Imekaaje Waziri Mkuu kumkaripia Daktari kwa ujenzi hafifu wa Hospitali?

Imekaaje Waziri Mkuu kumkaripia Daktari kwa ujenzi hafifu wa Hospitali?

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
20221019_080728.jpg

Kwanza nitangulie kusema kuwa sina chuki waka hila na mh. Waziri Mkuu Majaliwa. Waziri mkuu ndiye msimamizi wa shughuli ZOTE za kiserikali nchini.

Hata hivyo hili nililolisikia kwenye vyombo vya habari ndiyo vinaelezea ukakasi wa siasa tunazojiwekea zisivyoendana na kanuni na utaratibu wa hususan suala la ujenzi nchini.

Mh Waziri Mkuu anaonekana akimkaripia Daktari wa binadamu kwa ujenzi hafifu hasa milango katika hospitali ya Namtumbo huko Ruvuma.

Huyo Daktari anaonekana wala hajui kitasa na bawaba vinapatikana wapi!

Lakini inakuwaje madudu haya hayakuonekana mapema, ilhali wasimamizi wa mradi wapo, Mtendaji wa Halmashauri yupo, Mkuu wa Wilaya Yupo, Mkuu wa Mkoa yupo.
Waziri Mkuu atakagua yeye mwenyewe miradi mingapi kuibua madudu?

Hata hivyo, tunavuna tulichopanda, shoddy workmanship na ukanjanja katika ujenzi.

Hayo ndio matokeo ya FORCE ACCOUNT tuliyopigia kelele sana huko nyuma.

Jengo limekamilika ndiyo kwa fedha kiduchu, wanasiasa wanasema "value for money".
Lakini sasa ndio tunaona the real poor value for cheap and shoddy works, cannot endure durability in time of say 10 yrs.

Kifupi wanasiasa walioingiza FORCE ACCOUNT arbitralily katika sekta ya ujenzi watavuna matokeo mabaya hata kabla ya kumaliza muda wao madarakani.

Kitaalam tunahitaji kuwa na Technical Audit kwa miradi yote iliyotekelezwa kwa Force Account ili yafanyiwe tathmini na marekebisho kama hilo alilogundua Waziri Mkuu.
 
Nchi hii ya ajabu sana
Daktari anaacha taaluma yake anatakiwa kusimamia ujenzi
Mwalimu mkuu hafundishi kazi kusimamia ujenzi wa madarasa
Hivi ile PWD iliyokuwa inasimamia kazi zote za ufundi za serikali ilifia wapi?
 
Ni ujinga. Daktari siyo engineer.

Hii nchi viongozi wamejenga tabia ya kutafuta sifa na umaarufu kwa kufoka mbele ya kamera ama kusimamisha mtu kazi ndiyo .

Kila wilaya kuna mhandisi qmbaye kazi yake ni kusimamia ujenzi na kukagua ubora wa miradi iweje alaumiwe daktari?

Yaani huu ujinga utatuchelewesha Sana.
 
Hata kama ni chuki kwa waziri mkuu sasa zimekuzidi mpaka zinakuondoa akili kabisa ya kufikiria.

Naomba nikujibu kama utanielewa. Mara zote muwajibikaji mkuu ni mkuu wa sehemu husika ambao ni CEO au DG au DED na vivyo hivyo kwa upande wa hospitali za mikoa na wilaya ni waganga wafawidhi. Hao waganga wafawidhi ndio wasimamizi wa uendeshaji wa shughuli na ndio wawajibikaji wakuu wa maeneo hayo.

Pale waziri mkuu hajamkaripia daktari kama unavyotaka kupotosha ila amekaripiwa mtu ambaye alitakiwa kuhakikisha ubora na ufanisi.

Najua utaniuliza mganga mfawidhi atajuaje ubora wa vifaa vya ujenzi? Kwanza alitakiwa kufanya kazi kwa karibu na wataalamu ili wamsaidie vyema. Pia, kilichofanyika kwenye hiyo milango ni uhuni kabisa na wala hahitaji kuwa na elimu kubwa kujua kuna ubovu.

Mwisho, mpaka suala linaloonekana kwa macho kabisa kwamba ni bovu na bado wahusika hawakuona kuna mawili either milango hiyo ilikusudiwa kuwekwa kwa namna hiyo au kuna upigaji wa kutisha?
 
Hata kama ni chuki kwa waziri mkuu sasa zimekuzidi mpaka zinakuondoa akili kabisa ya kufikiria.

