Ipo siku Wapinzani watatamka hadharani kuwa Watamuunga mkono Rais Samia Uchaguzi ujao

Ipo siku Wapinzani watatamka hadharani kuwa Watamuunga mkono Rais Samia Uchaguzi ujao

Chakula Bei Juu, Wewe Unakwenda Lumumba Kusaini Huyaoni
Kilimo Ni Biashara kwa Sasa,Acha wakulima wafaidike na jasho lao maana kwa muda mrefu Sana wameumia Sana katika kubeba mzigo wa kulilisha Taifa hili lakini mwisho wa siku waliokuwa watu wa kupangiwa Bei na mahali pa kwenda kuuza , mpaka wakati huu alipopatikana mfariji wao na mkombozi wao Rais Mama Samia Suluhu Hassan aliyekuja kuwashika mkono na kuwafuta machozi yao
 
Ndugu Zangu Watanzania,

Huo Ni Utabiri wangu kwa jicho la mbali kwa kuangalia Hali ya mambo Inavyoendelea hapa nchini,Kwa namna Rais Samia anavyokubalika,anavyopendwa na watanzania,alivyoiteka mioyo ya watanzania,uchapa kazi wake uliotukuka,Dhamira yake njema katika kulijenga Taifa letu,upendo wake kwa watanzania, usikivu wake kwa watanzania, juhudi zake za kuimarisha maridhiano na kujenga umoja wa kitaifa, Naona Rais Samia Akiungwa mkono na vyama vya upinzani ili apite bila kupingwa .

Hakuna ajenda inayogusa hisia za watanzania ambayo Rais Samia hajaigusa na kuzifanyia kazi,hakuna kero au changamoto ambayo Rais Samia hajaitolea majibu,hakuna sauti ambayo imepuuzwa masikioni mwa Rais wetu mpendwa mama Samia,Hakuna kundi ambalo halijapewa sauti ya kusikika masikioni mwa Rais wetu Jasiri shujaa mzalendo na mcha Mungu.

Hakuna ajenda ambayo wapinzani wanaweza ibeba na kuipeleka kwa watanzania na kupokelewa kwa hisia,kwa kuwa kila ajenda imebebwa na kufanyiwa kazi na Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania, Ni kazi kila mahali amefanya Rais wetu,miradi ya kimkakati imechipua na kutamalaki maeneo mbalimbali,Taifa limetulia na kutamalaki amani,mioyo ya watanzania Ni yenye furaha na Tabasamu.

Hakuna mwenye chuki na Rais Samia,hakuna aliyeumizwa Wala kuonewa na Rais Samia,Hakuna aliye na kinyongo na Rais Samia,wote wanampenda Sana Rais Samia kwa kuwa kila mtanzania anajiona kuthaminiwa na kusikilizwa,kila mtu ana matumaini ya kutimiza Ndoto zake chini ya uongozi wa Rais Samia.

Sasa Nani wa kumpinga mama Samia wetu? Nani wa kushindana Naye? Umpinge ili uje ufanye Nini ambacho Rais wetu hajafanya? Kipi ambacho Rais wetu hajagusa? Sauti ya Nani ambayo haijasikika masikioni mwa Rais wetu? Nani ameonewa na Rais Samia? Nani kadhurumiwa? Kwani hamsikii namna ambavyo Rais wetu akihubiri Haki? Hamsikii na kuona namna ambavyo mh Rais akiwa mwenye huruma kwa kila mtu na kumtendea haki kila mtu?

Tuna taka Nini watanzania? Tunamtaka Nani Zaid ya Rais Samia? Tuna taka kipi kutoka kwa nani ambacho kimemshinda Rais Samia? Kipi ambacho tumekihitaji watanzania na hakijafanyiwa kazi na Rais Samia? Kwanini Tusimuunge mkono Rais samia? Tunamtaka malaika ashushwe ndio aje atuongoze? Kama Ni binadamu Basi niseme kuwa Rais Samia anatosha Kuendelea kutuongoza maana ametuvusha nyakati ngumu na kutufikisha hapa Kama Taifa tukiwa wamoja na wenye mshikamano,Na Ameonyesha uwezo mkubwa wa kiuongozi.

Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
oya Mwashambwa hii namba uliyoacha inapokea pesa?
 
Labda kwa ccm B lakini kwa chadema utasubiri sana.
 
Mambo aliyoyafanya mh Rais wetu mpendwa ndani ya muda mfupi Ni makubwa Sana,amekuwa mbele ya wakati kimaendeleo,Amefika haraka mahali ambapo mwingine asingeweza kufika kwa muda huu,hivyo Ni sahihi kumpongeza na kumpa nafasi ya Kuendelea kututumikia kututumikia watanzania
Kafanya Jambo gani lililowagusa WANANCHI moja Kwa moja ukitoa Hili la kuruhusu mikutano.
 
Nakubaliana na wewe mkuu.

Alichokifanya jana Mbowe hakina tofauti na wale wapinzani wa awamu ya tano, upinzani kuunga mkono, nahisi ni APPROACH na SLOGAN ndio tofauti awamu ya sita tunaita MARIDHIANO na awamu ya tano KUUNGA MKONO JUHUDI.

Zamu ya Mwenyekiti
 
Kwa nini isiwe hivyo katika eneo la Urais pia??
Kwenye Eneo la Urais Hakuna mpinzani wa kushindana na Rais Samia maana amefanya makubwa yenye tija yaliyomgusa kila mwananchi bila kujari chama chake,ndio maana umeona katika mkutano wa chadema jina la Rais Samia likitawala kwa kusifiwa
 
Serikali kazi take ni kuwainua watu kiuchumi na siyo kuwadidimiza,serikali ya Rais Samia Ndio kazi kubwa inayoifanya kwa Sasa kuwainua watu kiuchumi kwa kuwawezesha na kuwawekea mazingira rafiki na wezeshi
Nakukumbusha tena! Propaganda zako zinafaa sana huko vijijini tena ukisisitiza amani, mshikamano na upendo. Humu watu wameshavuka kiwango cha kuhitaji malazi, chakula na mavazi! Usikimbie point, umesema SSH anawasemea wanyonge - nimeuliza hao wanyonge wametengenezwa na nani kama wapinzani unaowasema hapa hawakuwahi kuongoza??

Kazi kubwa ulionayo ni kuwaaminisha watu kuwa kila kitu kinachofanyika sasa ni bora kabisa ambacho wapinzani hawawezi kufanya. Unawezaje kufanya ulinganifu katika watu wawili ambao mmoja hakuwahi kufanya chochote?? Unailinganishaje CCM na wapinzani katika kutatua matatizo ya taifa hili wakati wapinzani hawakuwahi kuongoza nchi??
Ndio maana nasema propaganda zako zilengwe kwa watu sahihi - wasiojua!! Humu wengi wanajua!!
 
Back
Top Bottom