Infosys IPS (T) LTD wakanusha kuhusika na LUGUMI katika kashfa ya ubadhirifu

Infosys IPS (T) LTD wakanusha kuhusika na LUGUMI katika kashfa ya ubadhirifu

Sina shida na Lizaboni kujibu kwa niaba yake ili mradi aje na majibu yanayokidhi

Mkuu ahsante sana kwa kuuliza maswali yenye tija, ila naomba tu niweke kumbukumbu sawa, huu mkataba wa Lugumi kuweka na kusambaza mitambo ya alama za vidole kwenye vituo vya polisi ulifanyika 2011, wakati huo waziri mwenye hiyo dhamana alikua ni mwingine. Hii haiondoi ukakasi wa uhusika wa huyu mheshimiwa ila itasaidia kujibu baadhi ya maswali yako.

Kubwa zaidi, ilikuwaje wakalipwa pesa karibia zote za mradi 99% wakati kazi hata nusu haijakamilika?
 
Kwanini usimtafute Kitwanga mwenyewe akujibu maswali yako, kama yule jamaa aliyeamua kwenda infosys kupata ukweli wake.
Unahisi humu utapata majibu sahihi? Au ndio unaanzisha mada kwa ID moja, unaijibu kwa ID tatu majibu uyapendayo wewe kwa manufaa yako.....



1. Wewe ni waziri tena wa wizara ambayo kampuni uliyoianzisha wewe wana mahusiano ya kibiashara. Je huoni kwamba kuna mgongano wa kimaslahi?

2. Ikiwa wizara yako imetangaza tenda kampuni yangu ikatenda na Infosys uliyoianzisha wewe ikatenda, naweza kupewa mimi? Hata nikikosa kwa haki na ikapata Infosys nitaridhika?

3. Hivi ni sahihi kampuni zenye mahusiano na mawaziri kufanya kazi na serikali wanayoitumikia?

4. Kampuni yako imekanusha kuijua wala kushirikiana na Lugumi. Wewe binafsi unaijua Lugumi na wamiliki wake? Kama unaijua inawezekanaje watu wa kampuni uliyoianzisha hawaijui?

5. Kelele kubwa zinaendelea kuhusu wizara unayoiongoza, kimya chako kinasababishwa na nini? Mbona hujatoka hadharani kuzungumza lolote kuhusu kinachoendelae ofisini mwako?

6. Unasubiri kutimuliwa? kwa nini usimwombe bwana mkubwa akuweke pembeni ili uchunguzi uendelee vizuri ofisini kwako?

7. Ni kweli kwamba una uhusiano/rafiki wa karibu na bwana mkubwa?

8. Uhusiano huo kama upo ni wa kawaida au wa kibiashara?

9. Kama ni wa kibisahara anahusika kwenye Infosys?

10. Kama mna uhusiano kama inavyosemekana huoni kwamba unampa mtihani mkubwa sana rafiki yako?
tt
 
Haya sasa ukweli umewekwa wazi kumbe ni juhudi za kumpiga vita Waziri Kitwanga na kutaka kuichafua serikali ya Magufuli.

Wapiga dili tafuteni kiki nyingine ukweli ndio huu.
Nani kakwambia alichosema ni ukweli? Kwani hawezi kudanganya? Yaani unaamini maneno ya mshukiwa? Je ulitegemea akubali? Watanzania ni wangese sana ndio maana tunaliwa kila kukicha! Yaani mlalamikiwa akubali shtaka ama kweli Tanzania yangu pongo na nyumbu ni wa kutisha! Ukiona chombo huru kimechukunguza na kusema hayo ndio utoke kwenye shimo Kuja kuchangia utumbo kama huu
 
Nani kakuuliza wewe jamaa uwa punguani kweli kila kitu Nairobi yaani wewe kwako Nairobi ni zaidi ya New York.
Ndio kwa sababu sishobokei wazungu,
Umenyimwa udiwani unataka kumalizia hasira zako kwangu
 
Lugumi kwa sasa hakuna hata anayetaka kusikia hilo jina......kila unayemgusa anaruka, hata kama wametoka kugawana pesa muda huu.....utaambiwa mimi sijui Lugumi........kazi kweli.
 
