Infosys IPS (T) LTD wakanusha kuhusika na LUGUMI katika kashfa ya ubadhirifu

Infosys IPS (T) LTD wakanusha kuhusika na LUGUMI katika kashfa ya ubadhirifu

Mkuu ahsante sana kwa kuuliza maswali yenye tija, ila naomba tu niweke kumbukumbu sawa, huu mkataba wa Lugumi kuweka na kusambaza mitambo ya alama za vidole kwenye vituo vya polisi ulifanyika 2011, wakati huo waziri mwenye hiyo dhamana alikua ni mwingine. Hii haiondoi ukakasi wa uhusika wa huyu mheshimiwa ila itasaidia kujibu baadhi ya maswali yako.

Kubwa zaidi, ilikuwaje wakalipwa pesa karibia zote za mradi 99% wakati kazi hata nusu haijakamilika?

Mkubwa, hii ishu ya mkataba wa kampuni hii ni very complicated.

Kwani kumbe nje ya kampuni hii kulipwa 99% ya fedha ya makubaliano ya mkataba sawa na Tshs. 34bn kati ya 37bn, pia mshauri mwelekezi (consultant) wa mradi huu ambao ni kama haujafanyika naye amelipwa Tshs. 46bn nje ya zile zilizopo ktk mktaba!!

Si hivyo tu, bali kampuni hii ilitumia kiasi kingine cha Tshs. 5bn kwa mafunzo ya watu watano nje ya nchi na hizi pia zikiwa nje ya fedha za mkataba wenyewe!!

Kwa hiyo tunapoongelea fedha iliyolipwa kwa kampuni hii tayari na kupotea kifisadi tu ni jumla ya 34bn + 46bn + 5bn = Tshs. 85bn!!

Just imagine, 85bn zinapotea kwa njia ya "mkataba hewa" halafu kuna watu humu wanasema "vijana tuache kuendekeza siasa...", nadhani wakimaanisha tunyamaze kimya,tusihoji!!

Hili haliwezekani kamwe kwa sababu hizi ni fedha zetu kutokana na kodi tunayolipa..... lazima tuendelee kuhoji na tuhakikishe kila anayetajwa kuhusika kwa namna hii au ile awe Kitwanga au Lugumi au Ridhiwan Kikwete anaibuliwa popote alipo na hatua zichukuliwe!!

Kwa kweli tukatae "double standard" ya vita ya kupigana na ufisadi na kutumbua majipu. Popote jibu lilipo likamuliwe tu.

Inasikitisha sana, kwamba jana niliona taarifa ya habari ITV mhandisi wa maji wa wilaya ya Rorya - Mara pamoja kampuni iliyotekeleza mradi wakitiwa pingu (sema wakitumbuliwa) kwa amri ya RC Mulongo kwa kushindwa kusimamia mradi wa maji ktk kijiji kimoja huko wenye thamani kama Tshs 200 milioni na kitu hivi.

Hakukuwa na ushahidi wa kuliwa pesa wala nini wa moja kwa moja wa hawa watu, bali ni kile tu kinachoitwa "kuisaidia polisi" ktk uchunguzi wao.

Leo mkataba wa Polisi na Lugumi una siri gani eti hata tushuhudie sarakasi zenye kila dalili za kulindana!!??
 
Tupo pamoja mkuu, sijui hujanielewa wapi. Issue ya Lugumi, Lugumi ndio direct client kwa Polisi, Lugumi kapelekea tenda ya supply and install kwa waamerika (Biometrica), Biometrica kusupply vifaa na kumpa kazi ya kuinstall Infosys ambayo kati ya wamiliki wake, Kitwanga yupo. Kwa trend hii, Infosys inakili kupokea $74,000.00 kutoka Biometrica kwa kazi aliyoifanya.

Issue yangu kubwa hapa ni vijana kujaribu kututoa kwenye reli, kujaribu kuiondoa Lugumi na kumtwisha mzigo Kitwanga.

Kazi aliyoifanya ni Ipi? je ina thamani ya hiyo dola 74,000?
 
Infosys IPS itasikilizwa na kutetewa tu sababu kuna Charles ila huko Lugumi kama kuna jina la Kiswahili umechambia nyembe
Mshaanza hivyo! Haya mualike Khaartan, big show na wenzako
 
Infosys yeye ni mtu wa tatu,anahusikaje hapo au ni uelewa wa watu tu?infosys ni kampuni ya tatu kutoka polisi.lugumi,biometrica ndiyo anakuja infosys.jamani kunakitu kinaitwa sub contract.
 
