Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Halafu bado haka kakundi kanalelewa tu: Kuhakikisha kwamba nchi haiwezi kurudi tena kule ilipotoka there's one place these people belong : The Cemetery, A Noose or A Bullet in the head!!! A prison term is not enough for these ruthless and deranged fanatics (This is legal, legitimate, justified and righteous).

Mara nyingine huwa naumia sana kuhusu Tanzania, natamani hata nisingekuwa nayafahamu haya yanayondelea.....
Ngoja ninywe maji kidogo. Nitarudi!
 
Nani anajifanya mwanadiplomasia ambaye amewahi kukupiga ???
Usihangaike na watu ambao hawataki kuelewa rejea kwenye maandiko ya Plato baba wa falsafa kutoka ugiriki "myth of the cave" utaelewa kwanini watu wanakuja na mihemko nikwa sababu Watanzania wengi wanaishi kwenye ndani ya pango lenye giza na hawataki kutoka na ukajaribu kuwatoa wanaweza kukutoa roho please note my words. Uongozi uliopita ilijaza watu ujinga sana
 
Unamaanisha kushirikiana kama 50/50 au maendeleo ya kisayansi au kushirikiana ambapo tanzania inapewa misaada na nchi ya kigeni inashikilia rasilimali zetu 100%
Ninavyosema mahusiano baina ya nchi (International Relations) nazungumzia vitu zaidi ya uwekezaji wa 50/50, zaidi ya sayansi na teknolojia, zaidi ya misaada. Hapa sasa kwenye mahusiano ya kimataifa (International Relations) ndiyo kinakuja kitu muhumu kabisa kiitwacho Diplomasia (Diplomacy): Mahusiano ya kimataifa (International Relations) na Diplomasia (Diplomacy) ni dhana mbili tofauti kabisa, japo huwezi kuzitenga.

Sasa ili ufanikishe mahusiano ya kimataifa (International Relations) ili uweze kupata hizo 50/50, teknolojia, ulinzi au hata misaada ni lazima uwe na chombo kiitwacho Diplomasia (Diplomacy). Lakini ili hichi chombo kiitwacho diplomasia kiweze kufanya kazi vizuri katika kujenga, kufanikisha na kuimarisha mahusiano ya kimataifa (International Relations) ni lazima nchi husika itengeneze kitu kiitwacho Sera ya Mambo ya Nje (Foreign Policy).

Sasa basi ili kuelewa nini kilifanyika hapa Tanzania ni lazima ufahamu mambo niliyoyataja hapo juu:
1. Mahusiano ya kimataifa (A State of International Relations).
2. Dhana ya neno diplomasia (A Concept of Diplomacy).
3. Sera ya mambo ya nje ya Tanzania (Tanzania's Foreign Policy).

Sisi ili kupima mafanikio ya mtu huwa tunaangalia haya mambo matatu ambayo huingiliana. Ulinzi, Rasilimali, Uwekezaji, haki za binadam, soko ya kimataifa, na Misaada ni sehemu ndogo sana ambazo zinaingia kwenye haya mambo makuu matatu. Bahati mbaya sana sasa, vijana wengi wa kitanzania ambao kazi yao ni kusifia na kuunga mkono kila kitu hawana uelewa wowote ule katika hili.

Ndiyo maana huishia kusema tunachuki na marehemu lakini ukweli wenyewe ndiyo huu ambao wengi wao hawataki kuukubali.
 
Usihangaike na watu ambao hawataki kuelewa rejea kwenye maandiko ya Plato baba wa falsafa kutoka ugiriki "myth of the cave" utaelewa kwanini watu wanakuja na mihemko nikwa sababu Watanzania wengi wanaishi kwenye ndani ya pango lenye giza na hawataki kutoka na ukajaribu kuwatoa wanaweza kukutoa roho please note my words. Uongozi uliopita ilijaza watu ujinga sana
My Maaan, my maaan!
Thanks for bringing allegory of the cave.......
 
Kuna mtu aliwajaza ujinga baadhi ya watanzania kwamba nchi yao ni tajiri na kuwaita hasa wazungu na wenye mitaji mikubwa kuwa ni Mabeberu - akaua wizara ya mambo ya nje - Finally akasepeswa baada ya kukiuka kiapo cha mwenyezi Mungu, sasa tunafanya u-turn kwenye main road ila nayo inagoma - maji hayatoki.
Populism ipo lakini haitakiwi ivuke mipaka na kuathiri sera ya mambo ya nje na diplomasia ya nchi. Ukisoma sana Diplomasia utakutana na kitu kinaitwa COMPARTMENTALIZATION OF FOREIGN POLICY AND NATIONAL DIPLOMACY. Kwamba utakuwa na ujinga wako ndani ya nchi au utakuwa na uadui na taifa fulani, lakini lazima mshirikiane nalo kwenye mambo muhimu.

