Ila kutapeliwa kunauma wakuu

Ila kutapeliwa kunauma wakuu

Hapana hata sio mtu wa dini, sema tu by nature nipo hivyo pia maisha yanatufundisha. Ila upande wa pili pia niko brutal sana pia, huwa sitabirikagi.
Anha sawa,.
Hongera lakin
 
Usikupate tu mkuu, maana kwa jinsi wanaongea na wewe huwezi kujua hata kama wanakutapeli akili sijui ilikuwa wapi maskini
Yaani mimi akili ingenijia tu 😅😅😅. Sista wa kanisa katoliki hawezi kukosa msaada kwenye kituo chake hadi aombe msaada kwa wapita njia.
Labda ingekuwa nje ya mji huko mahali ambapo hakuna mawasiliano.
Mimi nikisemeshwa tu na mtu nisiye mjua akili inaniambia hapo hapo tapeli huyu.
 
Hizo dawa nazijua, zishatumika sana kwangu hadi nikaona isiwe kesi acha nikajigange..😅😅😅

watu tunaofanya kazi za kukopesha huku mitaani tunatafuniwa sana hizo dawa

kwa kesi yako wewe, hao watu ni makonki.masta si mchezo, kuna Jini la utambuzi huwa wanalo so kabla ya kuongea na wewe unarushiwa kifurushi kwanza ndio unakaa sawa
Siamini katika kuibiwa kwa njia ya uchawi
 
Kwenye wakala nilikuwa smart lkn siku nakuta short ya 274,000 niliumwa kichwa vibaya mno.,,.....


Yaani wakala kwa ufupi wanalizwa.... Jamaa mmoja akatuma laki tisa + simu ya wakala na siku hiyo hiyo akaacha kazi..... Ni tandale huko.....

Mitaa iliyonilea
Wakala unaweza ukawa na mtaji na ukafilisika chapu
 
Anha sawa,.
Hongera lakin
Ushauri wangu; hao waliokutapeli uwezekano wa kuwapata ni mdogo sana ila amini kabisa hawana mwisho mzuri, wame win kuchukua pesa zako angalia wasi win focus yako. Maana tayari naona umeshaanza jikatia tamaa kuwa mwaka huu wote ni mbaya kwako.

Tumia hasira ulizonazo kupambana na kuzizalisha pesa nyingi zaidi ya hizo, chukulia kama funzo.

“MATAPELI WOTE WALAANIWE”
 
Wakala unaweza ukawa na mtaji na ukafilisika chapu
Nakumbuka alikuja dada mmoja alikuwa mteja tuu....

Kumbe bhn..... wale wazee wa umepokea laki tatu Salio lako ni laki tatu na nusu!!

Ikaingia mesejii hiyo kwa bidada yule,, ghafla wakampandia hewani....

Wazee: Kuna hela imeingia hapo nenda kwa wakala uitoe afu umwambie atutumie....

Dada: haya

Kaja mpaka kwenye kibanda changu.... Kaka niekee laki mbili na tisini....

Nikamwambia okay maake namjua Haina ttzo, nimeeka ghafla kapigiwa mpe wakala tuongee nao

Mimi Tena; Kuna nn

Wazee;:: huna nyongeza, utuongezee maake mgonjwa anahitaji kupatiwa matibabu..... wanakaza nikashtuka nikamuuliza yule dada kina nani Hawa?

Dada;;;;; hata siwajui

Aaaah kubbke nilivurugwa namuuliza haya nipe cash ananiambia ipo kwenye simu shika utoe.......

Kutoa mia tatu hamna Salio,

Maadam alinipa password nikachek Salio ana mia tatu sijui.....

Mimi!!! Mbn huna Salio ?

Dada:::: hamna Salio mbona naambiwa wametuma laki naa

Nikamwambia ushapigwa.... ko tunafanya nn ?

Nikampandia sister hewani kaja fasta.... Yule dada kaomba waende serikali za mitaa wakaandikishane na mumewe akirudi badae walipe kidogo kidogo......

Basii ikawa hivyo!!

