Ili kuepusha foleni za ajabu ajabu, kwanini Rais Samia na wenzake wasiwe wanatumia Helikopta?

Ili kuepusha foleni za ajabu ajabu, kwanini Rais Samia na wenzake wasiwe wanatumia Helikopta?

Hizo foleni za kijinga kwa nini Rais Samia na wenzake wasitumie ndege kata upepo kutoka uwanja wa ndege hadi huko Ikulu ya Dar es Salaam?

Viongozi wengi (waliochaguliwa kwa haki) hata huko Duniani wanatumia ndege upepo kuepusha misongamano isiyo na maana.

Tumechoka aisee!
Hata kutumia gari kusingekuwa shida kama wangesingekuwa wanamfanya rais kama mungu mtu. Wanasimamisha magari muda mrefu bila sababu. Nimeona nchi zilizoendelea wale polisi wenye pikipiki wanapishana pishana kutangalia mbele kwenda kuzuia magari kwenye junction tu wakati msafara unakaribia pale. Hii inafanya watu wasisubiri muda mrefu.
 
This is not as hard as you make it out to be.

It is more about lack of imaginatiin than anything else.

Otherwise, the president would not even be able to fly on a presidential plane.

What is so hard about installing a helipad at Ikulu and the airport, if we don't have one already, and designating special landing zones all over Dar?

If Mbowe and CHADEMA can use a helicopter to campaign successfully all over Tanzania, without using Ikulu's funds, why can't the president use a helicopter to get around Dar?

After all, presidents do use helicopters, so what is the difference between the times when they do use helicopters and when they don't?
Do you think it's safe if terrorist will attack the helicopter..?
Not that we can't,I think we are not mature enough!..
Our nyawawa can fly anytime but the problem it's about risk!.

Kindly you read people due to the way they are, in our country noise will rise immediately coz citizens thinks the using of nyawawa it's going to be a very bad cost of the year!.

Completely I say we are not yet big enough to risk our nyawawa...😅
 
Kwann iwe kwa Samia na sio waliopita? Ndio hoja yang, huu utaratib umekua kero kwa kila awamu, jukumu la lawama wapelekewe security system cz wao ndio hupanga utaratib wa kiusalama!!! NB; Makosa ya tangu zaman mpaka sasa asilaumiwe Samia!!! Over!
Wewe ni kihiyo wa ubongo. Unataka kero isitatuliwe kero kwa sababu tu zilikuwepo siku za nyuma? Aisee ni hatari kweli kweli!
 
Akianza kutumia helicopter mtaanza kusema anatumia gharama kubwa,hamkawii kusema tunanyonywa!.. by the way sidhani kama ni salama zaidi kutumia helicopter Kila mara kwa cheo chake it's keeping her life near crocodile mouth....
Atatumia helkopta 100 nini? Maana nijuavyo helkopta hazitapaswa kufika tatu. Hii tabia tuliipigia kelele sana wakati wa Magufuli maana ndio ilikuwa imekithiri, tena afadhali hata sasa. Wakati wa Magufuli barabara ilikuwa inafungwa hata masaa matatu kabla ya yeye kupita. Tabia ile ikaota mizizi hadi kwa viongozi wa chini. Na imeendelea hadi sasa, japo sio kwa vitisho kama wakati wa dhalimu.

Nilishangaa hadi kuona wakati wa Magufuli na sasa barabara inafungwa masaa kadhaa eti katibu Mkuu wa CCM, na ama mwenezi wa CCM anapita! Hizi ni tabia za ulevi wa madaraka sio zaidi ya hapo. Kiongozi wangalau wa barabara kufungwa awe rais, makamu ama waziri mkuu, tena wawe wameingia madarakani kwa chaguzi halali. Hao wengine wote wapite kwa king'ora tu kama ikibidi.
 
Hapo kuna tatizo la kumuangalia mtu badala ya kuangalia hoja.

The logical fallacy is called ad hominem.

Kwa msimamo huo, wewe unaweza kupotoshwa kirahisi sana siku DP World wakijua kwamba Watanzania wanamuamini sana Issa Shivji kutokana na misimamo yake ya awali, wakamuhonga, akaja aka support DP World, na wewe kwa sababu unapenda kuangalia mtoa hoja, badala ya hoja, ukasema "Hata Issa Shivji kaikubali DP World, mimi ni nani niikatae?".

Unajiweka katika hali ya kukataa neno la kichaa, kwa sababu limesemwa na kichaa.

Siku kichaa atapata nafuu, labda kapewa dawa, atakwambia usipite njia hiyo kuna joka kubwa mbele hapo.

