Imebaki miaka 18 mafuta kuisha United Arab Emirates

Hao jamaa wana akili kuliko sisi ndiomaana tumewazidi rasilimali na wao wametuzidi utajiri,

Mtu mwenye akili kuliko wewe hawezi kutegemea vitega uchumi vyako wewe husie na akili kuendesha maisha yake, vinginevyo hana akili ila ni mjanja na mlaghai .
 
... lango (entry/exit) likishadhibitiwa na third-party umekwisha! Hawa CCM sijui wana akili za aina gani.
 
Yaani masikini wa mwisho anapomcheka tajiri
Asante kwa kuongezea hili
Mtu akiwa masikini sijui kwa nini na roho inakuwa ya kishetani

Ndio maana kwenye dua tunaomba Mungu atuepushe na umasikini
 
Hawa wanaweza kutumia hata mabavu inavyoashiria sasa. Hasa ukichanganya na wadini uchwara wasiojitafakari!
 
We ndo mana unaitwa kilaza una google google tu hata huelewi maana zake.

Chukua kilichoandikwa hapo juu kwenye screenshot yako Dubai ilipeak 1991 kwa kuproduce barel 400,000 kwa siku hizo ni data za zamani siku hizi hawana uwezo huo ila kukuelewesha zinatosha.

Zidisha 400,000 x 100 unapata thamani ya barel kwa siku ni Dola 40,000,000 Zidisha kwa siku 365 Unapata Dola Bilioni 14.

Gdp ya Dubai ni Dola Bilioni 500 hebu nielezee Genious kama mafuta hayafiki hata Dola Bilioni 20 hizo zaidi ya Dola Bilioni 400 na zaidi zimetoka wapi?.
 
Mdogo wangu mimi ni kichwa Math. Je, unajua calculus?
 
Dalili za Nauru zinawanukia kwa kasi. Sasa wanatafuta kwa nguvu zote na kwa hila zote makoloni au ardhi katika nchi zingine.
Ndio maana wanakuja kwa kasi Africa na viongozi wetu bila aibu au soni wanagawa raslimali zetu kwa" vipande vya fedha"
 
Ngoja nikupatie maelezo marefu kidogo kuhusu ndugu zako. Na ujue kuwa hawana future


Baadhi ya hatari kuu ambazo zinaweza kuathiri uchumi wa UAE siku za usoni ni:

1. Mabadiliko ya Bei ya Mafuta: UAE inategemea sana mauzo ya mafuta, na mabadiliko ya bei ya mafuta yanaweza kuathiri sana uchumi wake. Kupungua kwa bei ya mafuta kunaweza kusababisha mapato ya serikali kupungua, nakisi ya bajeti, na hata kusababisha mdororo wa uchumi.

2. Utulivu wa Kisiasa: UAE iko katika eneo lenye mizozo ya kisiasa, na ongezeko la migogoro au mvutano wa kisiasa Mashariki ya Kati kunaweza kuathiri vibaya uchumi wake. Hatari hizi ni pamoja na migogoro ya kikanda, mzozo wa biashara, na vikwazo, ambavyo vinaweza kuvuruga biashara na kuathiri imani ya wawekezaji.

3. Mkwamo wa Uchumi wa Kimataifa: Kama uchumi unaotegemea sana biashara ya kimataifa, UAE inaweza kuathiriwa na kupungua kwa uchumi wa kimataifa. Kupungua kwa uchumi katika nchi kubwa kama Marekani, China, au Ulaya kunaweza kuathiri mahitaji ya bidhaa za UAE, utalii, na uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni (FDI).

4. Utegemezi kwa Wafanyakazi Kutoka Nchi Za Nje: UAE inategemea nguvu kazi kubwa ya wahamiaji katika sekta mbalimbali, ikiwa ni pamoja na ujenzi, ukarimu, na huduma. Mabadiliko katika sera za uhamiaji, sababu za kisiasa, au hali ya kiuchumi katika nchi za asili zinaweza kuathiri upatikanaji na gharama ya ajira, na hivyo kuathiri shughuli za biashara na ukuaji wa uchumi.

5. Hatari katika Soko la Makaazi: UAE imekuwa ikishuhudia ukuaji mkubwa katika sekta ya ujenzi, hasa Dubai na Abu Dhabi. Hata hivyo, ukuaji haraka na tabia ya kubahatisha inaweza kusababisha uwepo wa wingi wa nyumba, marekebisho ya bei, na hatari za uwezo katika sekta ya benki ikiwa thamani ya mali ishuke kwa kiasi kikubwa.

6. Mabadiliko ya Tabianchi na Upungufu wa Maji: UAE inakabiliwa na upungufu wa maji na ni hatari kwa athari za mabadiliko ya tabianchi, ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa usawa wa bahari na matukio ya hali ya hewa kali. Changamoto hizi zinaweza kuathiri kilimo, miundombinu, na uendelevu wa uchumi kwa ujumla, na hivyo kuhitaji uwekezaji katika usimamizi wa maji na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

7. Kuvurugika kwa Teknolojia: Ingawa UAE imekuwa mstari wa mbele katika kukumbatia teknolojia na uvumbuzi, maendeleo ya haraka na kiotomatiki yanaweza kuvuruga sekta za jadi na soko la ajira. Nchi inahitaji kuendelea kubadilika na kuwekeza katika kuendeleza nguvu kazi yenye ujuzi ili kupunguza mabadiliko yoyote ya kuzorota.

8. Magonjwa na Hatari za Afya: Mlipuko wa magonjwa ya kuambukiza, kama janga la COVID-19, yanaweza kuwa na athari kubwa kwa uchumi. Kuvurugika kwa usafiri, biashara, na utalii kunaweza kuathiri sekta muhimu za uchumi wa UAE,kama vile anga za ndege, ukarimu, na rejareja.
 
Mtu mwenye akili kuliko wewe hawezi kutegemea vitega uchumi vyako wewe husie na akili kuendesha maisha yake, vinginevyo hana akili ila ni mjanja na mlaghai .
Duuuh! Ndio umeandika upuuzi gani hapa? Nani anategemea rasilimali zako kuendesha maisha yake? Achana na stori za vijiweni wewe ishi kwenye uhalisia, wewe unategemea utalii ila mwenzio anaingiza pesa nyingi kwenye utalii kuliko wewe
 
"Madini hata kama yako mbugani lazima tuyachimbe. Wataweka wawekezaji. Roho iliniuma sana. Toka hapo niliona huyu mama kaja kutapanya na kuharibu mali ya wa Tanzania. Nilijua hatuna kiongozi."
Daaaah Duniani wawili wawili hiii kauli namimi ilifanya niwaze kama wewe.
 
Hivi wewe kweli unaijua UAE?
You must be joking.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…