Haya sasa ukweli umewekwa wazi kumbe ni juhudi za kumpiga vita Waziri Kitwanga na kutaka kuichafua serikali ya Magufuli.

Wapiga dili tafuteni kiki nyingine ukweli ndio huu.
Inaonekana unajua mengi hebu twambie kwanini hawataki kuutoa huo mkataba? kinafichwa nini?
 
Kwani lugumi mwenyewe yuko wapi
Eti yuko morogoro kwa mujibu wa magazeti ya leo. Sasa kama hana hatia na anasikia yote yasemwayo sijui kwa nini asijitokeze tu na kusema sijatoroka nchini. Hapa kuna mengi sana yanapikwa kunusuri hii kashfa.
 
Huyu mwandishi nae ni kanjanja maswali anayouliza ni kama waliyapanga kabla na iweje aseme tuwe tunafanya utafiti yeye amefanya utafiti upi mpaka aanze kuwatetea infoys au kwenda kumhoji huyo meneja ndio kajilidhisha mm sijasoma uandishi wa habari ila nadhani story yake ingekuwa nzuri kama angeenda jeshi la polisi awahoji ili story abalance story tofauti na hapo hakuna hoja ya msingi watu wamepiga dili wafungwe na waludishe hela zetu. Ooo! HAPA KAZI TU hapa kazi tumbueni na hilo jipu ndio tuwaamini
 
Mbona hii imekuja baada ya kuhakikisha mkataba hautoki bali unapelekwa kwa kamati ya ulinzi na usalama? Ambayo mkuu wake alikuwa polisi? Kwa nini haikutoka mapema... na je wabunge wa kamati ya ulinzi wanakula kiapo tofauti na wabunge wa PAC kwamba wao wanaaminiwa zaidi? ONLY IN TZ....
Hapo ndipo panapo shangaza, na mkuu wa hiyo wizara alikuwa polisi mdogo, mtuhumiwa wa Lugumi mwingine ni Saidi Mwema aliekuwa anaridhia huo ufujaji wa heal kwenda lugumi, hapa lazima huyu bwana atamlinda bosi wake, hii ndio Tz.yenye maziwa na asali wanaofaidi ni kina LUGUMI tu.
 
Infosys yeye ni mtu wa tatu,anahusikaje hapo au ni uelewa wa watu tu?infosys ni kampuni ya tatu kutoka polisi.lugumi,biometrica ndiyo anakuja infosys.jamani kunakitu kinaitwa sub contract.
Swali la msingi Infosys ilihusika au haikuhusika hata angekuwa ni mtu wa ishirini kwenye hiyo chain hakupata hela au alipata hayo mambo mengine mnaleta siasa mbona jambo ambalo ni washkaji mtawala hamtaki kuguswa mliwahi kuona nyumba ya miti inapigwa deki?
 
Wasituchezee hao huyo waziri alijitoa kwenye menejiment ili aweze kupiga dili kisawasawa kama hivyo
 
Toka lini kukanusha kukawa ndio ukweli? Hata Babu Seya alikanusha kubaka na bado akafungwa........BTW huyo msemaji mbon hasemi uhusikaji wa Kitwanga na kampuninya Infosys?
Hivi aliposema kuwa Kitwanga ndiye founder na pia ni shareholder hujamsikia?

Pia alikuwa general director kabla ya kuamua kung'atuka mwaka 2010
 
Hawataki kutuambia Lugumi kwa nini amelipwa hela kabla hajamaliza kazi? Kwa nini nguvu kubwa inatumika kumtoa mwenye hisa mwanasiasa Kitwanga na ufisadi uliofanywa na kampuni yake? Kitwanga kama Waziri mwenye dhamana alichukua hatua gani kuzuia, kushughulikia, kuhakikisha na kuwakamata wahusika kama yeye hahusiki?

Wanalazimisha watu wote wawe wanasifia tu kama majuha, leo wameuchukua mkataba toka kwenye kamati ya PAC na kuuhamishia kamati ya Adadi, mara wanasema hakuna ufisadi wowote katika mkataba kati ya LUGUMI na jeshi la Polisi, jitihada kubwa kuficha ukweli za nini?

.......na wamemsimamia jamaa (Lugumi) kwa kumpa ulinzi hadi ametoroka nchi kuficha ushahidi asiwaumbue ili badae watuite sisi wanachi "manyumbu" au "malofa!!"

.......yaani ni full sarakasi mithili ya zile za ufisadi wa EPA/BoT vs Daudi Balali gavana wa Benki kuu enzi hizo!!