Wewe utasema huyu kichaa tu, maneno yake hayana msingi, hutataka hata kuhakiki maneno yale kama yanaweza kuwa ya kweli.

Utapita kwa mbwembwe zote njia ile na kugongwa na joka kali.

Tujadili hoja, tuache kujadili mtu.

Kama hoja ni mbovu, ipangue tu hoja huna haja ya kumsakama mtu.Hoja mbovu ni mbovu tu hata ikitolewa na nani, sasa kwa nini unaangalia mtu badala ya hoja?

Ukianza kumsakama mtu wakati hujajibu hoja, unaonekana kama umeshindwa kuijibu hoja, na sasa unakimbilia kumsakama mtoa hoja.

Sent from my SM-S908U1 using JamiiForums mobile app
Kiranga katika ubora wake. Umemvua nguo, lakini atachutama?
 
Hizo foleni za kijinga kwa nini Rais Samia na wenzake wasitumie ndege kata upepo kutoka uwanja wa ndege hadi huko Ikulu ya Dar es Salaam?

Viongozi wengi (waliochaguliwa kwa haki) hata huko Duniani wanatumia ndege upepo kuepusha misongamano isiyo na maana.

Tumechoka aisee!
Kufa
 
Kumbe na wewe uliifuatilia Chandrayaan 3?

Ulichokisema hapo hata mimi niliwaza hivyo hivyo.

Pamoja na matatizo yao mengi waliyonayo, kidogo kidogo India itakuja kuwa nchi iliyoendelea sana katika nyanja za kisayansi.
Nimeifuatilia naona wa TZ wengi ama hawajui, ama wameipotezea tu.

India wameshaipita UK kwa ukubwa wa uchumi sasa hivi, ingawa hiki kigezo pia kinaendana na wingi wao.

Kuna Wahindi wanakuja US kufanya kazi wanakaa kidogo wanasema India kuna fursa nzuri zaidi ya US kwa kazi zao, kwa uchumi wao ulipofika. Wanarudi India wengi sana sasa hivi.

Wenzetu waliona wanahitaji kujipanga kwenye tech muda mrefu, wakachukua hatua kuanzisha vyuo vingi sana, hususan vya IIT, tangu 1950s, sasa wanavuna walichopanda ukitaja ma CEO wa Microsoft, Google etc, unakuta wahindi kibao.

Sisi bado tunaendekeza habari za "US is more advanced" mpaka leo, mpaka kwenye kumsafirisha rais kwa helikopta Dar!
 
Huwezi kumuelewa huyu Hadi upitie nyuzi zake zingine ..
Kuna nyuzi anamsafisha Philip Mpango...pitia ...halafu kuna nyuzi anampa pongezi Kardinali Rugambwa....

Huyu ana chuki za kidini...
Hatachukia foleni iwapo Rais angekuwa mkatoliki mwenzake
Wagalatia Wana chuki sana
 
Tabu itakuwa kwenye usalama wake...
Usalama upi boss, watu wana exaggerate tu ili wapate impresst za kujazana kwenye misafara kwa kisingizio cha usalama.
 
Do you think it's safe if terrorist will attack the helicopter..?
Not that we can't,I think we are not mature enough!..
Our nyawawa can fly anytime but the problem it's about risk!.

Kindly you read people due to the way they are, in our country noise will rise immediately coz citizens thinks the using of nyawawa it's going to be a very bad cost of the year!.

Completely I say we are not yet big enough to risk our nyawawa...😅
Terrorists can attack her motorcade, her jet, yet she uses these daily.

What is your point?
 
Nimeifuatilia naona wa TZ wengi ama hawajui, ama wameipotezea tu.

India wameshaipita UK kwa ukubwa wa uchumi sasa hivi, ingawa hiki kigezo pia kinaendana na wingi wao.

Kuna Wahindi wanakuja US kufanya kazi wanakaa kidogo wanasema India kuna fursa nzuri zaidi ya US kwa kazi zao, kwa uchumi wao ulipofika. Wanarudi India wengi sana sasa hivi.

Wenzetu waliona wanahitaji kujipanga kwenye tech muda mrefu, wakachukua hatua kuanzisha vyuo vingi sana, hususan vya IIT, tangu 1950s, sasa wanavuna walichopanda ukitaja ma CEO wa Microsoft, Google etc, unakuta wahindi kibao.

Sisi bado tunaendekeza habari za "US is more advanced" mpaka leo, mpaka kwenye kumsafirisha rais kwa helikopta Dar!
Uko sahihi sana kwenye upande wa IT. Ukigoogle lolote kwa sasa wahindi ndio watoa msaada/maelekezo na kiingereza chao chenye accent ya kihindi.
 
