Imani ya Bunge haiwezi kujengwa chini ya Tulia Ackson

Imani ya Bunge haiwezi kujengwa chini ya Tulia Ackson

Dah!!!

Watu wanataka Spika atakayemlamba miguu Rais...🤔🤔, yale yale mambo ya Job na JPM
 
Kwanza ni mfuasi na kiongozi mwandamizi wa lile kundi alilotoka Ndugai, kundi lililotaka Rais Samia asigombee 2025 na kupanga mikakati ya kumdhoofisha Mh. Rais.

Pili ni mtu asiyeamini katika kazi za Rais Samia, Tulia hakuwahi kuvaa barakoa wala kuhamasisha chanjo hadharani sio ndani wala nje ya bunge.

Tatu Tulia amekuwa aki provoke Mawaziri na wabunge walio nje ya kundi lao wakati wa vikao vya bunge na kuwapa credit wale walio katika kundi lao almaarufu "Sukuma Gang".

Nne Kundi la upinzani kwa Rais Samia bungeni almaarufu kama Sukuma Gang linamtegemea Tulia kama muhimili wao katika kujiimarisha kuelekea 2025 baada ya Ndugai kufurushwa

Tano Tulia hajawahi kujivunia kuwa na Rais Mwanamke. Tangu Samia aingie madarakani tulia is upset hatujui sababu ni msiba ule au ana conflict binafsi na Madam President

Vipimo vya uzani, vinakataa kuwa Tulia anaweza kubahatika kuwa kiongozi kwenye muhimili wa Bunge ama Spika ama kuendelea kuwa Naibu baada ya hili sakata la boss wake ambaye yeye ni mtu wa jikoni kabisa.

Vipimo vinasoma chini ya uzani wa wastani.

Rais Samia 2025
KAZI IENDELEE
Hapa hoja zingine ni mufilisi kabisa.
Mfano, "hajawahi kuvaa barakoa" so what? Tusiwe na akili za kushikiwa. Wewe unavaa barakoa kwasababu rais anavaa au kwasababu unajihisi uko hatarini?

Eti hajawahi kujivunia kuwa na raisi mwanamke? Hii ni hoja mfu kabisa. Tanzania haihitaji raisi mwanamke ila inahitaji rais atakayetoa dira ya kuondoa umasikini ujinga na maradhi bila kujali jinsia. Unapojivunia uwanamke kwani tunataka azae au unajivunia kipi?

Tumedhoofishwa kifikra hadi tunasifu vitu vya kipumbavu. Kwa namna hii tutatawaliwa na mabeberu hadi tunyooke.
 
Tano Tulia hajawahi kujivunia kuwa na Rais Mwanamke. Tangu Samia aingie madarakani tulia is upset hatujui sababu ni msiba ule au ana conflict binafsi na Madam President

Vipimo vya uzani, vinakataa kuwa Tulia anaweza kubahatika kuwa kiongozi kwenye muhimili wa Bunge ama Spika ama kuendelea kuwa Naibu baada ya hili sakata la boss wake ambaye yeye ni mtu wa jikoni kabisa
Mshana, huu utaratibu wa kuchangia hoja kwa kukopi hoja ya mtu unakera. Maadili ya uandishi hayaruhusu hii kitu. Ni total plagiarism. Unaweza kufanya vizuri zaidi. Wewe ni mkongwe hapa. Kama umependa mchango wa mtu basi like tu usonge mbele.
 
Mimi binafsi Nina Imani na Tulia anafaa na ni msomi mzuri sana wa sheria
 
Nashauri nafasi ya Spika itangazwe wenye sifa waombe maana Spika siyo lazima atokane na wabunge.Naamini kuna watanzania wazuri zaidi wa kuweza kuliongoza hilo bunge.Mungu ibariki Tanzania.
 
Kimsingi alishiriki uovu mwingi tu alioufanya boss wake, nimatarajio kuwa kilichotokea ni somo tosha, na hata covid19 atajitenga nao iwapo akamrithi boss wake.
Hivi Ana mume?
Naomba mwenye wasifu wake anisaidie.
 
Mshana, huu utaratibu wa kuchangia hoja kwa kukopi hoja ya mtu unakera. Maadili ya uandishi hayaruhusu hii kitu. Ni total plagiarism. Unaweza kufanya vizuri zaidi. Wewe ni mkongwe hapa. Kama umependa mchango wa mtu basi like tu usonge mbele.
Mwache mimi nimemruhusu
 
Nashauri nafasi ya Spika itangazwe wenye sifa waombe maana Spika siyo lazima atokane na wabunge.Naamini kuna watanzania wazuri zaidi wa kuweza kuliongoza hilo bunge.Mungu ibariki Tanzania.
Spika lazima atokane na CCM ni nafasi vyeti hawezi kupewa mtu from ni where
 
Mwache mimi nimemruhusu
Sawa mkuu. Lakini si kwako tu, yeye akipendezwa na mchango fulani hukopi na kupaste kama vile yeye ndiye kaandika. Unakuta baadhi yetu tunakerwa kusoma kitu kilekile kwa mchangiaji mwingine. Nimemshauri akiweza a "like" au a "quote" kisha aweke mchango wake pale.
 
Sawa mkuu. Lakini si kwako tu, yeye akipendezwa na mchango fulani hukopi na kupaste kama vile yeye ndiye kaandika. Unakuta baadhi yetu tunakerwa kusoma kitu kilekile kwa mchangiaji mwingine. Nimemshauri akiweza a "like" au a "quote" kisha aweke mchango wake pale.
Inaitwa kukazia maarifa
 
Back
Top Bottom