Imekaaje Waziri Mkuu kumkaripia Daktari kwa ujenzi hafifu wa Hospitali?

Imekaaje Waziri Mkuu kumkaripia Daktari kwa ujenzi hafifu wa Hospitali?

Waziri Mkuu anafanya vema kuonyesha usimamizi mbovu wa miradi.
Lakini nijiulize, nani alisimamia hili jengo hadi kukamilika?
Tatizo sio kusimamia. Liliagizwa lijengwe kwa shilingi ngapi? Je hicbo kiasi ndicho kinachotakiwa kujenga jengo la hospitali kwa ukubwa huo na standard inqyotakiwa? Hapi naona ni siasa inatumika kulaumu asiyestahili. Ukweli ukiwekwa wazi unaweza kuta hao wanaolaumu ndio wa kulaumiwa na sio watekelezaji.

Mfano unaweza kuta Halmashauri inahitaji majengo ya vyumba vya madarasa kumi na gharama za madarasa hayo ni sh milioni 300 lakini inaletwa hela milioni mia na unaambiwa lazima ijenge madarasa ku.mi na utumie force account yaani kila darasa milioni kumi. Afisa wa wilaya anamuita fundi na kumwambia nataka unijengee darasa kwa sh milioni 10 halafu darasa likikamilika kiongozi anataka liwe bora, mbao za milango na madirisha zikiwa ni sypras au bqti kikiwa geji 33 ushangae. Ndio maana mafundi wengine ukiwaambie wajenge kwa kiasi kidogo cha pesa wanakataa hiyo kazi kwa,sababu wanajua huko mbeleni itakuwa awama.

Utaratibu wa ujenzi jengo la umma lazima lichorwe, materials yote yatakayotumika yaainishwe na bei halisi za hayo meterials pamoja na gharama za ufundi ( BoQ inaandaliwa kabisa) ndipo anatqfutwa kqndarasi anajenga kwa kufuata michoro na anakaguliwa na consultant hatua kwa hatua na kulipwa kwa kila hatua, katika mazingira haya jengo likiwa halina viwango ni rahisi kumbana kandarasi na consultant aliyekuwa anaidhinisha kila hatua iliyojengwa kabla ya kandarasi kulipwa kwa kila hatua. Lakini force account haina michoro wala BoQ .
 
View attachment 2391683

Kwanza nitangulie kusema kuwa sina chuki waka hila na mh. Waziri Mkuu Majaliwa. Waziri mkuu ndiye msimamizi wa shughuli ZOTE za kiserikali nchini.

Hata hivyo hili nililolisikia kwenye vyombo vya habari ndiyo vinaelezea ukakasi wa siasa tunazojiwekea zisivyoendana na kanuni na utaratibu wa hususan suala la ujenzi nchini.

Mh Waziri Mkuu anaonekana akimkaripia Daktari wa binadamu kwa ujenzi hafifu hasa milango katika hospitali ya Namtumbo huko Ruvuma.

Huyo Daktari anaonekana wala hajui kitasa na bawaba vinapatikana wapi!

Lakini inakuwaje madudu haya hayakuonekana mapema, ilhali wasimamizi wa mradi wapo, Mtendaji wa Halmashauri yupo, Mkuu wa Wilaya Yupo, Mkuu wa Mkoa yupo.
Waziri Mkuu atakagua yeye mwenyewe miradi mingapi kuibua madudu?

Hata hivyo, tunavuna tulichopanda, shoddy workmanship na ukanjanja katika ujenzi.

Hayo ndio matokeo ya FORCE ACCOUNT tuliyopigia kelele sana huko nyuma.

Jengo limekamilika ndiyo kwa fedha kiduchu, wanasiasa wanasema "value for money".
Lakini sasa ndio tunaona the real poor value for cheap and shoddy works, cannot endure durability in time of say 10 yrs.

Kifupi wanasiasa walioingiza FORCE ACCOUNT arbitralily katika sekta ya ujenzi watavuna matokeo mabaya hata kabla ya kumaliza muda wao madarakani.

