Ilani ipi ya Uchaguzi inatumika kutekeleza issue hii nyeti?

Ilani ipi ya Uchaguzi inatumika kutekeleza issue hii nyeti?

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Ulifanyika uchaguzi 2020, Chama Cha mapinduzi kilimpa Magufuli na sa100 ilani waliyopitia nayo Nchi nzima kuinadi Kwa wananchi.

Katika ilani hiyo ya 2020, hakuna mahala popote CCM ilimuelekeza Magufuli na Sa100 kuuza au kukodisha bandari yetu ya Dar Kwa Miaka 100 au zaidi, Bali ilielekeza bandari hiyo iboreshwe na idhibiti wizi na ucheleweshaji wa mizigo Kutoka bandarini na kuongeza ufanisi Ili kuhudumia wananchi na majirani zetu.

Bandari ya Dar ni kitovu Cha Uchumi wetu, hivyo suala hili la kuuza bandari ni la kitaifa, linapasa litokane na ilani ya 2025.

Awamu ya nne, Rais Kagame aliwahi kuiomba bandari ya Dar aisimamie Kwa ufanisi, ombi Hilo wananchi tulilichukulia kama dharau Kwa Nchi yetu na tulikataa Kwa pamoja na kukubaliana kuwa tunaweza kuisimamia wenyewe bandari yetu.

Kama CCM haikuruhusu bandari kukodishwa kupitia ilani Ile ya 2020, Serikali ya Sa100 inatumia ilani ipi kutaka kuibinafsisha bandari ya Dar Kwa miaka 100 au zaidi, bila kupata ridhaa ya chama na wananchi kupitia SANDUKU la KURA?

Nawasilisha🙏🙏🙏🙏🙏
 
Wakati mwingine ili uendelee unahitaji maamuzi ambayo sio popular kama unayoyawaza mleta mada, na kikubwa kinachokusumbua ni fear of unknown.

Hao wazalendo unaowataka waendeshe bandari ndio wabinafsi kupita maelezo ni bora tuwe na partnership ambayo tutakuwa na uhakika wa steady revenue collection.
 
CCM hawana ilani
Nani kamtuma kiongozi wetu kugusa mahala nyeti kuliko nyeti za kuku?

Bunge halitoshi katika hili!!!

Hii ni issue ya kikatiba, Katiba inakiukwa,

Mtikila, Magu, Nyerere na wafufuke kuja kuzuia hili kama wenye AKILI katika Nchi yetu wamelifumbia macho.
 
Nani kamtuma kiongozi wetu kugusa mahala nyeti kuliko nyeti za kuku?

Bunge halitoshi katika hili!!!

Hii ni issue ya kikatiba, Katiba inakiukwa,

Mtikila, Magu, Nyerere na wafufuke kuja kuzuia hili kama wenye AKILI katika Nchi yetu wamelifumbia macho.
Hivi wamesahau ya Zimbabwe Ian Smith? Africa kusini ?
 
^Kwani tukiibinafsisha, wewe utafanya nini?^

Ndiyo wao wasemavyo, mkuu. Not me.
Kwa Katiba ipi?

Kwa ilani ipi?

Kwa ridhaa ipi Kutoka wa wananchi wepi?

Tukiendelea kunyamaa tutaamka asubuhi na kukuta Nchi imeuzwa!!

Ndugai uko wapi upaze sauti?
 
Kwa Katiba ipi?

Kwa ilani ipi?

Kwa ridhaa ipi Kutoka wa wananchi wepi?

Tukiendelea kunyamaa tutaamka asubuhi na kukuta Nchi imeuzwa!!

Ndugai uko wapi upaze sauti?
Mr Kazi anavuta zake pensheni nono, mkuu. Kamba yake ilikatwa, kaaah!
 
Wakati mwingine ili uendelee unahitaji maamuzi ambayo sio popular kama unayoyawaza mleta mada, na kikubwa kinachokusumbua ni fear of unknown.

Hao wazalendo unaowataka waendeshe bandari ndio wabinafsi kupita maelezo ni bora tuwe na partnership ambayo tutakuwa na uhakika wa steady revenue collection.
Hii itafanyika vipi?
 
Nani wa kumfunga paka kengele?

Miamba na majabali yapige ukunga kuiombolezea Nchi yetu labda watasikia!!!
Profesa J alishasema, ^Huko mwezini nimefanya utafiti, nimegundua kuna kambi za Osama. Ila mkinichagua tena, mtaenda huko hivi karibuni!^ hahaha politikkkks!
 