Utetezi wenu ungekuwa na maana mungekanusha Kitwanga kuhusika na Infosysy.
 
Kampuni ya INFOSYS IPS (T) LTD imekanusha taarifa zinazoenezwa katika mitandao ya kijamii kwamba kampuni hiyo inahusika na inashirikirikiana na Lugumi Enterprises katika kashfa ya ubadhirifu.

Katika habari zilizosambaaa inasemekana kwamba kampuni ya Infosys ilipokea mabilioni ya shilingi kutoka katika kampuni ya Lugumi, jambo ambalo wao wanadai si la kweli na ni la kupuuzwa na umma.

'Hatujawahi kufanya biashara na kampuni ya Lugumi Enterprises' Amesisitiza Bwana Sweki Donald, Naibu Meneja Mkuu Infosys IPS (T) LTD.

Video:


Huyu ni nani hasa? Hi video ni ngumu kuiamini. Sauti na lips ni mbali mbali! Huenda ni usanii mtupu! Lakini ndio dalili za wahusika kuwaacheni kwenye mataa.
Halafu hizo kampuni za kimarekani zinazoishia LLC (legal liability company) ni kama ile ya Richmond. Nyingi ni FEKI!!
Kwahiyo tungoje tuone kama Ndugai ana ubavu kama ule wa Sitta, kabla hajapigwa stop.
 
Haha utokaji wa hii taarifa na contribution za mwanzo umeniacha nikicheka.
Anyway mimi pia naona chuki tu binafsi na wivu wa baadhi ya watu. Kitwanga ni mtu safi kabisa.
umetumia nini Kujua ni msafi? Unajua kwanini watanzania tunaitwa majuha? Ni kwa sababu ya watu kama wewe! Nani kamchunguza akakwambia ni safi? Je ikijagundulika ameshiriki unasemaje? Yaani kwa akili ya kawaida tu ile sio NGO ya Kutoa msaada ambayo founder anaweza kujitoa ile ni kampuni ya kutengeneza faida! Hadi hapo umeshaelewa aliekuwa anahojiwa alikuwa anapambana kumnasua boss wake kwenye matope
 
1. Wewe ni waziri tena wa wizara ambayo kampuni uliyoianzisha wewe wana mahusiano ya kibiashara. Je huoni kwamba kuna mgongano wa kimaslahi?

2. Ikiwa wizara yako imetangaza tenda kampuni yangu ikatenda na Infosys uliyoianzisha wewe ikatenda, naweza kupewa mimi? Hata nikikosa kwa haki na ikapata Infosys nitaridhika?

3. Hivi ni sahihi kampuni zenye mahusiano na mawaziri kufanya kazi na serikali wanayoitumikia?

4. Kampuni yako imekanusha kuijua wala kushirikiana na Lugumi. Wewe binafsi unaijua Lugumi na wamiliki wake? Kama unaijua inawezekanaje watu wa kampuni uliyoianzisha hawaijui?

5. Kelele kubwa zinaendelea kuhusu wizara unayoiongoza, kimya chako kinasababishwa na nini? Mbona hujatoka hadharani kuzungumza lolote kuhusu kinachoendelae ofisini mwako?

6. Unasubiri kutimuliwa? kwa nini usimwombe bwana mkubwa akuweke pembeni ili uchunguzi uendelee vizuri ofisini kwako?

7. Ni kweli kwamba una uhusiano/rafiki wa karibu na bwana mkubwa?

8. Uhusiano huo kama upo ni wa kawaida au wa kibiashara?

9. Kama ni wa kibisahara anahusika kwenye Infosys?

10. Kama mna uhusiano kama inavyosemekana huoni kwamba unampa mtihani mkubwa sana rafiki yako?
Je unaweza kutwangana na Kitwanga?
 