Lkn wakala acheni unaweza rudi nyumbn huna mtaji tena
 
Huu mwaka umekua wa hovyo mapema mnoo aisee,

Habari zenu kwanza wakuu

Mwenzenu jana nimetapeliwa, na nikiri tu kuwaambia uchawi upo wakuu, Ilikua jana kuna hela nilipatiwa nikamlipie dogo Ada, Nimeenda bank( NMB)nimelipa, ile wakati natoka nikawa naelekea ile njia ya sokoni ili nikapite vile NBC then Mtaa wa zanzibar nichukue baadhi ya vitu halafu nirudi Nyumbani.. Asa wakati natembea mbele yangu kulikua na Gari Hillux ( sijui ndio hilohilo jina, ila ni haya wanatembeleaga sana wakandarasi sikufanikiwa kukariri plate number zake) Limeandikwa St. Joseph ila sikuweza kumalizia ni St Joseph nini maana kuna mtu alikua ameegemea pale kwenye Maandishi..

Napita akaniita kwa majina yangu matatu kabisa, Dada Lee habari?,, nikaitikia salama za kwako?, akanijibu tu safi za masiku nikamwambia salama nikawa nataka kuendelea kuondoka sikuwaza kwasabu nilijua huenda mteja niliwahi kumuhudumia kunijua majina yangu sio kesi,. Kabla sijafika mbali akaniita tena Akaniambia nashida mara moja naomba nisaidie nikamuuliza shida gani?,. Akasema yuko na sister mle ndani na kweli alishusha kioo ni mama mmoja hivi kavaa mavazi yale ya masista,.
Akaniambia mwanangu nina shida naomba nisaidie,. Nilikua natoa hela pale Atm bahati mbaya nimekosea pin mara3, Kadi Yangu imemezwa nasiwezi kwenda ndani kutoa sina kitambulisho,, sasa nataka uende kuna mtu nimeongea nae akahamishie hela kwenye account yako halafu utoe unipatie,,. ( Kwanza kwa maelezo kama hayo wakuu mtu mwenye akili timamu anaona kabisa hayana mashiko, kwanza kutoa hela kwenye Account yako na kitambulisho wapi na wapi?, alijuaje nina NMB account?, na kwanini asimtume yule kijana??,,. )

Basi dada enu ndo nlikua nisharogwa nahisi nikasema sawa,. Nipe namba ya huyo mtu akasema ukienda tu atakuona akachukua karatasi akaandika kiasi Tsh. 1.5m na akaomba nimtajie namba yangu ya Account nikamtajia basi nikaingia ndani, Mwenzenu nikiri tu sikua naelewa chochote mpaka wakati huo😥 ,. Nikaenda moja kwa moja nimejaza slip ya kutoa hizo hela na ni Account namba yangu niliandika,. Nimekaa foleni mpaka nimefika dirishani yule dada ananiambia mbona Acount yako haina hilo salio dada?,. Kiukweli sikua na hiyo hela ila akili yangu ilikua inaniambia kuna hela zinaingia so itakuwa ipo,. Nikamwambia yule dada basi tutoe kwanza hiyo iliyokuwepo nikarudi kujaza slip upya nikatoa laki6 na 15,. Nikarudi kule nje nikamwambia yule sista bado hawajaingiza ipo ileile yangu akaniambia nipe hiyo kwanza sisi tumwahi mgojwa wewe kaa dakika tano nenda tena watakua washahamishia hela kwako na sisi tunakuja mda sio mrefu,. Si nikakubali nimekaa weeee Pale nje sokoni kila nikienda ndani naambiwa hakuna salio..

Baadae sana ndio napata wazo hawa watakua washanitapeli maana hawakunipa hata namba yao, na Namba yao ya Account wala chochote ile karatasi waliandika tu kiasi na namba yangu ya account niliyowatajia ( Aisee jamani nimelia jana tena sanaaa),. Nikawafata wale walinzi nikawaambia nikawaelekeza na walikokua wamepark gari wanasema kule mbali sana Cctv camera haziwezi zinaonyesha kitu ( Ni kule karibu na mlango wa kuingilia soko kuu kwa mbele kidogo kama unataka Ukunje kona uende NBC),. Polisi nako ndio vilevile jana hamna hata cha maana nilijibiwa,. Na sijui ile gari ilikua ni ya St. Joseph University, St. Joseph Primary school, Hospital au ni nini??.

Nachoshukuru ni kwamba nilifanikiwa tu kulipa Ada ya dogo maana Bila hivyo walahi mzee angenikata kichwa au yeye afe kwa Pressure,.

