulisho wapi na wapi?, alijuaje nina NMB account?, na kwanini asimtume yule kijana??,,. )

Basi dada enu ndo nlikua nisharogwa nahisi nikasema sawa,. Nipe namba ya huyo mtu akasema ukienda tu atakuona akachukua karatasi akaandika kiasi Tsh. 1.5m na akaomba nimtajie namba yangu ya Account nikamtajia basi nikaingia ndani, Mwenzenu nikiri tu sikua naelewa chochote mpaka wakati huo😥 ,. Nikaenda moja kwa moja nimejaza slip ya kutoa hizo hela na ni Account namba yangu niliandika,. Nimekaa foleni mpaka nimefika dirishani yule dada ananiambia mbona Acount yako haina hilo salio dada?,. Kiukweli sikua na hiyo hela ila akili yangu ilikua inaniambia kuna hela zinaingia so itakuwa ipo,. Nikamwambia yule dada basi tutoe kwanza hiyo iliyokuwepo nikarudi kujaza slip upya nikatoa laki6 na 15,. Nikarudi kule nje nikamwambia yule sista bado hawajaingiza ipo ileile yangu akaniambia nipe hiyo kwanza sisi tumwahi mgojwa wewe kaa dakika tano nenda tena watakua washahamishia hela kwako na sisi tunakuja mda sio mrefu,. Si nikakubali nimekaa weeee Pale nje sokoni kila nikienda ndani naambiwa hakuna salio..

Baadae sana ndio napata wazo hawa watakua washanitapeli maana hawakunipa hata namba yao, na Namba yao ya Account wala chochote ile karatasi waliandika tu kiasi na namba yangu ya account niliyowatajia ( Aisee jamani nimelia jana tena sanaaa),. Nikawafata wale walinzi nikawaambia nikawaelekeza na walikokua wamepark gari wanasema kule mbali sana Cctv camera haziwezi zinaonyesha kitu ( Ni kule karibu na mlango wa kuingilia soko kuu kwa mbele kidogo kama unataka Ukunje kona uende NBC),. Polisi nako ndio vilevile jana hamna hata cha maana nilijibiwa,. Na sijui ile gari ilikua ni ya St. Joseph University, St. Joseph Primary school, Hospital au ni nini??.

Nachoshukuru ni kwamba nilifanikiwa tu kulipa Ada ya dogo maana Bila hivyo walahi mzee angenikata kichwa au yeye afe kwa Pressure,.

Ila kuna watu ni wakatili sana, mlaaniwe nyie wakujiita watumishi wa Mungu halafu kumbe ni wezi,. For real wamenitia Umasikini maana ndio ilikua hela yangu ya mwisho. Mwaka ushakua wa Hovyo huu,. Tuwe makini jamani matapeli bado wapo na ninahisi wanatumia uchawi maana sio bure🤔😭
Ulikutana na matapeli, hapo hakuna sista wala mdogo wake.
 
Huu mwaka umekua wa hovyo mapema mnoo aisee,

Habari zenu kwanza wakuu

Mwenzenu jana nimetapeliwa, na nikiri tu kuwaambia uchawi upo wakuu, Ilikua jana kuna hela nilipatiwa nikamlipie dogo Ada, Nimeenda bank( NMB)nimelipa, ile wakati natoka nikawa naelekea ile njia ya sokoni ili nikapite vile NBC then Mtaa wa zanzibar nichukue baadhi ya vitu halafu nirudi Nyumbani.. Asa wakati natembea mbele yangu kulikua na Gari Hillux ( sijui ndio hilohilo jina, ila ni haya wanatembeleaga sana wakandarasi sikufanikiwa kukariri plate number zake) Limeandikwa St. Joseph ila sikuweza kumalizia ni St Joseph nini maana kuna mtu alikua ameegemea pale kwenye Maandishi..