Sasa mtu usipofahamu jinsi mfumo wa dunia unafanya kazi unaweza kuyapeleka yale ya ndani ya nchi nje ya mipaka yako na yakakuletea madhara. Hili ndilo liliiukuta Tanzania yetu, tumepata madhara makubwa. Hebu angalia hapa:

1. Uchina na Marekani ni maadui wakubwa - Lakini ndiyo mataifa yenye mahusiano makubwa kibiashara.
2. Uchina na Japan ni maadui wakubwa - Lakini wanahusiana sana kwenye ulinzi na usalama wa Pasifiki.
3. Uchina na Australia wameanza kuwa maadui- Lakini biashara ya Real Estate Uchina ina mkono wa Australia.
4. Urusi na Marekani ni maadui - Lakini wanashirikiana sana kwenye teknolojia na usalama wa Mashariki ya Kati.
5. Urusi na Ukraine ni maadui - Lakini juzi Ukraine wameomba kuuziwa gesi na Urusi baada ya uhaba kutokea Ulaya.

Hujiulizi kwanini haya mataifa makubwa hayasusi au kuzira kama mataifa ya kiafrika, huku mkijivuna kwamba sisi ni matajiri na tunajenga kwa pesa za ndani. Mara hatuwahitaji hawa wanyonyaji, tunaweza kufanya wenyewe. Hizi kauli hata mtu binafsi huwezi kuzisema kwa jirani zako. Lakini watanzania wakaingia mkenge, ona leo sasa.......
 
Ushirikiano wa kutuletea Symbion na Aggreko na kutukamua na capacity charge halafu wao wanakuletea vyandarua vya msaada gharama zake ni sawa na pesa ya siku moja wanayotukamua kwenye capacity charge.
Tumia akiri Sasa kukwepana nao siyo kuwakimbia. Kuwakimbia bila strategy u akuwa kama digidigi tu na unaua wananchi wako. Hivi unajua kuwa Kuna watanzania wanaona Bora kutawaliwa na mzungu kiliko mwafrika?
 
Usihangaike na watu ambao hawataki kuelewa rejea kwenye maandiko ya Plato baba wa falsafa kutoka ugiriki "myth of the cave" utaelewa kwanini watu wanakuja na mihemko nikwa sababu Watanzania wengi wanaishi kwenye ndani ya pango lenye giza na hawataki kutoka na ukajaribu kuwatoa wanaweza kukutoa roho please note my words. Uongozi uliopita ilijaza watu ujinga sana
Umefunga mjadala.
 
Watu wenye akili timamu Tanzania?

Labda wenzetu walikuwa wagonjwa hatujui?

Wapo wengine hadi leo hawataki Mama asafiri na akisafiri ni matusi tu mwanzo mwisho
Hapa Tanzania wananchi na viongozi wenye akili timamu wapo wachacheee mnoooooo yaani mnoooo, inawezekana kwenye hili taifa zima la watu wapatao milion 55+ watu wenye akili timamu hawafiki 200.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Hapa Tanzania wananchi na viongozi wenye akili timamu wapo wachacheee mnoooooo yaani mnoooo, inawezekana kwenye hili taifa zima la watu wapatao milion 55+ watu wenye akili timamu hawafiki 200.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Aiseee umetutukana mno..Hebu tutake radhi watanzania!!
🤣 🤣 🤣 🤣
 
Huwa nawaza sana tulifikaje hapa tulipo leo,

Hivi ilikuwaje taifa lenye wasomi wazuri kabisa likaamua kufanya maamuzi ya kipumbavu ambayo hata Waroma wa kale walioishi miaka 2000 iliyopita wasingeyafanya. Hivi katika maksudi kabisa, taasisi nyeti za Tanzania ziliamini kabisa kwamba wao wangeweza kuifanya Tanzania nchi tajiri bila kushirikiana na dunia : Hivi ilikuwaje kabisa wataalamu wetu ambao wameenda shule, wanafahamu mifumo ya dunia ya kiuchumi, kiulinzi na kisiasa na wako kule USALAMA, BENKI KUU na MAMBO YA NJE wakakubaliana na huu upumbavu na kuanza kuutekeleza kabisa?