Ila kuna watu ni wakatili sana, mlaaniwe nyie wakujiita watumishi wa Mungu halafu kumbe ni wezi,. For real wamenitia Umasikini maana ndio ilikua hela yangu ya mwisho. Mwaka ushakua wa Hovyo huu,. Tuwe makini jamani matapeli bado wapo na ninahisi wanatumia uchawi maana sio bure🤔😭
pole sana. Ni kweli matapeli wanatumia nguvu za giza maana hata kazi yao ni ya kishetan so lazima wapate sapoti ya ibilis. Imeandikwa mwenye haki huanguka mara 7 akainuka tena. Jipe moyo uwe hodari tukio hilo likawe sababu ya wewe kusimama na kufanikiwa kiuchumi katika mwaka huu 2025. Wamechukua pesa hawajachukua uhai utafanikiwa tu.
 
pole sana. Ni kweli matapeli wanatumia nguvu za giza maana hata kazi yao ni ya kishetan so lazima wapate sapoti ya ibilis. Imeandikwa mwenye haki huanguka mara 7 akainuka tena. Jipe moyo uwe hodari tukio hilo likawe sababu ya wewe kusimama na kufanikiwa kiuchumi katika mwaka huu 2025. Wamechukua pesa hawajachukua uhai utafanikiwa tu.
Ameen🙏
 
Wakala unaweza ukawa na mtaji na ukafilisika c

Kwenye wakala nilikuwa smart lkn siku nakuta short ya 274,000 niliumwa kichwa vibaya mno.,,.....


Yaani wakala kwa ufupi wanalizwa.... Jamaa mmoja akatuma laki tisa + simu ya wakala na siku hiyo hiyo akaacha kazi..... Ni tandale huko.....

Mitaa iliyonilea
Ndugu yangu amefunga ofisi yake ya uwakala sababu ya ujinga km huu. Waliaza kumpiga mfanyakaz kama laki 6, akaona isiwe tabu akaka mwenyewe ofisini. Siku amekaa ofisini jion anafunga hesabu anakuta mil 1 haipo.
 
Huu mwaka umekua wa hovyo mapema mnoo aisee,

Habari zenu kwanza wakuu

Mwenzenu jana nimetapeliwa, na nikiri tu kuwaambia uchawi upo wakuu, Ilikua jana kuna hela nilipatiwa nikamlipie dogo Ada, Nimeenda bank( NMB)nimelipa, ile wakati natoka nikawa naelekea ile njia ya sokoni ili nikapite vile NBC then Mtaa wa zanzibar nichukue baadhi ya vitu halafu nirudi Nyumbani.. Asa wakati natembea mbele yangu kulikua na Gari Hillux ( sijui ndio hilohilo jina, ila ni haya wanatembeleaga sana wakandarasi sikufanikiwa kukariri plate number zake) Limeandikwa St. Joseph ila sikuweza kumalizia ni St Joseph nini maana kuna mtu alikua ameegemea pale kwenye Maandishi..

Napita akaniita kwa majina yangu matatu kabisa, Dada Lee habari?,, nikaitikia salama za kwako?, akanijibu tu safi za masiku nikamwambia salama nikawa nataka kuendelea kuondoka sikuwaza kwasabu nilijua huenda mteja niliwahi kumuhudumia kunijua majina yangu sio kesi,. Kabla sijafika mbali akaniita tena Akaniambia nashida mara moja naomba nisaidie nikamuuliza shida gani?,. Akasema yuko na sister mle ndani na kweli alishusha kioo ni mama mmoja hivi kavaa mavazi yale ya masista,.
Akaniambia mwanangu nina shida naomba nisaidie,. Nilikua natoa hela pale Atm bahati mbaya nimekosea pin mara3, Kadi Yangu imemezwa nasiwezi kwenda ndani kutoa sina kitambulisho,, sasa nataka uende kuna mtu nimeongea nae akahamishie hela kwenye account yako halafu utoe unipatie,,. ( Kwanza kwa maelezo kama hayo wakuu mtu mwenye akili timamu anaona kabisa hayana mashiko, kwanza kutoa hela kwenye Account yako na kitambulisho wapi na wapi?, alijuaje nina NMB account?, na kwanini asimtume yule kijana??,,. )