Kitaalam tunahitaji kuwa na Technical Audit kwa miradi yote iliyotekelezwa kwa Force Account ili yafanyiwe tathmini na marekebisho kama hilo alilogundua Waziri Mkuu.
Wewe tatizo lako ni utoto unakusumbua. Daktari ni procurement entity na ni kiongozi, hivyo anatakiwa kujua hivi vitu!!!!!
 
Jidu La Mabambasi

Hueleweki unatetea nini katika andiko lako.

Je!
Ni waziri kumkaripia Daktari mkuu wa hospitali husika?

Au ni kuiponda "FORCE ACCOUNT"kwa sababu kuna namna inaondoa ule upigaji wa kimfumo?
Mkuu naona tatizo hulioni bayana!
Waziri Mkuu anasimamia miradi yote ndani ya serikali, hilo ni jukumu lake na kwa kweli hana makosa kumchukulia hatua mtu yeyote aliye chini yake , alimradi anavurunda.
Ndiyo kazi yake.

Lakini sera mbovu za utekelezaji wa miradi ndiyo imempelekea Waziri Mkuu kumkaripia Daktari ambaye hana taaluma yoyote katika ujenzi.
Thats the paradox!
Unamtandika punda kwa kushindwa kuogelea kama samaki.

Kimsingi inabidi serikali itambue kuwa haya ndio madhara ya sera za kuitumia Force Account kwenye miradi ya serikali, badala ya traditional project management and execution method.

Miradi ya Force Account , iliyosimamiwa na watu wasion na utaalam wa ujenzi inabidi yote ifanyiwe tathmini ya ubora wake, kabla hayajatokea madudu kama alivyoyaona Waziri Mkuu hadharani.
 
Wewe tatizo lako ni utoto unakusumbua. Daktari ni procurement entity na ni kiongozi, hivyo anatakiwa kujua hivi vitu!!!!!
Procurement ya dawa na vifaa vya fani yake ya uDaktari, ndiyo haswa eneo lake.

Elewa kuwa daktari hawezi ku procure jengo la mabilioni.
Usipolielewa hilo basi hapo ulipo wewe ni mzigo.
 
20221017_213946.jpg



Hah
 
Madaktari walipewa dhamana ya Kusimamia hiyo miradi kama ilivyo kwa wakuu wa shule.... Pesa ziliwekwa kwenye akaunti za taasisi husika hivyo kwa vyovyote vile daktari anahusika....
Je ilikuwa ni sahihi, madaktari kuwa wasimamizi wa miradi wasio na taaluma nazo ?!
 
Tatizo sio kusimamia. Liliagizwa lijengwe kwa shilingi ngapi? Je hicbo kiasi ndicho kinachotakiwa kujenga jengo la hospitali kwa ukubwa huo na standard inqyotakiwa? Hapi naona ni siasa inatumika kulaumu asiyestahili. Ukweli ukiwekwa wazi unaweza kuta hao wanaolaumu ndio wa kulaumiwa na sio watekelezaji.

Mfano unaweza kuta Halmashauri inahitaji majengo ya vyumba vya madarasa kumi na gharama za madarasa hayo ni sh milioni 300 lakini inaletwa hela milioni mia na unaambiwa lazima ijenge madarasa ku.mi na utumie force account yaani kila darasa milioni kumi. Afisa wa wilaya anamuita fundi na kumwambia nataka unijengee darasa kwa sh milioni 10 halafu darasa likikamilika kiongozi anataka liwe bora, mbao za milango na madirisha zikiwa ni sypras au bqti kikiwa geji 33 ushangae. Ndio maana mafundi wengine ukiwaambie wajenge kwa kiasi kidogo cha pesa wanakataa hiyo kazi kwa,sababu wanajua huko mbeleni itakuwa awama.