Toka lini kukanusha kukawa ndio ukweli? Hata Babu Seya alikanusha kubaka na bado akafungwa........BTW huyo msemaji mbon hasemi uhusikaji wa Kitwanga na kampuninya Infosys?

Kampuni ya Kitwanga imepewa kazi na kampuni Lugumi kufanya kazi ya upembuzi baada ya kumaliza kazi ikalipwa na kuendelea na maisha yake hapo Kitwanga anatumbuliwa kwa kosa gani?

Nikupe mfano wewe una kampuni yako ya upishi... Umepewa kazi na Barrick uka supply chakula kwenye kampuni yao.. Baadae inagundulika Barrick imekuwa inafanya ujanja ujanja, alafu na wewe outsourced company wa chakula unawajibishwa unaona hiyo ipo sawa?? Hivi ukipewa tender usambaze mabuti jeshini alafu ikaja kubainika aliyekupa tender amefanya udanganyifu.. Wewe umepeleka viatu vilivyotakiwa na ukalipwa chako.. Vipi ni sawa hapo na wewe kuhukumiwa eti umefanya ujanja pia.


Tuwe wakweli Kitwanga hapa anaandamwa kisiasa ili kumyumbisha Magufuli na wengine ni hasira za kuzibiwa dili zao haramu wanataka wamuonyeshe hawajawahi kushindwa. Kitwanga mmuhukumu kwa lingine sio hili.
 
Hii ni mbinu chafu iliyotengenezwa na watu fulani hasa wa lumumba st ili kuuhamisha mjadala. Makandokando y waziri yameanzia bot na sasa polisi. Huenda mkulu hakujiuliza na alitawakiwa na uswhiba zaidi ndio maana alimteua kwenye hiyo nafasi. Na sasa anaogopa kumtoa kwa kisingizio cha serikali yake kutokuaminiwa na wananchi tena. Tabia ya marais kuendelea kufanya kazi na mawaziri wapiga dili kitatuondolea imani naye.
 
Ndugu wana JF, kama kuna jambo litakalothibitisha dhamira ya ndani ya JPM katika kuchukua hatua za kiuwajibikaji ni issue ya lugumi ambayo ni kampuni imefanya kazi kwa karibu na kampuni ya infosy IPS inayomilikiwa na mndani na msiri wa JPM Waziri kitwanga.

Bila kupepesa macho, KITWANGA amekula sehemu ya fedha za mkataba huo na anatakiwa kuchukuliwa hatua, propaganda za kuwa kitwanga anatafutwa sababu amebana wauza unga ni upuuzi, kitwanga ajibu tuhuma zake na lugumi kisha aendelee kusafisha wauza unga.
 
Japo mimi sio Waziri Kitwanga, wakati waziri akijiandaa kuja humu jf kukujibu mimi nitakupatia utangulizi tuu majibu kamili atayatoa waziri mwenyewe.
1. Wewe ni waziri tena wa wizara ambayo kampuni uliyoianzisha wewe wana mahusiano ya kibiashara. Je huoni kwamba kuna mgongano wa kimaslahi?- Hakuna mgongano wowote wa kimaslahi kutokana na procurement process. Kwanza mimi niliishajioa kwenye uendeshaji wa Infosys na aliyeipa kazi Infosys sio Jeshi la polisi bali ni supplier mwenyewe akitokea huko huko Marekani hivyo kungetokea mgongano Infosys ingepata tender toka Jeshi la Polisi.

2. Ikiwa wizara yako imetangaza tenda kampuni yangu ikatenda na Infosys uliyoianzisha wewe ikatenda, naweza kupewa mimi? Hata nikikosa kwa haki na ikapata Infosys nitaridhika?-mambo ya tenda ni mashindano ya sifa, uwezo, ujuzi, ubora, na gharama sasa kama kampuni yangu imeshinda kihalali na bila shinikizo lolote kutoka kwangu ni lazima wewe ukubali matokeo na usiporidhika uko huru kukata rufaa PPRA.