Napita akaniita kwa majina yangu matatu kabisa, Dada Lee habari?,, nikaitikia salama za kwako?, akanijibu tu safi za masiku nikamwambia salama nikawa nataka kuendelea kuondoka sikuwaza kwasabu nilijua huenda mteja niliwahi kumuhudumia kunijua majina yangu sio kesi,. Kabla sijafika mbali akaniita tena Akaniambia nashida mara moja naomba nisaidie nikamuuliza shida gani?,. Akasema yuko na sister mle ndani na kweli alishusha kioo ni mama mmoja hivi kavaa mavazi yale ya masista,.
Akaniambia mwanangu nina shida naomba nisaidie,. Nilikua natoa hela pale Atm bahati mbaya nimekosea pin mara3, Kadi Yangu imemezwa nasiwezi kwenda ndani kutoa sina kitambulisho,, sasa nataka uende kuna mtu nimeongea nae akahamishie hela kwenye account yako halafu utoe unipatie,,. ( Kwanza kwa maelezo kama hayo wakuu mtu mwenye akili timamu anaona kabisa hayana mashiko, kwanza kutoa hela kwenye Account yako na kitambulisho wapi na wapi?, alijuaje nina NMB account?, na kwanini asimtume yule kijana??,,. )

Basi dada enu ndo nlikua nisharogwa nahisi nikasema sawa,. Nipe namba ya huyo mtu akasema ukienda tu atakuona akachukua karatasi akaandika kiasi Tsh. 1.5m na akaomba nimtajie namba yangu ya Account nikamtajia basi nikaingia ndani, Mwenzenu nikiri tu sikua naelewa chochote mpaka wakati huo😥 ,. Nikaenda moja kwa moja nimejaza slip ya kutoa hizo hela na ni Account namba yangu niliandika,. Nimekaa foleni mpaka nimefika dirishani yule dada ananiambia mbona Acount yako haina hilo salio dada?,. Kiukweli sikua na hiyo hela ila akili yangu ilikua inaniambia kuna hela zinaingia so itakuwa ipo,. Nikamwambia yule dada basi tutoe kwanza hiyo iliyokuwepo nikarudi kujaza slip upya nikatoa laki6 na 15,. Nikarudi kule nje nikamwambia yule sista bado hawajaingiza ipo ileile yangu akaniambia nipe hiyo kwanza sisi tumwahi mgojwa wewe kaa dakika tano nenda tena watakua washahamishia hela kwako na sisi tunakuja mda sio mrefu,. Si nikakubali nimekaa weeee Pale nje sokoni kila nikienda ndani naambiwa hakuna salio..

Baadae sana ndio napata wazo hawa watakua washanitapeli maana hawakunipa hata namba yao, na Namba yao ya Account wala chochote ile karatasi waliandika tu kiasi na namba yangu ya account niliyowatajia ( Aisee jamani nimelia jana tena sanaaa),. Nikawafata wale walinzi nikawaambia nikawaelekeza na walikokua wamepark gari wanasema kule mbali sana Cctv camera haziwezi zinaonyesha kitu ( Ni kule karibu na mlango wa kuingilia soko kuu kwa mbele kidogo kama unataka Ukunje kona uende NBC),. Polisi nako ndio vilevile jana hamna hata cha maana nilijibiwa,. Na sijui ile gari ilikua ni ya St. Joseph University, St. Joseph Primary school, Hospital au ni nini??.

Nachoshukuru ni kwamba nilifanikiwa tu kulipa Ada ya dogo maana Bila hivyo walahi mzee angenikata kichwa au yeye afe kwa Pressure,.

Ila kuna watu ni wakatili sana, mlaaniwe nyie wakujiita watumishi wa Mungu halafu kumbe ni wezi,. For real wamenitia Umasikini maana ndio ilikua hela yangu ya mwisho. Mwaka ushakua wa Hovyo huu,. Tuwe makini jamani matapeli bado wapo na ninahisi wanatumia uchawi maana sio bure🤔😭
Pole sana aisee.
Cha msingi jipe muda utakaa sawa tu na ujifunze.

Mimi kuna limoja tena nalifahamu kabisaaa lilinitapeli likafanya niishi maisha magumu sana na familia LAKINI sasa ni zamu yake dunia inamnyoosha linaishi maisha ya ovyo sana.

Matapeli wote mlaaniwe.
 
Pole sana aisee.
Cha msingi jipe muda utakaa sawa tu na ujifunze.