Mpangilio wa dunia yetu ya sasa uliwekewa msingi mwaka 1814 kule Vienna baada ya miaka 25 ya vita za mfalme Napoleon Bonaparte. Mwanamfalme Von Matternich alifahamu kabisa ili dunia isirudie kuingia kwenye songombingo la vita au kadhia yoyote ile, basi ni lazima watengeneze mfumo ambao uko kama utandu wa bui-bui: Kwamba maamuzi ya nchi moja yakifanyika lazima yaathiri nchi zote, hivyo nchi lazima zikubaliane kwenye baadhi ya mambo muhimu yanayowagusa wote. Ndiyo nadharia ya MZANI WA NGUVU (Balance of Power) ikazaliwa.

Mfumo wa dunia ya yetu hii tunayoishi leo hii umejengwa na matukio yaliyotokea miaka ya 1913, 1914, 1918, 1920, 1927, 1928, 1933, 1935, 1939, 1941, 1944, 1945, 1947, 1948, 1971 na 2001 . Kiufupi mlolongo wa matukio haya yafuatayo ndiyo yanatoa mwelekeo mzima wa mwenendo wa dunia yetu ya leo : Nashauri tufanya utafiti wa ndani kuhusu hili.

Formation of the Federal Reserve, World War I, Versailles Peace Treaty, Formation of League of Nations, Signing of Kellog-Briand Pact, The Great Depression, The Monte-Video Convention, America's Abolition of Gold Standard, World War II, The Bretton Wood Agreement, Formation of UNO, Signing of the GATT, Publication of the Universal Declaration of Human Rights, Nixon's Abandonment of the Gold Standard and China's Admission to the WTO n.k.

Mtaalamu yoyote yule wa Uchumi, Diplomasia, Ulinzi na Sheria ni lazima afahamu fika kuhusu haya ninayoyasema hapa. Kwamba dunia nzima tuko ndani ya utandu moja wa bui-bui. Huwezi kufanya jambo lolote lile ukiwa nje ya hapo. Ndani ya huu utandu wa bui-bui kuna kila aina ya watu: Wema na wabaya, Huru na watumwa, Masikini na tajiri, Wenye matumaini na wasio na matumaini, Wababe na dhaifu na Waamini Mungu na Maadui wa Mungu.

Huu ndiyo mfumo wa dunia (The World Order), huwezi kufanya maajabu yoyote yale ukiwa nje: Hata mataifa makubwa yenye nguvu duniani yanaheshimu huu mfumo kwasababu yanafahamu siku mfumo huu unaharibika basi ndiyo utakuwa mwisho wao. Hivyo kuna baadhi ya sheria hata yenyewe yatazifuata tu kwasababu zina manufaa kwao. Mwandishi George Orwell kwenye The ANIMAL FARM aliwahi kusema "All animals are equal, but some are more equal than others" hivyo hata kama tunataka usawa kuna wale waliotutangulia watakuwa mbele yetu kwenye baadhi ya mambo tu.

Sasa kinachoumiza wasomi wa Tanzania wenye PhD za sheria, uchumi na diplomasia. Huku wengine wakiwa na shahada kwenye masomo ya ulinzi, usalama na sayansi za vita wakiwa na akili timamu kabisa, wakaamua kuwa wapumbavu. Wakatundika elimu zao nyuma ya milango na kuanza kutekeleza jambo ambalo hata watu wa kale walioishi miaka 2000 hawakuwahi kuliwaza. Tanzania ina matatizo mengi, lakini ilikuwa inarekebishika vizuri tu kwasababu waliofikisha nchi yetu hapa wanafahamika na tunakula na kunywa nao kila siku.

Kuanza kulaumu mabeberu peke yake haisaidii kwasababu kuna wenzetu ambao wamefanikiwa kutumia mifumo hii-hii ya mabeberu kuwashinda mabeberu kiuchumi, kiulinzi na kisiasa. Ukweli ni kwamba huu mfumo umejengwa na mabeberu lakini hata walioujenga hawaundeshi wanavyotaka wao. Mataifa ya Magharibi ndiyo waanzilishi wa World Trade Organization (WTO) lakini leo hii, WTO imemnufaisha Uchina kuliko tangu alivyojiunga nao mwaka 2001 na mpaka sasa wanajutia kumkaribisha.

Nchi kama Singapore, India, Korea-Kusini na Brazil wamewezaje kucheza vizuri kwenye huu mfumo wa mabeberu hadi kufikia kuwango cha kuwashinda mabeberu kwenye baadhi ya mambo ??? Inahitaji akili ya ziada kutoka kwa Mungu ili kuweza kucheza kwenye huu mfumo. Raisi Donald Trump alijaribu kuitoa Marekani kwenye huu mfumo wa Vienna, lakini pamoja na maguvu yote ya Marekani alifanikiwa ???

