Intelijensia ya Rwanda sio ya mchezo mchezo, kinara wa Hotel Rwanda anashangaa kujikuta Kigali Airport

Intelijensia ya Rwanda sio ya mchezo mchezo, kinara wa Hotel Rwanda anashangaa kujikuta Kigali Airport

Kweli kabisa mkuu. Wanyarwanda wenyewe japo nchi yao kijiografia ni ndogo wanaiita "great country" labda kutokana na operations kama hizi
Mmh basi kama hayo wayasemayo itakuwa ni kweli mana mtu anapanda ndege anajua alaelekea position X mwisho wa siku anafika anakuta yupo position Y ni hatar sana intelijensia yao sio ya kitoto kabisa
 
Wazungu wakampa uraia, akapewa tuzo nyingi kama shujaa kumbe naye ailikuwa "mdhamini" wa mauaji na msaliti wa nchi yake! (Kuna mambo mengi ya kujifunza kutoka kwa huyu jamaa hasa pale unapoona kiongozi anapewa support kubwa na mataifa ya magharibi na Marekani) Ingekuwa Tanzania Paul Rusesabagina angekuwa kiongozi wa chama cha siasa au NGO ya kutetea Haki za raia, na hata urais angegombea tu, ila kwa Rwanda ukiisaliti nchi na kuwatumikia "mabeberu" lazima wakuwinde tu!
View attachment 1568411

Kuna hakika gani PK hana support ya hao hao wazungu?
 
Mkuu, ripoti rasmi tunazozisoma na kuzisikia ni kwamba Paul Kagame na RPF yake ndio walisimamisha genocide baada ya siku 100 za kuogofya sana ambapo Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa wastani waliuliwa na Interahamwe
"Reports, reports, reports...there will always be reports, but who writes those reports???" Benjamin Wiliam Mkapa on BBC Hardtalk 2001
 
Mwenyewe nimebaki nashangaa
Kagame mwenyewe aliulizwa je,walimteka huyo jamaa?

Akakataa akasema alikamatwa in a 'flawless Operation' na akaendelea kusema:

“He got here on the basis of what he believed and wanted to do,It’s like if you fed somebody with a false story that fits well in his narrative of what he wants to be and he follows it and then finds himself in a place like that.And he will say it, when the time comes, he will tell the people what happened."

So Mpk hapo maelezo ya PK hayajatoa mwanga wa maana wa kitu gani kilitokea nadhani mpk huyo jamaa mwenyewe aliyekamatwa aseme alikamatwaje.

Ningependa kusikia maelezo ya huyo jamaa pia.
 
Kuna hakika gani PK hana support ya hao hao wazungu?
Huyo jamaa wa hotel Rwanda ni raia wa Belgium na Permanent resident wa US, so watu walitegemea hizo nchi zitapiga kelele balaa baada ya kukamatwa kwake lkn cha ajabu Belgium iko zake kimya tu huku US ikisema huyo jamaa awe treated kibinadamu huko mahakamani/police,wahakikishe anapata haki zake na bla bla bla nyingine.

Yaani hakuna kelele za maana sana/za kushtua sana zilizopigwa na wazungu zaidi ni ngo's,HRW na baadhi ya watu binafsi ndio wanapiga kelele kimtindo.
 
Kagame amesema hawakumteka, ni kama unapopiga simu halafu unakuta umekosea namba, ndio hivyo alivyokamatwa hapo Rwanda
Sasa mkuu hio sentensi ya kupiga wrong number maana yake ni nini?
 
Hii Serikali ya Rwanda ni tata sana. Jamaa yangu mmoja (Mnyarwanda) anaiponda sana, lakini ukichat naye WhatsApp au fb utashangaa anavyoitetea. Kama utataka muongee akiwa huru inabidi utumie mitandao mingine ya kijamii kama WeChat (ambayo ni less popular).
 
Huyo jamaa wa hotel Rwanda ni raia wa Belgium na Permanent resident wa US, so watu walitegemea hizo nchi zitapiga kelele balaa baada ya kukamatwa kwake lkn cha ajabu Belgium iko zake kimya tu huku US ikisema huyo jamaa awe treated kibinadamu huko mahakamani/police,wahakikishe anapata haki zake na bla bla bla nyingine.

Yaani hakuna kelele za maana sana/za kushtua sana zilizopigwa na wazungu zaidi ni ngo's,HRW na baadhi ya watu binafsi ndio wanapiga kelele kimtindo.

We have to love our continent and her progress. Hatuwezi kuendelea kupigana nyundo na kutafuta maendeleo. Stability ya DRC, Rwanda, Burundi ni muhimu kwa ustawi wa eneo letu. Hizi approach za kizamani hazina nia njema kabisa na eneo letu
 
Paul Rusesabina aliyecheza filamu maarufu inayoelezea mauwaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 ambapo yeye alikua Manager wa Hotel akiwaokoa Watutsi wasivamiwe na kuchinjwa na Interahamwe hatimaye amefikishwa mbele ya sheria kwa makosa ya kuhusika na njama za mauji hayo hayo!!

Baada ya Rusesabagina kucheza filamu ile wakati wote dunia ilimuona kama shujaa aliyesaidia kuokoa maisha ya makumi ya Watutsi wasio na hatia waliokimbilia Hotel Rwanda hadi pale uchunguzi ulipofanyika na kugundua naye alikua mmoja wa walioshiriki kutekeleza genocide ile. Suala kama ana hatia au la mahakama itaamua lakini kilichoacha watu midomo wazi ni namna alivyofikishwa Rwanda, maana alikua akiishi Ubelgiji na alishachukua urai wa huko.

Inasemekana alikua Dubai na alidanganywa kupanda ndege ambayo labda aliamini inaenda sehemu nyingine. Kuja kutahamaki anajikuta anashuka Kigali Airport na pingu zikimsubiri!!!. Kabda ya hapo kuna jamaa wa Kinyarwanda aliandika makala akisema alijipa jukumu la kufuatilia nyendo za Rusesabagina duniani kote na alifanya hivyo kwa miaka 15 na kwa kukamatwa kwa Paul Rusesabagina basi ametimiza kazi yake akiwa kama Mzalendo wa nchi yake! Maofisa wa Rwanda wanasema jamaa amerudi mwenyewe kwa hiyari yake jambo ambalo ndugu wanalikanusha wakidai kua ametekwa, na sababu ni kwamba alianza harakati za kumuondoa madarakani Rais Kagame kwa kuongoza kundi la FNL ambalo Kigali inasema ni lakigaidi

Serikali ya rais PK kama alivyo yeye mwenyewe ina mkono mrefu na wanamsemo wao kua "There is a price to pay in betraying Rwanda" na kwamba hicho ndio kilichomkuta mcheza filamu/mwanasiasa Paul Rusesabagina
Kwanini intelligence ya Rwanda ilishindwa kuzuia mauaji yasitokee?
 
We have to love our continent and her progress. Hatuwezi kuendelea kupigana nyundo na kutafuta maendeleo. Stability ya DRC, Rwanda, Burundi ni muhimu kwa ustawi wa eneo letu. Hizi approach za kizamani hazina nia njema kabisa na eneo letu
Upo sahihi sana mkuu. Nyumba ya jirani haiwezi ikawaka moto kisha ukafikiri kwako patakuwa salama.
 
Back
Top Bottom