Mimi kuna limoja tena nalifahamu kabisaaa lilinitapeli likafanya niishi maisha magumu sana na familia LAKINI sasa ni zamu yake dunia inamnyoosha linaishi maisha ya ovyo sana.

Matapeli wote mlaaniwe.
Mkuu kwanini hukumshitaki ulivyomfaham?
 
Kati ya banki ambazo ukienda unatakiwa uwe makini basi ni NMB. Matapeli wengi wanajichanganya ndani ya bank na wengine wanakuwa nje. Kuna dada mmoja mwaka Jana alitapeliwa mil 15 ndan ya bank. Wakat yupo ndan ya bank alifuatwa na mtu ambae hamjui ila wakajikuta wanaongea kama vile wanafahamiana.
Akili ilipokuja kuka sawa yule dada anajikuta hana hela amebaki na fomu ya kudeposit, ndo anakumbuka kumbe wakati wanaongea alimkabidhi yule jamaa hela yote.
 
Pole sana na kuibiwa. Mwenyezi Mungu atawalipa hao wezi na wewe atakufariji kwa namna usiyoijua.

Ya laiti ungesema kuwa aliyokutapeli ni mtu aliyevaa kanzu na mwanamke kavaa babui na gari lao limeandikwa maneno ya kiarabu ... basi humu watu wala wasingejadili kuhusu utapeli au kuibiwa bali wangejadili uislamu na kusema waislamu ni wachawi au washirikina.

Lakini kwa sababu wahusika wametoka kanisani na gari lao la St Joseph na mavazi ya mwanamke ni ya sista basi watu wanajadili kuhusu kutapeliwa kwako na wala hawajadili kabisa kuhusu ukristo wao au kanisa.
 
😂😂😂Mimi niliwahi kuwa Wakala wa pesa yaani mpaka nilichoka kila siku wanakuja na mbinu mpya nikistuka hii kesho wanakuja na hii mpaka walifanikiwa kunipiga 1million
Kwenye wakala nilikuwa smart lkn siku nakuta short ya 274,000 niliumwa kichwa vibaya mno.,,.....


Yaani wakala kwa ufupi wanalizwa.... Jamaa mmoja akatuma laki tisa + simu ya wakala na siku hiyo hiyo akaacha kazi..... Ni tandale huko.....

Mitaa iliyonilea
 
Mitaa yangu kabisa hiyo.

Kuna classmate wangu walimtapeli kwa style hiyo kule Peramiho. Kuna madawa wanatumia kukupumbaza.

Usiruhusu kuongea sana na sura ngeni mabarabarani humu. Mambo ni mengi.
 
Mkuu kwanini hukumshitaki ulivyomfaham?
Ni mtu ambaye tulikuwa tunafanya nae biashara afu tukawa na ukaribu hadi katika familia, polisi niliona nitapoteza muda na pesa.

Nilishauriwa nikamsuribishe kwa mtaalamu, na kwa hasira nilizokuwa nazo ilikuwa ni rahisi sana kwenda sema huwa siamini katika revenge, MUDA ni mwalimu kuliko yote aisee nilimuacha kama alivyo, nikajifunza kupitia upumbavu wangu maisha yakaendelea.
 
Huu mwaka umekua wa hovyo mapema mnoo aisee,

Habari zenu kwanza wakuu

Mwenzenu jana nimetapeliwa, na nikiri tu kuwaambia uchawi upo wakuu, Ilikua jana kuna hela nilipatiwa nikamlipie dogo Ada, Nimeenda bank( NMB)nimelipa, ile wakati natoka nikawa naelekea ile njia ya sokoni ili nikapite vile NBC then Mtaa wa zanzibar nichukue baadhi ya vitu halafu nirudi Nyumbani.. Asa wakati natembea mbele yangu kulikua na Gari Hillux ( sijui ndio hilohilo jina, ila ni haya wanatembeleaga sana wakandarasi sikufanikiwa kukariri plate number zake) Limeandikwa St. Joseph ila sikuweza kumalizia ni St Joseph nini maana kuna mtu alikua ameegemea pale kwenye Maandishi..