Basi dada enu ndo nlikua nisharogwa nahisi nikasema sawa,. Nipe namba ya huyo mtu akasema ukienda tu atakuona akachukua karatasi akaandika kiasi Tsh. 1.5m na akaomba nimtajie namba yangu ya Account nikamtajia basi nikaingia ndani, Mwenzenu nikiri tu sikua naelewa chochote mpaka wakati huo😥 ,. Nikaenda moja kwa moja nimejaza slip ya kutoa hizo hela na ni Account namba yangu niliandika,. Nimekaa foleni mpaka nimefika dirishani yule dada ananiambia mbona Acount yako haina hilo salio dada?,. Kiukweli sikua na hiyo hela ila akili yangu ilikua inaniambia kuna hela zinaingia so itakuwa ipo,. Nikamwambia yule dada basi tutoe kwanza hiyo iliyokuwepo nikarudi kujaza slip upya nikatoa laki6 na 15,. Nikarudi kule nje nikamwambia yule sista bado hawajaingiza ipo ileile yangu akaniambia nipe hiyo kwanza sisi tumwahi mgojwa wewe kaa dakika tano nenda tena watakua washahamishia hela kwako na sisi tunakuja mda sio mrefu,. Si nikakubali nimekaa weeee Pale nje sokoni kila nikienda ndani naambiwa hakuna salio..

Baadae sana ndio napata wazo hawa watakua washanitapeli maana hawakunipa hata namba yao, na Namba yao ya Account wala chochote ile karatasi waliandika tu kiasi na namba yangu ya account niliyowatajia ( Aisee jamani nimelia jana tena sanaaa),. Nikawafata wale walinzi nikawaambia nikawaelekeza na walikokua wamepark gari wanasema kule mbali sana Cctv camera haziwezi zinaonyesha kitu ( Ni kule karibu na mlango wa kuingilia soko kuu kwa mbele kidogo kama unataka Ukunje kona uende NBC),. Polisi nako ndio vilevile jana hamna hata cha maana nilijibiwa,. Na sijui ile gari ilikua ni ya St. Joseph University, St. Joseph Primary school, Hospital au ni nini??.

Nachoshukuru ni kwamba nilifanikiwa tu kulipa Ada ya dogo maana Bila hivyo walahi mzee angenikata kichwa au yeye afe kwa Pressure,.

Ila kuna watu ni wakatili sana, mlaaniwe nyie wakujiita watumishi wa Mungu halafu kumbe ni wezi,. For real wamenitia Umasikini maana ndio ilikua hela yangu ya mwisho. Mwaka ushakua wa Hovyo huu,. Tuwe makini jamani matapeli bado wapo na ninahisi wanatumia uchawi maana sio bPole sana
 
Nilitapeliwa pesa alf 60 na simu mwaka 2012 na mwamba aliyesema anataka niwe namtafutia coins za zamani baadae sikuelewa kinachoendelea nikajikuta nafanya kila anachonielekeza mwishoni akili inakuja kuzinduka simu sina na pesa vumbi nadhani alinitafunia kadawa ka ushawishi na ningekua na hela zingine zingeenda
 
Hujapumbazwa amini kwamba kuna jinsi ambavyo walikuingiza tamaa tu kwamba utanufaika kwa kiasi fulani ila huwezi kusema maana hapo ndo mwanzo wa kujionesha kwamba tamaa ilikuponza.

Sheria ya kwanza ya kuepuka kutapeliwa ni kuzuia tamaa isiponze kichwa.

“When the deal is too good, think twice”
 
Hapana mkuu, Ni sister kabisa ana kilemba na msalaba jamani
Sikatai kabisa mkuu, ila kuna namna hapo.

1. Kwa nini walilijua jina lako ( kwamba hao ma-sister) huwa ni wateja wako kwenye biashara yako ??
2. Ilikuwaje ukakubali kutoa hela yako bila wewe kujua nini unafanya.. ( hicho ni Kiini macho... ✍️ )

Hapo tunakubali kabisa kila kitu ulicho kiona pale kwenye tukio kilikuwa kitu siyo halisi..

Na ukienda mbali zaidi huu mchezo walikuwa wanakufuatilia pindi unaenda bank..( au walinusa tu kulingana na mbinu zao)
 
Back
Top Bottom