Inawezekana vipi Taifa linampata Rais kama huyu?

Ukumbuke rais kaongelea ufanyikaji wa vurugu hapo. Kama unahatarisha amani ya nchi utazuiwa tu
Huwa mna - bet kuwa kutakuwa na vurugu au kuna vurugu zimewahi kutokea?

Hebu toa mfano mmoja ni lini na wapi ktk mkutano wa chama cha siasa iwe CHADEMA au chochote kile kilifanya mkutano na kukatokea vurugu..?

Na hata ikitokea bahati mbaya ya namna hiyo ktk tukio moja mahali fulani, inakuwa si vyema wala haki kukihukumu chama cha siasa kizima kuwa ni "cha vurugu..!!". Hapa Rais ameongea uongo na hana uthibitisho...

By the way, nakumbuka mikutano ya kampeni za uchaguzi mwaka 2020, CHADEMA walikuwa wakikusanya maelfu ya watu kwenye mikutano yao lakini hakuna rekodi ya hata kiroboto kuumizwa wala gari au nyumba ya mtu kuharibiwa na wakati mwingine na maeneo fulani kulikuwa hakuna hata polisi waliolinda mikutano huo na licha ya hivyo iliisha salama kabisa...!

Nyie hii hoja huwa mnaitoa wapi ni ushahidi ni UPI..?
 
Mama Samia hapa amechemka, hapa mama amesema uongo na hii ni dhihaka kubwa kwa wapinzani na Katiba ya JMT,hajawatendea Haki Wapinzani na Watz wote kwa ujumla wake. Hii ni aibu. Yawezekana kuna masalia ya Jiwe yanayo mpotosha Rais kwa maslahi binafsi.
 
Wanafunga gazeti lako, wanavunja ukumbi wako, wanafunga account zako, wanakuvunja mguu wako, wanakunyang'anya ubunge wako, wakishamaliza wanakupa kesi ya Ugaidi halafu wanataka uwaombe msamaha. Wajue mbinguni hawataenda kwa vyeo vyao bali matendo waliyoyafanya walipokuwa na vyeo
 
Wewe

Huyu anafanya uungwana hata kuongea nao na akawasikiliza. Hayati JPM huo muda aliutoa siku moja tu pale Mwanza baada ya kumaliza hotuba yake.

Huyu hana mkono wa chuma, dialogue ndio inayopewa kipaumbele, maridhiano ndio yanayopewa kipaumbele.
She is hopeless fool.Maridhiano ya nini wakati mikutano ya kisiasa ipo kwa mujibu wa katiba?
 
Shule ni shida
 
Hawana dogo hao Wala shukrani Kila kitu kwao ni kupinga na kuleta vurumai.
Urongo mtupu! Hizi ni propaganda za CCM za kuendelea kuwaxuia Wapinzani kwa visingizio visivo kichwa wala miguu.
Yaani CHADEMA, ACT Wazalendo, NCCR Mageuzi wanafanya mikutano ya hadhara kwa kuvunja magari ya watu kweli? Hili ilitokea wapi, lini na saa ngapi. Chama gani kilihusika? Je, polisi na UWT walikuwa wapi?
Mama Samia mwogope Mungu. Kuwa makini na hao Mahafidhina wa CCM vinginevo watakuingiza chaka.
 
Hizo bado ni athari za ibilisi joka kuu. Aliwaaminisha watu kuwa kili kitu mpaka kifanyike nchini ni lazima rais aruhusu. Sasa mama naye anadhani utaratibu ni huo.
 
Maadama Mama kasema hivyo, basi huo ndio ukweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…