Ila ndoto nyingine zinachosha, ndoto niliyoiota usiku wa kuamkia leo imenitisha.

Ila ndoto nyingine zinachosha, ndoto niliyoiota usiku wa kuamkia leo imenitisha.

Naijua mkuu
Ok the issue is easy.
Nunua Chumvi ya 1000 tu kwanza,

Chota chumvi kwa mkono wako ijae kwenye kigonja, loweka kwenye maji size ya nusu ndoo.

wakati unaiweka inenee maneno ya kukemea khs kusahau ndoto, kuota ndoto mbaya, n.k kisha subiri dk kadhaa mpk itakapoyeyuka yote..

asubuhi ile unaamka oga kwanzq na maji ya kawaida (kwa sabuni)

ukishamaliza kuoga sasa chukua maji yale ya chumvi ukiyoloweka njoo yaoge mwili mzima

zoezi litafanyika Asubuhi na USIKU Ukikaribia kulala

Addition: wataalam wa mambo wanasema ukideki nyumba yako ni vizuri ukadekia hio kitu pia
 
Usiku ni mrefu ila ukilala na kuota ndoto za ajabu ajabu huufanya uwe mrefu zaidi. Kuna baadhi ya ndoto nikiota ni ngumu sana kuzikumbuka na hizi ndio hunipa hofu hasa nikiota ndoto mbaya.

Huwa ninapata hofu kwa sababu ndoto nyingi nisizozikumbuka huwa zina uwezekano mkubwa wa kutokea na zikishatokea huwa ndio nakumbuka tukio husika na kupata picha kuwa tukio husika niliona ndotoni kama lilivyo. Huwa nashangazwa sana na hii hali inawezekanaje nishindwe kuvuta kumbukumbu mda mfupi baada ya kuota lakini ukipita muda na nikaliona tukio nakumbuka kuwa niliwahi kuota kwenye ndoto ambayo sikuikumbuka?

Tukio la ndoto ya usiku wa kuamkia leo limenichosha, ni nafuu zaidi kwa sababu nalikumbuka, kwangu haina athari kama nisingekumbuka. Niliota hivi,

Kulikuwa na sherehe sijui ilikuwa ni yanini ila niliofanikiwa kuwaona
ndani ni baadhi ya maclass mate. Kwenye hiyo sherehe kiingilio kwa wanaume ni lazima uwe na kitambi tena kikubwa haswa na ukaguzi ulikuwa unaendelea kwenye lango la kuingia ukifika unavua saa, pete na shati unalikunja vizuri unaacha mlangoni unaingia tumbo wazi. Nikikumbuka hicho kitambi changu cha ndotoni nacheka sijui nilikipatia wapi mpaka kutembea ikawa shida, ni kile kitambi kikubwa kilichomwagikia pembeni na chini.

Baada ya kuingia ndani tulikaa kwa muda na hakukuwa na kinywaji chochote kile zaidi ya maongezi na niliowakuta, muda ulivyosogea likaanza zoezi la chakula, unanyanyuka kwa utaratibu kuelekea bufee zilipo na kupakuliwa chakula. Ilipofika zamu yangu nafika kwenye bufee hakuna sahani hata moja, mhudumu akaniomba nitafute sahani kwa waliomaliza nioshe ili niwekewe (muda huo vyakula kwenye bufee bado vimejaa).

Nilitembea kwa shida sana kutokana na kitambi changu kilichokuwa kinacheza kila nikipiga hatua na nilifanikiwa kupata sahani na kuiosha, ile nimerudi nafika kwenye bufee nanyoosha sahani niwekewe msosi naambiwa umeshachelewa chakula kimeisha (wazee wa sherehe ni chakula nadhani mnaelewa hii inavyokata), ile taarifa ya chakula kuisha ilinishtua hadi nikashtuka usingizini na ndoto ikaishia hapo.

Tukio lililotokea INAENDELEA COMMENT #1
Kama nakiona hiko kitambi kinavyocheza mkuu
 
Wewe ni mpiga nyeto.

Ndoto yako ina tafsiri ifuatayo. Ama uiamini ama uamue kuipotezea.

Sherehe ya wenye vitambi, ina maana shughuli ya wanaume wenye uwezo wa kutia mimba. Na bahati nzuri kwa wakati huo, ulikuwa na uwezo mzuri mno ndiyo maana kitambi chako kilikuwa kikubwa kiasi cha kupata tabu wakati wa kutembea.

Uliponyanyuka kwenda kuchukua chakula ni kuamka kwenda kufanya shughuli maalum ya kuijaza kitambi. Ambayo, kwa tafsiri hapo juu ina maana unaanza mchakato wa kumjaza mwenza wako.