Pengine wanasikia raha tunavyokaa masaa 2 bila movement
 
Uko sahihi sana kwenye upande wa IT. Ukigoogle lolote kwa sasa wahindi ndio watoa msaada/maelekezo na kiingereza chao chenye accent ya kihindi.
Hapa mwenyewe najiongeza mambo ya IT kuna kitabu cha muhindi nasoma, juzi nilikuwa naangalia video mambo hayohayo ilikuwa ya muhindi mwingine.

Accent kubwa ya kihindi, Kiingereza anakata maneno, lakini imebidi niwe mdogo mwenyewe kwa sababu nataka kuongeza kitu 🤣🤣🤣
 
Kiranga soma vzr nilishosema naona unabeba jukumu inconsistent!! Nilisema ashaur mfumo wa utawala na sio kutaja Samia cz haya c ya leo wala jana!! Kuna mamb ya kumuangushia jumba bovu Samia lkn sio hili!!
Matumizi ya lugha huzingatia muktadha fulani, unaposema ashauri mfumo kwa muktadha wa nchi yetu rais huonekana ndo mfumo na wakati mwingine kuwa juu ya mfumo ndio maana katajwa kwa sababu yeye ndo mfumo wenyewe
 
Usalama upi boss, watu wana exaggerate tu ili wapate impresst za kujazana kwenye misafara kwa kisingizio cha usalama.
Nafikiri pia marais wanapenda kutanua barabarani watu wawaone.

Ujue ukiwa katika helikopta hakuna anayekupisha njiani, hakuna anayeiona show yako ya kibabe, wanaona urais wao kama unadogoshwa hivi.

Wanaona urais wa kweli ni pale unapowaweka watu masaa kadhaa wanakusubiri barabarani upite, wakupungie mkono, wajue rais katabasamu vipi leo.

Ukipita juu kwa juu kwenye helikopta wananchi hawakuoni.

Rais anayependa kuenda na msafara wa magari 100 ukimwambia asafiri hata na helikopta tatu ataona umemdogosha sana.

Na kama hatujaweza kupunguza hata misafara ya magari iwe midogo, hiyo misafara ya helikopta hatuiwezi kwa sababu za kisiasa tu, kabla hatujafika kwenye usalama na teknolojia huko.
 
Matumizi ya lugha huzingatia muktadha fulani, unaposema ashauri mfumo kwa muktadha wa nchi yetu rais huonekana ndo mfumo na wakati mwingine kuwa juu ya mfumo ndio maana katajwa kwa sababu yeye ndo mfumo wenyewe
Ni sehem ya system but sio in general! Pia hoja yang ililenga kukosoa tang awamu zilizopita ambazo mfumo wake ni huu huu uliopo, ikimaanisha kumshutum Samia only kweny issue ya foleni c saw!!
 
Hizo foleni za kijinga kwa nini Rais Samia na wenzake wasitumie ndege kata upepo kutoka uwanja wa ndege hadi huko Ikulu ya Dar es Salaam?

Viongozi wengi (waliochaguliwa kwa haki) hata huko Duniani wanatumia ndege upepo kuepusha misongamano isiyo na maana.

Tumechoka aisee!
Ni ushauri mzuri. Sijaelewa kwa nini Waheshimiwa Ma-Rais wa Afrika, kasoro Nyerere, huwa wakienda Ulaya hawajifunzi masuala mazuri, yenye tija na kuyatumia katika uendeshaji wa nchi zao. Utadhani hawa Ma-Rais hawajawahi kuwa raia wa kawaida. Misafara ya magari mengi, misafara yenye mbwembwe, misafara inayopoteza muda mwingi wa raia, raia wengine wakiwa watoa huduma za kufa au kupona, MTU wa kwanza kuelekeza kuwa wahusika watafute njia ya kuirekebisha misafara hiyo ni RAIS mwenyewe na si vinginevyo! Huchukuwa Rais mwenye MAONO na UUNGWANA kufikiria hivyo! Zidisheni maombi kwa Mwenyezi Mungu.
 
Hizo foleni za kijinga kwa nini Rais Samia na wenzake wasitumie ndege kata upepo kutoka uwanja wa ndege hadi huko Ikulu ya Dar es Salaam?

Viongozi wengi (waliochaguliwa kwa haki) hata huko Duniani wanatumia ndege upepo kuepusha misongamano isiyo na maana.

Tumechoka aisee!
Dah m nimecheka tu helkopita

Helikopita jmni inatakiwa huku atumie raisi
 
Back
Top Bottom