Lakini leo hii kuna watu wako ndani ya IDARA ZA USALAMA ZA TANZANIA waliamini kabisa kwamba Tanzania inaweza kujitenga na dunia bila kupata madhara. Yaani waliamini kabisa na wengine bado wanaamini kabisa. Kuna wengine bado wanaamini kwamba mfumo wa Kileninisti na Kimaksisti (Marxist-Leninism) unaweza kutumika kuikomboa Tanzania. Sawa, lakini hata walioutuletea huu mfumo Warusi na Wachina, wamebadilisha sana baadhi ya hizi falsafa.

Dunia ya nchi moja kutawala wengine (Uni-Polar World) au nchi mbili kuamulia dunia nini kifanyike (Bi-Polar World) unakufa taratibu, ndiyo maana Marekani na Urusi wanapata shida kukubaliana na huu ukweli. Wao kama mataifa hawaanguki na bado wana nguvu, ila tu ni kwamba mataifa yale madogo na masikini kama Vietnam, Poland, Mexico yamekuwa makubwa yenye uchumi unaokua kwa kasi sana.

Tanzania tuliachiwa mtaji mkubwa sana kidiplomasia, ambao ulitujengea SOFT-POWER na INFLUENCE ambayo ilifanikisha ulinzi na usalama wa Tanzania kikanda na kidunia kwa kiwango kikubwa sana. Tuliingia sehemu ambazo hata nchi kubwa hazikuweza kuingia, tulipata taarifa nyeti kabla hata baadhi ya mataifa makubwa hayajazipata, tulipewa heshima ya kipekee (Special Treatment) ambayo mataifa mengine yenye uchumi mkubwa kuliko sisi barani Afrika hayakupewa.

Tuliogelea bwawa moja na mababeru, wakomunisti, wajahidina na wazayuni lakini tulitoka salama, kesho tena tukarudi kuogelea. We were a Shrimp among Whales, lakini bado tuliheshimika mno. Lakini leo hii hebu angalia, ile nguvu yote ambayo Mzee Nyerere na Raisi Mkapa walitutengenezea, imemomonyoka kisa kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uelewa mpana wa mahitaji ya nchi yetu na nafasi yetu hapa ulimwenguni.

Binafsi naamini ili tuweze kutoka hapa tulipo ni lazima NYUMBA ISAFISHWE aidha mbele ya majirani au kisiri. Mambo ya UHAINI, KUHODHI MADARAKA, KUPANGA KUUA MARAISI WASTAAFU,KUSHIRIKIANA NA MAADUI WA TAIFA na KUWINDANA KWA KUTUMIA MAKUNDI NDANI YA TASISI ZA KIUSALAMA (Cloack and Dagger Diplomacy) tulikuwa tunayasikia nchi jirani tu: Kwetu sisi yalikuwa ni MWIKO KABISA. Vitendo vya kihaini tulishaachana navyo awamu ya kwanza. Lakini leo kuna kakundi kalifikiri kabisa kangeweza kutupangia sisi Watanzania nani awe Mkuu wa nchi kweli?

Halafu bado haka kakundi kanalelewa tu: Kuhakikisha kwamba nchi haiwezi kurudi tena kule ilipotoka there's one place these people belong : The Cemetery, A Noose or A Bullet in the head!!! A prison term is not enough for these ruthless and deranged fanatics (This is legal, legitimate, justified and righteous).

Mara nyingine huwa naumia sana kuhusu Tanzania, natamani hata nisingekuwa nayafahamu haya yanayondelea.....
MALCOM LUMUMBA
 
Vizuri, naona ushaanza kukubali ukweli: Hii ni hatua nzuri kabisa ya kuanza kuelewa hoja nzito zinazojadiliwa hapa.
Sasa nawewe nakupa HOME-WORK kama mwenzako Mpinzire: Unafahamu maana ya neno DIPLOMASIA ???

NB: Ukinitajia maana ya hili neno basi ntaamini utakuwa kwenye nafasi nzuri kabisa ya kuelewa mifano yote nikupayo
Usianze kuleta habari za homework hapa! Hizo wape wanao hapo nyumbani kwako.

Mimi nataka uniambie ni wapi alisema hashirikiani na dunia na kwa vipi?
 