Umefika na kukuta sahani zimeisha. Maana yake wakati ukiwa na njaa na matamanio ya kupata mtoto, basi unafika na kukuta uwezo huo huna tena.

Unaelekezwa ukatafute sahani na kuiosha. Hii ina maana unaanza kutangatanga kutafuta msaada. Kuosha ina maana ya matibabu. Na baadae unafanikiwa kupona na kurudi sasa kutimiliza lengo lako.

Unafika unakuta chakula kimeisha. Hii ina maana hata baada ya kupata suluhisho, mwenza wako hayupo tena. Bali alishachukuliwa na wenzako waliokuwa kamili gado. Unafubaa kwa huzuni ya kumkosa.

Pete kiroho ina maana ya maagano. Na katika swala hili ina maana kuwa mwenza wako hakuona future njema nawe. Mwanaume asiye na uwezo wa kutenda kiume. Anavua pete yake na kukiachia. Kudhihirisha kuwa agano la ndoa baina yenu limetamatika.

Kuikuta juu ya t-shirt nyeusi.
Rangi nyeusi kiimani ina maana ya giza, huzuni, msiba, kukataliwa.
Na kwa mantiki ya ndoto yako, pete ya ndoa inawekwa kudhihirisha kuwa kwa huzuni mahusiano yenu yanatamatika.

Nini cha kufanya?
ACHA NYETO..
Aisee
 
Ok the issue is easy.
Nunua Chumvi ya 1000 tu kwanza,

Chota chumvi kwa mkono wako ijae kwenye kigonja, loweka kwenye maji size ya nusu ndoo.

wakati unaiweka inenee maneno ya kukemea khs kusahau ndoto, kuota ndoto mbaya, n.k kisha subiri dk kadhaa mpk itakapoyeyuka yote..

asubuhi ile unaamka oga kwanzq na maji ya kawaida (kwa sabuni)

ukishamaliza kuoga sasa chukua maji yale ya chumvi ukiyoloweka njoo yaoge mwili mzima

zoezi litafanyika Asubuhi na USIKU Ukikaribia kulala

Addition: wataalam wa mambo wanasema ukideki nyumba yako ni vizuri ukadekia hio kitu pia
Ahsante kwa maelezo mkuu, wataalam wa mambo ndio waganga? Sitaki kujihusisha kabisa na mambo ya shirki.
 
Tukio lililonishangaza nilipoamka na kukuta pete ipo juu ya t-shirt nyepesi niliyokuwa nimeivaa kabla ya kulala ikiwa imekunjwa vizuri na kuwekwa juu ya meza pembeni ya mlango. Hii pete ni zile rozari pete(kwa Waroma nadhani mnaijua vyema) muda mwingi huwa ipo kidoleni huwa naivua nikifua au kuoga na mpaka nalala ilikuwepo.

Nilivoshtuka na kuamka nashangaa mbona leo baridi kali sana, kujicheki nipo kifua wazi nikashtuka maana kumbukumbu zangu nililala na tshirt. Kuamka kuwasha taa ndio nikashuhudia hayo yote ya pete yangu kuwa juu ya tshirt iliyokunjwa vizuri. Na hata iweje siwezi weka nguo juu ya meza kwa namna ile.

Ni nini kimefanyika wakuu? Au ndio nilifanya kwa vitendo nilivyokuwa nafanya ndotoni maana kuna watu wakiota wanafanya kitu ndotoni na kwenye uhalisia wanafanya kweli kwa mfano kukimbia.

Sina historia ya kufanya matukio ndotoni baada ya miaka mingi sana kuota nacheza mpira nikapiga shuti ukutani mpaka vidole vikateguka.

Hili tukio kama utani ila limeniacha hoi, hii hii pete kuna siku niliikuta chini baada ya kuota kuna mtu anaivua. Inashangaza sana.

Sijui ina maana gani na inaashiria nini lakini naona ni ndoto tu.
Mkuu Kwanza hapo unakumbushwa kuwa makini na watu wako unaenda nao kwenye Kula Bata hata sehemu ya kutuliza akili. (marafiki) siku moja mtakuja kugombana Kwa sababu ya Kijinga ambayo wewe ndio sababu mwenyewe.

Pili kama unaweza kunywa mkojo wako wa asubuhi kunywa au Tafuta mzizi wa MTI wa mjohoro Choma kisha mkaa wake sugua alafu lile vumbi changanya na maji kunywa.

Tatu usipende kulala Chali yaani sura iangalie juu na pia jitahidi kitanda chako kiwe katika upande wa jua linapotoka au linapozama.

Nne Hakikisha una omba Kwa Mungu wako usiku unapolala.
 
Mkuu Kwanza hapo unakumbushwa kuwa makini na watu wako unaenda nao kwenye Kula Bata hata sehemu ya kutuliza akili. (marafiki) siku moja mtakuja kugombana Kwa sababu ya Kijinga ambayo wewe ndio sababu mwenyewe.

