Inakuwaje Marehemu Milton Lupa anateuliwa mkeka mpya wa Rais?

Inakuwaje Marehemu Milton Lupa anateuliwa mkeka mpya wa Rais?

Kwahiyo possibly kifo chake si cha kawaida pia. Huenda alikuwa mwiba kila alikokuwa anapelekwa.

Uteuzi umefanyika huku kukiwa na timu nyingine inamwinda kumla kichwa na wakati anaenda kuripoti timu ya mauaji ikawa nayo imefanikiwa sasa ile taharuki wakajikuta wamemiss mawasiliano au mwenyezi Mungu tu akaamua kuwaumbua.

Naamini kifo chake kina utata sana.
Aisee....
 
Rushwa na kuuza Mali ya Asili kumeshawalevya wanajifanyia mambo bila ya Umakini.
 
Watu wameamua kupambana ki oldschool hadi ifike 2025 kazi ipo
 
Je, watatengua uteuzi wake au itapita kimya kimya. Nimeona mkeka mwingine. Pengine atateuliwa mwingine qabadala yake kimya kimya.
 
Mkuu. Ukijua na kukubali kwamba HAKUNA BINADAMU ALIYE MKAMILIFU ninaamini hutaona ni kitu cha ajabu sana kwa jina la marehemu kuwepo miongoni mwa walioteuliwa kwani umauti ulimpata mhusika siku moja tu kabla ya jina lake kuwepo kwenye list ya wateule.
Halafu kosa hilo ni kosa linalosahihishika (curable) kwa kufanya replacement ya mtu mmoja tu.
Mbona tunaikuza sana dosari ndogo hivi na kuipa hadhi ya kuwa ni kosa kubwa? Tukio hili Halisameheki na wala halivumiliki kana kwamba ni Grave Offence?
Mimi nakubali kwamba ni kweli inashangaza lakini ninaona(kwa maoni yangu) ni jambo dogo na la kwaida na marekebisho yanaweza kufanyika mapema na mchezo ukamalizika. (I stand to be corrected)
Ukisema ni jambo dogo na linarekebishika utashindwa kuweka mstari, Dkt. atakata mkono wa mwanao tofauti na maelekezo ya matibabu na kusema ni kosa dogo la kibinadamu..utakubali? Kosa ni kosa bila kujali limetendwa wapi na nani!
 
This is a grave mistake.

Ndio maana hata mikataba ya mikopo ya fedha za Korea kila kiongozi wa serikali anasema lake.

Nchi hii chini ya serikali hii ya CCM imekuwa kama ni klabu ya pombe za kienyeji Mazense kwa mfuga mbwa.!

No coordination, no clarity, no anything tangible..
 
Ukisema ni jambo dogo na linarekebishika utashindwa kuweka mstari, Dkt. atakata mkono wa mwanao tofauti na maelekezo ya matibabu na kusema ni kosa dogo la kibinadamu..utakubali? Kosa ni kosa bila kujali limetendwa wapi na nani!
Kosa linapewa uzito kwa kuangalia Madhara yatokanayo na kosa hilo.
Katika hili la uteuzi wa marehemu (tena sio kwa kudhamiria) kuna madhara gani yaliyotokana na uteuzi huo ukiachilia hili la Serikali kuonekana haiko makini na watu mitandaoni kuisakama Serikali/Mamlaka ya Uteuzi?
 
Ni kama Rais anategewa kwa maksudi na wasaidizi wake ili abebe lawama na aibu yeye

Na bahati mbaya nadhani walishamjua udhaifu wake kuwa huwa hapitii na kusoma kile kimeletwa mezani

Wasidizi wake hawafanyi kazi ipasavyo, wanamfanyia maksudi mh Rais, na tunapoelekea uchaguzi mkuu, kwangu mimi naona ni kama wanaajenda yao ya siri

Najiuliza pia, ikiwa jambo dogo kama hilo limefanyika, tupo salama kwa kiasi gani kwenye mikataba ya kimataifa iliyosainiwa?
 
Punguza hasira yaani hasira zote hizi sababu ya marehemu? au chuki sasa mmepata sababu ya kuongea. Suti sijui mishahara yanakuhusu nini? ukitaka suti kanunue vaa tu sio big issue. Maisha hayataki hasira, Ikulu binadamu tu kama wewe hakuna malaika pal

Punguza hasira yaani hasira zote hizi sababu ya marehemu? au chuki sasa mmepata sababu ya kuongea. Suti sijui mishahara yanakuhusu nini? ukitaka suti kanunue vaa tu sio big issue. Maisha hayataki hasira, Ikulu binadamu tu kama wewe hakuna malaika pale.
🤣
 
Alikuwa anaenda kuripoti kwenye uteuzi wa mkurugenzi wa Veta ndiyo akapata ajali ina maana angeripoti na kukaa siku moja ofisini kisha kula uteuzi mwingine ambao umetangazwa jana. Amehama sekta nyingi huenda pia ajali yake ni ya kutengenezwa
 
Unaongelea sie kusalimika? Maadamu tukiwapata wageni ambao ni wakarimu watatusalimia tu licha ya umaskini wetu wa fikra.

Pengine wasaidizi waliopendekeza jina la marehemu walifanya hivyo kimakusudi ili kutufikisha ujumbe Watanzania kuhusu hali halisi ya utawala asasini (current leadership).

Kama ndivyo, ni wazi wametumia ubunifu wa hali ya juu sana. Sasa kazi kwetu sie wapiga-kura.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Mambo ya Korea kupewa bahari na madini KWISHA. Nampongeza sana aliyetoa hiyo taarifa ya Ikulu na kufanikiwa kuhamisha mjadala wote.
 
Ni kama Rais anategewa kwa maksudi na wasaidizi wake ili abebe lawama na aibu yeye

Na bahati mbaya nadhani walishamjua udhaifu wake kuwa huwa hapitii na kusoma kile kimeletwa mezani

Wasidizi wake hawafanyi kazi ipasavyo, wanamfanyia maksudi mh Rais, na tunapoelekea uchaguzi mkuu, kwangu mimi naona ni kama wanaajenda yao ya siri

Najiuliza pia, ikiwa jambo dogo kama hilo limefanyika, tupo salama kwa kiasi gani kwenye mikataba ya kimataifa iliyosainiwa?
Secretary anatupiga
 
Back
Top Bottom