Interview Rais Samia na Azam TV, azungumzia safari, Urais, Mikopo ya Miradi ya Magufuli, Ripoti ya CAG

Interview Rais Samia na Azam TV, azungumzia safari, Urais, Mikopo ya Miradi ya Magufuli, Ripoti ya CAG

amezungumzia miradi mikubwa ambayo ilikuwa ikitekelezwa wakati wa utawala wa Hayati John Magufuli kwa kueleza kuwa alikuwa akiijua lakini changamoto ni kwa kuwa ilikuwa ikiendeshwa kwa fedha za mikopo.
Si tulikuwa tunaambiwa tunajenga kwa fedha za ndani?
 
Nasikia marekani mafuta ni 6,000/= kwa kilo,
Eeh kwa lita
Eti kilo,
Tunawaza unga tuu
Haya twende kazi
 
Jambo hili kulilinganisha na Marekani ni uchache wa Busara kwasababu kuilinganisha kiuchumi Tanzania na Marekani ni upuuzi.
Kulinganisha kipato cha raia wa Tanzania na Marekani ni upumbavu.
Katika hili kilichoongelewa ni PUMBA TUPU
 
Watanzania bwana! Akili zetu kiduchu! Yaani mnakubaliana kabisa na maneno ya huyu mama! Eti sisi tuko bora kuliko marekani! Hivi unaweza kulinganisha nchi hii na mareakni kwa ishu yoyote ile? Na watu mpo mnasifia!
Afu eti sisi tuko bora kuliko Kenya, Rwanda, Uganda, na bado mtapiga makofi? Wenzetu wamepewa subsidy kusudi bei zisipande, sisi tukaambiwa kuwa bei zitapanda tuuu, na kweli zinapanda, na bado mko hapa mnaimba mapambio! Ama kweli wajinga ndiyo waliwao!
 
Rais Samia Suluhu Hassan amezungumza na Tido Mhando wa Azam TV, leo Mei 4, 2022


RAIS SAMIA: HAKUNA FUNDI WA URAIS, HAUZOELEKI
Rais Samia Suluhu Hassan amesema nafasi ya Urais haizoeleki kwa kuwa kuna mambo mengi.

“Sidhani kama kuna mtu anaweza kusema ni fundi katika nafasi ya Urais, labda kama mimi ni mgeni kwa kuwa nina mwaka mmoja.

“Nilipoteuliwa kuwa Rais mshtuko ulikuwa tukiola msiba haikuwa Urais kwa kuwa nilikuwa Makamu Rais kuna mambo nilikuwa nayajua,” - Rais Samia akizungumza na Azam TV.


SAMIA: TULIKOPESHWA FEDHA ZA MIRADI MIKUBWA
Rais Samia amezungumzia miradi mikubwa ambayo ilikuwa ikitekelezwa wakati wa utawala wa Hayati John Magufuli kwa kueleza kuwa alikuwa akiijua lakini changamoto ni kwa kuwa ilikuwa ikiendeshwa kwa fedha za mikopo.

“Miradi ilikuwa ya kwetu kwa kuwa nilikuwepo katika Awamu ya Tano na nilikuwemo katika mipango na utekelezaji, changamoto ni ukubwa wa miradi na uwezo wetu wa ndani.

“Kwa tafsiri ni kuwa tumeijenga kwa fedha zetu lakini tulikopeshwa, tatizo ni itaendeleaje? Lakini ni miradi yenye tija,” - Rais Samia akizungumza na Azam TV.


SAMIA: SAFARI ZINA FAIDA, LAZIMA TUTOKE TUKATAFUTE
Rais Samia amezungumzia kuhusu safari zake za nje ya nchi kwa kusema kuwa anatoka kwa kuwa safari zina faida nyingi kwa nchi ikiwemo kufungua biashara.

“Wanataka tujifungie hapa afu walie ukata mifuko ipo mitupu, sina miujiza ya kujaza mifuko yao, lazima tutoke tukatafute.

Wafanye tathmini za safari zenyewe, kila ninapoenda ninakuwa na wafanyabiashara, mfano nilikuta vikwazo 64 Kenya na vyote tulitatua baada ya kuzungumza,” Rais Samia akizungumza na Azam TV.

