Internet ya uhakika na bei sawa na bure ni Adsl ya TTCL

Speed Ya 25K Ipo Vipi Kwa Users Wa 4 Home Users
kuna office jirani walikua wanalipia package ya 42,000..sijajua hii package ilitoka wapi..internet ilikua slow sana ata kubrowse tu ilikua shida,,, alikuja fundi wao akawashauri wa upgrade kwenda 50k ambacho ni reliable...icho cha 25k sijajua kwa kweli..ika kwa gharama za vifiurushi ilivyopanda 50k ni bargain tena ni unlimited package..wana option ya prepaid au post paid kwa iyo chaguo lako tu..si tuna device almost kumi na zote zinatumia kwa wakati mmoja na internet haizingui kabisa
 
Hivi hii unlimited ya voda nikiwa jirani na mnara wao wenye 4g kuna uwezekano wa kuipata huduma?
 
Technologia ya kutumia nguzo kusambaza internet: nasisitiza ni UCHAFU kwa miji yetu.

Weka minara mikubwa. Afu tununue hizo Router. Punguzeni bei.
 
Nafkiri hio ya miaka 15 haina wifi ni zile zinatumia waya moja kwa moja waweza tumia ila ukipata router ya wifi ni much better.

Pia kama unajiweza angalia fiber, ina speed zaidi.
Fiber nje ya mji wa dar kama kibamba,mbezi n.k itakuwepo kweli mkuu?
 
Hivi hii unlimited ya voda nikiwa jirani na mnara wao wenye 4g kuna uwezekano wa kuipata huduma?
Wameandika hapa coverage mkuu

 
Technologia ya kutumia nguzo kusambaza internet: nasisitiza ni UCHAFU kwa miji yetu.

Weka minara mikubwa. Afu tununue hizo Router. Punguzeni bei.
Wireless haiwezi compete na waya mkuu, unless uwe huna budi. Fiber inawezekana kuchimbiwa chini ya Ardhi, Hata TTCL huioni Fiber yao ni chini kwa chini tu mpaka ifike mtaani.
 
Wireless haiwezi compete na waya mkuu, unless uwe huna budi. Fiber inawezekana kuchimbiwa chini ya Ardhi, Hata TTCL huioni Fiber yao ni chini kwa chini tu mpaka ifike mtaani.
Nashukru mtaalamu kwa maoni yako.

Hiyo option ya chimbiwa ardhini chini ni sawa.
Ila kwa Tz toka hiyo fibre, ichimbiwe chini zama za Kikwete ni miaka zaidi ya 5. Ila haijasambazwa ktk makazi, maeneo ya biashara au ofisi. Wa kusambaza ni huyu TTCL (a Government Agency) ila nashangaa kutuambia kama upo karibu na zile nguzo za zamani!! Hapo ndio nachoka kabisaaa!!

Fibre is the best. Ila Mazingira yake Tz, hayajawezeshwa. Wote tuna penda kabisa hiyo huduma. Meanwhile, TTCL wawafikie watanzania wengi kwa kutumia the best Alternative.

Ushauri wangu: TTCL waombe Budget ya Kusambaza Fibre cables mitaani.
 
Wameshambaza maeneo mengi sana miezi kadhaa iliopita, hakuna tu taarifa ni wapi ipo na wapi Hakuna, mpaka mikoani sasa hivi wamefika.
 
Wameshambaza maeneo mengi sana miezi kadhaa iliopita, hakuna tu taarifa ni wapi ipo na wapi Hakuna, mpaka mikoani sasa hivi wamefika.
Nafuatilia sana kiongozi. Mikoani hizo waya zime nyooka tu Main Road (underground). Tena barabara Kuu tu. Hata hawatangazi wanao taka kuvuta. Wavute (shs ngapi). It means hawaja jiandaa. Hizo ni porojo za huku mitandaoni mkuu.

Tz walio connect Fibre hawafiki hata 1%ya watumiaji wa Internet uki linganisha na Kenya. Huu Mkongo wa Mawasiliano ya Taifa hautukimi ipasavyo! Hata hivi vifurushi vya Voda, Airtel, Tigo, nk wangeshusha wenyewe bila kelele. Ila wamechukulia opportunity ya mapungufu ya Wizara, TCRA na TTCL ktk kusambaza fibre ktk makazi ya watu.

Napenda kuona wakisambaza kama Maji.
 
Ni sawa mkuu unachoongea ila realistically fiber haitakua maeneo yote even nchi zilizoendelea maeneo ya Vijijini Adsl na satelite zinatumika sana.
 
Sisi kwetu manzese huo waya umo ndani ya nyumba sababu marehemu mzee allikuwa posta na simu jiwe so alifunga hizo simu home, shida ni kwamba waya kutoka nguzo iliyopo barabarani hadi kwetu ulikatika miaka kadha na ukichunguza vizuri maeneo mengi zimekatika na kuterekezwa.
Nyayya nene za fiber kampuni 3 tofauli zimepita barabarani(mita 200 toka home) sema jamaa hawasomeki
 

Ulijiongeza kiaje aisee? Kila wiki napita pale ofisini jibu ni lilelile
 

Mkuu hiyo adsl modem umenunua TTCL kwa gharama hiyo ya 55,000? Huku Mafinga fundi ananiambia 150,000 tena mpaka aagize Dar.
 
Nunua mwenyewe mkuu, ni Router na converter tu.

Bei zake ziko vipi? Ili nisije nikaingia kichwa kichwa. Kwa huku Mafinga wanasema fiber bado wanayo hiyo huduma ya adsl tu. Ndio nilikuwa nataka kujua nei ya hizi router
 
Bei zake ziko vipi? Ili nisije nikaingia kichwa kichwa. Kwa huku Mafinga wanasema fiber bado wanayo hiyo huduma ya adsl tu. Ndio nilikuwa nataka kujua nei ya hizi router
Bei ya TTCL ndo hio 55000 ongea na fundi akutafutie either kwa mtu ambaye hatumii tena, used, mpya etc.

Mimi kwangu nilinunua Uhuru na msimbazi kwa wale jamaa wanaomwaga mwaga vitu wana ma router kibao ya adsl 5000 mpaka 15000 sema mengi hayana wifi uwe makini.

Then baadae nikaongea na jamaa wa TTCL kuna mtu ali upgrade kwenda fiber alikua hatumii, akaniuzia around 30K, converter nayo ni around 5 mpaka 10k hivi.

Sasa hivi wengi wana upgrade kwenda fiber ongea na watu wa TTCL kupata router ya Adsl sio kazi, huyo jamaa wa 150k anakudalalia.
 
Chief, mimi matumizi yangu ni zoom meetings na Ms Teams meeting nyingi na online streaming kwenye Smart TV kubwa.

Je kwa uzoefu wako hii ASDL internet ya TTCL inaweza kunifaa kweli nikifunga nyumbani kwaajili ya home office?

Let's say nikichagua plan ya 50K kwa mwezi.
What's the maximum Mbps kwa 50K plan?

Asante
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…