.....I am afraid huyu jamaa (Lugumi), naye baadae kidogo atarudi "maiti ndani ya box" au tutaletewa majivu yake tu...... amefia Canada au USA alikokwenda kutibiwa na kuzikwa huko!!

......lol, ama kweli mshahara wa dhambi ni mauti. Ni bora kuwa na chako kidogo cha halali kuliko kudhulumu cha watu wanyonge wasiokuwa na uhakika hata mlo mmoja wa siku!!
 
Kampuni ya INFOSYS IPS (T) LTD imekanusha taarifa zinazoenezwa katika mitandao ya kijamii kwamba kampuni hiyo inahusika na inashirikirikiana na Lugumi Enterprises katika kashfa ya ubadhirifu.

Katika habari zilizosambaaa inasemekana kwamba kampuni ya Infosys ilipokea mabilioni ya shilingi kutoka katika kampuni ya Lugumi, jambo ambalo wao wanadai si la kweli na ni la kupuuzwa na umma.

'Hatujawahi kufanya biashara na kampuni ya Lugumi Enterprises' Amesisitiza Bwana Sweki Donald, Naibu Meneja Mkuu Infosys IPS (T) LTD.

Video:






haka ka skendo ni mdogo wake na escrow kanapinda pinda ila katanyooka tu ngoja bunge lianze.
 
Kampuni ya Kitwanga imepewa kazi na kampuni Lugumi kufanya kazi ya upembuzi baada ya kumaliza kazi ikalipwa na kuendelea na maisha yake hapo Kitwanga anatumbuliwa kwa kosa gani?

Nikupe mfano wewe una kampuni yako ya upishi... Umepewa kazi na Barrick uka supply chakula kwenye kampuni yao.. Baadae inagundulika Barrick imekuwa inafanya ujanja ujanja, alafu na wewe outsourced company wa chakula unawajibishwa unaona hiyo ipo sawa?? Hivi ukipewa tender usambaze mabuti jeshini alafu ikaja kubainika aliyekupa tender amefanya udanganyifu.. Wewe umepeleka viatu vilivyotakiwa na ukalipwa chako.. Vipi ni sawa hapo na wewe kuhukumiwa eti umefanya ujanja pia.


Tuwe wakweli Kitwanga hapa anaandamwa kisiasa ili kumyumbisha Magufuli na wengine ni hasira za kuzibiwa dili zao haramu wanataka wamuonyeshe hawajawahi kushindwa. Kitwanga mmuhukumu kwa lingine sio hili.
Infosys hajawahi kuwa na mahusiano ya biashara na Lugumi...over! Ndivyo alivyosema huyo naibu

Infosys ilipewa tenda na Biometrica LLC
 
Kampuni ya INFOSYS IPS (T) LTD imekanusha taarifa zinazoenezwa katika mitandao ya kijamii kwamba kampuni hiyo inahusika na inashirikirikiana na Lugumi Enterprises katika kashfa ya ubadhirifu.

Katika habari zilizosambaaa inasemekana kwamba kampuni ya Infosys ilipokea mabilioni ya shilingi kutoka katika kampuni ya Lugumi, jambo ambalo wao wanadai si la kweli na ni la kupuuzwa na umma.

'Hatujawahi kufanya biashara na kampuni ya Lugumi Enterprises' Amesisitiza Bwana Sweki Donald, Naibu Meneja Mkuu Infosys IPS (T) LTD.

Video:







Inakupasa uwe na "Permanent Head Disorder(PhD)" ili walau uweze kuziamini hekaya hizi zilizo katika mfumo wa "series" zinazotoka kila siku ili kujaribu "kudivert" Ukweli huu mchungu.Hivi ni lini Taifa hili liliwahi kuweka rekodi ya kuukubari Ukweli ambao ghalama zake zinatishia uhai wa serikali yenyewe?

Kama kuna mtu alitarajia mtuhumiwa huyu akiri uhusika wake katika kadhia hii,basi mtu huyo ni wa kuonewa huruma kwa viwango vinavyostahili.

Ili kuweka kumbukumbu sawa,nitoe walau mifano miwili,mitatu ambayo serikali na vyombo vyake ilihaha kiasi cha kujaribu hata kulisimamisha jua ili kusipambazuke iendelee kujificha katika giza kuepuka kibano cha ufisadi uliofanywa na vyombo vyake.

