Inakuwaje mwanaume mpaka una miaka 30 au 40 haujaoa na una hela?

Inakuwaje mwanaume mpaka una miaka 30 au 40 haujaoa na una hela?

Asilimia kubwa ya binadamu mtu mzima anapenda na ana tamani kuoa na ukiona mtu hajaoa si jambo jema kumcheka kwani ukute ana mambo kibao ambayo yamepelekea yeye kutokuoa by the way ndoa ni ridhiko la nafsi mbili zilizoamua kuishi pamoja na si fedha na ndio maana ndoa nyingi zina fail kwa kuwa mtu ameweka malengo ya "NIKIPATA KAZI TU NAOA" na huwa hajiulizi je "JE KAZI IKIKATIKA NDANI YA NDOA ITAKUAJE?". Uwe huna kazi au una kazi au una hela au huna lakini kama mmekubaliana kwa pamoja kwamba mnahitaji kuishi pamoja kama mume na mke hapo ndio ndoa ya dhati
 
Uwe unafikiria unapowaza:disapointed::disapointed::disapointed::disapointed: sio ukurupuke
 
we endelea kujenga familia yako ya huyo jamaa hayakuhusu
 
Haha you sound hurt bro, calm down. Channel that anger and energy to the right places, your own affairs. Labda ungejaribu kuwaonyesha jinsi gani maisha ya familia ni baraka na mazuri wangetamani wafanye mambo. Ila kwa hii tone, inaonekana unatamani maisha yao. I'm just saying.

Besides, kama unawajua tafuta namna uwaambie moja kwa moja. Men say things about other men in their faces, bro.

And y'all bros in your 30s-40s, act your age. Family or not.

Absolutely right. Seems to be personal!
 
Duuuhh, maajabu makubwa. Tatizo letu Afrika akili na fikra zetu zimeganda. Badala ya kufikiri dunia ikukumbukeje wewe unafikiria yale yale ya Tunda la katikati
 
Hivi inakuwaje mwanaume mzima unakuwa na pesa za kutosha, umefika miaka 30 hadi 40 hapo katikati, lakini bado unashangaa anakuwa na girl friend tu, au pengine hata halijaoa?

Hivi huwa ni tatizo gani, huwa yananikera halafu dah.

Nilikuwa nasoma na jamaa mmoja hivi, watoto wa huko masakimasaki huko anajifanya mwenyewe ni mambo safi, lakini story zake zote "my girlfriend".

Wenzake tumeoa tangu tukiwa na 25 wakati hata maisha hayajawa mazuri na maisha yameboreka kuwa mazuri tukiwa ndani na wake zetu kwa kushirikiana na wake zetu kujenga maisha.

Sasahivi tuna watoto wakubwa kabisa tunahangaika kusomesha yeye hana mtoto anabadilisha tu wasichana, hela anayo, lakini akili ya kuoa hana.

Wanaume wenzangu mnakera sana wakati mwignine.

too personal kakufanya nini huyo jamaa??!!
 
Utumwa Mwingine Katika Maisha Ni Kujisumbua Kwa Kufuatilia Maisha Ya Mtu Mwingine Utapata Presha Bure!
 
Kwani kuoa ni lazima? Hujui hata Jullie Bishop foreign minister wa Australia (55) ana bf! Hata Jullie Gillard former Pm (57) ana bf tu! Sio vizuri kupangiana maisha, kuoa ama kuolewa sio lazima ishi utakavyo wewe

Acha kupotosha umma ww!
Hizo western culture haziingiliani na maisha halisi ya kibongo!

Ndio maana katiba ya Tz inasema mojawapo ya sifa za rais awe ameoa au kuolewa!

Alafu kuoa au kuolewa ni sifa nzuri kwa jamii na humpendeza Mungu.
 
Hivi inakuwaje mwanaume mzima unakuwa na pesa za kutosha, umefika miaka 30 hadi 40 hapo katikati, lakini bado unashangaa anakuwa na girl friend tu, au pengine hata halijaoa? Hivi huwa ni tatizo gani, huwa yananikera halafu dah.Nilikuwa nasoma na jamaa mmoja hivi, watoto wa huko masakimasaki huko anajifanya mwenyewe ni mambo safi, lakini story zake zote "my girlfriend".Wenzake tumeoa tangu tukiwa na 25 wakati hata maisha hayajawa mazuri na maisha yameboreka kuwa mazuri tukiwa ndani na wake zetu kwa kushirikiana na wake zetu kujenga maisha.Sasahivi tuna watoto wakubwa kabisa tunahangaika kusomesha yeye hana mtoto anabadilisha tu wasichana, hela anayo, lakini akili ya kuoa hana.Wanaume wenzangu mnakera sana wakati mwignine.
Hivi kwenu kuoa ni lazima? Au ndio mambo haya ya uanaume ni kuoa na uanamke ni kuolewa? Kwanini aige mkumbo wako? Kuna mwenzangu mmoja alioa akiwa darasa la 7, wengine walioa baada ya sekondari, wengine walioa chuo kikuu, wengine baada ya Phd. wengine waliangalia uwezo wa kichumi wengine waliangalia umri. Wewe miaka 25 uchumi wako na elimu yako vilikuwaje? Sasa kinakukera nini wakati maisha ni yake?
 
Back
Top Bottom