3. Hivi ni sahihi kampuni zenye mahusiano na mawaziri kufanya kazi na serikali wanayoitumikia?-Ni sahihi kabisa kama zinashinda kwa ushindani wa haki.

4. Kampuni yako imekanusha kuijua wala kushirikiana na Lugumi. Wewe binafsi unaijua Lugumi na wamiliki wake? Kama unaijua inawezekanaje watu wa kampuni uliyoianzisha hawaijui?- Hapa umechanganya mambo. Kuijua Lugumi hakuna mtu asiyeijua hata ofisini kwangu tunaijua na tumefanya nayo hiyo kazi ya polisi ila hatuna mahusiano ya kibiashara. Japo mzabuni ni Lugumi aliyetupa sisi kazi sio Lugumi bali ni supplier mwenyewe.

5. Kelele kubwa zinaendelea kuhusu wizara unayoiongoza, kimya chako kinasababishwa na nini? Mbona hujatoka hadharani kuzungumza lolote kuhusu kinachoendelae ofisini mwako?.-Hizo ni Kelele tuu za mlango na wala hazinihusu.

6. Unasubiri kutimuliwa? kwa nini usimwombe bwana mkubwa akuweke pembeni ili uchunguzi uendelee vizuri ofisini kwako?-sisubiri kutimuliwa, nitimuliwe kwa kosa lipi? . Hakuna uchunguzi wowote unaoendelea ofisini kwangu.

7. Ni kweli kwamba una uhusiano/rafiki wa karibu na bwana mkubwa?- Ni kweli upo Bwana mkubwa ni meti wangu na homeboy wangu.

8. Uhusiano huo kama upo ni wa kawaida au wa kibiashara?-wa kawaida na wa kibiashara kila mimi na maofisa wangu tukitembelea Chato tunafikia hoteli yake.

9. Kama ni wa kibisahara anahusika kwenye Infosys?-No haihusiki na Infosys ila miradi yote inayofadhiliwa na WB computers lazima ziwe ni Dell na Infosys ndio the one and only authorised supplier, dealers na after sales service wa Dell Tanzania .

10. Kama mna uhusiano kama inavyosemekana huoni kwamba unampa mtihani mkubwa sana rafiki yako?-Hakuna mtihani wowote kwa sababu anayeipa tenda Infosys sio mimi wala sio yeye bali inashinda tenda katika ushindani wa wazi na kwa haki bila upendeleo.

Pasco
 
Kwanini usimtafute Kitwanga mwenyewe akujibu maswali yako, kama yule jamaa aliyeamua kwenda infosys kupata ukweli wake.
Unahisi humu utapata majibu sahihi? Au ndio unaanzisha mada kwa ID moja, unaijibu kwa ID tatu majibu uyapendayo wewe kwa manufaa yako.....




tt
Ni mawazo yako ila kwa nini yeye asije akajibu yeye? Umetumwa?
 
Kiongozi mzuri na anayejua maana ya uongozi ni yule tu anayewajibika na bahati mbaya Tanzania hatuna viongozi wa aina hii! Kuhusishwa tu na kashfa kulitosha kumfanya a mwambie boss wake naomba nikae pembeni ufanyike uchunguzi wa kina ili ukweli ujulikane! Sasa ukiangalia hizi danadana zinazopigwa unapata wasiwasi mchezaji huenda ana mambo anayaficha
 
Hii nchi ya hovyo sana hii na Magufuli akitaka kuharibikiwa afanyie kazi taarifa za mitandaoni.
 
Infosys IPS itasikilizwa na kutetewa tu sababu kuna Charles ila huko Lugumi kama kuna jina la Kiswahili umechambia nyembe
 
Back
Top Bottom