Afufuke basi MTIKILA kufungua kesi ya kikatiba kupinga hili ikiwa KIBATALA na LISSU wameshindwa!!!!
Mtikila alishamaliza kazi yake, mkuu. Na kifo chake, sote tunajua kilivyokuwa. Swali la msingi ni kwamba, hivi yupo mwingineyo wa kuthubutu japo kufikia robo yake?

Au, tuwaache tu watupeleke mputa mputa watakavyo?

Nawaona majirani hapa wanafungasha mizigo, eti wanahamia Burundi. hahaha
 
Hata mwinyi nae anakodisha kisiwa kule, nadhani wanna balance equation ILI liwe sawa!!
Naamini Ile Katiba Huwa wanaishika kuapa tu, hawaisomi ndani nn kimeandikwa.

Katika hili CCM tujiulize, ni Kwa ILANI ipi na uchaguzi upi anafanya haya?
 
Tatizo Rais ana madaraka makubwa Tanzania kuliko mfalme. Ni kama mungu mtu.

Kwamba anaweza kujiamulia mambo nyeti kama haya yeye kama mtu mmoja. Anaweza asifuate maoni ya Watanzania milioni 60 na hakuna mtu, chombo cha kumuhoji, kumuwajibisha, kumuuliza kitu.

Maoni ya wananchi kwenye issue muhimu kama hii, loliondo, LNG ilitakiwa yazingatiwe, na issue kama tozo, matumizi ya mikopo/ kodi.

Kinga ya kutoshitakiwa iondolewe Kwa viongozi wote hadi Rais.

Bunge, mahakama, vyombo vya habari viwe na meno na uhuru wa kuhoji, kupiga kula ya kutokuwa na Imani na Rais kama anafanya vitu kinyume na maslahi ya Taifa.

Rais aweze kushtakiwa na mahakama kuwa huru kutoa hukumu bila kuingiliwa na yoyote.

Issue kama hii, umeme, loliondo na nyingine muhimu ingebidi Rais aulizwe maswali na vyombo vya habari / wananchi na atoe ufafanuzi.

Bila uwazi, uwajibikaji ni vigumu hii nchi kupiga hatua, kuepuka maamuzi yasiyo na tija kwa maslahi ya Taifa.
 
Ulifanyika uchaguzi 2020, Chama Cha mapinduzi kilimpa Magufuli na sa100 ilani waliyopitia nayo Nchi nzima kuinadi Kwa wananchi.

Katika ilani hiyo ya 2020, hakuna mahala popote CCM ilimuelekeza Magufuli na Sa100 kuuza au kukodisha bandari yetu ya Dar Kwa Miaka 100, Bali ilielekeza bandari hiyo iboreshwe na idhibiti wizi na ucheleweshaji wa mizigo Kutoka bandarini na kuongeza ufanisi Ili kuhudumia wananchi na majirani zetu.

Bandari ya Dar ni kitovu Cha Uchumi wetu, hivyo suala hili la kuuza bandari ni la kitaifa, linapasa litokane na ilani ya 2025.

Awamu ya nne, Rais Kagame aliwahi kuiomba bandari ya Dar aisimamie Kwa ufanisi, ombi Hilo wananchi tulilichukulia kama dharau Kwa Nchi yetu na tulikataa Kwa pamoja na kukubaliana kuwa tunaweza kuisimamia wenyewe bandari yetu.

Kama CCM haikuruhusu bandari kukodishwa kupitia ilani Ile ya 2020, Serikali ya Sa100 inatumia ilani ipi kutaka kuibinafsisha bandari ya Dar Kwa miaka 100 bila kupata ridhaa ya chama na wananchi kupitia Sanduku la kura?
Ebu kwanza kabla ya kwenda mbali tujiridhishe je ni kweli hiyo miaka tunayoisema? Sidhani kama kuna mtu mwenye akili zake timamu ataruhusu mkataba wa hiyo miaka, kwakua variables zitakazojitokeza katika muda huo ni nyingi mno kiasi ambacho huwezi kufikiria kuwa hicho kitu kitaendelea kufaa miaka hiyo kama ilivyo leo.

ikiwa hili ni la kweli basi watanzania hata kama nikwakupigwa risasi wote tukafa tusikubali, its something so dangerous ni kama kusema hakuna ulinzi tena kwa Taifa letu and a person or a group can decide anyhow na hakuna jambo tutamfanya, kitu ambacho kinahatarisha usalama wa kila mtu na kila kitu kwa taifa letu kwa precedence kama hii itakayo ingiwa.

Ndiyo sababu naamini hili haliwezi kuwa kweli, na kama si kweli basi tusipotoshe raia na kusababisha mihemko isiyo ya lazima.
 
Back
Top Bottom