Napita akaniita kwa majina yangu matatu kabisa, Dada Lee habari?,, nikaitikia salama za kwako?, akanijibu tu safi za masiku nikamwambia salama nikawa nataka kuendelea kuondoka sikuwaza kwasabu nilijua huenda mteja niliwahi kumuhudumia kunijua majina yangu sio kesi,. Kabla sijafika mbali akaniita tena Akaniambia nashida mara moja naomba nisaidie nikamuuliza shida gani?,. Akasema yuko na sister mle ndani na kweli alishusha kioo ni mama mmoja hivi kavaa mavazi yale ya masista,.
Akaniambia mwanangu nina shida naomba nisaidie,. Nilikua natoa hela pale Atm bahati mbaya nimekosea pin mara3, Kadi Yangu imemezwa nasiwezi kwenda ndani kutoa sina kitambulisho,, sasa nataka uende kuna mtu nimeongea nae akahamishie hela kwenye account yako halafu utoe unipatie,,. ( Kwanza kwa maelezo kama hayo wakuu mtu mwenye akili timamu anaona kabisa hayana mashiko, kwanza kutoa hela kwenye Account yako na kitambulisho wapi na wapi?, alijuaje nina NMB account?, na kwanini asimtume yule kijana??,,. )

Basi dada enu ndo nlikua nisharogwa nahisi nikasema sawa,. Nipe namba ya huyo mtu akasema ukienda tu atakuona akachukua karatasi akaandika kiasi Tsh. 1.5m na akaomba nimtajie namba yangu ya Account nikamtajia basi nikaingia ndani, Mwenzenu nikiri tu sikua naelewa chochote mpaka wakati huo😥 ,. Nikaenda moja kwa moja nimejaza slip ya kutoa hizo hela na ni Account namba yangu niliandika,. Nimekaa foleni mpaka nimefika dirishani yule dada ananiambia mbona Acount yako haina hilo salio dada?,. Kiukweli sikua na hiyo hela ila akili yangu ilikua inaniambia kuna hela zinaingia so itakuwa ipo,. Nikamwambia yule dada basi tutoe kwanza hiyo iliyokuwepo nikarudi kujaza slip upya nikatoa laki6 na 15,. Nikarudi kule nje nikamwambia yule sista bado hawajaingiza ipo ileile yangu akaniambia nipe hiyo kwanza sisi tumwahi mgojwa wewe kaa dakika tano nenda tena watakua washahamishia hela kwako na sisi tunakuja mda sio mrefu,. Si nikakubali nimekaa weeee Pale nje sokoni kila nikienda ndani naambiwa hakuna salio..

Baadae sana ndio napata wazo hawa watakua washanitapeli maana hawakunipa hata namba yao, na Namba yao ya Account wala chochote ile karatasi waliandika tu kiasi na namba yangu ya account niliyowatajia ( Aisee jamani nimelia jana tena sanaaa),. Nikawafata wale walinzi nikawaambia nikawaelekeza na walikokua wamepark gari wanasema kule mbali sana Cctv camera haziwezi zinaonyesha kitu ( Ni kule karibu na mlango wa kuingilia soko kuu kwa mbele kidogo kama unataka Ukunje kona uende NBC),. Polisi nako ndio vilevile jana hamna hata cha maana nilijibiwa,. Na sijui ile gari ilikua ni ya St. Joseph University, St. Joseph Primary school, Hospital au ni nini??.

Nachoshukuru ni kwamba nilifanikiwa tu kulipa Ada ya dogo maana Bila hivyo walahi mzee angenikata kichwa au yeye afe kwa Pressure,.

Ila kuna watu ni wakatili sana, mlaaniwe nyie wakujiita watumishi wa Mungu halafu kumbe ni wezi,. For real wamenitia Umasikini maana ndio ilikua hela yangu ya mwisho. Mwaka ushakua wa Hovyo huu,. Tuwe makini jamani matapeli bado wapo na ninahisi wanatumia uchawi maana sio bure🤔😭
Nilizani mjanja kumbe bhana 😅😅
 
Shangazi yangu akiwa njiani hasa maeneo ya Kariakoo akiitwa na mtu asiyemjua huwa anamwambia BWANA YESU ASIFIWE KAKA MUNGU ANAKUPENDA SANA 🤣🤣🤣
 
Jaribu kufanya hivi inaweza kukusaidia kiasi chake.

