Ilikuwaje mara ya kwanza ulipokutana na mtu mliyechati mtandaoni kwa nia ya kuwa wapenzi?

Ilikuwaje mara ya kwanza ulipokutana na mtu mliyechati mtandaoni kwa nia ya kuwa wapenzi?

Ila wizo unazingua ujue πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Na wewe ungemsonkola vidole vya macho aache ujinga.
Wizo umefunguliwa kutoka gerezani πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œ
 
Umenikumbusha mshikaji wangu Lumi. Tumevuka maji toka Kigamboni kumpokea demu katoka Bagamoyo hakuwani kumuona. Si akamkimbia baada ya kumuona kwa mbali. Eti sura haikuwa kama kwenye picha, kademu kembambaaa halafu kamepiga mkorogo hatari
πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Hapana siwezi fikia huko naiogopa dhambi sitaki kuzidi kumtesa Yesu msalabani kwa dhambi zangu.
Wee ngadu umeanza lini kuhubiri neno?? Mbona hatari hii jirani?!! Nimerudi na watu wameokoka?? Kwema?
 
Mwaka 2011 nikiwa nafanya kazi Njombe nikaongea na rafiki yangu anisaidie ku- process cheti cha kuzaliwa Cha mtoto niliyezaa na binti 1. Huyo rafiki yangu akaamua kumpa dada mmoja hiyo kazi akampa na namba yangu ya simu ili niwe nampa details na mambo mengine in case. Basi bana binti ndiye alianza kunipigia, mara ya kwanza sauti nzuri kweli, laini na nyororo. Siku zikaenda nikamtongoza akakubali, baadae akanambia ameolewa lakini mume wake amemtelekeza ameoa mke mwingine, anaishi kwenye nyumba ya huyo mme wake. Tulikuwa tunaongea kila siku usiku hadi mida ya saa saba, tunaagana ili nipimzike niamkie kibaruani. Nikaenda likizo kijijini kwetu, yeye alikuwa Bunda mjini, siku moja nikamwambia nakuja Bunda ninashida Musoma hivyo naomba tukutane Bunda stand. Nilikuwa wa kwanza kufika nikampigia simu akanambia ngoja achukue boda aje, nikawa alert kuona nani atanipigia simu, dakika 5 mbele boda inaingia ikiwa na mdada,akamlipa ajanipigia, hahaha! Sauti na muonekano tofauti kabisaa, tulikaa kama dakika 5 nikamwambia ngoja nifike Musoma nitakucheki wakati narudi. Jioni akaniuliza vp, nikamwambia nimekwama. (Musoma nilikuwa naenda kwa mchumba wangu ambaye ndiye mke wangu kwa sasa). Sikumtafuta tena, baadae rafiki yangu ajanipigia akinambia mme wa yule dada alituona wakati niko nae hapo stand ya mabus! Sikuwahi tena kujihangaisha na huyo dada
 
"Samahani sana ninavyokuona sio kama nilivyotegemea, HATUENDANI"... baada ya kusema hivyo jamaa aliyekuwa naye kwenye Toyota Hiace nyeupe akaniangalia na kutabasamu kisha akaondoa gari. Mimi nikaachwa nimesimama. Kibaya zaidi hata kwenye gari hakushuka. Sikuweza kujua yule kijana alikuwa nani yake hadi leo. Ilitokea Arusha maeneo ya Njiro nje tu ya Njiro Complex (Bugaluu).

Mwaka 2007 kupitia mtandao wa marafiki.com niliweza kupata mchuchu mwenye asili ya kiasia na kuanza kuchat naye. Chats zilikuwa nzuri sana za kuvutia utadhani tumejuana kitambo sana. Siku tunakutana kwa mara ya kwanza nje ya Njiro Complex ndo akakata tamaa na kunijibu kama nilivyoandika kwenye aya ya kwanza. Ilikuwa ni aibu kubwa sana kwenye haya maisha yangu. Bahati nzuri hakukuwa na mtu niliyeenda naye eneo la tukio kwahiyo aibu ilikuwa ni yangu binafsi.

Ila sikumchukia wala kumlaumu yule binti wa kishua kwa sababu kwa wakati ule kweli nilikuwa nimepigika haswa. Yaani nilikuwa mwembamba ila ule wembamba wa lishe duni. Kiufupi nilikuwa nimekonda. Kama unavyojua mtu mwenye njaa ndo mwenye sura mbaya kwahiyo hata mimi nilikuwa mtu mwenye sura mbaya sana kwa hisani ya NJAA. Zilikuwa nyakati ambazo kutembea kwa mguu kutoka Mianzini hadi Mbauda ni kitu cha kawaida sana. Au wakati mwingine Clock Tower - Njiro ilikuwa jambo dogo. Akitembea tajiri huwa ni matembezi ya hisani ila mimi sijui ilikuwa matembezi ya kuchochea umaskini?

Nakumbuka mwaka 2010 ndo nilipata matumaini makubwa sana baada ya manzi mmoja wa Chalinze kuniambia mimi ni handsome. Huyo manzi nilikutana naye nilipokuwa natoka Iringa kuchukua cheti cha form six.

Kimsingi baada ya tukio la 2007 nikaanza kuogopa sana kutongoza demu mtandaoni. Hadi leo nikiona manzi mtandaoni huwa hadi nifuatilie sana kumjua kiasi na sio kukurupuka.
Pole sana kijana. Wewe ni mtu mwenye nyota ya punda. Nenda ukasafishe nyota. Ulikataliwa kikatili sana.
 
Back
Top Bottom