Naomba nikujibu kama utanielewa. Mara zote muwajibikaji mkuu ni mkuu wa sehemu husika ambao ni CEO au DG au DED na vivyo hivyo kwa upande wa hospitali za mikoa na wilaya ni waganga wafawidhi. Hao waganga wafawidhi ndio wasimamizi
Acha ujinga mkuu, miradi yote ya serikali ina consultants ambao pia ni wasimamizi wakuu wa miradi.

Hawa ni wataalum wa ujenzi...sio sahihi kuwalaumu hawa wakuu wa shule au hospital kwa utendaji usioridhisha.

Usitufanye wote ni vilaza.
Ukitaka ufafanuzi sema nikueleze hadi aina na idadi ya condukts ambao husimamia.
 
waziri ana haki ya kumkalipia daktari km daktari ndio alipewa dhaman ya kusimamia ujenzi wa hospital.

ila je kwa akil ya kawaid tu daktari anaweza kusimamia maswala la ujenzi 🤔
Mkuu, kwa hiyo daktari akijenga nyumba yake binafsi atapigwa sana sababu hajui chochote kuhusu ubora kwenye ujenzi, pamoja na kwamba si taaluma yake na yeye ana macho anaona na pia anayo nafasi ya kufanya consultation kwa wataalamu husika ndani ya halmashauri na wengine wengi wamejaa huko mitaani.​
 
Mkuu, kwa hiyo daktari akijenga nyumba yake binafsi atapigwa sana sababu hajui chochote kuhusu ubora kwenye ujenzi, pamoja na kwamba si taaluma yake na yeye ana macho anaona na pia anayo nafasi ya kufanya consultation kwa wataalamu husika ndani ya halmashauri na wengine wengi wamejaa huko mitaani.​
Daktari ana mzigo mkubwa sana wa kutoa huduma kwa wagonjwa atashughulikia mangap kwa mda mmoja.

kwani Tanzania tuna wakandarasi wangap wa ujenzi kwanini asitafutwe mkandarasi asimimie ujenzi wa jengo ambalo ni kwa ajiri ya matumizi ya wengi ?
 
Acha ujinga mkuu, miradi yote ya serikali ina consultants ambao pia ni wasimamizi wakuu wa miradi.

Hawa ni wataalum wa ujenzi...sio sahihi kuwalaumu hawa wakuu wa shule au hospital kwa utendaji usioridhisha.
Nimeandika kila kitu hivyo sio kosa langu kwa kuwa umeamua kusoma unapopataka
 
View attachment 2391683

Kwanza nitangulie kusema kuwa sina chuki waka hila na mh. Waziri Mkuu Majaliwa. Waziri mkuu ndiye msimamizi wa shughuli ZOTE za kiserikali nchini...
Kwa kuongezea hapo, Waziri mkuu nae ni kiongozi wa kisiasa na ni mwalimu wa michezo/mazoezi kitaaluma lakini hili halizuii kuona kitu kibovu. Ila usaidizi wa kujua zaidi ubovu technically lazima wahandisi washirikishwe kwenye hili badala ya kuangalia vitu kwa je tu au finishings.

Dr anawajibika kwani ndie kiongozi wa eneo huzika lakini je alikuwa na wataalam wa kiuhandisi katika kumsaidia kusimamia ujenzi wenyewe? Back to force account, huu ni mpango unaochoma fedha za serikali badala ya kutekeleza malengo ya serikali kwa ufanisi na ubara unaotakiwa, the GOV shall learn it in a short while.

Standard practice/procedures in construction of infrastructures zipo na serikali inazijua na husimamiwa na ERB, CRB, Construction Council, Institution of engineers, TBS, FIDIC, PPRA, etc.

Sasa hizi methods mbadala kwa serikali zinatoka wapi tena kwa miradi yake kwa wananchi. Serikali imesomesha wahandisi wengi wanazurura mitaani bila kazi huku miradi inatekelezwa kwa wananchi ikisimamiwa na wanasiasa badala ya wataalam. Tujitafakari.
 
waziri ana haki ya kumkalipia daktari km daktari ndio alipewa dhaman ya kusimamia ujenzi wa hospital.

ila je kwa akil ya kawaid tu daktari anaweza kusimamia maswala la ujenzi 🤔
Ha ha ha !
Mbona unaunga mkono kilichaofanyika na kuhoji uhaali wake.
Jibu unalo!
 
Back
Top Bottom