Hapo ulipoibiwa ni Songea mjini, sasa hapo mbele ya hiyo bank ya Nmb kuna jengo la watawa wa mission ya Abasia Hanga monastery kabla hujafika mbele Nbc bank na jengo lao linatazamana na soko kuu, nafikiri wewe ndo umetapeliwa maeneo hayo. Kuna sister mmoja wa mission ya chipole ana sifa hizo za kitapeli alishawahi kumtapeli dogo mmoja wa Mpesa laki 4, issue nzima ilikuwa hivi:

Hawa watawa wana kawaida ya kutembeleana maana wapo wa mashirika mengi, mfano wa benedictine Ndanda wakawatembelea wachipole, wa peramiho wakaenda Bukoba... Kama hivyo.

Sasa huyo sister alitoka akaenda Hanga monastery, alivyofika akawa ana survey mitaa ya kijijini.... Akafika Mpesa flani kwa huyo dogo akamwambia amuwekee hela kwenye cm ndo hiyo 400k. Dogo kamaliza kuweka anamuomba hela....sister anajifanya kutafuta kwenye mkoba mara anamwambia nimesahau utawani ngoja nikachukue, sasa sijui mavazi yalimchanganya akamuamini ndo ikawa imeenda kihivyo. Dogo kwenda utawani anaambiwa mbona hapa wanakuja na kuondoka masister wengi! Huyo tutamjuaje? Basi ikabidi aondoke tu.

NIMETOA HIKO KISA ILI WATU WAJUE KUNA BAADHI YA WATUMISHI WA MUNGU SIO WA KWELI.


Nirudi sasa kumshauri mtoa mada, ila ikiwa bado hujasamehe laki 6 yako.

1. Ukiweza nenda kwenye hilo jengo la watawa ukifika ingia lile duka la vitabu halafu jitambulishe halafu useme hiyo siku ulipita ulikuwa unawahi bank ila kuna gari uliliona limepack hapo kulikuwa na Sr ndani yake limeandikwa sijui st Joseph nini vile... Sasa ulivyotoka bank hukulikuta, kwahiyo lengo la kuja hapo ni kuulizia pengine wanalijua labda la shule kati ya primary au secondary kwa sababu mpaka sasa bado unatafuta shule kwaajili ya kijana wako, hivyo ulivyoliona hilo gari (kama unakumbuka rangi na model yake litaje) ukahamasika kutaka kupata taarifa zake ni la shule gani.

Kama akikuuliza sasa imekuwaje umekuja kuulizia hapa? Simple mjibu nimekuja hapa sababu ni kwa wa mission halafu nilivyomuona yule sister nikajua haya mashirika huwa yanafahamiana kwahiyo naweza nikapata pa kuanzia ili nipate shule bora kwa kijana wangu. HEBU JARIBU HII UNAWEZA KUPATA PA KUANZIA KUMPATA MWIZI WAKO, (kibongo bongo jiwe 6 si mchezo!)



2. Nenda kwenye ma bank yote na Mpesa hizi kubwa kubwa, wale huwa wanabandika sehemu maalumu majina ya shule nyingi tu na taasisi mbali mbali kama za dini kwaajili ya michango mbali mbali. Hapo we chukua majina ya st. Joseph yote! Yawe ya shule au taasisi then ingia Google ingia jina moja baada ya lingine, zaidi we deal na images tu... Huwezi jua pengine unaweza kuliona gari linalofanana na hao matapeli ukaenda sehemu husika ukajikuta unakaribishwa na wezi wako 😂😁. (japo hii njia hai make sense kivile ila siku ukiyatimba! Kila njia utaona inafaa kujaribu).


Nb: hiyo hela ni nyingi jamani! Kwahiyo mpango mkakati ni muhimu. Ila kama mtoa mada umeamua kusamehe basi achana nazo, maana process zote hizo zina consume time!
 
Back
Top Bottom