Ameongeza kuwa safari zake za Marekani amesaini mikataba ambayo kama itatekelezwa Tanzania itaingiza Tsh. trilioni 11.

RAIS SAMIA: NITAWATAJA WALIOCHANGIA BILIONI 7 ZA ROYAL TOUR
Rais Samia Suluhu amesema kupitia vipande vya kuitangaza Filamu ya Royal Tour ambavyo vimekuwa vikirushwa kwa miezi mitatu sasa zimeleta faida kubwa ambayo ni zaidi ya kiasi kilichotumika kuandaa filamu hiyo.

Tsh. Bilioni 7 zilitumika kuandaa filamu huku Serikali ikisema zilitokana na michango ya wadau mbalimbali

“Ni fedha nyingi lakini faida zake zikianza kuingia wataona, kuhusu waliochangia juzi Arusha niliwashukuru kwa ujumla lakini nitawataja tu,” - Rais Samia akizungumza na Azam TV.


RAIS SAMIA: TUTAFUTA KODI YA MAFUTA YA KULA
Baada ya mafuta ya kula kupanda bei Rais Samia Suluhu ameelezea kilichotokea na njia inayofuata ni kuondoa kodi ya mafuta ghafi yanayotoka nje.

“Mwaka 2020 mabadiliko ya tabia nchi hatukufanya kilimo vizuri, bajeti ya 2019/20 tulipandisha kodi ya mafuta yanayoitwa crude ambayo hayakuwa na kodi.

“Mafuta yakawa hayaingizwi, nazi na chikichi hazikutosheleza soko, hivyo bajeti inayokuja tunaenda kupitia mfumo wote wa kodi, tutaondoa kodi ya mafuta ya kula ili walete crude oil tuichakate tupate mafuta tuyasambaze ndani,” Rais Samia akizungumza na Azam TV.


RAIS SAMIA: BEI YA MAFUTA TANZANIA NI NZURI KULIKO ILIVYO MAREKANI
Kufuatia kupanda kwa bei ya mafuta miezi ya hivi karibuni, Rais Samia Suluhu amesema pamoja na hali hiyo bado bei ya mafuta kwa Tanzania ni nzuri ukilinganisha na yanavyouzwa Marekani.

“Kwa Kusini mwa Afrika na Afrika Mashariki, Tanzania tupo pazuri, hata kwa Afrika Mashariki sisi hali ya maisha ni nzuri ukilinganisha na majirani zetu.

"Kwetu bei za mafuta ni nzuri zaidi kuliko mafuta yanavyouzwa Marekani, lakini watu hawataki kutafuta ukweli, wanapiga kelele za kienyeji. Tanzania hatuagizi chakula, kipo cha kutosha,” - Rais Samia alipozungumza na Azam TV, leo Mei 4, 2022.

Mama! Usikute hayo mafuta unalinganisha galoni na lita. Hivi ni vipimo tofauti.

Hallelujah
 
nimesikitishwa na kauli iliyotolewa baada kufananishwa na USA.kila nikipekenyua kujua tunalingana nao vipi japo kidogo .
wajuaji mnaweza kutupa maelezo
 
Yeye yuko wazi tunatekeleza kwa mikopo full stop.. Sio tulidanganywa tutembee kifua mbele eti tunajenga kwa pesa zetu z a ndani kumbe ni mikopo.. Je umeelewa sasa?
Kuna kitu hujaelewa, wakati Mirada inaanza Nchi Wahisani walitaka kutupa mikopo yenye masharti, ndipo kama nchi ikaamua kuanza Mirada hiyo kwa fedha za ndani, hata kama kuna Mikopo si kama anayokopa huyu Mama. Yeye anasema tulijenga kwa pesa zetu lakini tulikopeshwa bila kutoa ufafanuzi kuwa tulikopeshwa na nani? Hata lile daraja pale Kigamboni limejengwa kwa fedha zetu lakini tulikopeshwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii.

Hii nchi ina Rasilimali za kutosha, kama zingesimamiwa vizuri, hii Miradi midogo midogo hii kama ya ujenzi wa madarasa tungeweza kutumia fedha za tozo tu na si kuchukua fedha za COVID.
 
