Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 38,283
- 97,793
- Thread starter
-
- #41
Ndoto zinazoakisi uhalisia zipo, kuna watu huota wanakibia na wanatoka kitandani na kuanza kukimbia kweli. Inatisha sana kuna mda adi unaogopa kulala.Mkuu bora yako,niliwahi kuota nakimbizwa balaa na watu nawajua,
Watoto mashetani,mbwa wa kuzimu ,majoka ya ajabu na mahali napajua kabisa.
Mpaka ule usiku unaisha ulikua mrefu sana.
Niliruka ukuta mrefu ndotoni nikadondoka.
Kumbe nimedondoka toka kitandani.
Ndo ikawa escape from sorbibor yangu.
Na ndoto ikaishia hapo
Mrekodi halafu mtafute anaejua lugha yake akutafsirie, pambana ndoto ya kuvuliwa chochote na ukaamka ukaikuta hivyo hivyo sio kawaida,Huyu mtu kuna maneno huwa ananitamkia kwa kilugha na huwa sielewi kilugha chake, nikimuuliza amaanisha nini huwa anaishia kucheka tena kwa nguvu sijui huwa anamaanisha nini. Ntaanza kumuepuka maana sio mara moja kumuona kwenye ndoto.
Nafanya hivyo mkuu huwa silali bila kusali.Zidisha maombi wakati wa kulala
Hiyo ilimkuta Jose chameleon Arusha km utakikumbuka hicho kisa chanzo ilikuwa ni ndoto za namna hiyoNdoto zinazoakisi uhalisia zipo, kuna watu huota wanakibia na wanatoka kitandani na kuanza kukimbia kweli. Inatisha sana kuna mda adi unaogopa kulala.
Natamani nimrekodi lakini muda anavyoongea hayo nakuja kushtuka kashaongea anaishia kucheka. Nitamuepuka tu na kuzidisha maombi.Mrekodi halafu mtafute anaejua lugha yake akutafsirie, pambana ndoto ya kuvuliwa chochote na ukaamka ukaikuta hivyo hivyo sio kawaida,
Kuna classmate nae ilimtokea akapotea na kuja kuonekana baada ya miezi miwili huko kwao kigoma.Hiyo ilimkuta Jose chameleon Arusha km utakikumbuka hicho kisa chanzo ilikuwa ni ndoto za namna hiyo
Basi poa utatupa mrejeshoNatamani nimrekodi lakini muda anavyoongea hayo nakuja kushtuka kashaongea anaishia kucheka. Nitamuepuka tu na kuzidisha maombi.
Mazingara yapo alirudi akiwa kawaida au kulikuwa na mabadiliko?Kuna classmate nae ilimtokea akapotea na kuja kuonekana baada ya miezi miwili huko kwao kigoma.
Sawa mkuu.Basi poa utatupa mrejesho
Kinachowezekana uliwahi kukaribishwa mahali na walafi wala hovyo.Usiku ni mrefu ila ukilala na kuota ndoto za ajabu ajabu huufanya uwe mrefu zaidi. Kuna baadhi ya ndoto nikiota ni ngumu sana kuzikumbuka na hizi ndio hunipa hofu hasa nikiota ndoto mbaya.
Huwa ninapata hofu kwa sababu ndoto nyingi nisizozikumbuka huwa zina uwezekano mkubwa wa kutokea na zikishatokea huwa ndio nakumbuka tukio husika na kupata picha kuwa tukio husika niliona ndotoni kama lilivyo. Huwa nashangazwa sana na hii hali inawezekanaje nishindwe kuvuta kumbukumbu mda mfupi baada ya kuota lakini ukipita muda na nikaliona tukio nakumbuka kuwa niliwahi kuota kwenye ndoto ambayo sikuikumbuka?
Tukio la ndoto ya usiku wa kuamkia leo limenichosha, ni nafuu zaidi kwa sababu nalikumbuka, kwangu haina athari kama nisingekumbuka. Niliota hivi,
Kulikuwa na sherehe sijui ilikuwa ni yanini ila niliofanikiwa kuwaona
ndani ni baadhi ya maclass mate. Kwenye hiyo sherehe kiingilio kwa wanaume ni lazima uwe na kitambi tena kikubwa haswa na ukaguzi ulikuwa unaendelea kwenye lango la kuingia ukifika unavua saa, pete na shati unalikunja vizuri unaacha mlangoni unaingia tumbo wazi. Nikikumbuka hicho kitambi changu cha ndotoni nacheka sijui nilikipatia wapi mpaka kutembea ikawa shida, ni kile kitambi kikubwa kilichomwagikia pembeni na chini.
Baada ya kuingia ndani tulikaa kwa muda na hakukuwa na kinywaji chochote kile zaidi ya maongezi na niliowakuta, muda ulivyosogea likaanza zoezi la chakula, unanyanyuka kwa utaratibu kuelekea bufee zilipo na kupakuliwa chakula. Ilipofika zamu yangu nafika kwenye bufee hakuna sahani hata moja, mhudumu akaniomba nitafute sahani kwa waliomaliza nioshe ili niwekewe (muda huo vyakula kwenye bufee bado vimejaa).
Nilitembea kwa shida sana kutokana na kitambi changu kilichokuwa kinacheza kila nikipiga hatua na nilifanikiwa kupata sahani na kuiosha, ile nimerudi nafika kwenye bufee nanyoosha sahani niwekewe msosi naambiwa umeshachelewa chakula kimeisha (wazee wa sherehe ni chakula nadhani mnaelewa hii inavyokata), ile taarifa ya chakula kuisha ilinishtua hadi nikashtuka usingizini na ndoto ikaishia hapo.
Tukio lililotokea INAENDELEA COMMENT #1
Alirudi mchafu kama kachizika hasemi kitu ila mama yake alishuhudia alikurupuka ndotoni kama anakimbizwa na kutokomea.Mazingara yapo alirudi akiwa kawaida au kulikuwa na mabadiliko?
Walafi wala hovyo ndio watu gani mkuu?Kinachowezekana uliwahi kukaribishwa mahali na walafi wala hovyo.
Ngozi nyeusi tuna vitukoAlirudi mchafu kama kachizika hasemi kitu ila mama yake alishuhudia alikurupuka ndotoni kama anakimbizwa na kutokomea.
Kanisani au nkuombee mbali mbaliWapi huko ?
Hiyo sawa mkuu kwahiyo ni umasikini?
Neno moja ni hili,. Tafuta binti weka ndani uache kuota maruweruwe😃😂😂sema neno moja tu na roho yangu itapona 😅
Nitaoa.
Ee ndiwo😃Unaona marue rue
Kwamba ni upwiru au sio 😂Neno moja ni hili,. Tafuta binti weka ndani uache kuota maruweruwe😃😂😂