1.Sakata la ufisadi wa Kagoda Agricultural Co.Ltd na MEREMETA.Hekaya ya sakata hili ilivunja rekodi za wahusika kujitokeza katika rangi za aina mbalimbali zenye lengo la kuudanganya Umma ili kuuficha Ukweli.Awali serikali ilisema fedha za kagoda/meremeta zilienda kufanya kazi nyeti katika masuala ya ulinzi na usalama,lakini baada ya kibano iligundulika mkataba wa kagoda / meremeta waweza kurithiwa na watoto,wakwe ndugu na jamaa wa wenye Kampuni la Kagoda /meremeta,sasa kama Kagoda/meremeta,ilikuwa ya Jeshi kwa matumizi ya ulinzi Na usalama wetu, ni nani alikuwa Mke,mtoto au ndugu wa serikali ambaye alitajwa katika Kagoda/meremeta kuwa na sifa za kisheria kurithishwa kampuni la kagoda/meremeta?Kifo chenye utata cha Balali ndicho kilichozima ufisadi huu baada Aliyekuwa waziri wa fedha kuliambia bunge kuwa alipewa Taarifa za uwongo na Gavana Balali.


Siri ya Kagoda hii hapa | Gazeti la MwanaHalisi

2.Sakata la Pili ambalo serikali ilidharirika vya kutosha ni Escrow saga,pamoja na kuwa Taifa bado linaendelea kuteswa na ufisadi huu wa kampuni ya IPTL,serikali Na vyombo vyake ilijaribu kuuficha Ukweli kuwa katika mabilioni ya escrow hakukuwa na hata senti moja ya serikali na hadi mkuu wa nchi aliyaponda mabilioni hayo kwa kuyaita "hela ya madafu",lakini baadae serikali hiyohiyo iliyoyakana mabilioni ya Tegeta Escrow,iliiagiza TRA kukusanya kodi toka mabilioni hayo.

Juhudi za watendaji waandamizi wa serikali kutaka kujinasua toka kwenye kokoro hili la LUGUMI Na INFOSYS IPS(T)LTD zilianza mapema baada ya kushindwa kupeleka vielelezo kwenye kamati yenye mamlaka kisheria kusimamia matumizi ya Fedha za Umma,PAC badala yake vielelezo vimepelekwa kamati ya ulinzi na usalama ambayo kikatiba haina mamlaka ya kuchunguza matumizi ya fedha za Umma.

Sakata hili ni mwiba wa mchongoma ulionasa katika koromeo la serikali,wanaohusishwa na sakata hili wote ni vigogo wa ngazi za juu kabisa wa serikali na vyombo vyake,unategemea serikali italikubali sakata hili lenye kila dalili za kuidharirisha serikali yenyewe?

Sakata linalozigusa moja kwa moja familia za vigogo wa jeshi la polisi na wizara ya mambo ya ndani pamoja na ikulu yenyewe ulitarajia liwe jepesi kiasi cha watu kukiri kirahisi kuwa wanahusika nalo?Naungana na mwana GT Salary slip kumshukuru Mungu kwa kuliruhusu sakata hili mapema ili kuona kama " ngariba wetu wa majipu" ana ujasiri wa kutosha kuweza kuyatumbua majipu haya yaliyoota sehemu nyeti sana katika miili ya "wazazi wake"

Jambo la kujiuliza ni namna watu wanavyolihusisha sakata hili kama hujuma dhidi ya utawala wa Mh.Rais.Ni upumbavu uliopitiliza kuihusisha ukawa katika sakata hili badala ya kuuona Ukweli wa sakata lenyewe,watu wanaanza kuleta siasa nyepesi za uzito wa unyoya.Tunataka hatua zichukuliwe juu ya wale wote waliohusishwa na "shombo" ya uvundo wa sakata hili bila kujali nafasi zao katika jamii na serikalini,mazoea ya uswahili wa kuyaita mambo haya kuwa ni "upepo tu na utapita" hayakubaliki.Huu si upepo kama mnavyozani,sakata hili laweza kuwa tufani linaloweza kuwasomba baadhi ya vigogo wa serikali hii sikivu sana ya chama cha majipu (CCM).
 
Kitwanga ni kweli amewabana wazee wa dili chafu.
Hii kashfa ya Lugumi inanichekesha sana, eti Lugumi kakimbia, kakimbilia wapi? Eti haijulikani......
Swali langu, is Lugumi Invisible person?
Kakamatwa gaidi àliyekimbia (mwenye kofia ya pama) kwenye tukio la ulipuzi wa wamja wa ndege Ubelgiji, huyu Lugumi asiyejua hata kusoma atajifichaje asikamatike?
watu wangu wanaangamia kwa kosa maarifa is he declare interest before
 
Back
Top Bottom