Watanzania bwana! Akili zetu kiduchu! Yaani mnakubaliana kabisa na maneno ya huyu mama! Eti sisi tuko bora kuliko marekani! Hivi unaweza kulinganisha nchi hii na mareakni kwa ishu yoyote ile? Na watu mpo mnasifia!
Afu eti sisi tuko bora kuliko Kenya, Rwanda, Uganda, na bado mtapiga makofi? Wenzetu wamepewa subsidy kusudi bei zisipande, sisi tukaambiwa kuwa bei zitapanda tuuu, na kweli zinapanda, na bado mko hapa mnaimba mapambio! Ama kweli wajinga ndiyo waliwao!
Huyu Mama sijui kama ana Washauri wazuri wa masuala ya kiuchumi, hata kwa akili ndogo huwezi kulinganisha Marekani na Nchi zetu hizi za Afrika, Kule kuna allowance za kutosha, na kipato chao kipo juu hivyo hata kama vitu vikiwa bei juu wana uwezo wa kumudu.

Si kwamba Watanzania akili zao ni kiduchu, isipokuwa imefika mahali Watu wanapenda kuleta ushabiki usio na tija, yaani wanaleta utimu kwenye mambo ya msingi.
 
Sometimes ukijifanya unajua on the other side hujui kama hujui ni kitu kibaya san! Tuliambiwa miradi inayoendelea inaendeshwa kwa pesa za ndani!! Hapo ni Kiswahili lkn bado unahitaj tafsir ili uelewa ama unakaza tu fuvu hapa!!
Kwani kila pesa ya mkopo ni pesa ya nje, kama tulikopeshwa na Makampuni ya ndani je? Kwani lile daraja pale Kigamboni si limetumia pesa za ndani ambazo ni mkopo kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii? Huenda wewe ndiye unayekaza fuvu kuliko huyo unayemshutumu.
 
Kwamba miradi hiyo ilikuwa ikitendeshwa kwa fedha za mikopo. Awali tuliambiwa kuwa fedha iliyotumika ni toka hapa ndani ya nchi. Sasa tunaambiwa vinginevyo. Ama kweli wanasiasa si hasa.
Inawezekana ni fedha za mkopo kutoka ndani ya Nchi, sijaona mahali aliposema vinginevyo, yeye kasema tulijenga kwa fedha zetu lakini za mkopo, kwani lazima kila mkopo uwe wa fedha za nje?
 
hivi kweli mijianaume na midevu yetu tumekaa mwanamke ndiye anaenda kututafutia ?

vya kutafuta ni vingi na mama hajaweka wazi anaenda kutafuta nini sisi tukae tukenue meno tu ataleta
Kwa hiyo unataka tufanyaje? Yeye si ndiye Rais wa Nchi na ameona njia sahihi kwake ni hiyo?
 
Yeye yuko wazi tunatekeleza kwa mikopo full stop.. Sio tulidanganywa tutembee kifua mbele eti tunajenga kwa pesa zetu z a ndani kumbe ni mikopo.. Je umeelewa sasa?
Kwahiyo Kodi zilizokusanywa na magufuli alizikwa nazo!!?
 
Wabongo wengi mna upumbavu mobu , sasa wewe shida yako kama mwananchi ni nini? ni masharti au unataka miradi ifanyike? Hayo masharti umewahi wekewa hadharani tangu awamu ya kwanza ya fisiemu ?
Wewe unaangalia tu kwamba Miradi ifanyike bila kujali inafanyikaje? Unajua kuwa hii Mikopo si misaada? Unajua nani anatakiwa kulipa? Leo hii tumekewa tozo kwenye Miamala ya Simu na tozo ya Jengo kupitia LUKU, ina maana hiyo inamgusa hadi Mwananchi wa hali ya chini, hayo yote yanatokana na huo mzigo wa madeni, ambapo fedha zinazokusanywa zinatumika kulipa madeni badala ya kufanya shughuli za maendeleo.

Sijui kama unafahamu kuwa Mikopo hiyo inalipwa hata sasa? Unafahamu kuwa uwanja wa Ndege wa Entebe pale Uganda ulichukuliwa na Wachina kwa kushindwa kuwalipa madeni? Kuna faida gani hiyo Miradi ikaisha alafu ikachukuliwa na Nchi Wahisani kwa kushindwa kuwalipa?
 
Back
Top Bottom