Inawezekana Rais Mwinyi na Magufuli hawawasiliani katika uongozi?

Inawezekana Rais Mwinyi na Magufuli hawawasiliani katika uongozi?

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,377
Wanaojua masuala ya uongozi wa nchi zetu Zanzibar na Tanganyika wanisaidie juu ya haya Mawasiliano baina ya Marais wetu Dk. Hussein Mwinyi na Dk. Magufuli (Tanzania).

Nijuavyo ni kwamba Muungano wetu ni wa nchi moja ndani ya Serikali mbili. Uamuzi wa Rais Magufuli unaathiri maeneo yote ya nchi kwa maana ya Zanzibar na Bara kwa ujumla.

Swali langu, Rais Magufuli anaamini hakuna Covid-19 isipokuwa kuna "changamoto ya upumuaji" na ndio maana hapendekezi uvaaji wa barakoa kupambana na janga hilo.

Rais Mwinyi ameweka hadharani kuwa Zanzibar kuna Covid, inaua watu na inaua uchumi wa Zanzibar na kutaka wananchi kuchukua tahadhari. Je, Magufuli hawezi kumuadhibu Mwinyi kwa nini atangaze uwepo wa Corona ndani ya nchi ya Tanzania na si changamoto ya upumuaji?

Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Dk. Abbas anasema, "hatujasema Tanzania hakuna korona'! Watanzania tushike lipi na la nani? Kwa nini kabla ya kuzungumza masuala ya Kitaifa pakawepo Mawasiliano na uamuzi wa pamoja?

Nawasilisha!
 
Mkuu Rais ni binadamu kama wengine kwahiyo hawa watu wanautashi wa tofauti na imani za tofauti.
Ni kuulize swali mtoa Maada, je wewe unaona COVID-19 ipo au haipo?
 
Ninamheshimu sana Mh. Rais Dkt Hussein Mwinyi. Mwenye busara, akili na maarifa ya uongozi. Ninakuhakikishia Zanzibar itabadilika kila eneo. Take my words. Yaani sijui Wazanzibari walipitia kwa Mungu yupi mpaka akapatikana Hussein Mwinyi. Ataponyedha majeraha yote Zanzibar.
 
Mkuu Rais ni binadamu kama wengine kwahiyo hawa watu wanautashi wa tofauti na imani za tofauti.
Ni kuulize swali mtoa Maada, je wewe unaona COVID-19 ipo au haipo?
Gui1, kwahiyo unataka kutuaminisha kuwa anakosea Kama binaadam wengine?

Nami nikuulize,
Kama anakosea, kwani kelele za baadhi ya watanzania wenye akili kuwa mwenendo anaoenda nao kwa suala la covid siyo mzuri hasikii?
 
Ninamheshimu sana Mh. Rais Dkt Hussein Mwinyi. Mwenye busara, akili na maarifa ya uongozi. Ninakuhakikishia Zanzibar itabadilika kila eneo. Take my words. Yaani sijui Wazanzibari walipitia kwa Mungu yupi mpaka akapatikana Hussein Mwinyi. Ataponyedha majeraha yote Zanzibar.
Muong mkubwa ww si ndio nyie mlisem kapita kwa kumwaga damu leo mnasema mzuri angal kipindi cha chaguzi mlimktaa
 
Gui1, kwahiyo unataka kutuaminisha kuwa anakosea Kama binaadam wengine?

Nami nikuulize,
Kama anakosea, kwani kelele za baadhi ya watanzania wenye akili kuwa mwenendo anaoenda nao kwa suala la covid siyo mzuri hasikii?
Sio kila anaonyesha kutetea hilo swala la huo ugonjwa anamaanisha wengine wanajua kuwa ikiwa atahitaj chanjo itakuwa manufaaa alfu mbn inajulikana hii chanjo ni mnR vaccine mkuu kanywe ww alafu mbel ukileta mtot muundo wa mwili uko vibaya marufuku kunyenyua kinywaaa
 
" Mkimchagua Mwiinyiiii
"Mkimchagua Mwinyiiii.....

Ihiiiiiiiiiii!

Tulieni Sindano ziwaingie.
 
Kwani suala la afya ni la Muungano? Jiweke sawa.

Kama kawaida, akili kisoda!! Unazungumzia mamlaka na mleta mada anazungumzia mawasiliano na kuwa na meseji moja!!

Haiwezekani kila kinachosemwa kuhusu jambo moja ni sahihi. Kuna uwezekano wa kimoja kati ya vyote ni ukweli na vingine ni uongo au vyote ni uongo! Tafakari!!
 
Dr Hussein Mwinyi ni Daktari wa Binadamu kwa hiyo hawezi
kudanganya kuwa hakuna ugonjwa huku watu wanakufa kwa wingi wala hawezi kuupa majina ya ajabu, kama Changamoto ya kupumua au pneumonia kali, ugonjwa unaojulikana.

Kwa hili sidhani itakuwa rahisi Magufuli kumuadhibu Mwinyi kwa kutangaza kuwa Zanzibar ina Covid-19 kwa sababu inawezekana Chato kukawa na ugonjwa fulani Mtwara usiwepo vinginevyo amuadhibu Rais Uhuru maana Kenya ina ugonjwa Tanzania haina na Kenya iko karibu zaidi na Bara kuliko Zanzibar.

Rais Mwinyi anafanya mambo mengi mazuri kwa Zanzibar ya kuigwa kwa hiyo wajinga wa CCM Bara wanaweza wakajaribu kumuadhibu kama walivyomfanyia Jumbe kwa kuchafua hali ya hewa. Yajayo Zanzibar yatafurahisha Bara!
 
Kama kawaida, akili kisoda!! Unazungumzia mamlaka na mleta mada anazungumzia mawasiliano na kuwa na meseji moja!!

Haiwezekani kila kinachosemwa kuhusu jambo moja ni sahihi. Kuna uwezekano wa kimoja kati ya vyote ni ukweli na vingine ni uongo au vyote ni uongo! Tafakari!!
Mleta mada alipouliza JPM hawezi Kumuadhibu Mwinyi hilo sio suala la Mamlaka?

Sasa Afya sio suala la Muungano hivyo halazimiki kuwasiliana na JPM. Ad by the way, uamuzi wa JPM unaathiri pande zote mbili ikiwa ni suala la Muungano TU.
 
Mkuu Rais ni binadamu kama wengine kwahiyo hawa watu wanautashi wa tofauti na imani za tofauti.
Ni kuulize swali mtoa Maada, je wewe unaona COVID-19 ipo au haipo?
Saa 2 zilizopita jirani yangu anayeniuziaga bia mdada grosari amedondoka mbele yetu na kufa kwa kudai anashindwa kupumua. Hatujapeleka mwili mochwari.
 
Back
Top Bottom