Usihangaike na watu ambao hawataki kuelewa rejea kwenye maandiko ya Plato baba wa falsafa kutoka ugiriki "myth of the cave" utaelewa kwanini watu wanakuja na mihemko nikwa sababu Watanzania wengi wanaishi kwenye ndani ya pango lenye giza na hawataki kutoka na ukajaribu kuwatoa wanaweza kukutoa roho please note my words. Uongozi uliopita ilijaza watu ujinga sana
Ukiwajazaje watu ujinga?
 
Hakuna ambae hakutaka kushirikiana na nchi nyingine ila kushirikiana kwa kutunyonya hilo ndo tulikataa awamu ya tano na inatakiwa iwe hivo kwa nchi zote za Africa gasa kusini mwa jangwa la sahara! Ile mikata ya kusaini mi nakuletea kandamili ww nipe Tanzanite hatuitaki

Sent using Jamii Forums mobile app
Kichwa cha mada yake tu ni upotoshaji. Umemjibu vizuri sana.Yaani wao wanaamini kushirikiana na dunia ni kuwapa madini na kupokea neti na Condoms. Ukisema hapana nataka niuze madini mwenyewe na niende dukani kununua neti mwenyewe tayari unakua hutaki kushiriki na dunia.Hili jukwaa Kuna muda watu wanaoonekana wana akili TIMAMU huwa wanapost vitu vya ovyo sana.
 
Hivi ni wapi jpm alikataa kushirikiana na dunia?

Alikatakaa kushirikiana kwenye nini hasa.?

Tupe mfano wa wapi alisema mimi sitaki ushirika na mtu kwenye hili na lile! Hebu taja.
Hahahahhah mkuu huyu jamaa kaandika vitu vya ovyo kabisa. Yaani Magufuli kukataa Lockdown basi hataki kushirikiana na dunia.
 
Kichwa cha mada yake tu ni upotoshaji. Umemjibu vizuri sana.Yaani wao wanaamini kushirikiana na dunia ni kuwapa madini na kupokea neti na Condoms. Ukisema hapana nataka niuze madini mwenyewe na niende dukani kununua neti mwenyewe tayari unakua hutaki kushiriki na dunia.Hili jukwaa Kuna muda watu wanaoonekana wana akili TIMAMU huwa wanapost vitu vya ovyo sana.
Anakera sana hapo ukimuuliza akitajie wanadiplomasia hasa anaona wanafaa hapa Tanznlania utasikia January, Nape, Membe wapiga porojo tupu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninavyosema mahusiano baina ya nchi (International Relations) nazungumzia vitu zaidi ya uwekezaji wa 50/50, zaidi ya sayansi na teknolojia, zaidi ya misaada. Hapa sasa kwenye mahusiano ya kimataifa (International Relations) ndiyo kinakuja kitu muhumu kabisa kiitwacho Diplomasia (Diplomacy): Mahusiano ya kimataifa (International Relations) na Diplomasia (Diplomacy) ni dhana mbili tofauti kabisa, japo huwezi kuzitenga.

Sasa ili ufanikishe mahusiano ya kimataifa (International Relations) ili uweze kupata hizo 50/50, teknolojia, ulinzi au hata misaada ni lazima uwe na chombo kiitwacho Diplomasia (Diplomacy). Lakini ili hichi chombo kiitwacho diplomasia kiweze kufanya kazi vizuri katika kujenga, kufanikisha na kuimarisha mahusiano ya kimataifa (International Relations) ni lazima nchi husika itengeneze kitu kiitwacho Sera ya Mambo ya Nje (Foreign Policy).

Sasa basi ili kuelewa nini kilifanyika hapa Tanzania ni lazima ufahamu mambo niliyoyataja hapo juu:
1. Mahusiano ya kimataifa (A State of International Relations).
2. Dhana ya neno diplomasia (A Concept of Diplomacy).
3. Sera ya mambo ya nje ya Tanzania (Tanzania's Foreign Policy).

Sisi ili kupima mafanikio ya mtu huwa tunaangalia haya mambo matatu ambayo huingiliana. Ulinzi, Rasilimali, Uwekezaji, haki za binadam, soko ya kimataifa, na Misaada ni sehemu ndogo sana ambazo zinaingia kwenye haya mambo makuu matatu. Bahati mbaya sana sasa, vijana wengi wa kitanzania ambao kazi yao ni kusifia na kuunga mkono kila kitu hawana uelewa wowote ule katika hili.

Ndiyo maana huishia kusema tunachuki na marehemu lakini ukweli wenyewe ndiyo huu ambao wengi wao hawataki kuukubali.
We ni mshamba tuu wa wazungu.. kwako kuona rais anasafiri nje ya nchi ndio sera ya mambo ya nje
 
Back
Top Bottom