Utaratibu wa ujenzi jengo la umma lazima lichorwe, materials yote yatakayotumika yaainishwe na bei halisi za hayo meterials pamoja na gharama za ufundi ( BoQ inaandaliwa kabisa) ndipo anatqfutwa kqndarasi anajenga kwa kufuata michoro na anakaguliwa na consultant hatua kwa hatua na kulipwa kwa kila hatua, katika mazingira haya jengo likiwa halina viwango ni rahisi kumbana kandarasi na consultant aliyekuwa anaidhinisha kila hatua iliyojengwa kabla ya kandarasi kulipwa kwa kila hatua. Lakini force account haina michoro wala BoQ .
Asante sana mkuu.
Umelieeza tatizo kwa njia rahisi na inayoeleweka kwa kile kinachofaanyika kule mikoani.
Tatizo wanasiasa wamelifumbia macho hili tatizo.
Makandarasi na wataalam wa ujenzi Engineers, Quantity Surveyors na Architects wamekuwa wakilililalamikia sana suala hili.
 
Procurement ya dawa na vifaa vya fani yake ya uDaktari, ndiyo haswa eneo lake.

Elewa kuwa daktari hawezi ku procure jengo la mabilioni.
Usipolielewa hilo basi hapo ulipo wewe ni mzigo.
Naongea kitu nafahamu dogo
 
Mkuu jiridhishe kwamba wewe ni mbumbumbu wa kazi za miradi.

Mradi unapojengwa huwa unakuwa chini ya Clien(serikali)t, ambapo hapo ni wizara ya Afya na siyo Daktari.
Na Client hawezi kuhamishia majukumu ya usimamizi wa mradi kwa mtu ambaye hajauasisi.
Na hio ndio tatizo la viongozi/wanasiasa wengi.
Wao wanafikiria kiserikali kazi yao ni kutafuta fedha tu, usimamizi utafanywa na kilaza yeyote aliyekaribu, na mara nyingi hajui hata mradi wenyewe.
Katika hili, Daktari hapo hajui msingi unajengwaje wala wapi dawa ya mchwa unaokula mbao, na hata mix ya zege inaendaje.

Ujenzi wa mradi kiserikali katika miaka ya karibuni umefanywa kiholela kabisa kwa kutumia ati Force Account.
Kuna madudu mengi tu tutayagundua huko mbele ya safarai.

Mradi unapokwisha , sasa ndio operational staff wanaingia, yaani wakabid
Mkuu, labda niseme tu kwamba "waafrika bado tuna safari ndefu sana ya kuja kuwa kama wazungu kwenye suala zima la maendeleo"

Naongea kitu nafahamu dogo
Achana na huyo dogo ana kasumba ya migomo na maandamano. Hajui hata afisa manunuzi mkuu ni nani?
 
PM anatafuta publoc sympathy atupishe......amechafuka kashfa kibaoooo
 
Hakika ni ya ajabu sana
Nchi hii ya ajabu sana
Daktari anaacha taaluma yake anatakiwa kusimamia ujenzi
Mwalimu mkuu hafundishi kazi kusimamia ujenzi wa madarasa
Hivi ile PWD iliyokuwa inasimamia kazi zote za ufundi za serikali ilifia wapi?
 
Madaktari wala wakuu wa shule hawapaswi kusimamia miradi ya ujenzi kwani sio taaluma yao na pia wana majukumu mengine mazito na ya msingi zaidi.
Madaktari walipewa dhamana ya Kusimamia hiyo miradi kama ilivyo kwa wakuu wa shule.... Pesa ziliwekwa kwenye akaunti za taasisi husika hivyo kwa vyovyote vile daktari anahusika....
 
Atapigwa kama amewapa hiyo kazi ya kujenga vibaka wasiozingatia taaluma yao.
Mkuu, kwa hiyo daktari akijenga nyumba yake binafsi atapigwa sana sababu hajui chochote kuhusu ubora kwenye ujenzi, pamoja na kwamba si taaluma yake na yeye ana macho anaona na pia anayo nafasi ya kufanya consultation kwa wataalamu husika ndani ya halmashauri na wengine wengi wamejaa huko mitaani.​
 
Mafisadi yanamuwinda waziri mkuu ila hawindiki, analindwa na nguvu ya wananchi
 
Back
Top Bottom