Pili kama unaweza kunywa mkojo wako wa asubuhi kunywa au Tafuta mzizi wa MTI wa mjohoro Choma kisha mkaa wake sugua alafu lile vumbi changanya na maji kunywa.

Tatu usipende kulala Chali yaani sura iangalie juu na pia jitahidi kitanda chako kiwe katika upande wa jua linapotoka au linapozama.

Nne Hakikisha una omba Kwa Mungu wako usiku unapolala.
Kuhusu umakini nipo makini ila huwezi jua mbaya nani kwa namna binadamu tulivyo na wema machoni lakini wabaya rohoni.

Kunywa mkojo wangu hapo kipengele mkuu.

Kulala chali sipendi na nikilala hivyo hata kwa bahati mbaya nikishtuka nabadili style haraka sana.

Kuomba Mungu nitaendelea kila iitwapo leo maana ndipo imani yangu ilipo.

Shukrani kwa ushauri mkuu.
 
Kuhusu umakini nipo makini ila huwezi jua mbaya nani kwa namna binadamu tulivyo na wema machoni lakini wabaya rohoni.

Kunywa mkojo wangu hapo kipengele mkuu.

Kulala chali sipendi na nikilala hivyo hata kwa bahati mbaya nikishtuka nabadili style haraka sana.

Kuomba Mungu nitaendelea kila iitwapo leo maana ndipo imani yangu ilipo.

Shukrani kwa ushauri mkuu.
Tafuta huo MTI wa mjohoro.
Hilo tumbo litakuja kukusumbua Sana Mzee wangu na mwisho wa siku utaambiwa una vidonda vya tumbo.
 
Usiku ni mrefu ila ukilala na kuota ndoto za ajabu ajabu huufanya uwe mrefu zaidi. Kuna baadhi ya ndoto nikiota ni ngumu sana kuzikumbuka na hizi ndio hunipa hofu hasa nikiota ndoto mbaya.

Huwa ninapata hofu kwa sababu ndoto nyingi nisizozikumbuka huwa zina uwezekano mkubwa wa kutokea na zikishatokea huwa ndio nakumbuka tukio husika na kupata picha kuwa tukio husika niliona ndotoni kama lilivyo. Huwa nashangazwa sana na hii hali inawezekanaje nishindwe kuvuta kumbukumbu mda mfupi baada ya kuota lakini ukipita muda na nikaliona tukio nakumbuka kuwa niliwahi kuota kwenye ndoto ambayo sikuikumbuka?

Tukio la ndoto ya usiku wa kuamkia leo limenichosha, ni nafuu zaidi kwa sababu nalikumbuka, kwangu haina athari kama nisingekumbuka. Niliota hivi,

Kulikuwa na sherehe sijui ilikuwa ni yanini ila niliofanikiwa kuwaona
ndani ni baadhi ya maclass mate. Kwenye hiyo sherehe kiingilio kwa wanaume ni lazima uwe na kitambi tena kikubwa haswa na ukaguzi ulikuwa unaendelea kwenye lango la kuingia ukifika unavua saa, pete na shati unalikunja vizuri unaacha mlangoni unaingia tumbo wazi. Nikikumbuka hicho kitambi changu cha ndotoni nacheka sijui nilikipatia wapi mpaka kutembea ikawa shida, ni kile kitambi kikubwa kilichomwagikia pembeni na chini.

Baada ya kuingia ndani tulikaa kwa muda na hakukuwa na kinywaji chochote kile zaidi ya maongezi na niliowakuta, muda ulivyosogea likaanza zoezi la chakula, unanyanyuka kwa utaratibu kuelekea bufee zilipo na kupakuliwa chakula. Ilipofika zamu yangu nafika kwenye bufee hakuna sahani hata moja, mhudumu akaniomba nitafute sahani kwa waliomaliza nioshe ili niwekewe (muda huo vyakula kwenye bufee bado vimejaa).

Nilitembea kwa shida sana kutokana na kitambi changu kilichokuwa kinacheza kila nikipiga hatua na nilifanikiwa kupata sahani na kuiosha, ile nimerudi nafika kwenye bufee nanyoosha sahani niwekewe msosi naambiwa umeshachelewa chakula kimeisha (wazee wa sherehe ni chakula nadhani mnaelewa hii inavyokata), ile taarifa ya chakula kuisha ilinishtua hadi nikashtuka usingizini na ndoto ikaishia hapo.

Tukio lililotokea INAENDELEA COMMENT #1
Kumbe bora mimi ninae ota mimi ndie muhusika mkuu kwenye movie za kizombie hasa Train to busan😅😅tafuta tafsiri
 
Back
Top Bottom